Mo Ndani Ya Fox News

Mo Ndani Ya Fox News

Siku hizi hakuna kitu.

Waulize akina Jokakubwa ,Mag3 Fundi Mchundo zama hizo balozi wa nyumba kumi na majukumu na heshima yake

Kwa taarifa yako balozi wa nyumba kumi zama hizo alikuwa mjumbe bila kujali vyama
Bado kabisa na hujui nini ilikuwa Tanzania kiulinzi. Hakuna kitu siku hizi usijidanganye

True nakumbuka babu yangu alikuwa pia mjumbe sikuwai kumuona amevaa sale ya ccm

Ila nilikuja kupata fununu alikuwa usalama wa taifa baada ya Sumaye kuja kwenye mazishi yake mwaka 2003 akiwa waziri mkuu

Ilikuwa ni ngumu sana kuelewa imagene amekuwa usalama wa taifa toka nchi inapata uhuru mwaka 1961 mpaka anakufa hakuna ndugu hata mmoja anajua

Lakini ukija kwa wanausalama wa siku hizi ndio utashangaa sana.
 
Pesa Nguruvi3!. Ndo kitu pekee ninachoweza kukifikiria.Mo asingekuwa bilionea sidhani kama wangemzungumzia.
But I could be wrong...
Absolutely! Ndiyo maana handling yake ilitakiwa iwe na weledi

Pesa na marafiki wenye pesa ni habari kubwa. Ukishaona BBC, FOX, CNN, Le Figaro, Al ahram, Le mundo, The Sun, The Herald, Gulf news, Aljazeera n.k. wanazungumzia, ujue ni habari ya mjini

Handling ya hili suala ni disaster, kuna vipande vingi ukiunganisha huwezi ku solve the puzzle
Kuanzia kwa ''Mambosiasa hadi GIP 0'' ni colossal failure na kuacha jibu moja tu...
 
wengi ni CCM hata hivyo

upinzani ulitakiwa kupambana kuondoa hawa wawepo kama sehemu ya serikali na siyo ya chama chochote

kikubwa na tatizo ni walikuwepo siku zote before vyama vingi
Ndio wengi ni CCM kama ilivyo kwa wabunge. But utendaji wao wa kazi umebaki kuskiliza kesi za baba chanja na mkewe
 
kaka upo! kimya sana

sioni wa kunipa changamoto umekuwa kimya sana,
mimi na wewe kesi yetu ambayo tume i carry over ni kuwa zito msaliti au sio msaliti??. Bado nabisha sio msaliti! sijui umebadili mawazo yako au una msimamo ule ule??
Salama kabisa! Nipo ''tunakwaruzana'' na akina NN katika mitazamo ha ha ha, lakini katika hali nzuri ya kujenga fikra kwa kukubaliana au kukubaliana kutokubaliana

Kuhusu kesi, nipo katika nafasi nzuri kuliko wakati naijenga. Msimamo wangu ni ule ule!
Well, Kitila, Mwinyigamba , Kafulila n.k. wanasaidia hoja yangu ya kumpotosha ZZK
Kumbuka kesi zipo mbili, usaliti (covert operation) na hoja za wasaliti

Tusitoke nje ya uzi, kukiwa na fursa tutajadili kwa kina katika uzi mwingine
 
Absolutely! Ndiyo maana handling yake ilitakiwa iwe na weledi

Pesa na marafiki wenye pesa ni habari kubwa. Ukishaona BBC, FOX, CNN, Le Figaro, Al ahram, Le mundo, The Sun, The Herald, Gulf news, Aljazeera n.k. wanazungumzia, ujue ni habari ya mjini

Handling ya hili suala ni disaster, kuna vipande vingi ukiunganisha huwezi ku solve the puzzle
Kuanzia kwa ''Mambosiasa hadi GIP 0'' ni colossal failure na kuacha jibu moja tu...

Uko sahihi kabisa!

Handling ya hii issue haipishani sana na handling ya wa Saudia na mauaji ya Khashoggi...[silinganishi matukio...nalinganisha handling]

Wasaudia wamegeuka kuwa kituko kabisa!!

Ila Sirro and Co hawako mbali....
 
Hapo kwenye red hiyo habari umeipata wapi mkuu?! Mo hakupewa simu na hao watekaji bali alipewa simu na walinzi waliokua eneo lile na kwa vile alikua na namba ya baba yake kichwani ndio akampigia.
Hivi hao walinzi hawakuitaka ili bil 1 au hawakufahamu ni nani wanamwazima simu?
 
Uko sahihi kabisa!

Handling ya hii issue haipishani sana na handling ya wa Saudia na mauaji ya Khashoggi...[silinganishi matukio...nalinganisha handling]Wasaudia wamegeuka kuwa kituko kabisa!!

Ila Sirro and Co hawako mbali....
Umeona! Tunabahati wanaoandika habari za kichunguzi hawajapiga kambi Tz, hii ingekuwa aibu ya Kimataifa kama kituko cha Saudi Arabia

Sirro and Co si kwamba hawapo mbali, wamefikia kiwango cha aibu ya Khasoggi.
Tofauti ni kuwa Saudi Arabia wameshikiwa bango na weledi wa dunia kwa utajiri, sisi tumesahaulika kwa umasikini wa nchi. Handling ya Saudia na Sirro ni at par
 
wengi ni CCM hata hivyo

upinzani ulitakiwa kupambana kuondoa hawa wawepo kama sehemu ya serikali na siyo ya chama chochote. kikubwa na tatizo ni walikuwepo siku zote before vyama vingi
Rasimu ya Warioba ililenga hilo, wakagundua na kupiga torpedo

Nadhani wananchi kwa ujumla wanatakiwa wasimame kwa hili.

Wamefikia mahali hawana hata chembe ya soni wanasimama wakiwa na nembo ya Taifa, magwanda na virungu vinavyolipiwa kodi na Watz, halafu wanatamba 'Kidumu chama cha mapinduzi''. Polisi aliyetumwa kumwakilisha IGP anasema ''Kidumu chama cha Mpainduzi''

IGP anasikitishwa lakini hachukui hatua yoyote dhidi ya mhusika kwasababu anamuogopa Mwenyekiti wa CCM. Kwamba askari aliyesema alisifia chama cha mwenyekiti aliyemteua IGP
 
Rasimu ya Warioba ililenga hilo, wakagundua na kupiga torpedo

Nadhani wananchi kwa ujumla wanatakiwa wasimame kwa hili.

Wamefikia mahali hawana hata chembe ya soni wanasimama wakiwa na nembo ya Taifa, magwanda na virungu vinavyolipiwa kodi na Watz, halafu wanatamba 'Kidumu chama cha mapinduzi''. Polisi aliyetumwa kumwakilisha IGP anasema ''Kidumu chama cha Mpainduzi''

IGP anasikitishwa lakini hachukui hatua yoyote dhidi ya mhusika kwasababu anamuogopa Mwenyekiti wa CCM. Kwamba askari aliyesema alisifia chama cha mwenyekiti aliyemteua IGP

sikujua kumbe rasimu ya warioba iligusa vitu vingi

Polisi alitia aibu mno

Polisi kushika hatamu kwa niaba ya chama ni tatizo la msingi
 
sikujua kumbe rasimu ya warioba iligusa vitu vingi

Polisi alitia aibu mno
Polisi kushika hatamu kwa niaba ya chama ni tatizo la msingi
(c) Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano Jeshi la Polisi la Tanzania

227.-(1) Kutakuwa na Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano litakalokuwa na jukumu la ulinzi wa watu na mali zao chini ya masharti ya Katiba hii.

