Abdallahking
JF-Expert Member
- Mar 19, 2018
- 3,983
- 10,804
Mkasa : MKUKI KWA NGURUWE
Mwandishi: MSUYA M MSUYA (EMUTHREE)
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES
SEHEMU YA 1
Ni kisa na mkasa, chenye mafunzo ndani yake, kinachotokana na ushauri wa kirafiki kati ya marafiki wawili. Ushauri uliokuja kuzaa mtafaruku hadi marafiki hawa wawili wakaja kuwa maadui makubwa wakutaka hata kuuana.
Ulikuwa ushauri wenye nia njema kwa mlengwa, lakini ….athari zake kwa wengine zinaumiza,…je hao wengine wakiwa ni wewe mshauri itakuwaje….
Hutapenda kuona rafiki yako akiteseka, utafanya kila hali ili aondokane na shida hiyo, njia mbadala zilishindikana, ikabakia wazo hilo...lililokujia akilini na kumshauri mwenzako, afanye tu, bila kuangalia upande mwingine wa athari zake….
Kisa hiki ni kumbukumbu za wale wanaoteseka, wenye shida mbali mbali, wenye mitihani ya maisha, wengine wakihitajia kuolewa lakini hawajapata wa kuoa au kuolewa, hawa wanahitajia ushauri, je tuwape ushauri gani…
Wapo wengine wakihitajia watoto, lakini mola hajawajalia,..au wapo wengine walitendwa na wenza wao, wakaachika, au kuachwa kwa namna moja au nyingine. Wapo waliovumilia..wapo walioshindwa kuvumilia,…, na wapo waliojikuta kwenye njia panda…je tuwapatia ushauri gani…
Kisa hiki hiki ni maalumu kwako wewe mtoa ushauri, na wewe mshauriwa…tuweni makini sana kwa dhamana hii ya ushauri! Ushauri sio kuongea tu kwa vile…sio wewe utayefanyiwa, sio wewe …hapana shauri ukijiweka kwenye hiyo nafasi , kama ingelikuwa ni wewe..ingelikuwaje…
Japokuwa unaweza ukatoa wazo hilo kwa nia njema kabisa, ukitaka kumsaidia mwenzako, lakini jiulize huyo atakayetendewa hataumia,…au kama ungelitendewa wewe ungakubali kutendewa, ….maana isije ikawa MKUKI NI KWA NGURUWE TU.
*************
Ilikuwa vigelegele vya shangwe, pale nilipofunga harusi yangu, kiukweli ilikuwa harusi kubwa, kutokana na hali zetu, na aliyesaidia kuhakikisha kila kitu kimekwenda sawa, alikuwa rafiki yangu kipenzi…
‘Rafiki yangu, mume wako ni bonge la handsome…hapo sitii kasoro, na nikuambie kitu, wewe usisumbuke kwa lolote lile, mwili wako na wangu kila kitu niachie mimi, muhimu ni gharama, nipatie fungu, na wewe kaa, tulia, kama ningelikuwa na pesa, nisingelipenda wewe utoe hata senti moja, lakini nitajitahidi…’akasema
‘Ujitahidi kwa vipi, usije kutoa hata senti yako moja, pesa ya harusi hii ilishaandaliwa kwa kila kitu, wewe isimamie tu, na kila kitu nitakukabidhi wewe, nashukuru sana rafiki yangu, wewe ni mimi na mimi ni wewe, …wewe ni rafiki yangu tunajuana, kwa kila hali, nisingelipenda wewe kujiingiza kwenye madeni,… unasikia, ukifanya hivyo utaniudhi…’nikasema
Basi yeye akasimamia kila kitu, nikaja nikafunga ndoa na mume wangu..na maisha na rafiki yangu yakawa ni pale pale, ila alichojitahidi kwa hivi sasa yeye akawa hafiki mara kwa mara nyumbani kwangu, kama ilivyokuwa awali, yeye alifika akiwa na uhakika mimi nipo nyumbani…nilimuelewa, na sio kwamba nilimshuku vibaya hapana ni yeye tu, aliona isje ikajenga fitina…’akaendelea kusimulia.
Masiku, miezi, miaka, ikaenda mimi nikajaliwa watoto, lakini rafiki yangu bado akawa hajaolewa , sio kwasababu kuwa hakupata wachumba, hapana, wachumba ni wengi waliotaka kumuoa, lakini yeye akawa hawakubali kutokana na sababu hii na ile, aliyoiona yeye. Na awali sikupenda kumuingilia sana kwa maamuzi yake hayo, maana ninamfahamu alivyo…ana msimamo wake.
Lakini siku zilivyozidi kwenda mbele ikabidi mimi niingilie kati, nakuumuliza yeye anataka mume wa namna gani, ..japokuwa nafahamu kwa jinsi tulivyokuwa tukiongea awali kabla ya kuolewa, kuwa yeye angelipenda mume wa namna hii na ile, na mimi nikawa namuelezea hivyo, lakini mimi nilipoolewa nikaja kugundua kuwa ndoto za akilini za kuwa utampata mume mwenye kila kitu unachokitaka ni ndoto tu, aghalabu kuwa kweli…
‘Nikuambie rafiki yangu ukweli, huyo mwanaume unayemtaka wewe hajazaliwa, huwezi kumpata mume wa kila kitu unachokitaka wewe, vingine vitakuja huko mbele kwa mbele, na vingine hutaweza kuvipata hadi kufa kwako, ndivyo maisha yalivyo…’nikamshauri siku za mwanzoni,…
‘Usijali rafiki yangu, ipo siku nitaolewa tu, na mume ninayemtaka mimi, hilo la kuwa hajazaliwa halipo,..wapo, ninajua wapo…nitasubiri, ipo siku nitampata , hata hivyo, kuolewa, ni kuolewa, …mimi mwenyewe bado nina malengo yangu..nisingelipnda kukimbilia kuolewa kwanza…’akasema
Maisha yakaenda hivyo, na umri ukakimbia, umri hausemi, …unashangaa sura inabadilika, na majina yababadilika, kijana inageuka mtu mnzima, dada, inageuka kuwa mdada, baadaye…, mama,…mama bila mtoto, baba bila mtoto, mawazo yanaanza kuingia akilini, mawazo..
***************
‘Rafiki yangu nilimpenda sana, tulianza urafiki tukiwa shuleni, na hata tulipoanza kazi, ninafahamu kuwa mimi nina uwezo kuliko yeye kihali, maisha ya familia yangu yalikuwa juu, mwenzangu alitokea familia ya chini, ninaweza kusema hivyo…’ akaendelea kusimulia
‘Mimi nilijitolea kwa kila niwezavyo, rafiki yangu awe kama mimi, kila nilipoweza, akiniambia au hata kama hajaniambia, nilijikuta namsaidia mwenzangu, ilifikia muda kila ninachonunua namnunulia na mwenzangu, kwahiyo tulikuwa kama mapacha..
‘Unajua ilikuwa sifanyi jambo mpaka nishauriane na yeye kabla sijafunga ndoa, na baada ya ndoa, ikaendelea hivyo, japokuwa mengine ya ndani ya ndoa ilibidi nisimuhusishe sana,….kama ujuavyo sheria za ndoa zilivyo.
‘Lakini hata nilipoolewa, sikuacha hiyo tabia, ya kusaidiana na yeye..ila ikafika muda natakiwa kuwa na familia yangu na mume wangu zaidi, hii hali iliniuma pale rafiki yangu anapokuja ananikuta mimi nipo na mume wangu, yeye hana…iliniuma sana, nilitamani huyo mume awe wetu sote, lakini mmh…hapo pagumu.
Baada ya ndoa mambo mengine yalijiweka yenyewe rafiki yangu, alianza kupanga muda wake, ni lini aje kwangu, au lini tukutane naye, hakupenda kuja nyumbani kwangu kama mimi sipo,…sio kwamba sikumiani kwa hilo…au hakupenda wakutane na mume wangu kupata chakula cha mchana bila ya mimi kuwepo, hadi mume wangu akaja kuniuliza ni kwanini;
‘Huyo rafiki yako, ni mwaminifu sana, unajua kuna siku nakutana naye, namuomba nimpeleke lunch, hataki, eti kisa hapendi ije kulete fitina , mkaja kukosana wewe na rafiki yako…, sasa mimi ni shemeji yake nitamfanya nini , eti hivi kweli inaweza mimi nikakusaliti wewe mke wangu, kwa rafiki yako kipenzi…’akasema.
‘Lakini nyie wanaume hamuaminiki,….mimi namuunga mkono kwa hilo,..hata hivyo mimi sina wasiwasi kamwe na rafiki yangu…’nikasema.
‘Ina maana mke wangu kwa kusema hivyo huniamini…?’ mke akamuuliza mke wake.
‘Sio swala la kuaminiana hapo, shetani ana mbinu nyingi, …na kwanini ujiweke kwenye rehani ya mitihani, kama unaweza kuikwepa ni bora kufanya hivyo, kuliko kujitwika mitihani hiyo,….’akasema mke
‘Ok, nimekuelewa sana mke wangu, lakini nikuulize kitu ni kwanini rafiki yako hakubali kuolewa, yeye ni mnzuri ana umbo la mvuto, anataka nini na umri unakwenda…?’ akaniuliza mume wangu.
‘Hata sijui, hajajaliwa bado, siku itafika, ataolewa, ni kweli umri umekwenda, na hata sijui nifanye nini ili ampate mume anayemtaka,…hata sijui…’nikasema.
