Arushaone si nilikwambia mimi ukatoa povu?? Haya sasa kazi kwako
mwenzetu ulikuwa unaijua? sisi shuleni kwetu hata mwalimu wa english alikuwa haipendi maana ngumu........ mi nikahamia kwenye hesabuEnglish...................
Sio nilikua sipendi mkuu,bali walimu wa enzi hizo walikua wababe mno!!Filipo kwanini tena ulikuwa hupendi kiingilishi??
platozoom unakumbuka enzi hzo pale sabasaba shule ya msingi tulikuwa tunakalia mawe na vipande vya magogo? unakuta mtu anapanga mawe kama mafiga matatu afu anaweka jiwe bapa juu yake. weee ole wako ukakie!
platozoom unakumbuka enzi hzo pale sabasaba shule ya msingi tulikuwa tunakalia mawe na vipande vya magogo? unakuta mtu anapanga mawe kama mafiga matatu afu anaweka jiwe bapa juu yake. weee ole wako ukakie!
Acha tuu..ilikuwa balaa.......ila tulikuwa tunaona poa tu, nakumbuka kama huna dawati subiri msimu wa mtihani wenyewe watakukaribisha!!.......akina...........(wababe fulani). Kumbe na wewe ulikalia mawe..........nilifikiri utazuga ulisoma saint academy lol!
We Arushaone muongo wewe ulikuwa darasa moja na Mzee Mwanakijiji??? Mmmhhh haya bana
Haya na wewe nipe question tag kwa hii kitu: John also applied for a job
Unakumbuka question tags?? passive & active voice?? Ilikuwa vichomi darasani kwetu, sitasahau.
Umenikumbusha Question Tags. Mwanzoni Q/Tags ilikuwa issue;mwanafunzi mmoja alishawahi toa hii:
'You took my pen, tookn't you?
patience96 umenifanya nicheke asubuhi asubuhi!
you have made my day, made'nt you?
Kwa wale tuliosoma zamani ilikuwa raha sana.......angalia mwenyewe
Jogoo na Pazi
Sizitaki mbichi hizi ha ha ha sungura mjanja sana
Hiki kitabu bado kipo kweli........................