(2) Bunge litatunga sheria kuweka masharti ya utekelezaji wa kazi na majukumu ya Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano kwa kuzingatia haki za raia na sheria za kimataifa. Misingi ya utendaji wa Jeshi la Polisi 228. Katika utekelezaji wa majukumu yake, Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano litazingatia- (a) viwango vya juu vya kitaaluma na nidhamu miongoni mwa wafanyakazi wake;

(b) ulinzi na ukuzaji wa haki za binadamu; (c) kanuni za uwazi na uwajibikaji; (d) kuzuia rushwa na ufisadi; na (e) kukuza mahusiano na jamii. Uteuzi wa Mkuu wa Jeshi la Polisi 229.

Kutakuwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano ambaye atateuliwa na Rais baada ya kushauriana na Baraza la Ulinzi na Usalama wa Taifa.

Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi 231.-(1)
Kutakuwa na Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi itakayokuwa na jukumu la kusimamia masuala yote ya utumishi wa Jeshi la Polisi na idara zake. (2) Katika suala la uajiri wa maofisa na watumishi wengine wa Jeshi ‐ 91 ‐ la Polisi, Tume ya Utumishi waJeshi la Polisi itazingatia Kanuni na Misingi ya Utumishi iliyoainishwa katika Katiba hii. (3) Bunge litatunga sheria kuweka masharti ya muundo na utekelezaji wa kazi na majukumu ya Tume ya Utumishi waJeshi la Polisi.
 
Ndio wengi ni CCM kama ilivyo kwa wabunge. But utendaji wao wa kazi umebaki kuskiliza kesi za baba chanja na mkewe
Na kutekeleza ilani ya chama 'Kidumu chama cha mapinduzi'' wadogo wanaimba 'abebwe abebwe!'
 
Rasimu ya Warioba ililenga hilo, wakagundua na kupiga torpedo

Nadhani wananchi kwa ujumla wanatakiwa wasimame kwa hili.

Wamefikia mahali hawana hata chembe ya soni wanasimama wakiwa na nembo ya Taifa, magwanda na virungu vinavyolipiwa kodi na Watz, halafu wanatamba 'Kidumu chama cha mapinduzi''. Polisi aliyetumwa kumwakilisha IGP anasema ''Kidumu chama cha Mpainduzi''

IGP anasikitishwa lakini hachukui hatua yoyote dhidi ya mhusika kwasababu anamuogopa Mwenyekiti wa CCM. Kwamba askari aliyesema alisifia chama cha mwenyekiti aliyemteua IGP
Lakini upinzani uliona serekali tatu ni muhimu kuliko haya. Ukitafakari kwa utulivu bila ya kuongozwa na mapenzi ya vyama,utagundua kwamba,madaraka kwa wanasiasa ndio yalikuwa kipaumbele bila kujali jinsi ya kuyapata.

Au labda mi sijaelewa,hivi sehemu hiyo ya muundo wa jeshi la polisi nayo ilibishaniwa?
 
Uko sahihi kabisa!

Handling ya hii issue haipishani sana na handling ya wa Saudia na mauaji ya Khashoggi...[silinganishi matukio...nalinganisha handling]

Wasaudia wamegeuka kuwa kituko kabisa!!

Ila Sirro and Co hawako mbali....
Kwahio unamaanisha serikali yetu imehusika kama serikali ya Saudi?
 
Mo mwenyewe Amesema walikuwa na wasi wasi sana.

Tanzania sio nchi ya kuchezea. Kuna wajumbe wa nyumba kumi kumi. Hawa ni part ya wanachama wa CCM na wanalipwa kwa kazi yao. Hawafanyi bure. Katika security hapo utachoka mwenyewe. Mwalim Nyerere aliona mbali sana.

Nawashangaa vijana wa leo katika Press Conferences wanauliza maswali ya kinjinga kuhusu utendaji wa jeshi la usalama na ulinzi Tanzania. Hawajui jinsi hii nchi kiulinzi ikoje? Hiyo ndiyo msingi ya ulinzi wa nchi yetu. Vinginevyo moja wetu ungesha vunjika.

