Paparazi Muwazi
JF-Expert Member
- Dec 23, 2007
- 310
- 79
Dogo Mnyika uso kwa uso na Balille+Rostam Aziz
Katika hali inayoashiria kwamba sasa mambo yaliyonyuma ya pazia yanaanza kujitokeza hadharani. Dogo Mnyika ameanza kugongana vichwa na Ballile+Rostam Aziz. Katika kikao cha Jukwaa la Wahariri za jana, baada ya Sakina Datoo kueleza wazi wazi jinsi habari za magazeti matano zilivyofanana na Zitto kueleza jinsi gani habari hizo zilivyokuwa si za kweli. Mhariri wa gazeti la RAI hakuweza kukanusha hali hiyo badala yake alipopata muda kueleza hali hiyo, akasema kwamba wa kulaumiwa kutokana na kuliingiza taifa katika hali hiyo ni John Mnyika ambaye kauli zake ndizo zilizoliingiza taifa kwenye matatizo.
Bwana Ballile alitumia muda wote kumshambulia Bwana Mnyika. Ndipo Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Sakina Datoo, alipompa nafasi Bwana Mnyika naye kuweza kufafanua hali hiyo. Katika majibu yake kwa Ballile, Bwana Mnyika alitangaza wazi kuwa gazeti la RAI ndilo lililopotosha na kuudanganya umma, na kuliingiza taifa kwenye hisia tofauti kuhusu Kifo cha Chacha Wangwe. Bwana Mnyika akarejea taarifa za gazeti la RAI la alhamisi ya 31 Julai, 2008 lililokuwa na Kichwa cha Habari Wangwe kauwawa kuwa ndilo lilochochea hisia miongoni mwa wananchi kuhusu mauji na hatimaye yakatokea yaliyotokea Tarime siku hiyo na baadaye magezeti ya Ijumaa 1 Agosti, 2008 nayo yakabeba habari zisizo za kweli kuhusu Mbowe kukaribia kukatwa na mapanga na kuhusisha kifo hicho na Risasi. Bwana Mnyika alieleza wazi kwamba habari hiyo ukusara wa Mbele ambayo ilikuwa na by line inayosema Wataka Polisi iwabane Mnyika na Mallya, ililenga kujenga hisia za wasomaji kumhusisha yeye na kifo cha Wangwe.
Bwana Mnyika alielezea kwamba siku ya pili baada ya habari hiyo kutoka waandishi wa habari walifika kutaka msimamo wake kuhusu habari hiyo lakini alikataa kusema chochote kwa kuwa hiki ni kipindi cha maombolezo badala ya malumbano. Leo naomba niwaambie wahariri, kwamba naendelea kutafakari kuhusu habari hiyo, na pindi kipindi cha maombolezo kitakapokwisha, nitawaita waandishi kueleza hatua nitakazochukua kuhusiana na gazeti hilo, alisema Bwana Mnyika. Akiichambua habari hiyo, Bwana Mnyika amesema pamoja na kichwa cha habari kutaka polisi wamhoji, ndani ya habari yenyewe hakuna mahali popote ambapo chanzo chochote kimesema ahojiwe na polisi.
Akichambua aya ya kwanza na ya pili ya habari, ambayo inaeleza kwamba msimamo wa wazawa wa Tarime kuwa chacha ameuwawa umechochewa na kauli yake, Bwana Mnyika akamhoji Balille mbona habari yenyewe haitaji kauli ya Bwana Mnyika inayolalamikiwa na wazawa hao wala katika habari yenyewe hailezwi popote wazawa hao kuhusisha kauli zao na msimamo wa Bwana Mnyika. Akichambua aya za mwishoni mwa Habari hiyo, ambayo inataja kwamba msimamo wa Dr Slaa ulikuwa ni kutaka uchunguzi ufanyike wakati Bwana Mnyika alitoa taarifa kwamba vyombo vya habari kuwa kifo hicho hakitokani na mgogoro ndani ya CHADEMA.
Chini ya maneno ya habari hiyo, gazeti la RAI likaweka maswali yafuatayo: Kwanini Mnyika akimbie kutoa kauli hii? Je, Mnyika ni polisi kutangaza mazingira ya kifo cha Wangwe?Je, Mnyika alikuwepo eneo la tukio?, Je, Ni kinga ipi anayotaka kuweka Mnyika? Kutokana na Habari hiyo kuwa na maswali hayo, Bwana Mnyika aliweka bayana kwa Ballile kwamba maswali hayo yaliongezwa na RAI ili kujenga hisia kwa msomoji kwamba yeye anahusika na kifo cha Wangwe. Akichambua mapungufu ya hoja hiyo. Alisema, anasikitika kwamba katika kipindi chote cha msiba mpaka Ballile anaibua hoja hiyo katika Jukwaa la Wahariri, gazeti la RAI halijawahi kufanya mahojiano yoyote na yeye wakati wowote.