Mwandishi: MSUYA M MSUYA (EMUTHREE)
Imeletwa kwenu na: BURE SERIES
SEHEMU YA 1
Ni kisa na mkasa, chenye mafunzo ndani yake, kinachotokana na ushauri wa kirafiki kati ya marafiki wawili. Ushauri uliokuja kuzaa mtafaruku hadi marafiki hawa wawili wakaja kuwa maadui makubwa wakutaka hata kuuana.
Ulikuwa ushauri wenye nia njema kwa mlengwa, lakini ….athari zake kwa wengine zinaumiza,…je hao wengine wakiwa ni wewe mshauri itakuwaje….
Hutapenda kuona rafiki yako akiteseka, utafanya kila hali ili aondokane na shida hiyo, njia mbadala zilishindikana, ikabakia wazo hilo...lililokujia akilini na kumshauri mwenzako, afanye tu, bila kuangalia upande mwingine wa athari zake….
Kisa hiki ni kumbukumbu za wale wanaoteseka, wenye shida mbali mbali, wenye mitihani ya maisha, wengine wakihitajia kuolewa lakini hawajapata wa kuoa au kuolewa, hawa wanahitajia ushauri, je tuwape ushauri gani…
Wapo wengine wakihitajia watoto, lakini mola hajawajalia,..au wapo wengine walitendwa na wenza wao, wakaachika, au kuachwa kwa namna moja au nyingine. Wapo waliovumilia..wapo walioshindwa kuvumilia,…, na wapo waliojikuta kwenye njia panda…je tuwapatia ushauri gani…
Kisa hiki hiki ni maalumu kwako wewe mtoa ushauri, na wewe mshauriwa…tuweni makini sana kwa dhamana hii ya ushauri! Ushauri sio kuongea tu kwa vile…sio wewe utayefanyiwa, sio wewe …hapana shauri ukijiweka kwenye hiyo nafasi , kama ingelikuwa ni wewe..ingelikuwaje…
Japokuwa unaweza ukatoa wazo hilo kwa nia njema kabisa, ukitaka kumsaidia mwenzako, lakini jiulize huyo atakayetendewa hataumia,…au kama ungelitendewa wewe ungakubali kutendewa, ….maana isije ikawa MKUKI NI KWA NGURUWE TU.
*************
Ilikuwa vigelegele vya shangwe, pale nilipofunga harusi yangu, kiukweli ilikuwa harusi kubwa, kutokana na hali zetu, na aliyesaidia kuhakikisha kila kitu kimekwenda sawa, alikuwa rafiki yangu kipenzi…
‘Rafiki yangu, mume wako ni bonge la handsome…hapo sitii kasoro, na nikuambie kitu, wewe usisumbuke kwa lolote lile, mwili wako na wangu kila kitu niachie mimi, muhimu ni gharama, nipatie fungu, na wewe kaa, tulia, kama ningelikuwa na pesa, nisingelipenda wewe utoe hata senti moja, lakini nitajitahidi…’akasema
‘Ujitahidi kwa vipi, usije kutoa hata senti yako moja, pesa ya harusi hii ilishaandaliwa kwa kila kitu, wewe isimamie tu, na kila kitu nitakukabidhi wewe, nashukuru sana rafiki yangu, wewe ni mimi na mimi ni wewe, …wewe ni rafiki yangu tunajuana, kwa kila hali, nisingelipenda wewe kujiingiza kwenye madeni,… unasikia, ukifanya hivyo utaniudhi…’nikasema
Basi yeye akasimamia kila kitu, nikaja nikafunga ndoa na mume wangu..na maisha na rafiki yangu yakawa ni pale pale, ila alichojitahidi kwa hivi sasa yeye akawa hafiki mara kwa mara nyumbani kwangu, kama ilivyokuwa awali, yeye alifika akiwa na uhakika mimi nipo nyumbani…nilimuelewa, na sio kwamba nilimshuku vibaya hapana ni yeye tu, aliona isje ikajenga fitina…’akaendelea kusimulia.
Masiku, miezi, miaka, ikaenda mimi nikajaliwa watoto, lakini rafiki yangu bado akawa hajaolewa , sio kwasababu kuwa hakupata wachumba, hapana, wachumba ni wengi waliotaka kumuoa, lakini yeye akawa hawakubali kutokana na sababu hii na ile, aliyoiona yeye. Na awali sikupenda kumuingilia sana kwa maamuzi yake hayo, maana ninamfahamu alivyo…ana msimamo wake.
