Kenge (Eng)
JF-Expert Member
- Dec 7, 2006
- 543
- 156
Wenyewe wanasemaje?
Habari za leo Friends of Bukoba.
Hii hapa ni video ya watetezi wa Mkoa wa Kagera zidi ya hujuma za Mkoa wa Chato.
Tunawashukuru wote walioshiriki ikiwa ni pamoja na:
(1) Mh. Bernedetha Mushashu (Mbunge viti maalum)
(2) Mh. Charles Mwijage (Muleba Kaskazini)
(3) Mh. Dr. Oscar Kikoyo (Mbunge Muleba Kusini)
(4) Mh. Jackson Rweikiza (Mbunge Bukoba Vijijini)
Shukrani kwa wote walioshiriki katika kupinga kumegwa kwa Mkoa wa Kagera ili kuunda Mkoa wa Chato. Hawa wenzetu wamepigana sana kutetea maslahi ya Mkoa wa Kagera na hasa zile wilaya zinazobaki zisizohofishwe kiuchumi, kisiasa na utamaduni. Kama mtakavyoona kwenye hiyo video, sasa mambo yote yanakwenda ngazi za juu za serikali kwa majadiriano na maamuzi. Kulingana na mtazamo wangu kuhusu maandishi na hotuba za watetezi mbalimbali, petition ya FOB, na hoja hafifu za wawakilishi wa Wilaya za Biharamulo na Ngara, katika mantiki ya kawaida sioni jinsi mtu anavyoweza kuruhusu kumegwa Mkoa wa Kagera. Itabidi uwe kipofu au kiziwi kufanya hivyo baada ya mambo yaliyoandikwa na kusemwa. Hata Hivyo, katika mfumo wa kerikali kama ya Tanzania ambapo mtu mmjo ana mamlaka kamili ambayo siyo lazima yategemee mawazo ya wengine au kundi (absolute power) lolote linawezekana. Therefore, keep our "fingers crossed".
ANGALIZO
Jambo la kushangaza sana katika hii video ni kuona Mkuu wa Wilaya ya Bukoba (Mr. Moses Machali) akiwa msemaji mkuu na mkeleketwa wa kuunga mkono kumegwa kwa Mkoa wa Kagera na kumaanisha kwamba wale waliotoa hutuba za kupinga mkoa isimegwe ni wakabila. Nimejaribu kuangalia huyu mtu ni nani. Huyu ni mtu mwenye umri wa miaka 40, mzaliwa wa Kigoma na alikuwa Mbunge wa Kasulu. Alikuwa mwana chama wa CHADEMA (2007 - 2010), NCCR-Mageuzi (2010 - 2015), ACT Wazalendo (2015 - 2016) na CCM (2016-).
Hii ni rekodi mbuvu sana kwa mtu mwenye umri wa miaka 40. Mtu mwenye msimamo, busara na imani thabiti katika kitu chochote huwezi kuhama kirahisi namna hiyo. Kwa mantiki hii, huwezi kuwa kiongozi wa kundi au jumuiya yoyote kama mtazamo wako unakinzana ma matakwa au mahitaji ya kundi and jumuiya hiyo. Hii ndiyo maana ameshindwa kujua kwamba kama Mkuu wa Wilaya ya Bukoba ambayo ni moja ya wilaya zinazopinga kumegwa Mkoa wa Kagera kwa vile zitaathalika kiuchumi, hawezi kusimama hadhalani na kutoa hutuba kuunga mkono kudhohofishwa kwa Mkoa mama wa Wilaya yako. This cannot happen in public!
Unaweza kuwa na mtazamo tofauti na vilevile unaweza usiipende sehemu na watu ambao umekabidhiwa kuwaongoza, lakini inabidi ufiche hiyo nia yako kama inakinzana na matakwa ya watu wako. Je, huyu mtu anamtazamo gani kuhusu maendeleo ya Wilaya ya Bukoba na Mkoa wa Kagera kwa masuala mengine zaidi ya Mkoa kumegwa? Is this a person you can trust to defend you and resolve your problems? Ningekuwa Rais wa Tanzania, huyu mtu ningemuondoa kwenye hiyo nafasi siku hiyohiyo kwa vile ameonyesha kwamba hana maslahi ya sehemu na watu anaowaongoza.
