Sasa tuone kama na hili litafungiwa maana championi tayari wamefungiwa. Ukiuliza wengi wetu utaambiwa chanzo cha ajali ni mwendo kasi. Mie pia ni mpanda mabasi haya yaendayo mikoani na wakati mwingine huwa natumia kamkoko kangu siku mojamoja wakati wa likizo kuelekea kijijini kwetu. Mie natofautiana na wanaohukumu kuwa sababu zote za ajali ni mwendo kasi. Mie nakataa. Kwa kipindi chote ninachokuwa naelekea kijijini I swear upon God hakuna basi hata moja huwa linakatiza mbele yangu. Hadi nafika Mbeya. Si upendo wala basi lolote linanipita. Si kwamba najigamba ila nataka kueleza kuwa gari hizi za kisasa zinatengenezwa ili kuhimili speed iliyowekwa. Kwa mfano mabasi mengi huenda hadi speed 120 kwa saa bila wasiwasi wowote.
Nionavyo mimi ni kuwa makini kwa maan ya kuwa na uhakika na uzima wa gari hasa matairi, breki na vifaa vingine kwa maan kuliweka gari tayari kwa safari. Kwa wale wanaosafiri kwenda dodoma au sehemu yoyote kama moro au arusha, askari wa usalama wako kila baada ya kama km 100 na "vitochi" na mwendo wa mabasi yetu huwa si mkali kivile. Hivyo mie napingana kabisa kwamba sababu kuu ya ajali ni mwendo kasi.
Sababu niionayo mie ni miundombinu yaani barabara zetu. Mtakubaliana na mimi kwamba barabara zetu ni nyembamba mno na hivyo inapotokea hitilafu yoyote dereva hana namna ya ku manouvre na hivyo hujikuta nje ya barabara. Laiti kama barabara zingekuwa pana kiasi naamini ajali zingepungua.
Sababu nyingine ni regulators wa usalama barabarani kutokuwa makini. Kila mwaka huwa kuna wiki ya nenda kwa usalama barabarani ambapo kila gari linatakiwa kukaguliwa barabara ili kuhakikisha kama linastahiri kuwa barabarani. Hii haibagui kama ni la abiria au binafsi. Mtakubaliana na mimi kwamba kama zoezi hili lingekuwa linafanywa kwa ufasaha magari mabovyote yangebaibishwa na kutoruhusiwa kutembea barabarani. Lakini kwa sababu vyombo vyetu haviko makini, nadhani mnaelewa kinachoendelea. Naweza sema kwamba wiki ya nenda kwa usalama ni mradi wa kukusanya mapato kwani stika huuzwa bila ya hata kukagua gari.
Kama vyombo vingekuwa makini, naamini magari mabovu kila mwaka yangekuwa yanabainishwa na kutoruhusiwa kufanya safari ikiwa na ya abiria au ya binafsi.