Mkoa wa Tabora kugawanywa na kuwa mikoa miwili

Ukiuangalia mkoa wa Tabora utagundua ni mkubwa mno kieneo hata kiwilaya kuna Urambo, Kaliuwa, Nzega, Igunga, Manonga, Sikonge, Uliankuru na kadhalika, itafaa ukigawanywa.

Na mimi labda nitabahatisha ukuu wa mkoa.
Kuna faida gani ya kuugawa wakati kodi yoote inayokusanywa inaenda dodoma?
 
Hizi bangi hizi za mtu mweusi,hakuna tija ya kiuchumi ya kugawa mkoa,Kwanza haiingezi kipato kwa nchi, zaidi inaongeza matumizi tu, RC, DED.

Cha muhimu mungewaza kwamba viwanda vya kutengeneza matairi ya gari, au viwanda vya nondo au saruji, au sukari havitoshi, tuongeze viwe vingi, ili tutengeneza mapato, nyie mnawaza kuteuliwa. Bora kuongeza hospitari, vyuo vya Elimu ya juu, au kufungua campus ya UD mkoani Tabora, au Bora mseme, hatuwezi kutegemea mvua kwa kilimo, sasa tuje na mpango wa kutumia maji ya ziwa victoria kufanya umwagiriaji.

Mkoa wa Tabora, unatumia maji ya victoria, lakini na yenyewe ni mgao,maana mkoa hauna mapato ya kuwezesha kutembwza pump 24/7.
Hakuna faida ya kuongeza mkoa, ukisema unasogeza huduma kwa jamii, kwani eneo linaongezeka? Geographical area ipo vile vile, kuongeza mkuu wa mkoa. Kuna msaidia vipi mwananchi wa kawaida, sie hatutski kuona sura, tunataka huduma, vituo vya polisi, barabara, Elimu, afya.
Mindset is everything
 
Ukiuangalia mkoa wa Tabora utagundua ni mkubwa mno kieneo hata kiwilaya kuna Urambo, Kaliuwa, Nzega, Igunga, Manonga, Sikonge, Uliankuru na kadhalika, itafaa ukigawanywa.

Na mimi labda nitabahatisha ukuu wa mkoa.
Jiografia darasa la ngapi kufundisha kuwa mkoa wa Tabora kuna wilaya zinazoitwa Manonga ama Ulyankulu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hivi kuna improvement kwenye maisha ya wananchi sehemu ambazo wamegawa mikoa na wilaya? mwenye mfano atusaidie hapa.

Kitu cha uhakika wakigawa mikoa na wilaya japo si la mara zote, ni watu fulani kunufaika kwa tenda za ujenzi wa makao makuu ya wilya au mkoa husika. Guest House au Lodge za waheshimiwa kupata biashara ya uhakika wakati wilaya au mkoa unaanzishwa sehemu fulani ambako tayari wametegesha vitu vyao.

Hizo hela za wilaya au mkoa mpya wakipeleka kwenye huduma za afya au mashule katika maeneo hayo itakuwa bora zaidi.

Kama unataka kuona faida ya kugawa Mikoa nenda kaone Chato ambako hata vipofu wameona, hebu fikiria wakti ule Bariadi ilivyokuwa wilaya ndani ya Mkoa wa Shinyanga ni jinsi gani watu walipata shida kufuata mahitaji ya kiutawala?

Au fikiria mtu wa Bukene/Nzega anapataje kutatua shida za kiofisi Tabora mjini au chukulia mfano wa mtu aliyeko Igunga anasafirije siku mzima kufika Tabora na kutatua mambo yake ya kiofisi?
 
Tabora likubwa jinga haliendei, sijui kwanini serikali imekaa kimya, why wasimege nusu ya eneo ikawapatia Shinyanga/Kahama na Singida!!!
 
Mkuu hatugawi kulingana na km squire bali ni population density ya eneo na demographic distribution data.
 
