Pretty-baby
Member
- Jan 25, 2012
- 56
- 7
jamani mr rocky umenena, mtoa mada fuata ushauri wa mr rocky,he z gud kwa kweli anjua dhamani ya mke! na njia ya kufanya ili kumpata mke na ujue sio wote ni mcharuko1
Ila kweli mkuu wanawake wengi nimcharuko lakini siyo wote wewe jitaidi kutafuta kanisani kwako na pia umuombe mungu
he he he tupo kwenye same boat ndugu,ngoja tuchukue mawaidha hapa
Kwani nani kakuambia ukamtafute wa kanisanikumuomba mungu ndio, ila wa kanisani nao siku hizi vimeo tu, haswa kwaya ya vijana ndo mastar wao kuwang'oa
wewe kweli kilaza flani!!
Ikifika siku Mungu atatuma malaika uitaona anakuonyesha huyu ndo mke wako.
Lakini wewe hutamuona malaika.
nyie ndo walee mnaotafuta wanawake wenye sijui wezere kubwa,ooo awe na sura nzuri,pua ndefu,mguu wa bia,macho ya kulegea,mrefu,awe na pozi.......badala ya kutafuta wenye sifa za kumcha mungu,,ndo mana matokeo yake mnaishia kupata micharuko
nielemishe mkuu
asa unadhani ntampenda vipi bila kumtamani kwanza? mwenyewe mbaya, mama watoto nae akiwa kapinda si adhabu kwa watoto
Hongereni wana jf kwenye thread hii mmenishangaza maana wengi wenu mmeongea point....haleluuuuuuyaaaaa
Sa unaguna kwanini sitoa point wapi kuna kosa, au kusikia malaika ndo imekuwa ajabu...wewe unaelewa nini mana ya malaika? malaika sio lazima umuone au mungu unadhnai utamuona? kama unadhani utamuona mungu ujuwe unaota.mmhhhhh
ahsante mdada!!kwanza jiulize ulishajitambua ni mwanamke wa aina gani unamtaka,coz kuna baadhi ya wavulana japo wanakuwa wanona ni wanaume ukimuliza aina ya mke anayetaka hizo sifa anazotaja mpaka aibu kwa uankuta kabase kwenye sifa za nje ambazo ni ngumu kwa mtu mmoja kuwa nazo zote labda mpaka kutoa oda kwa mungu amtengenezee,so kumpata inakuwa ishu,nakushauri tuliza akili,mke sio sura wala umbo,mshirikishe mungu ktk kumtafuta utampata tu coz kila mtu kaumbiwa mtu wake,jiweke km mwanaume alietayari kuwa baba wa familia sio ujiweke kivulana utaishia kupata visichana mcharuko,hata ukimpata anayefanania kuwa mke uwe na subira na mvumilivu kwan wengi huwa hawakurupuki kukukubali ni lzm auone userious wako,pia angalia namna unavowaaprochi,ulimi wako ndio silaha pekee hata km utakuwa na mwonekano wa aina gani!epuka kutumie pesa km ushawishi wakati wa kujieleza ni sumu kali kwa wadada walio makin,japo wengi hawaamin hili.
Mimi nilimpatia kwenye computer kozi alikuwa mwanafunzi wangu, kwanza nilimpenda kwa muonekano wake, tabia yake na nilipogundua kabila na dini yake vitaendana na matakwa yangu na kuwafahamu ndugu zake na tabia zao bila hata yeye kufahamu kwamba ninafanya uchunguzi niliamua kujaribu kuanzisha uhusiano, na kweli nilipomuomba kutoka nae hakukataa. Katika maongezi yetu swali la kwanza aliloniuliza ni kama mimi ni mume wa mtu au la, nilipomjibu kwamba mi sijaoa nilimuona ametabasamu na kuwa na amani sana. Tulianza urafiki wetu bila kujificha kabisa na ndugu zetu walijua toka miezi miwili ya mwanzo. Kusema ukweli kabla ya hapo nilikuwa kicheche nakwenda disko na marafiki zangu mpaka saa nane za usiku na huko kila mtu anachukua changudoa, tulikuwa na tabia ya kuchukua machangu tu, tulikuwa hatutaki kabisa kuwa na GF tuliona ni usumbufu usiokuwa na maana, unamchukua changu kesho hamjuani tena. Ila nilipompata mke wangu mpaka marafiki ilibidi nitengane nao kabisa kwenye mambo ya starehe, mpaka ilifikia wakawa wanasema nimelishwa limbwata. Ndugu yangu kitu cha muhimu ni kufanya uchunguzi na kujua tabia, elimu, dini, mila (kabila) kama vitaendana na matakwa yako na umuombe Mungu akusaidie umpate Mke mwema. Usiweke mbele tamaa za mwili na kufanya mapenzi ovyo, usimwambie kwamba unataka kumuoa kabla ya kufanya maamuzi. Tabia yako inaweza kukufanya kazi ya kumpata mke ikawa ngumu au rahisi sana jichunguze.
Wapo wengi sana tena wa kumwaga.....sema tu wewe ndo umeishiwa ujanja...Omba tu wataalamu wakusaidi ku-recharge!!
Uko tayari nikugawie mmoja wa wale nilionao??
Nataka kudispose mmoja ili nitafute mupya!!
Babu DC!!
fumba macho na masikio ziba
Night club wapo wakutosha sana