Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
- Thread starter
- #21
SEHEMU YA 15
Ikapita wiki, kutokana na shughuli za kazi nyingi, nikawa kama nimeshamsahau rafiki yangu huyo, na nikawa na migongano ya hapa na pale ya kifamilia, ni kawaida, lakini safari hi ilizidi, maana mume wangu ratiba zake zikawa hazieleweki sio kama ilivyokuwa awali, tukawa tunabishana, lakini kwangu nilichukulia ni mambo na kawaida tu.
Basi siku moja nikapokea simu kutoka kwa huyo rafiki yangu, akaniambia kuwa anajiandaa kuondoka kwenda Zanzibar, kuna mambo muhimu anatakiwa kuyafuatilia
‘Mambo gani mbona mapema hivyo…?’ nikamuuliza
‘Kuna jambo natakiwa kwenda kulifanya, natakiwa kukabidhi kabidhi ofisi, kwani inawezekana nikasafiri kwenda kusoma nje ya nchi…niliwahi kukuambia kipindi fulani kuwa niliomba kwenda kusoma, sasa imetokea kipindi hiki na mimi siwezi kuachia hiyo nafasi,…’akasema nilitaka kumuuliza na mtoto vipi, nikasita yeye akasema
‘Na uzuri..haitakuwa muda wote, nitaweza kulea na kusoma, mfadhili wangu kasema hilo halina shida..kwahiyo sitakuwa na muda wa kukabidhi, nikimaliza likizo yangu ya maternity, yawezekana nikaondokea huku….’akasema
Ilinisthua kidogo, ikizingatiwa kuwa mtoto bado mdogo, sikumuulizia sana kuhus mtoto,…. kwasababu hapa kati kati tulifikia sehemu hatuelewani na yeye kabisa, alichoka na maswali yangu na hata kufikia kusema niache kumfuta fuata masiha yake na mtoto wake.., kauli hiyo ikaniudhi sana, ikabidi kweli nimuache na maisha yake. Hata hivyo kiukweli, sio kwasababu hiyo, ila sikuwa na muda wa kukutana naye mara kwa mara, majukumu yalizidi sana.
Tuliongea kidogo kwenye simu …tukamaliza hivyo tu, na sikuweza kumpigia tena , na siku mbili baadae akapiga yeye, nahisi ni pale aliponiona nipo kimia, akasema;
‘Rafiki yangu vipi, nilijua utakuja, kabla sijaondoka, si nilikupigia simu jamani, sawa najua labda, bado umenikasirikia,… lakini utakuja kuelewa tu, baadae, …ila nilikuwa na ombi moja kwako, kwa vile wewe nyumba yako ina nafasi naomba baadhi ya vitu vyangu nije kuviweka kwako maana hizi nyumba za kupanga nikiondoka, vitakuwa havina usalama kabisa....’akasema
Kiukweli mimi sikuwa na hasira kihivyo, hasira zangu ni za hapo kwa hapo..na ukiniudhi naweza kufanya jambo kubwa hapo hapo…baada ya hapo, mambo yamekwisha, ila …kiukweli naweza kufany ajambo baya huwezi amini,..mimi kwa hilo nilishaliondoa nafsini kwangu sikuwa na kinyongo na yeye,..nikasema hakuna shida, nyumbani kwangu ni kwake, nikazidi kumsisitizia kwa kusema;
‘Wewe ni rafiki yangu bwana, hakuna haja ya kuniomba, hapa ni nyumbani kwako pia, watoto wanakuulizia kila siku, wewe lete vitu vyako na wewe kama mkataba umekwisha kwenye hiyo nyumba haina haja ya kulipia tena, njoo ukae hapa, mapak siku ukiondoka, ...’nikamwambia.
‘Hapana, sina maana hiyo, na sitaweza kufanya hivyo, urafiki wangu usiwe mzigo kwako, umeshanisaidia mengi sana, kiasi kwamba najihisi vibaya, na ..hata sijui nitawezaje kulipia hayo,…. ninachokuomba kwa sasa ni hilo tu....’akasema.
‘Sawa hamna shida, wewe vilete wakati wowote utakapopata nafasi, au nikipta nafasi, hata kama wewe haupo ninaweza kuja au kutuma gari likaja kuvichukua haina haja ya kusumbuka sana, ila nitajitahidi nije kabla hujaondoka..’nikasema, nikiwa na mambo yangu mengi shughuli zangu, na sikutaka kuongea naye zaidi, hasa kuhusu maisha yake alishasema hataki nikikutana naye tuyaongelee maisha yake, hasa kuhusu mtoto na aliyezaa naye.
Kesho yake nikapata nafsi nikaona nimpitie kidogom, nijua kinachoendelea, na kama vitu hivyo sio vingi, na kaviandaa, basi ninaweza kuondoka navyo, kwa kukodi gari, sikutaka kumpigia simu, mimi mwenyewe nikaenda nyumbani kwake…kwa mbali niliona gari kama ya mume wangu, lakini sikuwa na uhakika kama ilitokea kwake, au ilikuwa inapita tu, na mume wangu alikuwa kwenye mkutano.
‘Hivi mkutano ulishamalizika,..au kuna mtu kamtuma na gari lake…?’ nikajiuliza, nikataka kupiga simu kwake, lakini ikaingia simu ya mteja wangu muhimu, nikajikuta naipokea kwanza, na nilipomaliza kuongea naye , nikiwa nimesimamisha gari nyumbani kwa rafiki yangu,..nikawa nimeshaua kumpigia simu mume wangu
Rafiki yangu alikuwa kasimama mlangoni kwake kunikaribisha, nikamsogelea tukasalimiana kama ada yetu, nikaingia ndani na swali la kwanza likawa hili.
‘Mtoto kalala…?’ nikamuuliza
‘Ndio….’ Akasema ile ya kulazimishwa, sio sauti kama ile niliyo-izoea, halafu akauliza
‘Hujakutana na….’akasita,kwani simu yake iliita, akaisikiliza kwanza kwa muda, akasema
‘Nimekuelewa hamna shida, lakini niache kwanza, sitaki, sikiliza, nilikuelezea, msimamo wangu basi…’akasema na kukata simu.
Alionekana kama ana hasira na hataki kuongea, akawa kama anataka kuniambia jambo lakini anasita, nilihisi hivyo, ila na mimi nikasimamia kwenye msimamo wangu kuwa sitamuuliza tena kuhusu maisha yake na mtoto, …kwa jinsi alivyo nilijua ana tatizo.
Baadae mtoto akawa analia, kwahiyo akaenda kumchukua, na kumnyonyesha alipomaliza, akanipa nimpakate ili aniandalie kinywaji, ndivyo tulivyozoeana , nilitaka kujiandalia mimi mwenyewe, maana anajua mimi ni mpenzi wa sharubati ya baridi,… lakini akasema hapana
‘Wewe mpakate mtoto ..hujamshika tokea siku ile….’akasema na mimi sikukataa nikamchukua mtoto.
Unajua mtoto wa mwenzako hakawii, sasa anageuza macho, anangalia, na sura halisi inaanza kuonekana, sura haikujificha alikuwa akifanana kila kitu na watoto wangu, maana watoto wangu wanafanana, ni wale mapacha wanaofanana kwa kila kitu, mimi akilini nikaweza hitimisho kuwa rafiki yangu atakuwa atakuwa katembea na mdogo wa mume wangu. Hata hivyo sikuweza kuvumilia nikamwambia;
‘Hapa sasa haijifichi kitu, lakini tuyaache hayo, lini unaleta hiyo mizigo, au nitafute mtu tupakie, kukurahisishia kazi…’nikasema
‘Haijifichi nini, usianze yale mazungumzo tena, nimefikiria kwa makini nimeona, ni bora iwe hivyo, libakie kama tulivyokuliana basi… sasa ibakie utakavyofikiria wewe inatosha,..’akasema.
‘Hamna shida, isiwe taabu, sasa unasemaje…?’ nikamuuliza
‘Nilitamtafuta ,mtu, kuna mambo sijayaweka sawa, kuna mtu ananisumbua akili yangu, sipo sawa, ila nimeshukuru kuwa umafika….’akasema
‘Ok, sawa mimi naondoka…’nikasema
‘Kuna kitu nilitaka kukuambia, lakini bado sijawa na uhakika, nataka nipate ushahidi halafu tutaongea….’akasema
‘Kuhusu nini….?’ Nikauliza
‘Nataka uwe na amani na hili jambo tulimaliza kabisa….’akasema
‘Jambo gani…?’ nikamuuliza
‘Kuhusu huyo mtu niliyezaa naye….’akasema
‘Sijakuelewa bado…na usiumize kichwa chako kabisa,..kama hutaki nijue haina shida, ..mimi nakujali sana, sitaki uumie, uwe na wakati mgumu kwa ajili yangu,…mimi nina amani kabisa, sina kinyongo na wewe, naahamu una sababu yako muhimu tu y akufany ahivyo….’nikasema
‘Unajua mimi linanisumbua sana, nimejaribu kuliwazia tukio zima la siku ile sijaweza kulithibitisha,…sijawa na uhakika ilikuwaje…’akasema
‘Tukio gani…?’ nikamuuliza
‘La kuipata hiyo mimba….’akasema
‘Mhh..sikuelewi, ...usinidanganye rafiki yangu..wewe sio mtu wa kubakwa, wewe sio mtu wa kufanyiwa tendo bila rizaa yako, nakufahamu sana, kwa hilo usinidanganya....’nikamwambia, ni kweli rafiki yangu ni mbabe, mjasiri na anajiamini, anaweza kupambana na midume, hata kama ni kwa kupigana ngumi.
‘Kwakweli siku ile, nilizidiwa, na sijui kwa vile nilitaka iwe hivyo, ndio maana sikujali, hata hivyo nikuambie ukweli, sikuwa nimepanga itokee hivyo, sio siku ambayo nilisema leo nataka nikafanye hivyo, hapana, ...ilitokea tu , na huenda ilipangwa iwe hivyo, kwa kifupi siwezi kukumbuka siku ile nililewa...’akasema.
‘Ulilewa, ulianza lini kunywa…?’ nikamuuliza
‘Siku hiyo hiyo…na nilijuta …na mara pili, nikarudia tena, ..na kilichotokea ndio nikasema sitakunywa tena,…najuta…’akasema
‘Wewe mtu…..ina maana ukinywa pombe…na wewe uliwahi kuapa kuwa katika vitu ambavyo hutaweza kuvitumia kimojawapo ni pombe…?’ nikamuuliza
Ikapita wiki, kutokana na shughuli za kazi nyingi, nikawa kama nimeshamsahau rafiki yangu huyo, na nikawa na migongano ya hapa na pale ya kifamilia, ni kawaida, lakini safari hi ilizidi, maana mume wangu ratiba zake zikawa hazieleweki sio kama ilivyokuwa awali, tukawa tunabishana, lakini kwangu nilichukulia ni mambo na kawaida tu.
Basi siku moja nikapokea simu kutoka kwa huyo rafiki yangu, akaniambia kuwa anajiandaa kuondoka kwenda Zanzibar, kuna mambo muhimu anatakiwa kuyafuatilia
‘Mambo gani mbona mapema hivyo…?’ nikamuuliza
‘Kuna jambo natakiwa kwenda kulifanya, natakiwa kukabidhi kabidhi ofisi, kwani inawezekana nikasafiri kwenda kusoma nje ya nchi…niliwahi kukuambia kipindi fulani kuwa niliomba kwenda kusoma, sasa imetokea kipindi hiki na mimi siwezi kuachia hiyo nafasi,…’akasema nilitaka kumuuliza na mtoto vipi, nikasita yeye akasema
‘Na uzuri..haitakuwa muda wote, nitaweza kulea na kusoma, mfadhili wangu kasema hilo halina shida..kwahiyo sitakuwa na muda wa kukabidhi, nikimaliza likizo yangu ya maternity, yawezekana nikaondokea huku….’akasema
Ilinisthua kidogo, ikizingatiwa kuwa mtoto bado mdogo, sikumuulizia sana kuhus mtoto,…. kwasababu hapa kati kati tulifikia sehemu hatuelewani na yeye kabisa, alichoka na maswali yangu na hata kufikia kusema niache kumfuta fuata masiha yake na mtoto wake.., kauli hiyo ikaniudhi sana, ikabidi kweli nimuache na maisha yake. Hata hivyo kiukweli, sio kwasababu hiyo, ila sikuwa na muda wa kukutana naye mara kwa mara, majukumu yalizidi sana.
Tuliongea kidogo kwenye simu …tukamaliza hivyo tu, na sikuweza kumpigia tena , na siku mbili baadae akapiga yeye, nahisi ni pale aliponiona nipo kimia, akasema;
‘Rafiki yangu vipi, nilijua utakuja, kabla sijaondoka, si nilikupigia simu jamani, sawa najua labda, bado umenikasirikia,… lakini utakuja kuelewa tu, baadae, …ila nilikuwa na ombi moja kwako, kwa vile wewe nyumba yako ina nafasi naomba baadhi ya vitu vyangu nije kuviweka kwako maana hizi nyumba za kupanga nikiondoka, vitakuwa havina usalama kabisa....’akasema
Kiukweli mimi sikuwa na hasira kihivyo, hasira zangu ni za hapo kwa hapo..na ukiniudhi naweza kufanya jambo kubwa hapo hapo…baada ya hapo, mambo yamekwisha, ila …kiukweli naweza kufany ajambo baya huwezi amini,..mimi kwa hilo nilishaliondoa nafsini kwangu sikuwa na kinyongo na yeye,..nikasema hakuna shida, nyumbani kwangu ni kwake, nikazidi kumsisitizia kwa kusema;
‘Wewe ni rafiki yangu bwana, hakuna haja ya kuniomba, hapa ni nyumbani kwako pia, watoto wanakuulizia kila siku, wewe lete vitu vyako na wewe kama mkataba umekwisha kwenye hiyo nyumba haina haja ya kulipia tena, njoo ukae hapa, mapak siku ukiondoka, ...’nikamwambia.
‘Hapana, sina maana hiyo, na sitaweza kufanya hivyo, urafiki wangu usiwe mzigo kwako, umeshanisaidia mengi sana, kiasi kwamba najihisi vibaya, na ..hata sijui nitawezaje kulipia hayo,…. ninachokuomba kwa sasa ni hilo tu....’akasema.
‘Sawa hamna shida, wewe vilete wakati wowote utakapopata nafasi, au nikipta nafasi, hata kama wewe haupo ninaweza kuja au kutuma gari likaja kuvichukua haina haja ya kusumbuka sana, ila nitajitahidi nije kabla hujaondoka..’nikasema, nikiwa na mambo yangu mengi shughuli zangu, na sikutaka kuongea naye zaidi, hasa kuhusu maisha yake alishasema hataki nikikutana naye tuyaongelee maisha yake, hasa kuhusu mtoto na aliyezaa naye.
Kesho yake nikapata nafsi nikaona nimpitie kidogom, nijua kinachoendelea, na kama vitu hivyo sio vingi, na kaviandaa, basi ninaweza kuondoka navyo, kwa kukodi gari, sikutaka kumpigia simu, mimi mwenyewe nikaenda nyumbani kwake…kwa mbali niliona gari kama ya mume wangu, lakini sikuwa na uhakika kama ilitokea kwake, au ilikuwa inapita tu, na mume wangu alikuwa kwenye mkutano.
‘Hivi mkutano ulishamalizika,..au kuna mtu kamtuma na gari lake…?’ nikajiuliza, nikataka kupiga simu kwake, lakini ikaingia simu ya mteja wangu muhimu, nikajikuta naipokea kwanza, na nilipomaliza kuongea naye , nikiwa nimesimamisha gari nyumbani kwa rafiki yangu,..nikawa nimeshaua kumpigia simu mume wangu
Rafiki yangu alikuwa kasimama mlangoni kwake kunikaribisha, nikamsogelea tukasalimiana kama ada yetu, nikaingia ndani na swali la kwanza likawa hili.
‘Mtoto kalala…?’ nikamuuliza
‘Ndio….’ Akasema ile ya kulazimishwa, sio sauti kama ile niliyo-izoea, halafu akauliza
‘Hujakutana na….’akasita,kwani simu yake iliita, akaisikiliza kwanza kwa muda, akasema
‘Nimekuelewa hamna shida, lakini niache kwanza, sitaki, sikiliza, nilikuelezea, msimamo wangu basi…’akasema na kukata simu.
Alionekana kama ana hasira na hataki kuongea, akawa kama anataka kuniambia jambo lakini anasita, nilihisi hivyo, ila na mimi nikasimamia kwenye msimamo wangu kuwa sitamuuliza tena kuhusu maisha yake na mtoto, …kwa jinsi alivyo nilijua ana tatizo.