Hii system Mwalim Nyerere kaitoa kwa wachina. Unachosema na kufanya mitaani tayari kimesha reportiwa kwa wahusika na wanajua nini kinatendeka. Nyie kaeni tu na utaalam wenu fake na kuuliza maswali yenu ambayo ni irrelevant.
Wakati mwingine fucha tu aibu yako ndugu,hivi kama kila kinachofanyika kinajulikana unamaanisha kwamba hata tukio la kutekwa kwa Mooo,hao mabalozi wa nyumba kumi walikuwa wanajua!?

Na kama mfumo wetu wa ulinzi upo strong kwa kiasi hicho waliopotea na wengine kuuawa,na wengine kujeruhiwa vibaya bila kukamata hata suspect mmoja,unatwambia nini!?

Waliouawa,mfano Alphonce Mawazo,
Waliojeruhiwa vibaya,mfano Tundu Lissu
Waliopotea mfano Azory Gwanda!

Hao ni wale ambao hakuna suspect au ufafanuzi wa kueleweka juu ya ni kina nani waliohusika kufanya unyama dhidi ya raia wenzetu hawa,na hao ni kwa wale tunaowafahamu,yamkini kuna wengine wengi tusio kuwa na taarifa zao!

Hii ni nchi yetu wote,tusiiharibu kwa mikono yetu,kwa mahaba ya kiitikadi,na rangi za bendera za vyama vya siasa,tukaacha msingi muhimu wa Upendo na mshikamano kwa maslahi ya wachache walio na kiburi na jeuri!
 
Jumamosi usiku mishale ya saa tatu, nikiwa naangalia kipindi cha Justice With Judge Jeanine, ghafla naona habari kupatikana kwa Mo zikipita chini kwenye kioo cha tivii [news ticker ].

Interesting....

View attachment 905571View attachment 905572View attachment 905573View attachment 905574View attachment 905575View attachment 905576View attachment 905577
Ngosha unamuangalia huyu mama mbaguzi namba moja akishirikiana na Tucker Carlson???? Hawa ni watendaji wa Trump siyo
 
(c) Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano Jeshi la Polisi la Tanzania

227.-(1) Kutakuwa na Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano litakalokuwa na jukumu la ulinzi wa watu na mali zao chini ya masharti ya Katiba hii.

(2) Bunge litatunga sheria kuweka masharti ya utekelezaji wa kazi na majukumu ya Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano kwa kuzingatia haki za raia na sheria za kimataifa. Misingi ya utendaji wa Jeshi la Polisi 228. Katika utekelezaji wa majukumu yake, Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano litazingatia- (a) viwango vya juu vya kitaaluma na nidhamu miongoni mwa wafanyakazi wake;

(b) ulinzi na ukuzaji wa haki za binadamu; (c) kanuni za uwazi na uwajibikaji; (d) kuzuia rushwa na ufisadi; na (e) kukuza mahusiano na jamii. Uteuzi wa Mkuu wa Jeshi la Polisi 229.

Kutakuwa na Mkuu wa Jeshi la Polisi la Jamhuri ya Muungano ambaye atateuliwa na Rais baada ya kushauriana na Baraza la Ulinzi na Usalama wa Taifa.

Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi 231.-(1)
Kutakuwa na Tume ya Utumishi ya Jeshi la Polisi itakayokuwa na jukumu la kusimamia masuala yote ya utumishi wa Jeshi la Polisi na idara zake. (2) Katika suala la uajiri wa maofisa na watumishi wengine wa Jeshi ‐ 91 ‐ la Polisi, Tume ya Utumishi waJeshi la Polisi itazingatia Kanuni na Misingi ya Utumishi iliyoainishwa katika Katiba hii. (3) Bunge litatunga sheria kuweka masharti ya muundo na utekelezaji wa kazi na majukumu ya Tume ya Utumishi waJeshi la Polisi.

wamekosea mkuu, uko sahihi kabisa
 
Back
Top Bottom