Mnyika, Balille, Rostam Aziz na kisa cha sms!

Mnyika, Balille, Rostam Aziz na kisa cha sms!

hasira hasara ....hasa kwenye siasa. mnyika inabidi uwe na subra kama unataka kuwa mkombozi wa kweli

Subra gani, FISADI ni FISADI tu hakuna cha SUBRA wala CHUBRA. FIsadi apewe ukweli wake, serikali imeshindwa kuwataja na kuwachukulia hatua. Kilichobaki ni wananchi akiwemo Mnyika kuanza kuwahesabu kisha kuwapa wanachostahili. Nyie subirini tu......pale hiyo SUBRA itakapoyeyuka kwa wananchi ndo mtajua kuwa hata mrenda unaweza ukawa JAM kwa mkate.
 
Subra gani, FISADI ni FISADI tu hakuna cha SUBRA wala CHUBRA. FIsadi apewe ukweli wake, serikali imeshindwa kuwataja na kuwachukulia hatua. Kilichobaki ni wananchi akiwemo Mnyika kuanza kuwahesabu kisha kuwapa wanachostahili. Nyie subirini tu......pale hiyo SUBRA itakapoyeyuka kwa wananchi ndo mtajua kuwa hata mrenda unaweza ukawa JAM kwa mkate.

Indume, Tazama nchi hii iko mikononi mwa haya kanjanja, tukikurupuka kwa matusi basi tutaishia pabaya,

Ushauri wangu ni kwamba tufanye juhudi za dhati kuzuia hayo yajayo 2011,
 
Mh D.W Slaa..
Napenda kuchukuwa fursa hii kuuliza kile ambacho bado hamjataka kunijibu either kwa kupuuzia ama labda kwa kuona hakuna umuhimu huo.

Kama kweli mnapinga ukabila...Then naomba muwe HONEST na ili kweli tuweze kuja pamoja bila chuki.

Na kwenye posting yako uliyomjibu Isaya Mwita..Ni jibu ambalo liko deircted kwangu kwani mimi ndio nilikosea na kusema ni makamu Mwenyekiti badala ya kaimu makamu.

Sasa kwasababu umeshaweka wazi kuwa yeye ni kaimu katibu mkuu...Napenda maelezo HONEST kutoka kwenu...Na mkiweza kunieleza vizuri basi na mimi nitakubali tu..Kwani wakuu mtakuwa mmeshiriki kunifundisha historia kamili ya Tanzania.

Mnyika...Kwenye ile thread ya mashujaa wa Tanzania iliyopostiwa naMpaka Kieleweke...Alisema wazi kuwa Mangi Sina ni MSALITI kwa kumsaliti mangi MELI dhidi ya WADACHI!?

Sasa mheshimiwa...Naomba muweke rekodi straight kwasababu mwenyekiti ni mmachame na bado hamjanieleza USALITI WA SINA.

Kama ni kweli alisaliti..Niambieni..Kwasababu labda mimi kuwa mjukuu wa Sina...Hakuna anayeweza kuniambia UBAYA wa BABU YANGU HUYO KUHUSIANA NA USALITI WA TAIFA LETU.

Nitashukuru sana...Kwani hata marehemu amesababisha nyie kuhusishwa na kifo chake kwa kuwa hamkujibu tuhuma za UKABILA wala kuzifanyia kazi.

Hata ile tume ya Mziray ilionekana ni USALITI!?

Na mimi na UKABILA NI MBALI MBALI...Hata ndugu zangu wamachame wanjuwa kuwa mimi huwa na reach out bila matatizo..Napenda ushirikiano...UNAFIKI SITAKI!

