CalvinKimaro
JF-Expert Member
- Sep 11, 2017
- 244
- 312
Kuna kisa cha wayunani cha kale kuwa kulitokea ubishi nani awe kiongozi wa siku. Wayunani walikuwa wanachagua kiongozi kila siku. Mtu anatawala siku ikipita anachaguliwa mwingine. Mtu hachaguliwi tena mpaka wengine wote wachaguliwe. Ikafika muda walioanza kuchaguliwa wakajihoji: hivi mpaka zamu yetu ifike tena si tutakuwa tuko kaburini?
Wakajiunga wakaleta hoja kuwa watu wachaguliwe kwa sifa na sio kwa zamu! Ambao zamu yao ilikuwa bado wakapinga. Mjadala ukawa mkali watu wakatoana ngeu. Baada ya muda kupita bila kiongozi kila mmoja akaumia kivyake. Mwisho wakakubaliana hivi:
1. Wanawake wasichaguliwe tena.
2. Watu wachaguliwe kwa kuangalia kama wana nidhamu.
3.Asiwe na sifa ya wizi.
4. Pawepo ukomo wa uongozi na
5. Mtu asichaguliwe mara moja tu.
Watu wakaona huu ndio utaratibu unakidhi pande zote. Ndio muafaka wa kwanza.
Ni utaratibu huu ndio uliendelea duniani karne nyingi mpaka ulipokuja kuvunjwa karne ya 15.
Uteuzi wa hivi karibuni wa mnadhimu mkuu kutoka CHADEMA umenifanya nikumbuke kisa hiki cha wayanunani wa kale.
Ni kama chadema wametupa kila kitu cha wayunani ambao hakika ndio baba wa demokrasia!
Sawa kweli zama hizi haifai kumbagua mwanamke kama ana uwezo. Lakini kazi ya kuhakikisha nidhamu bungeni haipaswi kukabidhiwa mtu asiye na nidhamu. Aliyeteuliwa ana historia ya kutokuwa na nidhamu bungeni na amewahi kuadhibiwa mara kadhaa kwa vitendo vya utovu wa nidhamu. Kijamii, kimila na kidini anakabiliwa na tuhuma nzito sana! Japo ni tuhuma haifai mtunza nidhamu atuhumiwe vile! Mke wa Pilato hapaswi kutuhumiwa!
Tutegemee nini bungeni?
Hakika ataongoza kuvunja badala ya kusimamia nidhamu! Hivi chadema wanawaza kweli? Hivi hawakuona heshima waliyopata mara tu baada ya mtani wangu kumpokea mnadhimu mwingine asiye na nidhamu?
Hivi kiranja anayepiga kelele darasani anafaa?
Mnadhimu ataadhibiwa kwa kukosa nidhamu! Chadema iandae atakayemshikia kiti bungeni!
Wakajiunga wakaleta hoja kuwa watu wachaguliwe kwa sifa na sio kwa zamu! Ambao zamu yao ilikuwa bado wakapinga. Mjadala ukawa mkali watu wakatoana ngeu. Baada ya muda kupita bila kiongozi kila mmoja akaumia kivyake. Mwisho wakakubaliana hivi:
1. Wanawake wasichaguliwe tena.
2. Watu wachaguliwe kwa kuangalia kama wana nidhamu.
3.Asiwe na sifa ya wizi.
4. Pawepo ukomo wa uongozi na
5. Mtu asichaguliwe mara moja tu.
Watu wakaona huu ndio utaratibu unakidhi pande zote. Ndio muafaka wa kwanza.
Ni utaratibu huu ndio uliendelea duniani karne nyingi mpaka ulipokuja kuvunjwa karne ya 15.
Uteuzi wa hivi karibuni wa mnadhimu mkuu kutoka CHADEMA umenifanya nikumbuke kisa hiki cha wayanunani wa kale.
Ni kama chadema wametupa kila kitu cha wayunani ambao hakika ndio baba wa demokrasia!
Sawa kweli zama hizi haifai kumbagua mwanamke kama ana uwezo. Lakini kazi ya kuhakikisha nidhamu bungeni haipaswi kukabidhiwa mtu asiye na nidhamu. Aliyeteuliwa ana historia ya kutokuwa na nidhamu bungeni na amewahi kuadhibiwa mara kadhaa kwa vitendo vya utovu wa nidhamu. Kijamii, kimila na kidini anakabiliwa na tuhuma nzito sana! Japo ni tuhuma haifai mtunza nidhamu atuhumiwe vile! Mke wa Pilato hapaswi kutuhumiwa!
Tutegemee nini bungeni?
Hakika ataongoza kuvunja badala ya kusimamia nidhamu! Hivi chadema wanawaza kweli? Hivi hawakuona heshima waliyopata mara tu baada ya mtani wangu kumpokea mnadhimu mwingine asiye na nidhamu?
Hivi kiranja anayepiga kelele darasani anafaa?
Mnadhimu ataadhibiwa kwa kukosa nidhamu! Chadema iandae atakayemshikia kiti bungeni!