Mkutano wa CCM Mbeya

Mkutano wa CCM Mbeya

Kwa wale mliopoteza zenu poleni sana! Wanaume tunazisaka sana!
Mngekua mnazisaka na mnazitilia maanani hao “waliopoteza zao“ kama unavyowaita wote wangekua wake za watu kama ndio kigezo maana nao walikua nazo once na waliozitoa hawakuziona ni mali.Huwezi tu kusema mnazisaka (hapa sijui unaongelea wanaume wangapi) wakati nyie nyie ndio mliochukua za hao “waliopoteza“ na bado mkawaacha.Ukiweza kutetea hoja yako kwa kusema ni kwanini “hao waliopoteza zao“ bado wapo wapo ndo utakua umeonyesha kweli kwamba wanaume “WENGI“ kama unavyosema mwenyewe wanatilia maanani na kuthamini hizo bikira.
 
nilimwamini mwanzo, lakini nimekuja kugundua ni mzushi tu...... pale aliposema Richmond discussions BASI.... nikaona hee huyu Babu vipi?? kwanza umri umekwenda...hawezi kufikiri ... he cannot think, judge and decide....halafu bado yupo ndanwi ya CCM... huwezi kupigania haki ukiwa ndani ya CCM ya Leo...heb u atuondokee....
 
Mngekua mnazisaka na mnazitilia maanani hao “waliopoteza zao“ kama unavyowaita wote wangekua wake za watu kama ndio kigezo maana nao walikua nazo once na waliozitoa hawakuziona ni mali.Huwezi tu kusema mnazisaka (hapa sijui unaongelea wanaume wangapi) wakati nyie nyie ndio mliochukua za hao “waliopoteza“ na bado mkawaacha.Ukiweza kutetea hoja yako kwa kusema ni kwanini “hao waliopoteza zao“ bado wapo wapo ndo utakua umeonyesha kweli kwamba wanaume “WENGI“ kama unavyosema mwenyewe wanatilia maanani na kuthamini hizo bikira.
Mi naisaka kwa udi na uvumba, kama unayo nambie nitangaze ndoa!
 
6 ni mnyamwezi au msukuma, hawa jamaa wanatabia ya kutodhubutu kufanya sole decision. Ni waoga wanapenda kwenda kimakundi kama nyumbu wakiwatanguliza wengine wao wako nyuma. 6 hana uwezo wa kufanya kitu peke yake. Anayataka madaraka lakini anaogopa kuchukua risk ya kuikana ccm maana hana uhakika na matokeo ya maamuzi yake.

Mfano mwingine ni Mbunge mpiganaji wa Nzega Mzee Selelii aliyenyamazishwa kama moto uliomwagiwa maji ghafla.

Kutokana na uoga wa hili kabila amekaa kimya anasubiria hisani ya Jk labda ka ukuu wa wilaya au mkoa. Kama angekuwa mwanaume mwingine angeingia chadema na kulichukua jimbo lake bila jasho.

Wana siasa wa type hii hawawezi Kupambana na ccm hata kama wanajifanya kuipinga leo na kesho wanalazimishwa kwenda kuandamana mbeya wanakwenda.

6 hafai kuwa kwenye orodha ya wapiganaji nchi hii.

Huwezi kuwa ccm halafu ukajidai mpigananji. Wako wapi akina Mwakyembe na Eng. Manyanya? Kama kweli ni wapiganaji kwanini walikimbia CCJ.

Mkutano wa mbeya ulikuwa wa ccj nambayo ni nyumba ndogo ya ccm. Wanadhani 2015 ni zamu ya nyumba ndogo hiyo. Thubutu waatakutana na mizengwe ya kufa mtu ya JK mwaka huu ni wawenzetu wazanzibar au akina mama zetu!

Vyovyote itakavyokuwa iwe ni mke mkubwa au mdogo ccm haina mvuto tena!



.
 
Watanzania tunayo matatizo makubwa... Viongozi wetu hawana budi watupe mwelekeo wa kuweza kuyabadishi maisha yanayoeleka kuturudisha kwenye maisha ya karne ya kumi na mbili. Wimbo wa maamuzi magumu, kujivua gamba will not help us..

