Mlima Kitonga vs Mlima Sekenke, upi mkali?

Mlima Kitonga vs Mlima Sekenke, upi mkali?

kwa wale watu wa kusafiri safiri sana kati ya mlima sekenge uliopo singida mlima ulioua abiria kibao kwa ajari zake yaani mkifika na basi mnasali kwanza , enzi zile mkifika na basi abiria wanashuka na kutangulia kwa miguu than basi linakuja na mizigo na dereva, na mlinga kitonga wa iringa wenye kona kibao, upi unatisha sana kwa madereva?

senkenke zamani sa hizi kawaida sana...
 
yote cha mtoto,kuna kitu inaitwa kaburi wazi na kona ya mkasi.toka sumbawanga kwenda ziwa rukwa.we acha tuu.nashangaa hata serikali kutopeleka hili eneo kwenye maajabu 8 ya dunia
 
Tatizo la sekenke ya zamani lilikuwa ni barabara maana ilikuwa ni vumbi tupu lakini ingekuwa lami zile ajali wala tusingezishuhudia kwa kiwango kile,wachina walipoanza kuweka lami wakaiamisha barabara toka kule juu kuileta huku chini ndo wamemaliza kabisa makali ya sekenke, hatari zaidi ipo sehemu zifuatazo:-
1:kitonga
2:nyang'oro
3:lukumburu
 
siku hiz sekenke hakuna mlima ni barabara tu ya kawaida ila kitonga nomaaa,enzi zle tunaenda mza kupita singida na mashiku bus service ni balaa mkuu,

Kabisa mkuu,umenikumbusha Mashiku bus,pia kulikuwa na super najmunisa abiria wamebanana km daladala za Gongolamboto

mkuu umelisahau. zuberi bus na king kross bus

wakuu namaanisha ile sekenge ya 90 na 2004 hivi ambapo palikua panatisha mbaya

Aiss kumbe wewe wa zamani...umesafiri na mashiku...enzi hizo mimi nikiisafiri na mamba safaris arusha mwanza...

Hizo bus mnazoziongelea nyingi hamjaifaidi sekenke aliyepanda Nzega bus, Sekenke bus, USAI bus na Tanganyika bus ambalo lilikuwa linatoka Mwanza kwenda Arusha Moshi hao ndio watakusimulia sekenke ilikuaje
 
Sijawahi pita njia ya sekenke. Kitonga ya kawaida sana. Pamoja na ulena wangu napita bila shida
 
Tatizo la sekenke ya zamani lilikuwa ni barabara maana ilikuwa ni vumbi tupu lakini ingekuwa lami zile ajali wala tusingezishuhudia kwa kiwango kile,wachina walipoanza kuweka lami wakaiamisha barabara toka kule juu kuileta huku chini ndo wamemaliza kabisa makali ya sekenke, hatari zaidi ipo sehemu zifuatazo:-
1:kitonga
2:nyang'oro
3:lukumburu

mkuu kumbe huijui sekenge vizuri ni hivi wakati ule ukitoka mwanza mpaka singida ilikua vumbi tupu isipokua pale sekenge ndio palikua na lami
 
Hizo bus mnazoziongelea nyingi hamjaifaidi sekenke aliyepanda Nzega bus, Sekenke bus, USAI bus na Tanganyika bus ambalo lilikuwa linatoka Mwanza kwenda Arusha Moshi hao ndio watakusimulia sekenke ilikuaje

Sikuwahi kupita njia hiyo hadi 1993 nilipopita na west star...tulipandisha mlima kwa kutembea...gari lilishindwa kupanda na abiria tukiwemo....
 
jamani kweli milima ipo, ila pia kuna barabara ya kutoka mombo to lushoto jamani hatari tupu, watu huwawanatapika kama wajawazito vile, afu conda wa burudani anakupa rambo anakwambia atakaejaza anarudishiwa nauli yake. duh
 
kwa wale watu wa kusafiri safiri sana kati ya mlima sekenge uliopo singida mlima ulioua abiria kibao kwa ajari zake yaani mkifika na basi mnasali kwanza , enzi zile mkifika na basi abiria wanashuka na kutangulia kwa miguu than basi linakuja na mizigo na dereva, na mlinga kitonga wa iringa wenye kona kibao, upi unatisha sana kwa madereva?
Ubora na mbinu mpya za technologia katika ujenzi wa barabara na uundwaji wa vyombo vya usafiri zimesaidia sana katika kupunguza hatari kwa watumiaji barabara. Nakumbuka sehemu nyingi zilikuwa zikisimuliwa ni sehemu za hatari lakini siku hizi tunaziona za kawaida sana kwani hata kwa gari ndogo unaweza kwenda kwa kasi ya 60km/h.
Hebu jionee na hizi za Mzee Mandango

https://www.jamiiforums.com/jamii-p...ifo-worlds-most-dangerous-road-bolivia-4.html
 
Na ule mlima ile njia ya kwenda Chunya ukiingilia Kabwe, panaitwaje?
 
kuna mlima upo kama unaenda wilaya ya ulanga unaitwa NDORORO nao ni mlima mkali sana
 
Naona kuna wanaochanganya kati ya salanda na sekenke..

Ila kwa sasa kati ya milima aliyotaja mtoa mada, kitonga ndy hatari zaidi..

Lakini kwa miaka ya nyuma, sekenke ilikua habari nyingine...hilo bonde la ufa lilitushia usalama..maana madereva hufika pale na kupaki kwanza na kuanza kukagua magari yao kabla ya kushuka au kupanda..pale kati kulikua na alama kama S..scania na jeuri yake ya kupanda milima zilikua zinapanda kwa heshima na taadhima..
 
jamani kweli milima ipo, ila pia kuna barabara ya kutoka mombo to lushoto jamani hatari tupu, watu huwawanatapika kama wajawazito vile, afu conda wa burudani anakupa rambo anakwambia atakaejaza anarudishiwa nauli yake. duh

wewe ulijaza rambo ngapi?
 
Naona kuna wanaochanganya kati ya salanda na sekenke..

Ila kwa sasa kati ya milima aliyotaja mtoa mada, kitonga ndy hatari zaidi..

Lakini kwa miaka ya nyuma, sekenke ilikua habari nyingine...hilo bonde la ufa lilitushia usalama..maana madereva hufika pale na kupaki kwanza na kuanza kukagua magari yao kabla ya kushuka au kupanda..pale kati kulikua na alama kama S..scania na jeuri yake ya kupanda milima zilikua zinapanda kwa heshima na taadhima..

nakubaliana nawe mkuu
 
kwa wale watu wa Lisa fork safiri sana kati ya mlima sekenge uliopo singida mlima ulioua abiria kibao kwa ajari zake yaani mkifika na basiLisa fork mnasali kwanza , enzi zile mkifika na basi abiria wanashuka na kutangulia kwa miguu than basi linakuja na mizigo na dereva, na mlinga kitonga wa iringa wenye kona kibao, upi unatisha sana kwa madereva?
Milima yote hiyo haitishi kama zamani,iliishakarabatiwa.kitonga inaweza kumtia kiwewe dereva asiye na uzoefu.Kwa ligi za zamani ilikuwa: 1. Lukumbulu Songea
2. Lyamba lya mfipa ambayo ni tishio hadi Leo
3. Kitonga Iringa
4. Sekenke Singida.
Barabara nyingi za kisasa hazitakiwi kupita milimani badala yake milima inatobolewa kama ilivyo reli ya Tazara.
 
Back
Top Bottom