Mnakosea mahesabu wadada wa mjini

Mnakosea mahesabu wadada wa mjini

Sky Eclat una hoja ya maana lakini hiyo mada ni tata sana. Mimi kwa mtizamo wangu maisha hujengwa na jinsi mtu anavyoyaona maisha.

Anaweza mtu kuwa mkaanga chips maisha yake yote na akaishia kupanga na mwisho wa siku akawa ni mkaanga chips kwenye vilabu vya pombe za kienyeji ama kwenye Bar za mchafukoge.

Awe ni mkaanga chips ama Afisa ya wa benki, kama mwanamke anataka mwanaume wa kubadili maisha yake ni lazima atazame kwanza akili ya huyo mwanaume.

Mtazamo wa mwanaume au mwanamke hujengwa toka alikolelewa. Wanasaikolojia wanadai ni rahisi mwanaume kujenga mtazamo toka kwa mwanamke aliyemlea kuliko mwanaume aliyemlea. Jinsi mwanaume anavyoyatazama maisha ndivyo nafasi ya kusonga mbele inavyokuwa.

Maana hata mkaanga chips anaweza kuwa ni mkaanga chips anayetumia banda lake la kukaangia chips kama tego la kupatia wanawake. Huyu naye hana uwezo

Wanawake zijaribuni kwanza akili za wanaume mnaotaka kufanya nao maisha badala ya kuangalia walivyo navyo. Akili ndizo hubadili maisha ya mtu na si vile alivyo navyo. Ndiyo maana tajiri wa leo anaweza kuwa maskini wa kesho na maskini wa leo akawa tajiri wa kesho.

FaizaFoxy wanawake wengi (Siyo wote) wanaoishi kwenye nyumba za urithi ndiyo wanaongoza kwa kuwa na watoto kwa baba tofauti tofauti kwa kuwa wao ni maslahi mbele.
Rudia kusoma uzi vizuri uuelewe kwanza.

Anachozungumzia mtoa mada ni tamaa za Wanawake wengi wa mjini kupenda sana status za Wanaume kuliko kuangalia upeo, maarifa ya vitega uchumi kwaajili ya future wala siyo akili.

Kumbuka unaweza kuwa na akili nzuri lakini ukakoswa na upeo, maarifa na bidii ktk utafutaji.

NB: Mipango siyo matumizi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cha msingi wanatoa, hayo mengine watajibeba nayo wenyewe.
 
Hapo mjini dar kuna mambo, unakuta mwanamke kazalishwa kaachika na mumewake kutokana na tabia zake, ana mtoto anahtaj matumz na hana kazi yoyote na anataka kuish vzuri unafkr nini kinafuata? wanawake wengi wa style hyo ni kama wanajiuza tuu kutwa wanawaza kupata mwanaume mwenye hela zaid ya alioko nae kwenye mahusianno mmda huo . . Nnachowaomba tu msihamie kudanga kwa wauza chips mtawafilisi

Write your reply...
 
Good examples. Na wanawake hao ni wale wa mipango. Huenda kuwa sio romantic kivile lakini ni yule mwaname anaekupa fursa. Mipango. Michongo.. yaaan mwanamke anakupush mfanye kitu. Yeye sio spender bal ni mtafutaji pia.

Hawa wa pwan wengi wao wanajua kula tu.. kutwa kudanga. Lakin ukimwambie nipe idea ya biashara. Hana hata moja.

Sent using Jamii Forums mobile app
Idea ya biashara unataka mke ama consultant lol
 
Kama mwanamke huna kazi...
Upo upo tu mjini. Au una kazi na una kipato kidogo.
Lazima uwe umeshawahi kuwaza hata business fulani labda .. labda kuna mrad unatakao saidia. Mm nita act kama supportive element kwa kuleta funds.

Sasa kama mwanamke umezubaa.. kutwa kupaka rangi.. na kuangalia tv.. huna hata idea yoyote ya kujiigizia kipato. Ww ni HASARAAAAAAA.
Idea ya biashara unataka mke ama consultant lol

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yeah but for how long? Yes atatoa ila to what end?
Muda utafika atasepa.
Atakuja mwingine nae hivyo hivyo.. atatoa vihela akishakula papuchi mbele.
Sasa hapa tofauti yako na wanajiuza pale sinza itakuwa ni eneo tu ma style ya biashara.

Mwanamke inatakiwa uamke kiakili. Sio kutwa uawaza mbinu mpya za kudanga. Utakimbiwa na kila mwanaume.. baadae uje useme wanaume wabaya.

(Sorry kwa kukutolea mfano, lengo ni kufikisha ujumbe kwa wadada wengi)
Cha msingi wanatoa, hayo mengine watajibeba nayo wenyewe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Je Huyo mkaanga chips hiyo 200,000/- anayoingiza kwa siku moja ni “net amount “?
Au ni ghafi yaani gross amount?

Je hiyo laki mbili ni baada ya kutoa gharama za kununulia mafuta, viazi, makaa/gesi, kumlipa kijana, tomato, n.k.?

Nimeona nitoe angalizo kidogo maana isijekuwa ni gross figure ambapo akitoa gharama zote anabaki na 50,000/- tu


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Je Huyo mkaanga chips hiyo 200,000/- anayoingiza kwa siku moja ni “net amount “?
Au ni ghafi yaani gross amount?

Je hiyo laki mbili ni baada ya kutoa gharama za kununulia mafuta, viazi, makaa/gesi, kumlipa kijana, tomato, n.k.?

Nimeona nitoe angalizo kidogo maana isijekuwa ni gross figure ambapo akitoa gharama zote anabaki na 50,000/- tu


Sent using Jamii Forums mobile app
Hata kama ni 50,000 kwa siku kumi ana 500,000 wakati teller ana 750,000 kwa mwezi
 
Hata kama ni 50,000 kwa siku kumi ana 500,000 wakati teller ana 750,000 kwa mwezi

Sawa, hiyo elfi hamsini nimetoa kama mfano tu lakini yaweza kuwa chini ya hapo au kuzidi kidogo!
Na hapo jamaa wa chips anakuwa bado hajalipa kodi ya pango ya hapo anapouzia chips umeme n.k!

Najaribu kufikiria kuona sizani kama mkaanga chips anapata faida kubwa kiasi hicho kwa mtizamo wa wengi jinsi ulivyo!

Nimeona nichangie mada kwa kujaribu kuchambua kiundani kidogo !


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Labda kwa wale wauza chips ambao wako maeneo ambayo yako strategic, kama vile maeneo ya vituo vya mabasi, vyuoni , n.k

Vinginevyo kwa wastani wauza chips walio wengi wamechoka tu huwezi walinganisha na maafisa wa banks!


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom