Mkurugenzi Mkuu wa Mradi wa Mwendokasi analipwa zaidi ya milioni kumi kwa mwezi; hajawahi hata kutembelea abiria aone kero zao

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
877
4,105
Naambiwa mkurugezi wa mwendo kasi akijumuisha salary, posho, safari na usafiri kwa mwezi mmoja anatumia zaidi ya milioni kumi za wananchi.

Lakini pamoja na kulipwa fedha zote hizo bado hakuna siku amewahi kuonekana katika eneo la Mradi ambalo ni pungufu ya urefu wa kilomita 40. Yupo ofisini anasoma mafaili na kuidhinisha matumizi ya fedha.

Kwa ubosi alionao hata waziri anasubiri. Sambamba na kulipwa fedha zote hizo hataki anaamini Mradi wa Mwendokasi kubinafsishwa kwa mzawa hawataweza kuuendesha labda aletwe mchina au mzungu. Unajiuliza anafanya nini ofisini? Temekosa watu wakuwapa hii kazi?

Leo watanzania wanafanya biashara ya usafiri wa mabasi na hakuna kelele, watashindwa kusimamia Mwendokasi ambayo abiria wanasubiri masaa 2 hadi matatu kwa trip?

Mwendokasi ni jambo la kumuumiza kiongozi wa nchi kichwa? Mwoneni mama huruma ; acheni kumhujumu Mhe. Rais . Tokeni ofisini mkafanyr kazi aliyowatuma.
 
Madhara ya kuteuliwa kwa fadhila badala ya kupata kazi kwa vigezo. Kwani kuna anayejua ni sifa gani zimepelekea akateuliwa kwenye hiyo nafasi??
 
Naambiwa mkurugezi wa mwendo kasi akijumuisha salary, posho, safari na usafiri kwa mwezi mmoja anatumia zaidi ya milioni kumi za wananchi.

Lakini pamoja na kulipwa fedha zote hizo bado hakuna siku amewahi kuonekana katika eneo la Mradi ambalo ni pungufu ya urefu wa kilomita 40. Yupo ofisini anasoma mafaili na kuidhinisha matumizi ya fedha.

Kwa ubosi alionao hata waziri anasubiri. Sambamba na kulipwa fedha zote hizo hataki anaamini Mradi wa Mwendokasi kubinafsishwa kwa mzawa hawataweza kuuendesha labda aletwe mchina au mzungu. Unajiuliza anafanya nini ofisini? Temekosa watu wakuwapa hii kazi?

Leo watanzania wanafanya biashara ya usafiri wa mabasi na hakuna kelele, watashindwa kusimamia Mwendokasi ambayo abiria wanasubiri masaa 2 hadi matatu kwa trip?

Mwendokasi ni jambo la kumuumiza kiongozi wa nchi kichwa? Mwoneni mama huruma ; acheni kumhujumu Mhe. Rais . Tokeni ofisini mkafanyr kazi aliyowatuma.
VIONGOZI WENGI WA NCHI HII MASIKINI NDIVYO WALIVYO KWANI WABUNGE WANAOLIPWA MILIONI 16+ MAPOSHO ZAIDI YA KUKAA BUNGENI NA KUPITISHA MISWAADA KWENYE MAJIMBO YAO WANAFANYA NINI? HATA KUSURUHISHA MIGOGORO TU YA ARDHI HAWATAKI

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
 
Ogopa sana mambo ya nasikia, niliambiwa

Ukiambiwa utoe ushahidi huna utabaki ivo ivo kua nilisikia au niliambiwa

Hlf watu wanajiita GT nao wanasupport mada
 
Huo mradi wa mwendokasi ni pasua kichwa. Kuuzungumzia unahitaji ujasiri kiasi. Waziri Mchengerwa ameutembelea hivi karibuni tena akapanda kabisa hayo mabasi na hata mkuu wa mkoa Chalamila pia kautembelea hivi karibuni lakini hakuna mabadiliko yoyote. Mwendokasi wenyewe walishakuja hapo JF kuomba ushauri na GT wa JF wakawapa nondo za kutosha lakini hakuna hata moja lililotekelezwa. Kwa kifupi ni sikio la kufa magari yanazidi kupungua barabarani hakuna magari mapya yaliyoinginzwa na yaliyoharibika yamejazana Ubungo na Gerezani.

Kuna wakati najiuliza hivi mkuu wa mkoa, wakuu wa wilaya, wabunge, madiwani, mameya wote wapo hapo hapo Dar lakini wapo kimya hakuna ayeshtuka jinsi abiria wanavyogombania mabasi. Subiri sasa litokee la kutokea halafu raisi, makamu au waziri mkuu aende kuibua madudu ndio utashangaa kila mtu anajifanya kuwajibika. Na hali ikizidi kuendelea kama ilivyo sasa muda si mrefu kuna janga litakwenda kutokea wakati abiria wanapogombea kupanda magari machache yaliyopo. Kwani sasa hivi abiria anaweza kukaa kituoni zaidi ya hata ya saa moja hajapata usafiri hasa wale ambao hawana uwezo/nguvu za kugombania kupanda.

Kwa kifupi huo mradi aliunzisha Kikwete halafu Magufuli (RIP) akauendeleza wapewe maua yao. Walioachiwa sasa wanaenda kuumaliza. Wanachofanya sasa tofauti kabisa badala waongeze magari na kusimamiwa abiria wapande magari kwa utaratibu wao wanapiga rangi stendi/mabanda ya abiria kusubiria mabasi hata sijui ni akili ya wapi hiyo. Nahisi hapo kwenye kupiga rangi labda kuna kitu wananufaika.

Ukitafakari sana utaona wazi kuwa tuna tatizo kubwa la ubunifu na kutoa maamuzi. Hivi baadhi ya njia kwanini wasiwape wafanyabiashara hata kwa majaribio? Hivi ukimpa Azam/Mo/GSM labda njia moja tu ya Mbezi to Feri halafu ukampa labda Shabiby/Aboud/BM njia ya Morocco to Gerezani wao mwendkasi wakabaki na njia zilizobaki na mabasi ya mabovu shida ipo wapi? Si watapata tu pesa ya kutosha kupitia tozo kutoka kwenye hao wawekezaji wa ndani. Huu mradi hatakiwi kabisa mwekezaji toka nje kwani ni mradi ambao wawekezaji wa ndani wanaweza kuwekeza bila wasiwasi na kufanya vizuri tu. Ni sualal a kuweka tu mabasi mazuri yenye viyoyozi na utaratibu mzuri wa abiria kupanda kwa mistari vituoni na kusimamia idadi ya abiria wanaotakiwa ndani ya basi moja badala ya sasa kuweka walinzi kibao wanasinzia na kuchati na simu zao muda wote wawpo vituoni.

Mbaya zaidi serikali inaedelea kujenga njia ya Mbagala na Gongolamboto huku hii njia Mbezi inawatoa jasho. Anyway huwezi jua labda mbele ya safari huko watakuja viongozi wenye uwezo wa kufanya maamuzi sahihi kwa wakati.. Na iwapo serikali imeshindwa si vibaya ikakiri hivyo hadharani halafu ikaruhusu dala dala za kawaida zifanya kazi kama zamani kuliko haya mateso wanayopata abiria kwa sasa.

Hivi na hili wasaidizi wa raisi wanasubiri mama Samia aje awaelekeze cha kufanya hapana aisee hebu muhurumieni huyo mama.
 
Back
Top Bottom