samirnasri
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 1,388
- 213
Kwa wakazi wa Dodoma jina Martin Luther sio geni unapozungumzia suala zima la elimu. Ni shule iliyopo eneo la kisasa njia ya kuelekea Dar es Salaam. kwa ujumla shule ina mazingira ya kuvutia kwa muonekano wa nje.
Kwa upande wa taaluma pia imekuwa miongoni mwa shule bora mkoani Dodoma ikiwa kwenye nafasi tano za juu. Pamoja na kufanya vizuri mkoani Dodoma, matokeo ya shule hiyo kwa ngazi ya kitaifa sio mazuri sana. Mfano, mwaka 2019 ilishika nafasi ya pili kimkoa wakati kitaifa ilishika nafasi ya 128 kati ya shule 9929. Mwaka 2018 ilishika nafasi ya 6 kimkoa na nafasi ya 118 kitaifa; mwaka 2017 shule hiyo ilikuwa bado ina utaratibu wa kusajili shule mbili ndani ya eneo moja ambapo wanafunzi wenye uwezo mkubwa walisajiliwa kwa jina la Martin Luther King Primary School. Hawa WALIKUWA WANAFUNZI 42 tu na walifanikiwa kuongoza kimkoa na kushika nafasi ya 10 kitaifa. wanafunzi wengine walisajiliwa kwa jina la Martin luther primary school na walishika nafasi ya 2 kimkoa na nafasi ya 95 kitaifa.
Mmiliki wa shule hii amekuwa na tabia ya kuongeza ada kiholela bila kushauriana na wazazi. Licha ya shule yake kuwa na ada ya juu bado amekuwa akiongeza ada kila kukicha. Kati ya mwaka 2017 na 2018 alipandisha ada kwa jumla ya shilingi laki tatu (300,000). Watoto wa nursery na std one waliokuwa wakilipa tsh 1,200,000 KWA mwaka walitakiwa kulipa 1,500,000 kwa mwaka; watoto wa darasa la pili na la tatu waliokuwa wakilipa 1,800,000 kwa mwaka walitakiwa kulipa tsh 2,100,000 na wale wa la nne mpaka la saba waliokuwa wakilipa tsh 2,100,000 walitakiwa kulipa 2,400,000.
Kama hiyo haitoshi mmiliki wa shule hiyo tayari ametoa taarifa ya kupandisha ada kwa ongezeko la tsh laki tatu kuanzia kuanzia Jajuary 2021 ambapo. maana yake watoto wa awali watalipa 1,800,000; wa la pili na la tatu watalipa 2,400,000 na wa la nne mpaka la saba watalipa 2,700,000. hizi ada zote ni kwa wanafunzi wa kutwa (day). Maana yake ndani ya miaka mitatu ameongeza ts 600,000.
Sababu za kuongeza ada kwa mujibu wa barua aliyoiandika ni zifuatazo. Moja, kuboresha chakula cha wanafunzi; pili, kuongeza idadi ya magari ya kubebea wanafunzi; tatu, kuboresha mishahara ya watumishi.
Watumishi wenyewe wanalalamikia maslahi madogo. Binafsi sioni sababu ya msingi kati ya hizo zote. Wanafunzi wa awali watakaotakiwa kulipa ada ya tsh milioni moja na laki nane wanakunywa uji tu asubuhi na mchana hawali chochote kwa kuwa wanaruhusiwa sa saba mchana. Suala la kununua magari ya kubebea wanafunzi ni jukumu la mmiliki wa shule. Alitakiwa awe na magari ya kutosha kabla ya kufungua shule.
Kwa ufupi, mtu huyu amekuwa akiendesha shule kibiashara zaidi. Kwa kuwa ana majengo mengi ana wanafunzi wengi sana hivyo anahisi yeye kupata wanafunzi wengi sio shida. Binafsi sidhani kama mmiliki wa shule ana haki ya kuongeza ada atakavyo hata kama shule ni yake. Lazima kuwe na sababu za msingi za kuongeza ada.