Kama mnataka ushirikiano wa wachagga wote wekeni wazi mambo mengine ili tusonge mble na kama mki prove kuwa SINA alikuwa MSALITI...Basi sitakuwa na kinyongo wala nini na nitasonga mbele tu.
JMUshi
Thanks kwa posting yako directed kwangu.
i) Sina tabia ya kujadili au kujibu hoja ambazo sijazifanyia kazi. Mimi Mwiraq wa Karatu utanionea kujibu swala la Mangi Sina na Meli ilhali hata kuisoma thread yenyewe sijaisoma.
2) Umeingiza ulichoita "Tume ya Mziray". Kwanza niseme kuwa hakuna kitu kinachoitwa "Tume ya Mziray" katika Chadema kulikuwa na "Kamati ya Mziray. Sijui umeliunganisha vipi. Nilidhani the best approach ilikuwa ni kuniuliza background ya Kamati hiyo, hadidu za rejea na jinsi ilivyojadiliwa na maamuzi yalifanywa na Kamati Kuu. Nimeisoma yote kwenye magazeti na yeyote aliyeipeleka huko na kwa malengo aliyokuwa nayo. Ningelifurahi zaidi ningeliona mjadala wake ulivyohitimishwa na Kamati Kuu bila upotoshwaji. Hivyo nilitaka niweke sawa hayo mawili.
 
Sikuwahi kujua kuwa hapa jf tumejaza watu waoga kiasi hiki. Maana hawa wanaomuogopa RA kuambiwa fisadi hata nimeshindwa kubaini uoga wao umeanzia wapi. Jamani mwizi si mwizi?
Mbona hata BWM hakuwahi kuwashitaki wale vijana wa mtaani pale Mwenge waliothubutu kumuita raisi mstaafu fisadi, pamoja na kwamba walikamatwa?
Hivi kweli tunaweza kupoteza muda wetu hapa jukwaani tukimuita RA fisadi na akitokea na tukapata fursa tusimuite kwa kuogopa mahakama wakati tuna ushahidi kuwa ni fisadi kweli? Kama ni vifungo kwa wapigania haki si ni kitu cha kawaida? Maana najua hili pia lawezekana kwa mafisadi kutumia pesa za wizi kukandamiza wapiganaji. Lakini hili laweza kutufikisha mahali pa kuogopa kiasi hiki jamani?
Mnyika anastahili pongezi nyiingi sana. Ni mmoja wa watu wachache katika nchi hii wanaoweza si kuandika hapa jf tu kwa jina lake kamili lakini hata kumwambia mfalme kwamba yuko uchi.
Ninaamini huyu aweza hata kumwambia raisi wetu ukweli katika mambo yasiyo sawa. Ni tofauti na hawa vijana wa ccm ambao kila siku utasikia wanasifu tuuuuuuuuuuuuu na nadhani hiyo ndiyo sifa ambayo PM aliyeanzisha thread hii anavyotaka iwe maana anadhani usipofanya hivyo basi unakufa kisiasa. Na hapa ndipo uoga woooote wa vijana wa kitanzania unapoanzia kunishangaza.
Tupo katika nyakati ambazo tunatakiwa kuwa wakweli na kutetea utanzania wetu bila kujali nani ni nani. Hapa wala RA asiwe ni mtu wa kutisha kila Mtanzania ili tu apate namna ya kutuibia zaidi. Ikiwezekana kila Mtanzania akiweza amwambie yeye ni fisadi.
Kama tulivyofanya kwa Siclair tunaweza kufanya na kwa RA. Tupewe namba zake za simu au email yake tui flood kwa mails na SMS kwamba yeye ni fisadi, na ajue kwamba wa Tz tumeshamchoka kwa kuliibia taifa letu. Hapa bado nampongeza Mnyika kwa kuwa mkweli kwa fisadi. Tena kwa kuwa muwazi kwake kwamba si kwamba hakusema bali ni kweli alimuandikia smna kuwambia RA ni fisadi.
Lakini kwa upande wa pili namshangaa sana huyu Balile.
Yeye alikuwa mwana Chadema na tena mkeleketwa wakati yuko na gazeti la mwananchi, na hata alipotoka kwenda kuanzisha gazeti la Tanzania Daima kule Free Media. Huko alikuwa kitumika sana kupinga ukandamizaji na ufisadi sana. Wakati huo alikuwa ni Mhariri mtendaji mwanzilishi wa Free media. Beef yake na Chadema ilianza pale alipopata nafasi ya kwenda kusoma Uingereza na aliporudi alikuta nafasi yake ikiwa imechukuliwa na mtu mwingine. Nakumbuka hata makala aliyoandika mara ya mwisho katika gazeti la TD kwamba amekubaliana na Mbowe hataandikia gazeti la TD na ameamua kuondoka kwa maelewano mazuri.
Kumbe yeye naye ni mtu wa njaa tu. Akikutana na wezi yuko tayari ku side nao ili mradi anapata kitu kidogo siyo. Nilikuwa mpenzi wa makala zake at that time, na shame upon him kwa side na mafisadi hata kama anapata milioni kwa mwezi. Naye ni wa kulaaniwa kama RA. Na kwa kuanzia yale magazeti ya Rai yalishapoteza mvuto na hayana kitu tena. to hell with them.
Eddy, Masatu na wengine mliojaa uoga wa kwenda mahakamani, kaeni pembeni wengine wasonga mbele. Kama mnadhani ujumbe kwa mtu haumfikii kwa SMS nyie wote ni wa kushangaza tu maana hata hapa jf sijui mnatafuta nini maana hapa hatupo kupiga porojo kama ujumbe huu haufiki kwa walengwa. Nyie ni mashahidi kwamba tunawaandika sana humu hao mafisadi tukiamini kwa jinsi yoyote ujumbe utakwenda, iweje tusiwaandikie SMS pia? au hata kuwaambia phyisically? Waoga hapa hawatakiwi. Jiondokeeni hata hapa maana hamna maana.
Tunao tayari ushahidi wa wasio waoga kusema ukweli akina Dr Slaa mbona leo ndio wanaoonekana kama wabunge pekee bungeni? yaani bunge limekuwa kama la watu wiwili watatu tu hivi. Kwa nini? kwa sababu wanasema iliyo kweli. Tukiendelea kubaki kimya tukiwaogopa wezi hawa nakwambia watavunja nyumba zetu na mwisho watateka hata wake zetu.

