Mnaoagiza magari nje mnapata wapi dola?

Mnaoagiza magari nje mnapata wapi dola?

Tukianza kuruhusu black market haya ndio madhara yake, dawa nikuacha ku regulate exch rate tuache soko liamue maana ni wazi ukiona black market basi juwa soko kiuhalisia haliamini exch rate ni 2550 Tsh lazima ni zaidi. Kwa haraka sana ni wazi exch ilitakiwa kuwa juu ya 2600 Tsh. Maana Bank wanauza kwa mujibu wa BOT hawawezi kuuza zaidi lakini wanajuwa wazi nje iko mpaka 2800, akili ya kawaida tu wakiuza watu watasoma zote na kufanyia biashara kuuza nje.

Dollar iachwe iamuliwe na uhakisia wa soko ni demand and supply, kikubwa tusiruhusu utofauti wa exch banks na nje litapotezea serikali pesa nyingi sana, mtu anakuja na dola 100 atachange nje sio bank tena sababu anapata pesa zaidi.
 
Jiulize mtu kama niffer anayesafiri kila day na kuleta mizigo ya milions anazipataje. Mjini hapa watu wanafanya biashara ya dollar fresh tu
Biashara toka zamani kabla ya matatizo haya sio kila mtu alikuwa ananunua cash dollar, kuna watu unawapa pesa Tanzania tena Tsh wao wanakupa currency ya huko kama uko China ni Yuan na Dubai Dirham. Sababu hata Dubai pesa ya kwanza ya matumizi ni Dirham ukitoa dola mtu anakupigia kama exch rate ya dukani na ziko sehemu zingine wanakwambia nenda ka change ulete Dirham.
 
Unaweza ukapata kwa kukusanya kidogo kidogo hizo usd 100 wanazotoa Nmb mpaka ukafikia kiasi unachotaka. Pia nilichojifunza zinatolewa kwa kujuana au connection maana kuna watu wanazipata kwa kuomba kibali maalum.
Kuna umuhimu wa kufungua account ya USD kama wewe ni mfanyabiashara maana tshs inaporomoka kwa kasi kila kukicha
Hata kama una USD account bado unapewa hizo 100. Mwanzoni kabisa watu walifungua USD wakawa wanaweka tshs then wanachukua USD wanaenda kuuza black market wka 2700-2900 ila baadaye order from BOT ikaja hata USD account ukitaka kutoa unatoa 100 per day.
 
Duh mwaka Jana nakumbuka nimeenda NMB walikuwa wanauza mwisho dollars 3,000 kwa siku.

Sasa hivi imeadimika hadi kufikia kuuza dola 100 tu kwa siku?

Kweli hali ni mbaya.

Nilikuwa nanunua gari sbt japan ya dola 8,000 niliwasiliana nao kuhusu uhaba wa dola wakakubali niwalipe kwa siku tatu kwa kiwango cha dollars 3,000 walichokuwa wanauza NMB mwaka Jana February.

Sasa kwa dola mia mia Sijui utatakiwa Ununue kwa siku ngapi hadi kukamilisha pesa unayonujulia hilo gari.
 
Chukua cash, nenda nayo ofisi unayoagiza gari (mfano BF), wao wana convert wanazo. Sema rate yao mbaya, katika Mil 10 unaweza poteza like Laki 1-2
 
Mbona BE forward wana accept transfer ya Tsh mkuu.
Namshangaa huyu mtu au kaamua kututangazia tu kwamba anataka kununua gari? Online transaction zinahusiana nini na upungufu wa dollar bongo?? Anyways kampuni kubwa zote za magari kama be foward wana ofisi bongo si akalipe cash ofisini asubiri gari??
 
Hakuna hiki kitu, lazima bank wafanye exchange.
Kwani nimekwambia unalipa TZS, nimesema wanae xchange dola to TZS wanaweka na charges zao then wanakata TZS kutoka kwenye akaunti ya TZS kiasi sawa na dola, we have done that mara kibao tu. Sema now kuna wapuuzi wanatesa wenzao kwa manufaa yao, Hata ukiwa na akaunti ya dola bank bado wanakwambia huwezi kufanya miamala mikubwa dola hamna, which is bullshit. Mtu una dola 40,000+ unataka lipia dola 13000 nje unaambiwa haiwezekani dola hamna.
 
Wakuu habari zenu.

Naomba kuuliza kwa wajuzi wa mambo hasa kwenye kufanya malipo kwenda nje ya nchi. Leo nimeshindwa kulipia gari Japan sababu kubwa ni dollar, niliienda NMB wakasema mwisho kuchange ni $100.

Nimeshindwa kuelewa, ina maana hata kama Pesa ipo kwa account yangu inakuwa ngumu kufanya payment? Hata kuexchange pesa juu kwa juu inakuwa shida?

Nilikuwa najua kupata noti ya dollar ndo kipengele, hata kwa Pesa iliyo kwa account kubadili kuwa dollar nayo ni kipengele???.

Nataka kulipia gari Japan, naombeni msaada bank ambayo haina MBAMBAMBA.
Kama una acc ya dola crdb chukua invoice inayoonesha kiasi cha dola unachohitaji kununua hiyo bidhaa then nenda nayo crdb. Hata kama unataka dola 3000 wanakupa ikiwa tu una acc ya usd kwao na hayo malipo utayafanya kupitia hiyo account.

NB: Haya ni maneno niliyoambiwa na mfanyakazi wa crdb.
 
Wakuu habari zenu.

Naomba kuuliza kwa wajuzi wa mambo hasa kwenye kufanya malipo kwenda nje ya nchi. Leo nimeshindwa kulipia gari Japan sababu kubwa ni dollar, niliienda NMB wakasema mwisho kuchange ni $100.

Nimeshindwa kuelewa, ina maana hata kama Pesa ipo kwa account yangu inakuwa ngumu kufanya payment? Hata kuexchange pesa juu kwa juu inakuwa shida?

Nilikuwa najua kupata noti ya dollar ndo kipengele, hata kwa Pesa iliyo kwa account kubadili kuwa dollar nayo ni kipengele???.

Nataka kulipia gari Japan, naombeni msaada bank ambayo haina MBAMBAMBA.
wakikujibu niite
 
Back
Top Bottom