Kwenye hili wazazi wanapaswa kuungana pamoja kumshitaki mahakamani mmiliki huyu wa shule pamoja na bodi ya shule. Mimi nitakuwa tayari kutoa msaada wa kisheria na tayari nimepata grounds za kumshitaki. Atapaswa kuondoa ongezeko hilo la ada.
Kwa upande wa taaluma pia imekuwa miongoni mwa shule bora mkoani Dodoma ikiwa kwenye nafasi tano za juu. Pamoja na kufanya vizuri mkoani Dodoma, matokeo ya shule hiyo kwa ngazi ya kitaifa sio mazuri sana. Mfano, mwaka 2019 ilishika nafasi ya pili kimkoa wakati kitaifa ilishika nafasi ya 128 kati ya shule 9929. Mwaka 2018 ilishika nafasi ya 6 kimkoa na nafasi ya 118 kitaifa; mwaka 2017 shule hiyo ilikuwa bado ina utaratibu wa kusajili shule mbili ndani ya eneo moja ambapo wanafunzi wenye uwezo mkubwa walisajiliwa kwa jina la Martin Luther King Primary School. Hawa WALIKUWA WANAFUNZI 42 tu na walifanikiwa kuongoza kimkoa na kushika nafasi ya 10 kitaifa. wanafunzi wengine walisajiliwa kwa jina la Martin luther primary school na walishika nafasi ya 2 kimkoa na nafasi ya 95 kitaifa.
Mmiliki wa shule hii amekuwa na tabia ya kuongeza ada kiholela bila kushauriana na wazazi. Licha ya shule yake kuwa na ada ya juu bado amekuwa akiongeza ada kila kukicha. Kati ya mwaka 2017 na 2018 alipandisha ada kwa jumla ya shilingi laki tatu (300,000). Watoto wa nursery na std one waliokuwa wakilipa tsh 1,200,000 KWA mwaka walitakiwa kulipa 1,500,000 kwa mwaka; watoto wa darasa la pili na la tatu waliokuwa wakilipa 1,800,000 kwa mwaka walitakiwa kulipa tsh 2,100,000 na wale wa la nne mpaka la saba waliokuwa wakilipa tsh 2,100,000 walitakiwa kulipa 2,400,000.
Kama hiyo haitoshi mmiliki wa shule hiyo tayari ametoa taarifa ya kupandisha ada kwa ongezeko la tsh laki tatu kuanzia kuanzia Jajuary 2021 ambapo. maana yake watoto wa awali watalipa 1,800,000; wa la pili na la tatu watalipa 2,400,000 na wa la nne mpaka la saba watalipa 2,700,000. hizi ada zote ni kwa wanafunzi wa kutwa (day). Maana yake ndani ya miaka mitatu ameongeza ts 600,000.
Sababu za kuongeza ada kwa mujibu wa barua aliyoiandika ni zifuatazo. Moja, kuboresha chakula cha wanafunzi; pili, kuongeza idadi ya magari ya kubebea wanafunzi; tatu, kuboresha mishahara ya watumishi.
Watumishi wenyewe wanalalamikia maslahi madogo. Binafsi sioni sababu ya msingi kati ya hizo zote. Wanafunzi wa awali watakaotakiwa kulipa ada ya tsh milioni moja na laki nane wanakunywa uji tu asubuhi na mchana hawali chochote kwa kuwa wanaruhusiwa sa saba mchana. Suala la kununua magari ya kubebea wanafunzi ni jukumu la mmiliki wa shule. Alitakiwa awe na magari ya kutosha kabla ya kufungua shule.
Kwa ufupi, mtu huyu amekuwa akiendesha shule kibiashara zaidi. Kwa kuwa ana majengo mengi ana wanafunzi wengi sana hivyo anahisi yeye kupata wanafunzi wengi sio shida. Binafsi sidhani kama mmiliki wa shule ana haki ya kuongeza ada atakavyo hata kama shule ni yake. Lazima kuwe na sababu za msingi za kuongeza ada.
Kwenye hili wazazi wanapaswa kuungana pamoja kumshitaki mahakamani mmiliki huyu wa shule pamoja na bodi ya shule. Mimi nitakuwa tayari kutoa msaada wa kisheria na tayari nimepata grounds za kumshitaki. Atapaswa kuondoa ongezeko hilo la ada.