PreGE2025 Mkutano wa Heche washambuliwa Igunga, Tabora

PreGE2025 Mkutano wa Heche washambuliwa Igunga, Tabora

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla)
CHADEMA kupitia ukurasa wao wa X(Twitter) wamesema watu waliokuwa na mapanga na visu wamevamia mkutano wao maeneo ya Igunga mkoani Tabora, watu hao walianza kwa kurusha mawe msafara wa makamu mwenyekiti wa chama John Heche.

CHADEMA pia wamethibitisha kujeruhiwa kwa mlinzi wa makamu Mwenyekiti John Heche, aidha wakati hayo yanatokea jeshi la polisi halikuwepo eneo la tukio.
Ni muda wananchi nao waje na mapanga yao tu sasa.

NO REFORMS NO ELECTION
 
chama cha demokrasia na maendeleo CHADEMA wamesema watu waliokuwa na mapanga na visu wamevamia mkutano wao maeneo ya igunga mkoani Tabora,watu hao walianza kwa kurusha mawe msafara wa makamu mwenyekiti wa chama john heche.

CHADEMA pia wamethibitisha kujeruhiwa kwa mlinzi wa makamu mwenyekiti john heche, aidha wakati hayo yana tokea jeshi la polisi halikuwepo eneo la tukio.View attachment 3363059
Toeni taarifa Police mapema iwezekanavyo.
 
hivi Brenda Rupia yuko wapi sikuhizi, au ndo bado anauguza mdomo
 
Unatumikishwa hivi kuwajeruhi watu na bado upo kwenye wimbi la umasikini. Mtu mwenye kazi zake na kipato chake hawezi kutumwa kufanya upuuzi huu. Watanzania aisee, unatengenezewa life gumu ili uagizwe kufanya upuuzi kwa malipo ya vijisenti vya kula siku 1 huku kesho hujui utaimalizaje
 
CHADEMA kupitia ukurasa wao wa X(Twitter) wamesema watu waliokuwa na mapanga na visu wamevamia mkutano wao maeneo ya Igunga mkoani Tabora, watu hao walianza kwa kurusha mawe msafara wa makamu mwenyekiti wa chama John Heche.

CHADEMA pia wamethibitisha kujeruhiwa kwa mlinzi wa makamu Mwenyekiti John Heche, aidha wakati hayo yanatokea jeshi la polisi halikuwepo eneo la tukio.
Week hii litatolewa tamko kusitisha ziara ya CHADEMA kisingizio kulinda amani
 
Back
Top Bottom