Mlima Kitonga vs Mlima Sekenke, upi mkali?

Mlima Kitonga vs Mlima Sekenke, upi mkali?

lukelo sakafu

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2015
Posts
2,938
Reaction score
517
Kwa wale watu wa kusafiri safiri sana,

Kati ya mlima Sekenge uliopo Singida, mlima ulioua abiria kibao kwa ajali zake, yaani mkifika na basi mnasali kwanza. Enzi zile mkifika na basi abiria wanashuka na kutangulia kwa miguu then basi linakuja na mizigo na dereva; na mlima Kitonga wa Iringa wenye kona kibao, upi unatisha sana kwa madereva?
 
Kagua tu Guard Rails zilizopo kwenye milima hiyo ndo utajua ni mlima upi mkali kwa maana ya Vertical na Horizontal curves. Lakini pia wakati mwingine angalia material iliyotumika kujenga kipande hicho cha mlima.
 
siku hiz sekenke hakuna mlima ni barabara tu ya kawaida ila kitonga nomaaa,enzi zle tunaenda mza kupita singida na mashiku bus service ni balaa mkuu,

Mashiku ya juzi Mkuu kulikuwa na kitu kinaitwa Tanganyika bus iliuwa watu 62 pale sekenke. Mashiku inapita mlima umechongwa ule, kitonga labda zile kona tu. Kwa ninavyoona mimi Hata saranda ilikuwa ni mbaya kabla haijachongwa kuliko kitonga.
 
Mashiku ya juzi Mkuu kulikuwa na kitu kinaitwa Tanganyika bus iliuwa watu 62 pale sekenke. Mashiku inapita mlima umechongwa ule, kitonga labda zile kona tu. Kwa ninavyoona mimi Hata saranda ilikuwa ni mbaya kabla haijachongwa kuliko kitonga.
mwaka gani huo?
 
Sekenke ulipita lini mara ya mwisho? Sekenke ya sasa hata ma-learner wanapita bila hata kujua kuwa wamepita sekenke

Sekenke unayoisema wewe mkuu ni hii ya kuanzia 2006 hadi Leo. Mimi Sekenke nimepita 1976, 1996, 2001, 2006 kuanzia hapo napita Mara kwa Mara na miaka yote hiyo ilikuwa kila ukipita kuna mabadiliko. Kitonga nimepita 1993 kwa kweli haikunitisha kama sekenke na saranda
 
kitonga panatisha,huwa naogopa mkiongozana na lori,assume linashishindwa kuapanda mlima halafu lirudi acha kabisa

tena yale maroli yalobeba nguzo hasa ndo huwa yanatisha, alafu madereva wengne wanapita kiboya wanaovatek kwa spidi kwenye vile vikonakonj
 
mlima nungwi ndo balaa maana kuna kona za maji za kufa mtu
 
....weka vigezo vya kucompare , unawezaje kufanya comparison kati ya vitu viwili bila muongozo...
 
Back
Top Bottom