Mkuu usiusahau mkoa wa Morogoro, nao ni balaa. Ukubwa wa mkoa wa Morogoro ni sawa na Burundi+Rwanda.
 
Haya maujinga yalianzishwa na mwenda zake hata kama vigezo havikuwepo jamaa alitaka tu kulazimisha ndiomaana alianza na uwanja wa ndege kabisa
 
Sekretarieti ya Mkoa wa Tabora imependekeza kuugawa Mkoa wa Tabora ugawanywe na kuwa mikoa miwili ,kutokana na ukubwa kuliko yote nchini,kwa lengo la kutoa huduma kwa wananchi kwa urahisi na ufanisi zaidi.

Akisoma mapendekezo hayo, Katibu Tawala wa Mkoa wa Tabora , Bibi Kudra Mwinimvua amesema, Mkoa wa Tabora una eneo la Kilomita za mraba Elfu-75 na 865, ukiwa na wakazi milioni- 2, laki 2 Elfu-91 na 623.

Unapendekezwa kugawanywa katika mikoa ya Tabora ukiwa na wilaya saba na mkoa wa Nzega ukiwa na wilaya nne.

Naufahamu mkoa wa Tabora...

Ni kweli ni Mkubwa, lakini sehemu kubwa ni mapori yasiyokuwa na wakazi...

Ni ukweli kwa ujumla ni mkoa wenye wakazi milioni 2.5 (labda)..

Hata hivyo watu hawa wengi wako mijini. Sehemu kubwa ya eneo la mkoa wa Tabora ni wazi likiwa na misitu na mapori tu..

Hakuna haja ya kuugawa mkoa. Haukidhi vigezo...
 
2,091,863 / 2= 1,045,932 ndio idadi ya watu kila mkoa wanaotarajiwa kudogezewa huduma.
Gharama ni kubwa kuliko faida, ikizingatiwa kuwa hakuna vyanzo vya mapato vinavyoeleweka
 
Naufahamu mkoa wa Tabora...

Ni kweli ni Mkubwa, lakini sehemu kubwa ni mapori yasiyokuwa na wakazi...

Ni ukweli kwa ujumla ni mkoa wenye wakazi milioni 2.5 (labda)..

Hata hivyo watu hawa wengi wako mijini. Sehemu kubwa ya eneo la mkoa wa Tabora ni wazi likiwa na misitu na mapori tu..

Hakuna haja ya kuugawa mkoa. Haukidhi vigezo...

Wakate nusu wapewe Shinyanga/Kahama na Singida. Tabora ilitakiwa wawe na eneo dogo sana kulingana na poulation na uchachu wa maendeleo.

Dar kwa eneo ni dogo sana kwa tbr na population yao ni kubwa may be mara tatu ya tbr, akili kweli hii!!! Mwanza eneo dogo kwa tbr na population yao iko juu + maendeleo,akili kweli hii!!! Mbeya pia eneo dogo kwa tbr akili kweli hii!!! Serikali wafanye kila namna wakate nusu ya eneo wapewe Shinyanga/Kahama na Singida.
 
Huduma za jamiii jamani ziwafikie wanachi naungana sekretariet ya mkoa kwa mapendokezo yao kuugawa mkoa wa tabora ni mkoa mkubwa sana.wewe ambae unabisha bisheni kwa hoja jamani na so kujibu hovyo kama hamjisikii kuchangia mada
Ya msingi kama hiyo ni afadhali ukalale tu
Kuna mikoa midogo kieneo lakin huduma za wananchi HAKUNA.. Kwahiyo nayenyewe waigawe? Mi nadhan wilaya zote ziitwe mikoa na tarafa ziwe wilaya... Na kata ziwe tarafa, na vijiji viwe kata, na vitongoji viwe vijiji Ili mfurahi... Maana ni upumbavu mnatuletea kila wakati... Eti kuwasogezea wananchi maendeleo..MAENDELEO YANAKUJA KWA KUFANYA KAZI KUWA WABUNIFU NA KUWATUMIKIA WANANCHI..

Sent from my TECNO F2 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom