BICHWA KOMWE -
JF-Expert Member
- Jul 21, 2022
- 4,690
- 10,194
Japo madaktari wote ni makasuku wanaomeza madesa ya shule na kuyakariri jinsi yalivyo, lakini mnyonge mnyongeni, nchi hii walikuwepo madaktari bwana!
Kuna madaktari ukiwaambia naumwa kichwa anakimbilia kukudunga chanjo ya FANSIDA, sijui ni kukariri ama ndivyo walivyofundishwa huko mashuleni?
Mimi mzee wangu alikuwa daktari, tena daktari nguli aliyeheshimika haswa kutokana na huduma zake. Hawa ni wale madaktari wa zamani ambao akikuhudumia unasema kweli hapa nimehudumiwa na DOKTA HASWA!
Madaktari wa enzi hizo ukiwafuata hadi unahisi raha kuhudumiwa. Utakaguliwa, utabonyezwa bonyezwa vimashavu vyako, unaachama mdomo unamulikwa koromelo na kitochi, yaani hadi raha!!!
Baadaye unawekewa la kupimia moyo, huku daktari anakuhoji kitaalamu na kwa ufanisi.
Lakini siku hizi kumezuka wimbi la MACHEKIBOBU wanaojiita madaktari. Hawawezi kukuhudumia wana mapepe na mawenge muda wote.
Unashtukia daktari amerukia kipima moyo, mara amekitupa mezani, anakurupuka nduki anawahi kuchungulia meseji ya Instagram. Akikuhurumia sana anakudunga chanjo la KOVIDI.
Akikuhoji wala hakuangalii usoni, kaweka EARPHONES anasikiliza singeli ati! Ni mwendo wa Unasemaaaa!!!??? Eeeeh, unasemajeee!!??? Eeeeeeeh?? sijasikia umesemaaa??? Eeeh nasemajeeee!
MY TAKE: Hili nalo mkalitizame.
Kuna madaktari ukiwaambia naumwa kichwa anakimbilia kukudunga chanjo ya FANSIDA, sijui ni kukariri ama ndivyo walivyofundishwa huko mashuleni?
Mimi mzee wangu alikuwa daktari, tena daktari nguli aliyeheshimika haswa kutokana na huduma zake. Hawa ni wale madaktari wa zamani ambao akikuhudumia unasema kweli hapa nimehudumiwa na DOKTA HASWA!
Madaktari wa enzi hizo ukiwafuata hadi unahisi raha kuhudumiwa. Utakaguliwa, utabonyezwa bonyezwa vimashavu vyako, unaachama mdomo unamulikwa koromelo na kitochi, yaani hadi raha!!!
Baadaye unawekewa la kupimia moyo, huku daktari anakuhoji kitaalamu na kwa ufanisi.
Lakini siku hizi kumezuka wimbi la MACHEKIBOBU wanaojiita madaktari. Hawawezi kukuhudumia wana mapepe na mawenge muda wote.
Unashtukia daktari amerukia kipima moyo, mara amekitupa mezani, anakurupuka nduki anawahi kuchungulia meseji ya Instagram. Akikuhurumia sana anakudunga chanjo la KOVIDI.
Akikuhoji wala hakuangalii usoni, kaweka EARPHONES anasikiliza singeli ati! Ni mwendo wa Unasemaaaa!!!??? Eeeeh, unasemajeee!!??? Eeeeeeeh?? sijasikia umesemaaa??? Eeeh nasemajeeee!
MY TAKE: Hili nalo mkalitizame.