Nashukuru kwa JF. Hapa ndipo sebuleni kwangu siku hizi..
 
ATAKA WALIOSABISHA MGAWO WAWAJIBISHWEBrandy Nelson na Hawa Mathias,MbeyaSUALA la mgawo wa umeme unaoendelea nchini kote linazidi kuchukua sura mpya baada ya Waziri wa Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Samwel Sitta kutaka wote waliofikisha nchi kwenye mgawo huo wawajibishwe.Sitta alisema haitoshi kwa watu hao kuomba msamaha pekee kwa kulingiza taifa katika makali na kadhia ya mgawo huo unaoendelea kuporomosha uchumi wa nchi.Kauli ya Sitta imekuja wakati wabunge mjini Dodoma wakiwa wamebana Waziri wa Nishati na Madini, William Ngeleja wakitaka aeleze jinsi atakavyomaliza mgawo huo nchini baada ya kuwasilisha bajeti ya wizara yake juzi, vinginevyo hawataipitisha. Sitta akizungumza na Vijana wa CCM kutoka vyuo vikuu mkoani Mbeya jana alisema: “Ni lazima tuwaombe radhi Watanzania kwa kuwapo kwa mgawo wa umeme kwani hii siyo nchi ya kupata mgawo.”“Tunazo rasilimali nyingi ambazo zinaifanya Tanzania kuwa na umeme wa kuuza na siyo mgawo,” aliongeza Sitta.“Haitoshi kuwaomba radhi Watanzania lazima waliotufikisha kwenye mgawo wawajibishwe, hili lazima tutalishughulikia tunawaahidi lazima nchi yetu ibaki kuwa na heshima aliyoiacha Baba wa Taifa (Mwalimu Julius Nyerere), ”alisema Sitta.Sitta ambaye ameongozana na Naibu Waziri wa Ujenzi, Dk Harrison Mwakyembe (ambaye ni Mbunge wa Kyela), Mbunge wa Simanjiro, Christopher ole Sendeka, Mbunge wa Same Mashariki, Anne Kilango Malecela, alisema ili nchi iweze kurejea katika hadhi yake iliyokuwa nayo lazima utaratibu wa kuwajibishana urejewe.Wengine waliohudhuria kongamano hilo ni Naibu Waziri wa Viwanda Biashara na Masoko ambaye pia ni Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu, Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Mary Mwanjelwa, Mbunge wa Mbozi Mashariki, Godfrey Zambi na Mbunge wa Mbarali, Dickson Kilufi.Katika kongamano hilo pia, Sitta ambaye alikuwa Spika wa Bunge la Tisa alizungumzia jaribio la kutaka kuvuliwa uanachama wa CCM mwaka 2009, akisema kuwa kundi la watu wachache wenye fedha walitaka kutumia fedha zao kumng’oa na kumvua uanachama.“Nataka kuwaeleza haya matukio yapo ya kutaka kufukuzwa kwenye chama, kwani hata mimi nilitaka kufukuzwa na watu wenye fedha, lakini walishindwa, tunamshukuru Rais Jakaya Kikwete aligundua kuwa kuna ulazima wa kuvua gamba katika chama chetu,”alisema.“Nawapa matumaini katika chama chetu kuwa sisi mnaotuona hapa ndio tunaotumia akili siyo tumbo katika kufikiri, hivyo chama chetu kitakwenda vizuri,”aliongeza Sitta.Alisema kuna baadhi ya viongozi wa Serikali na wanachama wa CCM wanatanguliza ubinafsi, kwani hivi karibuni walidiriki hata kusafirisha wanyama na kuwapeleka nje ya nchi.