Serikali: Unaweza kuamka kesho mgawo wa umeme umeisha

Mjanja M1

JF-Expert Member
Oct 7, 2018
3,660
12,306
"Mahitaji ya umeme nchini ni kati ya megawati 300 mpaka 400, mfano leo asubuhi tulikuwa na mahitaji ya megawati 304 ukiingiza megawati 235 (Kutoka kwenye mtambo wa bwawa la Mwalimu Nyerere) utaona kwa kiasi gani itapunguza uhaba wa umeme, zaidi ya asilimia 80 ya tatizo litapunguzwa kwa kuwasha tu ule mtambo ambao taratibu zake ziko mwishoni kabisa , unaweza ukajikuta kesho au keshokutwa unaamka asubuhi unashangaa mgao wa umeme haupo," - Eng Mramba, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati

20240222_120702.jpg
 
Katibu Mkuu wa wizara ya Nishati mh Felician Mramba amesema Mgao wa Umeme utamalizika mwezi March 2024 baada ya kukamilika Majaribio ya mtambo wa kufua Umeme megawatt 235 Bwawa la Mwalimu Nyerere

Source: Mwanahalisi Digital
 
"Kesho au kesho kutwa" kumbe Eng mramba nae anatetesi tu kuhusu mwisho wa mgao wa umeme enewei kesho au kesho kutwa.
 
Wasitugeuke tu....ila nauliza siri ya gas yetu ni nini ? Imeuzwaje ? Ilikuwaje?
Nilimsikia marehemu akisema kuwa eti aliambiwa na born town aliyeasisi uchimbaji wa gas kule kwa bibi kuwa eti hata yeye hajui ilikuwaje,ila nikajiuliza tu,gas si huwa ina evaporate? So itakuwa ilipotelea hewani,sasa hatuna tech ya kuikusanya ikishaingia kwenye hewa,wachina ndiyo wakatuzidi hapo,hata mama hajui ilikuwaje,hakuna anayejua ilikuwaje
 
Nilimsikia marehemu akisema kuwa eti aliambiwa na born town aliyeasisi uchimbaji wa gas kule kwa bibi kuwa eti hata yeye hajui ilikuwaje,ila nikajiuliza tu,gas si huwa ina evaporate? So itakuwa ilipotelea hewani,sasa hatuna tech ya kuikusanya ikishaingia kwenye hewa,wachina ndiyo wakatuzidi hapo,hata mama hajui ilikuwaje,hakuna anayejua ilikuwaje
Kuna mkatana JK aliingia na wachina sijui kwa sbb gani ( rizmoko....labda ipo siku tutajua) ....huwezi kuuza gas yooote bila maelezo kwa nini ....mali nchi haina maelezo ? Ipo siku tutajua tu....tutanyongana hapa.....time will tell subiri tu
 
  • Thanks
Reactions: rr3
Back
Top Bottom