Nikiangalia kwa haraka haraka tatizo la miuondo mbinu ni kama linakaribia kumalizika kwa upande wa barabara hasa ambapo sasa zimebakia KM15 kama ulivyosema, na kwa upande wa bandari pamoja na bandari ya Lindi kujaa michanga , mpo jirani na Bandari kubwa ya asili yenye kina kirefu ya Mtwara, kwani mna tatizo la kutosafirisha mazao sababu ya miundo mbinu kama mikoa ya Katavi na Rukwa? sioni kwa namna gani hili linaweza kuwa kipaumbele muhimu kwa nyakati zijazo labda ni za kutoka vijijini na wilayani?
Umeeleza suala la kuanzisha shule za sayansi kwa wingi ili kutoa ajira nyingi kwenye gesi asilia, sina uhakika kama una takwimu za wanafunzi wanaomaliza shule kwa mwaka iwe msingi, sekondari za chini na juu, maana mkoa wa Lindi ni miongoni mwa mikoa yenye watu wachache pamoja na ukubwa wa eneo lake, hivyo hali kadhalika inaweza kuwa hata na wanafunzi wanaomaliza kwa mwaka. Vile vile mkae mkikumbuka sekta hii ya gesi ni ya kimataifa zaidi hivyo ushindani wake kwenye soko la ajira ni mpana na mrefu. Ni kweli elimu hii ya gesi ndiyo iwe ya kipaumbele kwa hapo kaibuni? au kwenye maeneo mengine?
Lakini nina wasiwasi na uwezo wenu wa kuzalisha mazao ya chakula, maana baa la njaa hugonga hodi kila mara, vile vile hata na uzalishaji wa mazao ya ufuta, korosho, ambayo inaweza kuwa inatokana na kilimo duni na wa kimaskini.