“Hivi karibuni kuna wenzetu walisafirisha wanyama wetu aina ya twiga wapatao130 kuwapeleka Uarabuni, hii hali hatutaweza kukubaliana nayo, lazima tupambane,” alisema.Akijibu maswali ya wanafunzi hao, Sitta alisema kuhusu soko la ajira katika Jumuia ya Afrika Mashariki, vijana wategemee kuwapo kwa ajira hizo na kwamba watapimwa uwezo huku akiwahakikishia kuwa wapo watakaoajiriwa na kufanya kazi Kenya.Kuhusu ubinafsishaji wa shamba la Kapunga, wilayani Mbarali, Sitta alisema kuna uwezekano mkubwa kuwa baadhi ya viongozi wa Serikali wana mikono yao kwa wawekezaji na kwamba atahakikisha wakulima wanarudishiwa mashamba yao na wale waliohamishwa katika maeneo yao ili waendelee kujikita zaidi katika kilimo.Waziri Sitta alisisitiza kuwa hawezi kuvumilia viongozi wanaowalangua wananchi na anashangaa kuwekeza wakulima wakubwa“Huu ni upuuzi na hata sintoafiki ardhi yetu kuingiliwa kwa kuwanufaisha wachache na wenye nayo kuishi maisha duni,” alisema.Sitta na wenzake wapo mkoani Mbeya kwa ajili ya kukisafisha chama (CCM) na kujibu hoja mbalimbali ambazo zimekuwa zikitolewa na wapinzani kwa siku za karibuni.Katika hatua nyingine Katibu wa Itikadi,Siasa na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi Taifa (CCM), Nape Nauye amesema sumu ya nyoka aliyejivua gamba kazi yake ni kuwajibisha watendaji wote serikalini ambao kazi yao ni kushughulikia matumbo yao badala ya maendeleo ya Wananchi. Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Luanda Nzovwe jijini Mbeya alisema kumekuwepo na watendaji ambao wamekuwa wakitumia vibaya madaraka waliyonayo kwa kushughulikia matumbo yao na familia zao badala ya kufanya shughuli za umma. Alisema wananchi masikini ndiyo wamekuwa wakiumia kwa kuwa na maisha magumu huku CCM na serikali ikiwa imekamatwa na watu wachache ambao wamekuwa wakifuja mali za wananchi. “Misingi ya CCM inataka kukosoa na kukosoana bila unafiki hivyo ni lazima wale wote ambao wanafanya kazi kinyume na matakwa ya Watanzania na kusababisha wananchi wetu kuwa masikini, wawajibishwe.” “Walioko Serikalini atakayefanya vibaya tutamshughulikia kwani sisi tunataka kutatua kero za Wananchi hivyo tutawashughulikia kabla ya wananchi kutushughulikia sisi na chama chetu cha mapinduzi,”alisema. Kuhusu mgao wa umeme Nape alisema ni lazima Serikali ikiri “Tunaiagiza Serikali tunataka tatizo la umeme liishe kwani nchi kuwa gizani ni suala la aibu,”alisema. Naye Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara na Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu alisema saa imefika ya kurudisha viwanda na mashamba yaliyobinafsishwa kwa Wananchi ili waweze kunufaika na rasilimali zao. Alisema kuna viwanda na mashamba ambayo yamechukuliwa na wawekezaji, lakini wananchi wenye mali hizo hawanufaiki na rasilimali hizo huku wakishuhudia zikiwanufaisha watu wachache.
Wapendwa wana wa JF naomba mnikumbushe huenda nimesahau...ni line Sitta akiwa kama mbunge aliongea hayo aliyoyaongea mbeya? My feeling ni kwamba bungeni ndio sehemu sahihi za kujadili hoja hizo ambazo kwa kweli ni za msingi sana?
 