Baadae mtoto akawa analia, kwahiyo akaenda kumchukua, na kumnyonyesha alipomaliza, akanipa nimpakate ili aniandalie kinywaji, ndivyo tulivyozoeana , nilitaka kujiandalia mimi mwenyewe, maana anajua mimi ni mpenzi wa sharubati ya baridi,… lakini akasema hapana
‘Wewe mpakate mtoto ..hujamshika tokea siku ile….’akasema na mimi sikukataa nikamchukua mtoto.
Unajua mtoto wa mwenzako hakawii, sasa anageuza macho, anangalia, na sura halisi inaanza kuonekana, sura haikujificha alikuwa akifanana kila kitu na watoto wangu, maana watoto wangu wanafanana, ni wale mapacha wanaofanana kwa kila kitu, mimi akilini nikaweza hitimisho kuwa rafiki yangu atakuwa atakuwa katembea na mdogo wa mume wangu. Hata hivyo sikuweza kuvumilia nikamwambia;
‘Hapa sasa haijifichi kitu, lakini tuyaache hayo, lini unaleta hiyo mizigo, au nitafute mtu tupakie, kukurahisishia kazi…’nikasema
‘Haijifichi nini, usianze yale mazungumzo tena, nimefikiria kwa makini nimeona, ni bora iwe hivyo, libakie kama tulivyokuliana basi… sasa ibakie utakavyofikiria wewe inatosha,..’akasema.
‘Hamna shida, isiwe taabu, sasa unasemaje…?’ nikamuuliza
‘Nilitamtafuta ,mtu, kuna mambo sijayaweka sawa, kuna mtu ananisumbua akili yangu, sipo sawa, ila nimeshukuru kuwa umafika….’akasema
‘Ok, sawa mimi naondoka…’nikasema
‘Kuna kitu nilitaka kukuambia, lakini bado sijawa na uhakika, nataka nipate ushahidi halafu tutaongea….’akasema
‘Kuhusu nini….?’ Nikauliza
‘Nataka uwe na amani na hili jambo tulimaliza kabisa….’akasema
‘Jambo gani…?’ nikamuuliza
‘Kuhusu huyo mtu niliyezaa naye….’akasema
‘Sijakuelewa bado…na usiumize kichwa chako kabisa,..kama hutaki nijue haina shida, ..mimi nakujali sana, sitaki uumie, uwe na wakati mgumu kwa ajili yangu,…mimi nina amani kabisa, sina kinyongo na wewe, naahamu una sababu yako muhimu tu y akufany ahivyo….’nikasema
‘Unajua mimi linanisumbua sana, nimejaribu kuliwazia tukio zima la siku ile sijaweza kulithibitisha,…sijawa na uhakika ilikuwaje…’akasema
‘Tukio gani…?’ nikamuuliza
‘La kuipata hiyo mimba….’akasema
‘Mhh..sikuelewi, ...usinidanganye rafiki yangu..wewe sio mtu wa kubakwa, wewe sio mtu wa kufanyiwa tendo bila rizaa yako, nakufahamu sana, kwa hilo usinidanganya....’nikamwambia, ni kweli rafiki yangu ni mbabe, mjasiri na anajiamini, anaweza kupambana na midume, hata kama ni kwa kupigana ngumi.
‘Kwakweli siku ile, nilizidiwa, na sijui kwa vile nilitaka iwe hivyo, ndio maana sikujali, hata hivyo nikuambie ukweli, sikuwa nimepanga itokee hivyo, sio siku ambayo nilisema leo nataka nikafanye hivyo, hapana, ...ilitokea tu , na huenda ilipangwa iwe hivyo, kwa kifupi siwezi kukumbuka siku ile nililewa...’akasema.
‘Ulilewa, ulianza lini kunywa…?’ nikamuuliza
‘Siku hiyo hiyo…na nilijuta …na mara pili, nikarudia tena, ..na kilichotokea ndio nikasema sitakunywa tena,…najuta…’akasema
‘Wewe mtu…..ina maana ukinywa pombe…na wewe uliwahi kuapa kuwa katika vitu ambavyo hutaweza kuvitumia kimojawapo ni pombe…?’ nikamuuliza