Hata mimi nadhani cha kwanza ni uendeshaji wa madereva, mbovu sana, we angalia kwenye daladala tu, ukijifanya unasema kitu wanakuja juu. Pili baadhi ya abiria tunachangia ajali kwani kuna tunaoshabikia mwendo mkali na utakuta abiria tunabishana wengine wasema acha dereva aendeshe usimfundishe kazi na wengine aaah bwana speed kali mno tunawahi wapiii? hapo utakuta dereva hata hajachangia lkn tayari abiria hawaelewani. Tatu baadhi ya madereva hawataki kukososlewa uendeshaji wao, wakidhani wao ndo waliokabidhiwa dhamana ya gari then, kila kitu ni juu yake na si vinginevyo. Mwisho naomba kuuliza hivi zile leseni mpya lengo lake lilikua nini hasaaaa? C kupunguza ajali kwelii??????????????