Mi naisaka kwa udi na uvumba, kama unayo nambie nitangaze ndoa!
Hayo ni mawazo yaliyoganda kwahiyo hata siku moja usitegemee mwanamke anaejielewa akaona ofa yako ni ya maana.Hiyo bikira haiishi milele na siyo itakayohangaika kulea ndoa.Nyie ndio wale mnao watu kwa sura zao siku akipata ajali tu mnakimbia!
 
Wana JF na declare kuwa Mbeya is my origin home. Hao wanachuo ni wakuja, inamaana mkutano haukuwa na mashiko kwa wakazi wa Mbeya. Sera za kizamani za kudanganya waTz, kuuza umeme nje wakati hata megawatt 800 hawajafikia miaka 50 ya uhuru. Kweli hii ni serikali legelege kuzidi hata Somalia. Mungu tuondolee hii laana ya CCM.
 
Mtanzania ya leo kwenye front page yenye font size ya 2000 wamesema,(Nanukuu) CCJ YAHAMIA MBEYA. Kwa hiyo list umeitaja hapo Mtanzania hawajakosea
 
Wana JF na declare kuwa Mbeya is my origin home. Hao wanachuo ni wakuja, inamaana mkutano haukuwa na mashiko kwa wakazi wa Mbeya. Sera za kizamani za kudanganya waTz, kuuza umeme nje wakati hata megawatt 800 hawajafikia miaka 50 ya uhuru. Kweli hii ni serikali legelege kuzidi hata Somalia. Mungu tuondolee hii laana ya CCM.
Mkuu kwa wanachuo kupewa kadi za CCM wala halinipi shida kwakuwa wakati nipo chuoni na mimi nilijidanganya, ofcourse nilidanganywa pia kuwa ukiwa nje ya CCM ukimaliza chuo hutapata kazi kwa urahisi. Jambo ambalo baadae nilithibitisha kuwa ni ujuha grade one. Hao vijana ngoja wawe mtaani, wakutane na mfumo kandamizi wa ccm kwenye kila nyanja, waone mfumo unavyowabagua wasionacho, nakuhakikishia hizo kadi watazichambia na kutafuta za chadema wenyewe.
 
Hayo ni mawazo yaliyoganda kwahiyo hata siku moja usitegemee mwanamke anaejielewa akaona ofa yako ni ya maana.Hiyo bikira haiishi milele na siyo itakayohangaika kulea ndoa.Nyie ndio wale mnao watu kwa sura zao siku akipata ajali tu mnakimbia!
Hahahahahaa! Babygal unanifurahisha, ongoa hofu bwana!
 
mkuu tunashukuru sana,umejaribu sana kutulia ili taarifa ieleweke,
naomba niseme neno moja tu,kujiuzulu kwa yule fisadi ndio chanzo cha mkutano wa mbeya,
hiyo ilishapangwa kwamba ajiuzulu ili wapate nafasi ya kupenya kwa wanachi
lakini wanashindwa kuelewa hawa wananchi walishawachoka long time ago
 
big up duble cris kwa detailed taarifa ya kilichojiri Mby jana. heading ya Mtanzania sijaiona but kama wameandika hivo live at least we are now moving. bado njia ni nyeupe kwa cdm
 
Mimi napenda used.
Haina usumbufu.
Haina kuleteana ubabe.
Yaingia bila shida.
Napenda used.
 
Aina ya wasomi tulionao bongo ni laana tupu. How comes wanafunzi 300 wa TEKU wanajiunga na CCM? Yaani wanashindwa hata na wasukuma mikokoteni ambao wanaweza kuyaona matatizo ya nchi na kuikimbia CCM? Hapa ndo naona kabisa ukombozi wa nchi hii upo mbali sana.
 
Sita hapo kaongea kisiasa tu... mtu yeyote kuongea aliyoyaongea sita angeweza... Story kibao hakuna la maana... Sasa kama wao ndo kati ya CCM wasafi kwa nini asiseme katika tatizo la umeme mimi kama member wa BARAZA la mawaziri natoa mapendekezo a, b, c, d... ambayo yakitekelezwa na serikali then hili giza litateketea kabisa....Ila yeye ni kusema wenzake tu!!!! MAJUNGU, FITINA na UZANDIKI....

Na kuhusu CCJ why didnt he come out clean b4 hajatajwa??? Kipindi kapewa PROPOSAL ya kugombea URAIS CCJ why in the next morning didn't tell us??? SIASA MAJI TAKA.... He is also filthy RICH possibly more than RA!!!!
 
Back
Top Bottom