Wanajamii nafkiria kuna watu wakiona mada tu wanachangia moja kwa moja bila kujua anaemjibu alikuwa ana maana gani.
Jibu la matukioa haya ni jepesi sana kama ifuatavyo:-
Mfano:Sheikh alieuwawa Mombasa na vijana wa kiislam alikuwa ni mfano kama wa Sheikh alieuwawa Zanzibar,wote lengo lao ni kupinga machafuko,na kuweka wazi misimamo ya Amani kidini kama alivyoamrisha Mtumwe wetu S.A.W.
Wote walikuwa ni wahubiri wa Amani,nakundi lilomuuwa ni kundi la kupinga amani na kutaka Dola ya kiislam na kujitenga.
Nakumbuka iliwahi kusemwa kwamba Mombasa wanataka wajitenge iwe Nchi ya Dola ya Kiislam,na hili limekuwa likifanyiwa majaribio mara kadhaa,na kama Sheikh ukionekana unatetea tu basi unawekwa kwenye Mtego.
Sasa kwa Zanzibar,hakuhitaji kupepesa jicho hii issue ni UAMSHO.
Kuna mwanajamii mmoja aliwahi kuandika kwamba Serikali ilipofuta mashtaka yote ya kikundi cha uamsho pale ndio imejiroga.
Kama walishindwa kupata ushahidi wakati ule ambao watu kadhaa walikufa na kujeruhiwa ikiwemo kifo cha askari ambae ni dola.Na hatimae kusema hakuna hatia na wapo huru,hili ndio janga na halizibiki tena.
Na watu waliwahi ku comment wakati ule kwamba hawa jamaa kama wamewaachia basi makubwa zaidi yanakuja.Ndio haya sasa.
Sheikh aliefariki hata CD zake ukisikiliza ni za Kuhubiri amani na mshikamano kwa waislam,kuheshim viongozi na mamlaka zilizopo kama alivyoamrisha Mungu,sasa alikuwa anachukuliwa kama Sumu kwa wapenda Uamsho(yaani misimamo mikali ya kidini na kisiasa).
Ifahamike kwamba Lengo la Uamsho ni kuitenga Zanzibar iwe Dola ya kiislam.
Sasa wale wote wanaotaka kuonyesha hali hii basi wanakumbwa na balaa kubwa kamahilo.
Niwapeni mfano mdogo tu kabla yatukio hili,Zanzibar ilikuwa katika harakati za Shughuli ya Ijitmai ambapo wageni wengi sana ndani na nje ya nchi uhudhuria katika kongamano hilo.Sasa wiki iliyopita siku ya Ijumaa kama sikosei kulikuwa na makundi kama matatu,yamejigawa maeneo ya Amani round about kuja mpaka Mwanakwerekwe,makundi hayo yalikuwa na Bendere za Taifa,ilikuwa mada ya Jioni hivi na baadae yalitawanyika na kuanza kujigawa nakupita maeneo huku Wakiimba,"Tunatakaaa Nchiiii Yeetuuu,Tunatakaaa Nchiiii Yeetuuu".
Wakati makundi hayo yakipita bila hata kibali haikujulikana kama serikali ilikuwa haijajua au vipi na haijulikani nani aliyeratibu upangwaji wa makundi yale,,na ilikuwa kwa siku moja tu.
Sasa hata wiki haijaisha kazi ndio hiyo.
Siombei mabaya lakini kwakuachia wale jamaa wa UAMSHO tu basi hapo ndio serikali ilipojimaliza yenyewe.Na kama pale walikosa ushahidi katika uwazi wa ukweli kama ule basi hawatopata tena ushahidi wanaotaka wao.
Mungu Amlaze Mahala Pema Peponi Sheikh wetu "Ameen"
Na ifahamike kwamba unapomuuwa kiongozi wa Dini,mungu ataanza kukuhukumu hapa hapa duniani kabla hujakutanana nae uso kwa uso