Well spoken!!!
 
Sisimizi akiingia katika mkonga wa tembo. Tembo anaweza kujipigiza mpaka akafa. Sasa ndio hapa, sasa kama SMS haikuwa silaha yenye kukera kwanini Rostam apige simu kwa wabunge, viongozi wa vyama na wahariri kulalamika? Si angepuuza tu maana kila siku anaandikwa magazetini kuwa ni fisadi? Au huwa ni kelele za chura? Mafisadi lazima kuwaendea kabisa. Ndio maana mi nimeomba anayepajua kwake anielekeze kupitia ashawazenj@gmail.com au ashabdala@yahoo.com jamani!

Asha
 
Dr Slaa,

Kwanza nianze kwa kukushukuru kwa kuweza kuweka rekodi staight katika kipindi kigumu baada ya msiba mkubwa .

Dokta nilitaka kujua tuu vipi kuhusu ishu muhimu kama EPA, Richmond na Ripoti ya kamati ya madini amabzo kwa kipindi kirefu zimekuwa azizungumziwi , nini haswa msimamo wa chama kuhusu hizi ishu .Na jee mtatumia strategy gani kuhakikisha wale wote waliohusika na wizi huu mkubwa wanafikishwa kwenye mikono ya dola ?
 
This is the longest paragraph I ever seen in my life...

Yaani ukiambiwa useme ulichoona utasema hicho,inanyesha ujapendezwa na objective na sasa unachambua format of writing .

BiG up to Mnyika,SMS nadhani alijua what next he just did wonderful math.
 
Niliwahi kuweka maoni yangu hapa kuhusu RA na spins zake kuwa zinaweza kuhatarisha amani kama kule Rwanda. Kuna baadhi ya memba hapa wakasema kuwa mie ndo ninachochea ghasia. Wa kwanza kumlaumu ni JK ambaye ni rafiki wa RA, yeye kanyamaza tu anaona madudu anayofanya huyu Muajemi. Alianzia kanisani na sasa anaingia kwenye jamii moja kwa tisa. Amani ikitoweka yeye atakimbilia huko kwa Iran huku wananchi wetu wakitoana roho.