Mnyika akaendelea kuelezea kwamba wao kama CHADEMA wanafanya kazi kama timu, na pindi habari za msiba walipozipata usiku walipeana taarifa kamili. Na hata asubuhi waliendelea kupeana taarifa mbalimbali ili kutoa misimamo bila kukinzana. Akasema kwamba siku hiyo ya Jumanne 29 Julai 2008, waandishi wa habari walimfuata ofisini kuuliza jinsi CHADEMA ilivyopokea msiba huo mzito. Alieleza bayana kwamba waandishi wengi walifika baada ya kikao cha sekretariati ya chama hicho ambayo yeye kama kaimu katibu mkuu, alikuwa Mwenyekiti wa Kikao. Anasema akawaeleza waandishi hao jinsi ambayo wamekipokea kifo hicho kwa mshtuko na masikitiko makubwa na kwamba wataendelea kumkumbuka Chacha kama kiongozi jasiri aliyesimamia yale aliyoyaamini.
Anasema mara baada ya kuhitimisha kutoa kauli hiyo ya chama ya jinsi ambavyo chama kimepokea msiba huo, waandishi wa Mwandishi wa Habari wa Mtanzania, na wa TBC1 waliuliza maswali, wakati yule wa Mtanzania akiuliza swali kwamba habari za mitaani zinasema kwamba CHADEMA ndio imemuua Chacha nini kauli ya chama kuhusu suala hilo? Yule wa TBC1 aliuliza kama kifo hicho hakitokani na mgogoro ndani ya CHADEMA? Bwana Mnyika alisema kwamba CHADEMA haihusiki na kifo hicho wala hakihusiani na mgogoro ndani ya chama hicho, na kwamba taarifa za awali walizozipokea toka kwa Kamanda wa Polisi ni kwamba kifo hicho kimetokana na ajali.
Bwana Mnyika alisema kwamba alilisitiza kuwa watu wasianze kuitizama CHADEMA badala yake vyombo vya usalama ndio vinawajibu wa kutoa taarifa kamili. Katika jukwaa la Wahariri, Bwana Mnyika aliweka bayana kwamba huu ndio uliokuwa msimamo wa pamoja, na ni msimamo huo huo ulitolewa na viongozi wengine wa CHADEMA siku hiyo akiwemo Dr Slaa, na hata viongozi wa kiserikali akiwemo Spika wa Bunge na Rais wa nchi katika salamu zao. Bwana Mnyika akamhoji Balille kwamba ni vipi kati ya watu wote walionukuu taarifa ya polisi kuwa kifo hicho kimetokana na ajali hawakuandikwa na RAI kwamba wamekurupuka kujikinga na kutaka wahojiwe na polisi kama alivyoandikwa yeye na gazeti hilo? Bwana Mnyika akaendelea kusema kwamba kinachoshangaza zaidi ni kuwa Jumatano ya tarehe 30 Julai, 2008 yeye mwenyewe alimwandikia Barua IGP kutaka uchunguzi wa utata wa mazingira ya ajali uliotokana na kauli tofauti tofauti ambazo zilitolewa na Deus Mallya ukilinganisha na watoto wa marehemu kuhusiana na ajali hiyo.
Wakati vyombo mbalimbali vya habari viliinukuu barua hiyo, ikiwemo gazeti dada la Mtanzania, Gazeti la RAI halikutumia kabisa habari hiyo. Bwana Mnyika akahitimisha kwa kumwambia Balille hadharani kwamba kwa mwelekeo wa Habari hiyo umeonyesha wazi kwamba aliyekuwa analengwa kuchafuliwa ni Mnyika na kwamba habari hiyo imekiuka misingi ya maadili ya uandishi wa habari na hivyo akaeleza wazi wazi kwamba anatarajia kuchukua hatua juu ya gazeti hilo. Hapa si mahali pake kuzungumzia hilo, bado tuko kwenye maombolezo, na hapa tulikuja kukutana na Jukwaa la Wahaririri. Pindi wakati ukifika nitawaita waandishi wa habari na kuwaeleza hatua nitazochukua, alisema Mnyika.
Wakati huo huo, mmiliki wa Kampuni ya Habari Corporation yenye gazeti la RAI, Bwana Rostam Aziz amelalamika kwa baadhi ya wabunge, baadhi ya viongozi wa vyama vyama vya siasa na na baadhi ya wahariri kwamba Mnyika amemtukana kupitia simu yake ya mkononi. Hata hivyo alipotakiwa kueleza ametukanwa matusi gani, bwana Rostam hakuwa tayari kueleza. Kwa upande wake Bwana Mnyika alipoulizwa amekana kumtukana Bwana Rostam na kutaka aulizwe na atoe ushahidi ametukanwa nini. Mimi nimemwambia kuwa nimesibitisha kuwe yeye ni fisadi. Sasa kama anasema mimi kumuita fisadi ni matusi basi aende mahakamani.
Na nimemwambia wazi wazi , sikutaka kuzunguka, nimemwandikia kwenye SMS kuwa yeye ni fisadi. Na sijajificha kwa kweli. Nimewandikia kwa namba yangu na nimeandika jina langu ili abaki na ushahidi akipenda aende mahakamani. Wadadisi wa mambo, wanasema kwamba uamuzi huu wa Bwana Mnyika unaweza kuzua mivutano kati yake na Ballille+Rostam. Itakumbukwa kwamba mara baada ya uchaguzi mkuu 2005, wakati Makamba anafanya jitihada za kumnunua Mnyika kwenda CCM alimtumia Bwana Rostam Aziz. Hata hivyo, Bwana Mnyika alikataa kata kata akieleza kwamba yeye hana bei(price less).
Suala hili la CCM kutaka kumnunua Mnyika liliwahi kuwekwa hadharani na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe. Kwa mujibu wa vyanzo vilivyo karibu na Bwana Balille, mara baada ya kikao hicho cha Jukwaa la Wahariri, Bwana Balille alimjulisha Rostam mambo yote na umuhimu wa kuandaa mbinu ya kumkabili Bwana Mnyika katika suala hilo. Kwa mujibu wa chanzo hicho, imekuwabaliwa kwamba kikao kitafanyika ikiwemo kupanga mbinu ya kukabiliana na Zitto Kabwe kutokana na uamuzi wake wa kukabiliana na wahariri wa vyombo vya habari kutokana na kuruhusu habari ya uongo ya kupikwa kuweza kutolewa na vyombo vyao. Katika mkakati huo, imeelezwa kuwa kiongozi mmoja wa upinzani aliyekwenda mazikoni Tarime atashirikishwa.
PM
Kwa maoni yangu huu ndio mwanzo wa kifo cha kisiasa cha Bwana Mnyika
Katika hali inayoashiria kwamba sasa mambo yaliyonyuma ya pazia yanaanza kujitokeza hadharani. Dogo Mnyika ameanza kugongana vichwa na Ballile+Rostam Aziz. Katika kikao cha Jukwaa la Wahariri za jana, baada ya Sakina Datoo kueleza wazi wazi jinsi habari za magazeti matano zilivyofanana na Zitto kueleza jinsi gani habari hizo zilivyokuwa si za kweli. Mhariri wa gazeti la RAI hakuweza kukanusha hali hiyo badala yake alipopata muda kueleza hali hiyo, akasema kwamba wa kulaumiwa kutokana na kuliingiza taifa katika hali hiyo ni John Mnyika ambaye kauli zake ndizo zilizoliingiza taifa kwenye matatizo.
Bwana Ballile alitumia muda wote kumshambulia Bwana Mnyika. Ndipo Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Sakina Datoo, alipompa nafasi Bwana Mnyika naye kuweza kufafanua hali hiyo. Katika majibu yake kwa Ballile, Bwana Mnyika alitangaza wazi kuwa gazeti la RAI ndilo lililopotosha na kuudanganya umma, na kuliingiza taifa kwenye hisia tofauti kuhusu Kifo cha Chacha Wangwe. Bwana Mnyika akarejea taarifa za gazeti la RAI la alhamisi ya 31 Julai, 2008 lililokuwa na Kichwa cha Habari Wangwe kauwawa kuwa ndilo lilochochea hisia miongoni mwa wananchi kuhusu mauji na hatimaye yakatokea yaliyotokea Tarime siku hiyo na baadaye magezeti ya Ijumaa 1 Agosti, 2008 nayo yakabeba habari zisizo za kweli kuhusu Mbowe kukaribia kukatwa na mapanga na kuhusisha kifo hicho na Risasi. Bwana Mnyika alieleza wazi kwamba habari hiyo ukusara wa Mbele ambayo ilikuwa na by line inayosema Wataka Polisi iwabane Mnyika na Mallya, ililenga kujenga hisia za wasomaji kumhusisha yeye na kifo cha Wangwe.
Bwana Mnyika alielezea kwamba siku ya pili baada ya habari hiyo kutoka waandishi wa habari walifika kutaka msimamo wake kuhusu habari hiyo lakini alikataa kusema chochote kwa kuwa hiki ni kipindi cha maombolezo badala ya malumbano. Leo naomba niwaambie wahariri, kwamba naendelea kutafakari kuhusu habari hiyo, na pindi kipindi cha maombolezo kitakapokwisha, nitawaita waandishi kueleza hatua nitakazochukua kuhusiana na gazeti hilo, alisema Bwana Mnyika. Akiichambua habari hiyo, Bwana Mnyika amesema pamoja na kichwa cha habari kutaka polisi wamhoji, ndani ya habari yenyewe hakuna mahali popote ambapo chanzo chochote kimesema ahojiwe na polisi.
Akichambua aya ya kwanza na ya pili ya habari, ambayo inaeleza kwamba msimamo wa wazawa wa Tarime kuwa chacha ameuwawa umechochewa na kauli yake, Bwana Mnyika akamhoji Balille mbona habari yenyewe haitaji kauli ya Bwana Mnyika inayolalamikiwa na wazawa hao wala katika habari yenyewe hailezwi popote wazawa hao kuhusisha kauli zao na msimamo wa Bwana Mnyika. Akichambua aya za mwishoni mwa Habari hiyo, ambayo inataja kwamba msimamo wa Dr Slaa ulikuwa ni kutaka uchunguzi ufanyike wakati Bwana Mnyika alitoa taarifa kwamba vyombo vya habari kuwa kifo hicho hakitokani na mgogoro ndani ya CHADEMA.
Chini ya maneno ya habari hiyo, gazeti la RAI likaweka maswali yafuatayo: Kwanini Mnyika akimbie kutoa kauli hii? Je, Mnyika ni polisi kutangaza mazingira ya kifo cha Wangwe?Je, Mnyika alikuwepo eneo la tukio?, Je, Ni kinga ipi anayotaka kuweka Mnyika? Kutokana na Habari hiyo kuwa na maswali hayo, Bwana Mnyika aliweka bayana kwa Ballile kwamba maswali hayo yaliongezwa na RAI ili kujenga hisia kwa msomoji kwamba yeye anahusika na kifo cha Wangwe. Akichambua mapungufu ya hoja hiyo. Alisema, anasikitika kwamba katika kipindi chote cha msiba mpaka Ballile anaibua hoja hiyo katika Jukwaa la Wahariri, gazeti la RAI halijawahi kufanya mahojiano yoyote na yeye wakati wowote.
Mnyika akaendelea kuelezea kwamba wao kama CHADEMA wanafanya kazi kama timu, na pindi habari za msiba walipozipata usiku walipeana taarifa kamili. Na hata asubuhi waliendelea kupeana taarifa mbalimbali ili kutoa misimamo bila kukinzana. Akasema kwamba siku hiyo ya Jumanne 29 Julai 2008, waandishi wa habari walimfuata ofisini kuuliza jinsi CHADEMA ilivyopokea msiba huo mzito. Alieleza bayana kwamba waandishi wengi walifika baada ya kikao cha sekretariati ya chama hicho ambayo yeye kama kaimu katibu mkuu, alikuwa Mwenyekiti wa Kikao. Anasema akawaeleza waandishi hao jinsi ambayo wamekipokea kifo hicho kwa mshtuko na masikitiko makubwa na kwamba wataendelea kumkumbuka Chacha kama kiongozi jasiri aliyesimamia yale aliyoyaamini.
Anasema mara baada ya kuhitimisha kutoa kauli hiyo ya chama ya jinsi ambavyo chama kimepokea msiba huo, waandishi wa Mwandishi wa Habari wa Mtanzania, na wa TBC1 waliuliza maswali, wakati yule wa Mtanzania akiuliza swali kwamba habari za mitaani zinasema kwamba CHADEMA ndio imemuua Chacha nini kauli ya chama kuhusu suala hilo? Yule wa TBC1 aliuliza kama kifo hicho hakitokani na mgogoro ndani ya CHADEMA? Bwana Mnyika alisema kwamba CHADEMA haihusiki na kifo hicho wala hakihusiani na mgogoro ndani ya chama hicho, na kwamba taarifa za awali walizozipokea toka kwa Kamanda wa Polisi ni kwamba kifo hicho kimetokana na ajali.
