Mkuu wa Mkoa wa California, Davin Newsom, atangaza mgao wa umeme

Kwameh

JF-Expert Member
Dec 3, 2011
1,770
2,087
blackout.jpg


90


planned-electricity-blackouts-california.jpg


Kutokana na mahitaji kuzidi uwezo wa ugavi, umeme utakuwa ukikatwa muda wowote kuanzia saa tisa alasiri mpaka tatu usiku kwa kupokezana baina ya viunga tofauti tofauti vya mkoa wa California, kwa mujibu wa Mheshimiwa Davin Newsom, Mkuu wa Mkoa.

Bwana Newsom ameziomba kampuni zenye mivyombo mizito ya umeme kama vile meli zilizoegeshwa bandarini kutumia nishati ya generator katika kipindi hiki kigumu kwa Wamarekani wa California.

Nchi mbalimbali duniani zikiwemo Ethiopia na Tanzania zimekuwa mstari wa mbele kufikiria mikakati mipya ya kuzindua vyanzo mbadala vya umeme wa ziada ili kukidhi mahitaji ya uchumi na idadi za watu zinazokua kwa kasi.
 
Ingekuwa ni bongo, kuna watu wangesema ni hujuma katika kipindi cha kampeni ili mtu ang'oke.
 
Hii kitu ni Kweli kabisa ila habari umeileta nusu nusu sana halafu source ya hio blackout sio hio uliyotaja
 
Ungeeleza uzalishaji wa nishati ya umeme hapo California ni megawatt kiasi gani na kwa sasa baada ya mgao zitapatikana megawatt ngapi.kuitaja Ethiopia na Tanzania kama mfano wa nchi zinazopambana sawa na California kuzalisha umeme.ni kufananisha mlima na kichuguu.
 
Ungeeleza uzalishaji wa nishati ya umeme hapo California ni megawatt kiasi gani na kwa sasa baada ya mgao zitapatikana megawatt ngapi.kuitaja Ethiopia na Tanzania kama mfano wa nchi zinazopambana sawa na California kuzalisha umeme.ni kufananisha mlima na kichuguu.

California has approximately 80,000 MW of electric generation capacity installed across the state amongst more than 1,500 power plants utilizing a broad array of technologies. Total installed renewable generation capacity is 26,500 MW with almost 12,000 MW from solar and 6,000 MW from wind.
 
Hawa ni wajinga tupu humu, Tatizo Joto lmezidi kiwango na wanalazimila kuzima mitambo isine lipuka, kuna joto la kutisha ambalo halijawahi tokea kwa karine nzima so wanazima mitambo ya kufua umeme
Ungeeleza uzalishaji wa nishati ya umeme hapo California ni megawatt kiasi gani na kwa sasa baada ya mgao zitapatikana megawatt ngapi.kuitaja Ethiopia na Tanzania kama mfano wa nchi zinazopambana sawa na California kuzalisha umeme.ni kufananisha mlima na kichuguu.
 
Mkuu muwe mbatafuta habari sio muda wote msubilie kuletewa humu, kuna Joto kari ambalo halijawahi tokea kwa miaka 100 so wanalazimika kuzima line za kusafirisha umeme wakihofia wild fire, si kwamba wana uhaba wa umeme bali kuna joto kari mno na power line zinaweza lipuka muda wowote so wanazima, elewa kwamba wanazima si kwamba wana uhaba wa meme,
The American Empire on the decline.Ni aibu kwa Marekani.
 
Back
Top Bottom