Haya ni madogo, nyie subirini maombolezo yaishe na jimbo litangazwe tayari kwa kampeni ya uchaguzi mdogo. Nyie mtasikia tu, kuna mtu/watu watatoana roho kama vyombo hivi vya habari vitaendelea kupotosha ukweli.
Tarime, Serengeti hawa jamaa hawaogopi mtu wala serikali. Mie niliwahi kuishi huko zaidi ya miaka 5, nawaelewa hawa jamaa. Wanasimama kidete pale wakiamini wako sahihi, SISIEMU, ROSTAM, BALILE, TBC, CHADEMA na wengineo mtapeleka spins zenu lakini kama wenyewe wakiamua kuwa wanataka kitu fulani na ndivyo itakuwa. Hivyo ni vyema Rostam na vyombo vyake kutumia busara kuandika ukweli kuhusu jimbo la Tarime na si vinginevyo.

BALILE: Huyu mtu naye ni wa kuogopa kama Ukoma. Awe makini na kazi pamoja na taaluma yake. Kama anafikiri ni busara kupata kitoweo chake kwa bei ya WATANZANIA, adhabu kali inaweza kumshukia kichwani kwake. Balile ni moja ya matatizo katika viungo vya AMANI nchini. Na kama kiungo mojawapo kinaleta shida mwili hata Biblia inasema ukiondoe. Sasa kuna njia nyingi tu za kukiondoa........fungua kesi za uchochezi, fungua kesi kwa ukiukwaji wa maadili n.k

TANZANIA INA WENYEWE, HATUWEZI KUBALI KUENDESHWA NA FISADI KWA PESA YETU ALIYOIBA. THE TIME FOR PATIENCE IS RUNNING OUT.
 
Why atakufa kisiasa, weka analyisis zako hapa!! please conclusion imekuwa cheap sana


Anaongozwa na jazba
Sukwa saidi Sukwa yupo wapi
Hivi ndiye huyu waliyedai CCM wantaka kumnunua kwa kigezo Gani au kuropoka
 

Anaongozwa na jazba
Sukwa saidi Sukwa yupo wapi
Hivi ndiye huyu waliyedai CCM wantaka kumnunua kwa kigezo Gani au kuropoka

Bei yake ni kubwa ccm hawaiwezi. Si mropokaji ni msema ukweli. Sukwa kilichomuua ni kile kile kitaua wote wanaogombea uenyekiti UVCCM huku wakipigia kelele ufisadi. Wanapiga kelele za kioga na hawawezi kum point fisadi kwa kidole chao hata kimoja. Nakwambia hata mmoja hatateuliwa (Mark you sio hatachaguliwa, bali hatateuliwa. You got what I mean?) na kama hiyo ndiyo unayombezea nayo Sukwa. To hell with your party na pesa za ufisadi. I better stay poor than killing my fellow Tanzanian with poverty.
 
Dr Slaa,

Kwanza nianze kwa kukushukuru kwa kuweza kuweka rekodi staight katika kipindi kigumu baada ya msiba mkubwa .

Dokta nilitaka kujua tuu vipi kuhusu ishu muhimu kama EPA, Richmond na Ripoti ya kamati ya madini amabzo kwa kipindi kirefu zimekuwa azizungumziwi , nini haswa msimamo wa chama kuhusu hizi ishu .Na jee mtatumia strategy gani kuhakikisha wale wote waliohusika na wizi huu mkubwa wanafikishwa kwenye mikono ya dola ?
Naomba kwa leo nisijibu hoja kuhusu EPA. Richomond na kadhalika japo unajua sina tatizo kutoa msimamo wangu. Ninaomba tu msiba huu mgumu kwetu uishe, tukirudisha bendera zetu kwenye hali ya kawaida nitakuwa tayari kujibu hoja zingine zote. Nimekuwa kwa leo natoa pale ninapoona pana hitaji kuweka rekodi sahihi. Nimegundua kuachia upotoshaji kwa muda mrefu kuna gharama kubwa sana, kwetu sisi binafsi, kwa chama na kwa Taifa pia. Ni msingi huo tu umenisukuma kutoa mawazo yangu katika maeneo haya machache.
 