Lakini siku zilivyozidi kwenda mbele ikabidi mimi niingilie kati, nakuumuliza yeye anataka mume wa namna gani, ..japokuwa nafahamu kwa jinsi tulivyokuwa tukiongea awali kabla ya kuolewa, kuwa yeye angelipenda mume wa namna hii na ile, na mimi nikawa namuelezea hivyo, lakini mimi nilipoolewa nikaja kugundua kuwa ndoto za akilini za kuwa utampata mume mwenye kila kitu unachokitaka ni ndoto tu, aghalabu kuwa kweli…
‘Nikuambie rafiki yangu ukweli, huyo mwanaume unayemtaka wewe hajazaliwa, huwezi kumpata mume wa kila kitu unachokitaka wewe, vingine vitakuja huko mbele kwa mbele, na vingine hutaweza kuvipata hadi kufa kwako, ndivyo maisha yalivyo…’nikamshauri siku za mwanzoni,…
‘Usijali rafiki yangu, ipo siku nitaolewa tu, na mume ninayemtaka mimi, hilo la kuwa hajazaliwa halipo,..wapo, ninajua wapo…nitasubiri, ipo siku nitampata , hata hivyo, kuolewa, ni kuolewa, …mimi mwenyewe bado nina malengo yangu..nisingelipnda kukimbilia kuolewa kwanza…’akasema
Maisha yakaenda hivyo, na umri ukakimbia, umri hausemi, …unashangaa sura inabadilika, na majina yababadilika, kijana inageuka mtu mnzima, dada, inageuka kuwa mdada, baadaye…, mama,…mama bila mtoto, baba bila mtoto, mawazo yanaanza kuingia akilini, mawazo..
***************
‘Rafiki yangu nilimpenda sana, tulianza urafiki tukiwa shuleni, na hata tulipoanza kazi, ninafahamu kuwa mimi nina uwezo kuliko yeye kihali, maisha ya familia yangu yalikuwa juu, mwenzangu alitokea familia ya chini, ninaweza kusema hivyo…’ akaendelea kusimulia
‘Mimi nilijitolea kwa kila niwezavyo, rafiki yangu awe kama mimi, kila nilipoweza, akiniambia au hata kama hajaniambia, nilijikuta namsaidia mwenzangu, ilifikia muda kila ninachonunua namnunulia na mwenzangu, kwahiyo tulikuwa kama mapacha..
‘Unajua ilikuwa sifanyi jambo mpaka nishauriane na yeye kabla sijafunga ndoa, na baada ya ndoa, ikaendelea hivyo, japokuwa mengine ya ndani ya ndoa ilibidi nisimuhusishe sana,….kama ujuavyo sheria za ndoa zilivyo.
‘Lakini hata nilipoolewa, sikuacha hiyo tabia, ya kusaidiana na yeye..ila ikafika muda natakiwa kuwa na familia yangu na mume wangu zaidi, hii hali iliniuma pale rafiki yangu anapokuja ananikuta mimi nipo na mume wangu, yeye hana…iliniuma sana, nilitamani huyo mume awe wetu sote, lakini mmh…hapo pagumu.
Baada ya ndoa mambo mengine yalijiweka yenyewe rafiki yangu, alianza kupanga muda wake, ni lini aje kwangu, au lini tukutane naye, hakupenda kuja nyumbani kwangu kama mimi sipo,…sio kwamba sikumiani kwa hilo…au hakupenda wakutane na mume wangu kupata chakula cha mchana bila ya mimi kuwepo, hadi mume wangu akaja kuniuliza ni kwanini;
‘Huyo rafiki yako, ni mwaminifu sana, unajua kuna siku nakutana naye, namuomba nimpeleke lunch, hataki, eti kisa hapendi ije kulete fitina , mkaja kukosana wewe na rafiki yako…, sasa mimi ni shemeji yake nitamfanya nini , eti hivi kweli inaweza mimi nikakusaliti wewe mke wangu, kwa rafiki yako kipenzi…’akasema.
‘Lakini nyie wanaume hamuaminiki,….mimi namuunga mkono kwa hilo,..hata hivyo mimi sina wasiwasi kamwe na rafiki yangu…’nikasema.
‘Ina maana mke wangu kwa kusema hivyo huniamini…?’ mke akamuuliza mke wake.
‘Sio swala la kuaminiana hapo, shetani ana mbinu nyingi, …na kwanini ujiweke kwenye rehani ya mitihani, kama unaweza kuikwepa ni bora kufanya hivyo, kuliko kujitwika mitihani hiyo,….’akasema mke
‘Ok, nimekuelewa sana mke wangu, lakini nikuulize kitu ni kwanini rafiki yako hakubali kuolewa, yeye ni mnzuri ana umbo la mvuto, anataka nini na umri unakwenda…?’ akaniuliza mume wangu.
‘Hata sijui, hajajaliwa bado, siku itafika, ataolewa, ni kweli umri umekwenda, na hata sijui nifanye nini ili ampate mume anayemtaka,…hata sijui…’nikasema.