Mniwie radhi nilikosea kusupport ujio mpya wa Paul Makonda, huyu jamaa ni Lopolopo sana hana staha

Wadiz

JF-Expert Member
Nov 10, 2022
5,411
11,061
Makonda Makonda kwanini lakini tumia busara acha Lopolopo, Leo huko Dodoma kaongea utumbo, hivi huyu dogo anaweza kuwatisha wastaafu, bado anakivuli cha enzi za Magufuli et eeh.

Jamaa tulidhani kajifunza hekima na ustaarabu kwa kukaa benchi kumbe ni jitu lenye uchuro tu.

Makonda anaweza kumnyamazisha nani huyu, hana audacity ya kunyoosha kidole kwa wazee, pia anawaita wajumbe wa kamati kuu ya CCM kuwa ni Chura? Wajumbe wa NEC halmashauri kuu kuwa ni Chura?

Makonda ajipange tutapambana nae kwa kadri ya upumbavu wake, CCM ya namna hii ya kuwa na mwenezi bwege na Lopolopo imepitwa na wakati.

Tulikuwepo na tutakuwepo hatuwezi kukubali ujinga kupitia jina CCM hiki chama sio cha wajinga na wanunua vyeti.

Comments free from above and under the surface.

Wadiz
 
Wewe ukimpinga Makonda tutakutaja kwamba unawalipa wanaotukana viongozi mitandaoni
Huyu bwege tutakula nae sahani moja tumekesha kumuombea arudi then analeta kauli za uchuro pumbavu zake, Makonda ni kidagaa tu hana utiisho wowote ule. Ahadi 10 za mwana TANU na sasa CCM ziko wazi kabisa
 
Waambieni babu zenu wakae pembeni kwani nini maana ya kustafuuu.......
Makonda upo sawa mkuu
 
Anachokifanya ndicho haswa alichoteuliwa kukifanya.

Makonda ni mithili ya udongo, unamfinyanga vile unataka awe.

Makonda ni mouthpiece ya waliomteua ili aongee yale wasioweza kuyaongea kwa wanaotakiwa kufikishiwa ujumbe.
 
Huyu bwege tutakula nae sahani moja tumekesha kumuombea arudi then analeta kauli za uchuro pumbavu zake, Makonda ni kidagaa tu hana utiisho wowote ule. Ahadi 10 za mwana TANU na sasa CCM ziko wazi kabisa
Ulikuwa unakesha kumuombea arudi? Hili ni tatizo la watanzania wengi. Tuna akili kama za wanyama. Jambo mpaka limpate ndiyo anaona kasoro na kulalamika. Makonda utahitaji hata dakika kumi kujua kuwa ni kiongozi wa hovyo kupata kutokea?
 
Kampa waziri mkuu miezi 6 atatue matatizo yaliyodumu toka ukoloni hadi leo.

Kweli akili za mjinga hukaa kifuani!!!
 
Jamaa huenda yeye anajua TABIA zake na MATENDO yake ndio yamempa tena cheo leo
 
Makonda ndio kijana shupavu na kidekteta anayeweza kuendesha nchi kwa kutumia mamlaka kamili.

Makonda sio muoga na mnamuanya .
 
Huyu bwege tutakula nae sahani moja tumekesha kumuombea arudi then analeta kauli za uchuro pumbavu zake, Makonda ni kidagaa tu hana utiisho wowote ule.
Wakati mnakesha kwa kumuombea hadi mkafikia kumteua hamkufunuliwa huo uchuro wake?
 
Anachokifanya ndicho haswa alichoteuliwa kukifanya.

Makonda ni mithili ya udongo, unamfinyanga vile unataka awe.

Makonda ni mouthpiece ya waliomteua ili aongee yale wasioweza kuyaongea kwa wanaotakiwa kufikishiwa ujumbe.
Para ya mwisho ndo lengo kuu LA uteuzi wake.
 
Back
Top Bottom