Now wait a minute, Mnyika tuwekee namba ya Rostam kwenye PM zetu, ili wale wenye ubavu na uchungu na taifa letu tumtumie more SMS zaidi,

Enough is enough, kama haelewi huo ujumbe wa Mnyika, basi tupe namba yake tumtumie SMSs zaidi, kitendo ulichokifanya ni kikubwa sana kuliko hata kumfikisha mahakamani, haya sasa atuuuwe wote na ajali kama anaweza!

Yes I said it! tumechoka sasa!
 
Naomba kwa leo nisijibu hoja kuhusu EPA. Richomond na kadhalika japo unajua sina tatizo kutoa msimamo wangu. Ninaomba tu msiba huu mgumu kwetu uishe, tukirudisha bendera zetu kwenye hali ya kawaida nitakuwa tayari kujibu hoja zingine zote. Nimekuwa kwa leo natoa pale ninapoona pana hitaji kuweka rekodi sahihi. Nimegundua kuachia upotoshaji kwa muda mrefu kuna gharama kubwa sana, kwetu sisi binafsi, kwa chama na kwa Taifa pia. Ni msingi huo tu umenisukuma kutoa mawazo yangu katika maeneo haya machache.
 
Wewe JMushi mbona unaongea mambo ya ajabu sana!You too fast but not smart ,maneno yako yanaonyesha ww ndiye mbaguzi uliyetukuka.Kama babu yako ni Sina basi inabidi ujue historia yake,kama hujui go back to history books.
Sasa unasema kama "Chadema wanataka ushirikiano wa wachaga wote "huoni kwamba ww huangalii unachoongea na ww ndio racist uliyejikita.
 
Pamoja na kuwa sikuwa na nia ya kuchangia katika hatua hii kwa sababu zinazoeleweka, lakini nadhani lazima nimpongeze Dogo Mnyika kama ilivyoitwa. Tofauti na aliyedhani ndiyo mwisho wake kisiasa, nadhani wakati wa siasa za maficho sasa umepitwa na wakati. Ufisadi hauna dawa nyingine isipokuwa kupigwa vita wazi. Wenye uwoga ni wale wasiojiamini. Yaliyoandikwa na Magazeti yaliyotajwa hayahitaji lugha nyingine isipokuwa kukemewa na wale wote wenye kupenda ukweli katika nchi hii. Nilikuwepo mimi kama mhusika mmojawapo, nilivyopokelewa na nilivyoagwa ni ishara tosha kuwa vyombo vilivvyoandika yaliyoandikwa yalikuwa na agenda tofauti kabisa na msiba uliotupeleka Tarime. Cha kutisha zaidi ni TBC1 chombo cha Taifa, kinachoendeshwa kwa kodi ya Watanzania wa makabila yote, itikadi zote inapoanza kuchukua sura ya uchochezi badala ya kujenga umoja wa kitaifa, na hasa kuwa na 'deliberate biased reporting'. Ningependa kuichallange TBC ilipatwa na kigugumizi gani baada ya mbinu yake kukwama? Sasa ndiyo ninaanza kutambua kwanini hotuba yangu siku ya TAMISEMI/Waziri Mkuu haikutangazwa. Sote tu watu wazima, wasomi wa kutosha hata kama hatujui sana IT kwa maana ya ufundi wa kurusha habari. TBC1 lazima ije clear katika hili. Hii haina maana ya kwamba naingilia hatua ya Jukwaa la Wahariri. Lakini kwa ujumbe Jukwaa lifahamu kuwa wadau tupo, na tunamaoni ya kutoa iwapo watahitaji katika jitihada za kutafuta ukweli. Naomba radhi kulazimishwa kutoa 'comment yangu' wakati tuko bado kwenye maombolezo. Maslahi ya Taifa yanahitaji ukweli bila kuchelewa, na ikilazimu vitabu vitakatifu vinajieleza vya kutosha kuhusu hatua yangu hii.