Deogratias
Canada
Habari za leo Friends of Bukoba.
Hii hapa ni video ya watetezi wa Mkoa wa Kagera zidi ya hujuma za Mkoa wa Chato.
Tunawashukuru wote walioshiriki ikiwa ni pamoja na:
(1) Mh. Bernedetha Mushashu (Mbunge viti maalum)
(2) Mh. Charles Mwijage (Muleba Kaskazini)
(3) Mh. Dr. Oscar Kikoyo (Mbunge Muleba Kusini)
(4) Mh. Jackson Rweikiza (Mbunge Bukoba Vijijini)
Shukrani kwa wote walioshiriki katika kupinga kumegwa kwa Mkoa wa Kagera ili kuunda Mkoa wa Chato. Hawa wenzetu wamepigana sana kutetea maslahi ya Mkoa wa Kagera na hasa zile wilaya zinazobaki zisizohofishwe kiuchumi, kisiasa na utamaduni. Kama mtakavyoona kwenye hiyo video, sasa mambo yote yanakwenda ngazi za juu za serikali kwa majadiriano na maamuzi. Kulingana na mtazamo wangu kuhusu maandishi na hotuba za watetezi mbalimbali, petition ya FOB, na hoja hafifu za wawakilishi wa Wilaya za Biharamulo na Ngara, katika mantiki ya kawaida sioni jinsi mtu anavyoweza kuruhusu kumegwa Mkoa wa Kagera. Itabidi uwe kipofu au kiziwi kufanya hivyo baada ya mambo yaliyoandikwa na kusemwa. Hata Hivyo, katika mfumo wa kerikali kama ya Tanzania ambapo mtu mmjo ana mamlaka kamili ambayo siyo lazima yategemee mawazo ya wengine au kundi (absolute power) lolote linawezekana. Therefore, keep our "fingers crossed".
ANGALIZO
Jambo la kushangaza sana katika hii video ni kuona Mkuu wa Wilaya ya Bukoba (Mr. Moses Machali) akiwa msemaji mkuu na mkeleketwa wa kuunga mkono kumegwa kwa Mkoa wa Kagera na kumaanisha kwamba wale waliotoa hutuba za kupinga mkoa isimegwe ni wakabila. Nimejaribu kuangalia huyu mtu ni nani. Huyu ni mtu mwenye umri wa miaka 40, mzaliwa wa Kigoma na alikuwa Mbunge wa Kasulu. Alikuwa mwana chama wa CHADEMA (2007 - 2010), NCCR-Mageuzi (2010 - 2015), ACT Wazalendo (2015 - 2016) na CCM (2016-).
Hii ni rekodi mbuvu sana kwa mtu mwenye umri wa miaka 40. Mtu mwenye msimamo, busara na imani thabiti katika kitu chochote huwezi kuhama kirahisi namna hiyo. Kwa mantiki hii, huwezi kuwa kiongozi wa kundi au jumuiya yoyote kama mtazamo wako unakinzana ma matakwa au mahitaji ya kundi and jumuiya hiyo. Hii ndiyo maana ameshindwa kujua kwamba kama Mkuu wa Wilaya ya Bukoba ambayo ni moja ya wilaya zinazopinga kumegwa Mkoa wa Kagera kwa vile zitaathalika kiuchumi, hawezi kusimama hadhalani na kutoa hutuba kuunga mkono kudhohofishwa kwa Mkoa mama wa Wilaya yako. This cannot happen in public!
Unaweza kuwa na mtazamo tofauti na vilevile unaweza usiipende sehemu na watu ambao umekabidhiwa kuwaongoza, lakini inabidi ufiche hiyo nia yako kama inakinzana na matakwa ya watu wako. Je, huyu mtu anamtazamo gani kuhusu maendeleo ya Wilaya ya Bukoba na Mkoa wa Kagera kwa masuala mengine zaidi ya Mkoa kumegwa? Is this a person you can trust to defend you and resolve your problems? Ningekuwa Rais wa Tanzania, huyu mtu ningemuondoa kwenye hiyo nafasi siku hiyohiyo kwa vile ameonyesha kwamba hana maslahi ya sehemu na watu anaowaongoza.
Deogratias
Canada