Mlipuko mkubwa waitikisa Arusha!

Mlipuko mkubwa waitikisa Arusha!

Arusha hivi punde watu wamerusha bomu la mkono kweny bar maarufu inayoitwa Arusha Night Park au ------ Bar iliyopo eneo la Mianzini inasemekana watu wawili wamepoteza maisha ila majeruhi ni wengi sana tukio hili ni ndani ya nusu saa iliyopita. Watu kibao walikuwa wanacheki mpira unaambiwa watu wamekatika mikono yaani balaa majeruh ni wengi mno........
 
mtungi wa gesi ule mkubwa kbs..... au ni kitu chenye umbo la kitenesi na draft draft kwa juu kina kama ufunguo?
 
Hatari sana hii mkuu, natamani sana wahusika watiwe nguvuni ili tupate kujua ni kina nani haswa na nia yao...

Ni bomu mkuu, watu wengi wameumia na wamekimbizwa Selian Hospital na Mt. Meru Hospital, MUNGU awape kupona majeruhi wote.

TANZANIA LEO NI MAJANGA!
 
poleni sana mkuu. zidi kutupa up dates zaidi ikiwezekana hadi na picha.

Muda mfupi tu baada ya tukio lile watu tumekimbilia makwetu, pale eneo la Arusha Night Park Bar wamejaa polisi na wanajeshi wa mabomu mkuu!
 
Isije kuwa ni kuhamisha attention ya kesho, maana nikikumbuka kipindi kile cha mfumuko wa bei na kupanda kwa gharama za maisha na jinsi ustadi ulivyotumika kumleta hewani babu wa Loliondo sina hamu na hii system ya Msafiri.
 
Mpaka sasa inasadikika watu sita wamepoteza maisha
 
Wenzetu Kenya wanafuatilia lakini sisi janga likitokea tunaliweka kapuni.Au ni njia ya kutubadilishia upepo wa Katiba?Maana joto limekuwa kali mjengoni na viyoyozi vimeshindwa kazi.

Great thinking. Ukweli ndio huo mkuu. Lengo ni kuhamisha akili za watu kutoka Dodoma ikizingatiwa kuwa kesho watu walikuwa wanasubiri kwa hamu kumsikiliza Tundu Lissu.
 
Back
Top Bottom