Mheshimiwa Dr. Slaa,

Mimi natofautiana na wewe kabisa juu ya hili. Mwanasiasa makini haendeshi siasa kwa vijembe, anaendesha kwa hoja.

Alichofanya Mnyika ni tofauti sana na kile ambacho nyie mlifanya katika mkutano wenu mlipowataja mafisadi wale 11 (kama sijakosea namba).

Mlijenga hoja juu ya kwanini hao watu 11 ni mafisadi. Mlikuwa mnaelemisha umma juu ya mafisadi wa Tanzania.

Kutuma sms ya kumwita mtu fisadi lengo ni kutukana na wala sio kuelemisha jamii kwa hoja. Mwanasiasa yoyote makini hawezi kufanya kitu kama hicho. Nina uhakika hata Dr. Slaa pamoja na ujasiri wako hata siku moja huwezi kufanya kitu kama hicho.

Mnyika anaweza kufurahisha wapenzi wa CHADEMA lakini nina wasiwasi kama hicho kitendo kitamwongezea kura za watu wenye mawazo huru na wale ambao wako katikati na wanatafuta kwa kuhamia.

Sina tone la penzi kwa RA lakini hata siku moja siwezi kumwandikia yeye binafsi ujumbe au hata barua ya kumtukana. Naweza kuelemisha jamii kwamba RA ni fisadi au naweza kwenda mahakamani kumshitaki kwa ufisadi lakini sio kumwandikia sms yeye binafsi. Hoja za matusi zinaongozana na hoja za manguvu.
 
Hivi RA alipokwenda kumtongoza ajiunge na CCM unafahamu walikuwa wana uhusianio wa namna gani? Mnyika amesema aende mahakamani, sasa nani analalamika?
 
Now wait a minute, Mnyika tuwekee namba ya Rostam kwenye PM zetu, ili wale wenye ubavu na uchungu na taifa letu tumtumie more SMS zaidi,

Enough is enough, kama haelewi huo ujumbe wa Mnyika, basi tupe namba yake tumtumie SMSs zaidi, kitendo ulichokifanya ni kikubwa sana kuliko hata kumfikisha mahakamani, haya sasa atuuuwe wote na ajali kama anaweza!

Yes I said it! tumechoka sasa!

Sawa kabisa mkuu
Sioni ubaya wa kutumia sms,kwani ni sawa tu na kutumia petition katika kumfikishia mtu ujumbe.Mnyika alitaka huyu mtu ujumbe umguse zaidi na kumwonyesha kwamba hamwogopi,kwani labda RA kelele za magazeti ziko too general hivyo hazimuumizi sana.Sasa wote tukimtumia sms zijae kwenye inbox yake lazima itakuwa na effect fulani kwake hata psychologically tu.
 
nadhani wachangiaji wengi hapa jf, hamjui impact ya propaganda za rostam aziz kuhusu kifo cha wangwe na athari zake kwa taifa hili, muda mfupi tu tangu kuandikwa habari ya kuwa wangwe kauuwa, tayari kulkuwa na tension kali sana katika miji ya tarime na moshi, mjini moshi ambako nilikuwa wakurya walikuwa na wasiwasi sana, kama wachaga walioko tarime wangeshambuliwa, nasikia maduka ya wachaga tarime yalifungwa siku nzima. wakati huo rostam azizi alikuwa yuko bize akichochea vita, na hali anayo ticket ya ndege ya kukimbilia ughaibuni, na mamilioni ya dola ya kula mpaka afe, yale aliyioiba pale benki kuu

kuna lugha gani ya kuongean na hayawani, punguani, zandiki, nduli, mpuuzi, fala, mnafiki, kama huyu? nisiikosee bure jf kwani ningemkuta ningemzaba kibao na tusi kama.....


Naomba ma Mods muiangalie hii lugha
 
Back
Top Bottom