Damaso
JF-Expert Member
- Jul 18, 2018
- 6,132
- 10,514
Ubalozi wa Marekani unatarajia kupiga mnada wa kukata na shoka Jumamosi ya Januari 24, 2026, pale Golden Resort, Sinza. Kuanzia magari hadi vifaa vya TEHAMA, kila kitu kinauzwa "kama kilivyo." Lakini je, ni kweli bei ni rafiki kwa mlalahoi na mtanzania?
Wadau wanalalamika kuwa bidhaa bora na zenye afya huchukuliwa na "wakubwa" na bei ya kianzio huwa ni juu sana. Kama unalenga kwenda kuchukua gari au samani, zingatia haya: Kwanza, nenda siku ya ukaguzi kesho (Januari 23) ukiwa na fundi wako; kumbuka hakuna dhamana. Pili, piga hesabu ya kodi na ushuru mapema ili usiumie baadaye, kuna raia watalia na kusaga meno.
Usikurupuke kwa mihemko ya mnada! Je kama mdau wa Jamii Forums una chochote cha kumshauri mtu ambaye anatamani Jumamosi kuondoka na kitu Ubalozini? Na kwa wale wenye uzoefu, je kuna bidhaa zipi na zipi? Na makadirio ya kodi?
Wadau wanalalamika kuwa bidhaa bora na zenye afya huchukuliwa na "wakubwa" na bei ya kianzio huwa ni juu sana. Kama unalenga kwenda kuchukua gari au samani, zingatia haya: Kwanza, nenda siku ya ukaguzi kesho (Januari 23) ukiwa na fundi wako; kumbuka hakuna dhamana. Pili, piga hesabu ya kodi na ushuru mapema ili usiumie baadaye, kuna raia watalia na kusaga meno.
Usikurupuke kwa mihemko ya mnada! Je kama mdau wa Jamii Forums una chochote cha kumshauri mtu ambaye anatamani Jumamosi kuondoka na kitu Ubalozini? Na kwa wale wenye uzoefu, je kuna bidhaa zipi na zipi? Na makadirio ya kodi?