Bwana Mnyika alisema kwamba alilisitiza kuwa watu wasianze kuitizama CHADEMA badala yake vyombo vya usalama ndio vinawajibu wa kutoa taarifa kamili. Katika jukwaa la Wahariri, Bwana Mnyika aliweka bayana kwamba huu ndio uliokuwa msimamo wa pamoja, na ni msimamo huo huo ulitolewa na viongozi wengine wa CHADEMA siku hiyo akiwemo Dr Slaa, na hata viongozi wa kiserikali akiwemo Spika wa Bunge na Rais wa nchi katika salamu zao. Bwana Mnyika akamhoji Balille kwamba ni vipi kati ya watu wote walionukuu taarifa ya polisi kuwa kifo hicho kimetokana na ajali hawakuandikwa na RAI kwamba wamekurupuka kujikinga na kutaka wahojiwe na polisi kama alivyoandikwa yeye na gazeti hilo? Bwana Mnyika akaendelea kusema kwamba kinachoshangaza zaidi ni kuwa Jumatano ya tarehe 30 Julai, 2008 yeye mwenyewe alimwandikia Barua IGP kutaka uchunguzi wa utata wa mazingira ya ajali uliotokana na kauli tofauti tofauti ambazo zilitolewa na Deus Mallya ukilinganisha na watoto wa marehemu kuhusiana na ajali hiyo.
Wakati vyombo mbalimbali vya habari viliinukuu barua hiyo, ikiwemo gazeti dada la Mtanzania, Gazeti la RAI halikutumia kabisa habari hiyo. Bwana Mnyika akahitimisha kwa kumwambia Balille hadharani kwamba kwa mwelekeo wa Habari hiyo umeonyesha wazi kwamba aliyekuwa analengwa kuchafuliwa ni Mnyika na kwamba habari hiyo imekiuka misingi ya maadili ya uandishi wa habari na hivyo akaeleza wazi wazi kwamba anatarajia kuchukua hatua juu ya gazeti hilo. Hapa si mahali pake kuzungumzia hilo, bado tuko kwenye maombolezo, na hapa tulikuja kukutana na Jukwaa la Wahaririri. Pindi wakati ukifika nitawaita waandishi wa habari na kuwaeleza hatua nitazochukua, alisema Mnyika.
Wakati huo huo, mmiliki wa Kampuni ya Habari Corporation yenye gazeti la RAI, Bwana Rostam Aziz amelalamika kwa baadhi ya wabunge, baadhi ya viongozi wa vyama vyama vya siasa na na baadhi ya wahariri kwamba Mnyika amemtukana kupitia simu yake ya mkononi. Hata hivyo alipotakiwa kueleza ametukanwa matusi gani, bwana Rostam hakuwa tayari kueleza. Kwa upande wake Bwana Mnyika alipoulizwa amekana kumtukana Bwana Rostam na kutaka aulizwe na atoe ushahidi ametukanwa nini. Mimi nimemwambia kuwa nimesibitisha kuwe yeye ni fisadi. Sasa kama anasema mimi kumuita fisadi ni matusi basi aende mahakamani.
Na nimemwambia wazi wazi , sikutaka kuzunguka, nimemwandikia kwenye SMS kuwa yeye ni fisadi. Na sijajificha kwa kweli. Nimewandikia kwa namba yangu na nimeandika jina langu ili abaki na ushahidi akipenda aende mahakamani. Wadadisi wa mambo, wanasema kwamba uamuzi huu wa Bwana Mnyika unaweza kuzua mivutano kati yake na Ballille+Rostam. Itakumbukwa kwamba mara baada ya uchaguzi mkuu 2005, wakati Makamba anafanya jitihada za kumnunua Mnyika kwenda CCM alimtumia Bwana Rostam Aziz. Hata hivyo, Bwana Mnyika alikataa kata kata akieleza kwamba yeye hana bei(price less).
Suala hili la CCM kutaka kumnunua Mnyika liliwahi kuwekwa hadharani na Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe. Kwa mujibu wa vyanzo vilivyo karibu na Bwana Balille, mara baada ya kikao hicho cha Jukwaa la Wahariri, Bwana Balille alimjulisha Rostam mambo yote na umuhimu wa kuandaa mbinu ya kumkabili Bwana Mnyika katika suala hilo. Kwa mujibu wa chanzo hicho, imekuwabaliwa kwamba kikao kitafanyika ikiwemo kupanga mbinu ya kukabiliana na Zitto Kabwe kutokana na uamuzi wake wa kukabiliana na wahariri wa vyombo vya habari kutokana na kuruhusu habari ya uongo ya kupikwa kuweza kutolewa na vyombo vyao. Katika mkakati huo, imeelezwa kuwa kiongozi mmoja wa upinzani aliyekwenda mazikoni Tarime atashirikishwa.
PM
Kwa maoni yangu huu ndio mwanzo wa kifo cha kisiasa cha Bwana Mnyika
Last edited by a moderator: