Mkoa wa Lindi: Historia na Taarifa Muhimu

Mkoa wa Lindi: Historia na Taarifa Muhimu

Hiko ni kilio chetu cha mda mrefu kiukweli barabara ya nachingwea liwale ni kero ya mda mrefu.. Mpk sasa serikali inatupiga danadana tu na hatujui hatim yake kama unavyojua watawala wa nchi yetu walivyojaa maneno kuliko vitendo ila nimesikia upo mpango wa kuweka lami masasi~nachingwea~liwale
Serikali ingefanya vyovyote ijuavyo kuinganisha barabara ya Masasi-Nachingwea kwa lami kufanya urahisi wa usafirishaji wa mazao kingine wangeunganisha barabara ya Nach-Nanganga kwa lami ingekuwa urahisi wa usafirishaji wa mazao maana kwa Lindi wilaya zilimazo sana ni Nachingwea,Liwale na Ruangwa.
 
Me nataka kujua kuhusu yule dinosaur wa ujerumani, je ni kweli alitoka lindi? Pia ni kwel kuna mwaka walitaka kumrudisha bongo?
 
kama unavyojua Nchi yetu hii kila raia anaruhusiwa kuishi popote na kufanya shughuli zake ili mradi afuate sheria na taratibu
yapo makabila mengi ila makabila ya asili ya mkoa wa Lindi ni
WAMWERA WAMAKUA WAMAGINGO WAMAKONDE WAMATUMBI WANGINDO WAYAO n.k

kwa upande wa wilaya mkoa wa lindi unaundwa na wilaya 6 ambazo ni NACHINGWEA. RUANGWA. LIWALE. KILWA. LINDI VIJIJINI. LINDI MANISPAA
nyongeza hapo mkuu; wamagingo na wangindo ni kabila moja tu na wanapatikana wilayani liwale. utofauti huo wa majina ni utofauti uliojitokeza katika matamshi tu baina ya lugha yenyewe ya kingindo na lugha ya kiswaahili
 
Nasikia kuna jiwe linaitwa 'jiwe la mzungu',je ni kweli lipo na kama lipo naomba historia yake!
 
ram binafs sijui mama salmer anatoka kijij gan.ila Lindi makabila yapo mengi,maarufu ni wamakua na wayao,na wasichana bado wanachezwa kama kawaida,umaskin bado upo tena mkubwa tu,ila ubovu wa miundombinu pia tatizo,maana kaz wanafanya(wanalima sana) wananyonywa

Lakini Wamakua wengi wapo wilaya ya masasi na wayao wengi Tunduru... wilaya kama Nachingwea, Ruangwa, Liwale, Lindi vijijini hasa kuanzia Mtua, Nyengedi hadi kule Rondo kwakina Membe, Mtama,Nyangao,Nangaga.. huku wengi ni Wamwera... Kilwa wamejaa Wangindo na Wamatumbi.

So asilimia kubwa ya Wenyeji wa mkoa wa Lindi ni Wamwera,Ngindo,Matumbi.
Makua na Yao wapo wengi lakini wanatoka Ruvuma na Mtwara.

Wamakonde wa Lindi na ukanda wa pwani hadi Mtwara wanaitwa Wamaraba na kimakonde chao ni cha kipwani kinechanganyika na kiswahili.
 
Last edited by a moderator:
Nasikia nyerere aliidhoofisha eneo hilo sababu ni la waislam kwani nasikia ulijengwa vizuri na waarabu na wajeruman pia nasemea kilwa (si sehemu ya lindi)?
 
Kama ilivyo mikoa mingine.. Huduma bora za jamii kwa kawAida hupatikana maeneo ya mjini hasa ktk makao makuu ya mikoa na wilaya mfn lindi mjini kilwa mjini. Nachingwea mjini. Liwale mjini na ruangwa mjini.. Hata hivyo zipo pia common challenges ktk utoaji wa huduma hizo ktk maeneo ya mjini

kwa upande wa vijijin vipo vijiji vilivyokua kiuchumi na hata huduma zake za kijamii zinaridhisha nitavitaja baadhi ya vijiji ktk mkoa mzima wa lindi ktk wilaya zote jumla ambavyo kidogo navifahamu vinatoa huduma za kuridhisha kwa wastani

Mchinga-Lindi. Mnazi mmoja~lindi. Ngongo~lindi. Nyangao~lindi. Mtama~lindi. Kiwalala~lindi. Nyengedi~lindi. Rondo~lindi. Nangulukuru~kilwa. Nkowe~ruangwa. Namikango~nachingwea. Lionja~nachingwea. Nangano~liwale. Kibutuka~liwale. Mnero~nachingwea. Luponda~nachingwea. Kilimarondo~nachingwea. Likotwa~Lindi. Mtandi~lindi. Matangini~nachingwea. Mandawa~ruangwa. Mbekenyera~ruangwa. Likunja~ruangwa. Nandagara~ruangwa. Nnacho~ruangwa. Nangumu~ruangwa. Micheka~ruangwa. Matambalare~ruangwa. Ng'apa~lindi. Marambo~nachingwea. Naipanga~nachingwea. Namupa~lindi. Milui~Ruangwa. Mitwero~lindi. Mandai~ruangwa

N.k... Hivyo ni baadhi ya vijiji ambvyo mimi nimewahi kufika nikaridhishwa na angalau ktk utoaji wa huduma zake ikiwemo afya. Maji. Umeme n.k...

Mkuu umenena ukweli na ukiangalia hivyo vijiji tajwa ni kwavile wa missionari walikaa hapo na kuna hali ya hewa nzuri na vyanzo vya uhakika kama maji vijiji kama
Mnero- Kuna hospitali ya Mission

Kiwalala/Narunyu hadi Mtua -- Kuna wamissionari wanaishi kule hadi leo kuna umeme , mashamba na mifugo yao na maji yapo kwa wingi, na kuna sehemu wa Sweedish wanaishi hadi leo na panaitwa Sweeden ni porini mbali kutoka barabarani ila ni kuzuri mno..

Mtama pamechangamka kwavile ni barabarani na kuna shule kongwe ya sekondari na ndio imebeba jina la jimbo analoongoza mh. Membe.

Nyangao pia kuna hali ya hewa nzuri na kuna hospitali kongwe na Maarufu kusini ikiifatia Ndanda ingawa hii ni bora zaidi.. na shule zipo inshort kuna huduma zote za kijamii na ipo barabarani pia.

Namupa nako huduma za jamii zipo maana kuna wamisionari na ndio kuna Seminari pekee ya kikatoliki kwa Kanda ya kusini Mtwara na Lindi ingawa ipo seminari nyingine ila bado ni changa na ni ya jimbo la Tunduru-Masasi.

Nkowe pia kuna huduma za kijamii hosp, shule n.k kwavile kuna Wamissionari pia pale Parokiani Nkowe.

Mbekenyera Nako pia jivyohivyo kunawamissionari wanakanisa kule na huduma zinapatikana na kuna shule hadi ya A level

Malambo nako si haba kuna maendeleo na Chiola pia.
 
Kinachonishangaza kwa nini mkoa huu haujafunguka katika tasnia ya habari na upashanaji habari. Tunaulizia habari za mkoa huu kana kwamba mkoa huu upo huko Kandahar, kuna "gap" kubwa sana ya uhabarishaji wa mambo ya uchumi na jamii, hauoni kuwa ni moja ya vipaumbele mnavyotakiwa kuvifanyia kazi katika kutangaza fursa, na vivutio kwa wawekezaji wa ndani na nje ya nchi?
 
Serikali ingefanya vyovyote ijuavyo kuinganisha barabara ya Masasi-Nachingwea kwa lami kufanya urahisi wa usafirishaji wa mazao kingine wangeunganisha barabara ya Nach-Nanganga kwa lami ingekuwa urahisi wa usafirishaji wa mazao maana kwa Lindi wilaya zilimazo sana ni Nachingwea,Liwale na Ruangwa.

Distance ya Masasi - Nachingwea ni fupi mno mwendo wa nusu saa tu kwa coaster ila tiseme si uzembe tu wa serikali ni uzembe wa Mkoa wa Lindi kwa ujumla mbona mtwara wanaweza. Ukiangalia hicho kipande kutoka Masasi hadi Lukuledi ambapo ni mpaka wa Mkoa wa Mtwara na Lindi utaona upande wa Mtwara kuna lami japo imeishia pale Masasi girls tu ila kutoka pale utaona barabara ikichongwa na kuwekwa kifusi mpaka Lukuledi.

Ila ukianza Lukuledi mpaka ufike Nachingwea mjini pori vichaka tu barabara imezongwa na nyasi kama sio ya wilaya vile.Wananchi wawajibishe viongozi wao mbona Barabara Kutoka Nanganga hadi Ruangwa kupitia Likunja na kutoka pale Likunja kwenda Nachingwea kupitia Chiola atleast imechongwa vizuri, na ni mwendo wa 2hrs kutoka Ruangwa kwenda Nachingwea kwa bodaboda.
 
Mkuu umenena ukweli na ukiangalia hivyo vijiji tajwa ni kwavile wa missionari walikaa hapo na kuna hali ya hewa nzuri na vyanzo vya uhakika kama maji vijiji kama
Mnero- Kuna hospitali ya Mission

Kiwalala/Narunyu hadi Mtua -- Kuna wamissionari wanaishi kule hadi leo kuna umeme , mashamba na mifugo yao na maji yapo kwa wingi, na kuna sehemu wa Sweedish wanaishi hadi leo na panaitwa Sweeden ni porini mbali kutoka barabarani ila ni kuzuri mno..

Mtama pamechangamka kwavile ni barabarani na kuna shule kongwe ya sekondari na ndio imebeba jina la jimbo analoongoza mh. Membe.

Nyangao pia kuna hali ya hewa nzuri na kuna hospitali kongwe na Maarufu kusini ikiifatia Ndanda ingawa hii ni bora zaidi.. na shule zipo inshort kuna huduma zote za kijamii na ipo barabarani pia.

Namupa nako huduma za jamii zipo maana kuna wamisionari na ndio kuna Seminari pekee ya kikatoliki kwa Kanda ya kusini Mtwara na Lindi ingawa ipo seminari nyingine ila bado ni changa na ni ya jimbo la Tunduru-Masasi.

Nkowe pia kuna huduma za kijamii hosp, shule n.k kwavile kuna Wamissionari pia pale Parokiani Nkowe.

Mbekenyera Nako pia jivyohivyo kunawamissionari wanakanisa kule na huduma zinapatikana na kuna shule hadi ya A level

Malambo nako si haba kuna maendeleo na Chiola pia.

Para ya nne kutoka chini; usiisahau ABBEY ya pale ndanda nayo inapatikana hukohuko kusini nadhan Ndanda kama sikosei
 
Para ya nne kutoka chini; usiisahau ABBEY ya pale ndanda nayo inapatikana hukohuko kusini nadhan Ndanda kama sikosei

Yeah naifahamu ila Ndanda ni Mkoa wa Mtwara ndio maana nikaiacha kusudi. Ila tungezungumzia general ningeitaja ingawa kwa upande wa wamissionari wamejenga sana vituo vya elimu na afya Mkoa wa Lindi hasa vijijini tofauti na Mtwara ila Mkoa wa Lindi umekuwa nyuma kimaendeleo na Elimu kushinda Mtwara. Ingawa wasomi na viongozi wengi wa zamani wanatoka mkoa huu ukilinganisha na Mtwara ila tatizo la watu wa Lindi hawapendi kurudi kwao mtu akishatoka ana hama na familia kabisa kuja mjini.
 
Mkuu umenena ukweli na ukiangalia hivyo vijiji tajwa ni kwavile wa missionari walikaa hapo na kuna hali ya hewa nzuri na vyanzo vya uhakika kama maji vijiji kama
Mnero- Kuna hospitali ya Mission

Kiwalala/Narunyu hadi Mtua -- Kuna wamissionari wanaishi kule hadi leo kuna umeme , mashamba na mifugo yao na maji yapo kwa wingi, na kuna sehemu wa Sweedish wanaishi hadi leo na panaitwa Sweeden ni porini mbali kutoka barabarani ila ni kuzuri mno..

Mtama pamechangamka kwavile ni barabarani na kuna shule kongwe ya sekondari na ndio imebeba jina la jimbo analoongoza mh. Membe.

Nyangao pia kuna hali ya hewa nzuri na kuna hospitali kongwe na Maarufu kusini ikiifatia Ndanda ingawa hii ni bora zaidi.. na shule zipo inshort kuna huduma zote za kijamii na ipo barabarani pia.

Namupa nako huduma za jamii zipo maana kuna wamisionari na ndio kuna Seminari pekee ya kikatoliki kwa Kanda ya kusini Mtwara na Lindi ingawa ipo seminari nyingine ila bado ni changa na ni ya jimbo la Tunduru-Masasi.

Nkowe pia kuna huduma za kijamii hosp, shule n.k kwavile kuna Wamissionari pia pale Parokiani Nkowe.

Mbekenyera Nako pia jivyohivyo kunawamissionari wanakanisa kule na huduma zinapatikana na kuna shule hadi ya A level

Malambo nako si haba kuna maendeleo na Chiola pia.

duh hayo maeneo uliyoyataja yamenisisimua maana miaka ya 1990's nimechepitapita sana
 
nyongeza hapo mkuu; wamagingo na wangindo ni kabila moja tu na wanapatikana wilayani liwale. utofauti huo wa majina ni utofauti uliojitokeza katika matamshi tu baina ya lugha yenyewe ya kingindo na lugha ya kiswaahili

MTIMBO Ruangwa kijijini kwetu huko.
 
Yeah naifahamu ila Ndanda ni Mkoa wa Mtwara ndio maana nikaiacha kusudi. Ila tungezungumzia general ningeitaja ingawa kwa upande wa wamissionari wamejenga sana vituo vya elimu na afya Mkoa wa Lindi hasa vijijini tofauti na Mtwara ila Mkoa wa Lindi umekuwa nyuma kimaendeleo na Elimu kushinda Mtwara. Ingawa wasomi na viongozi wengi wa zamani wanatoka mkoa huu ukilinganisha na Mtwara ila tatizo la watu wa Lindi hawapendi kurudi kwao mtu akishatoka ana hama na familia kabisa kuja mjini.

Mi nimeanzisha kampeni, mwaka jana mwezi wa saba nilihamasisha ukoo wetu tukachanga tukakodi coaster ikatupeleka kijijini kwetu.

Tulipofika tukagawana maeneo na tunashindana kujenga sasa!! Lengo ni kuhakikisha tunajenga kwetu Mtwara, naona wamenogewa sasa hivi tupo kwenye maandalizi ya kukodi coaster tena ili twende kama mwaka jana. Nimefurahi kwa kweli
 
Distance ya Masasi - Nachingwea ni fupi mno mwendo wa nusu saa tu kwa coaster ila tiseme si uzembe tu wa serikali ni uzembe wa Mkoa wa Lindi kwa ujumla mbona mtwara wanaweza. Ukiangalia hicho kipande kutoka Masasi hadi Lukuledi ambapo ni mpaka wa Mkoa wa Mtwara na Lindi utaona upande wa Mtwara kuna lami japo imeishia pale Masasi girls tu ila kutoka pale utaona barabara ikichongwa na kuwekwa kifusi mpaka Lukuledi.Ila ukianza Lukuledi mpaka ufike Nachingwea mjini pori vichaka tu barabara imezongwa na nyasi kama sio ya wilaya vile.Wananchi wawajibishe viongozi wao mbona Barabara Kutoka Nanganga hadi Ruangwa kupitia Likunja na kutoka pale Likunja kwenda Nachingwea kupitia Chiola atleast imechongwa vizuri, na ni mwendo wa 2hrs kutoka Ruangwa kwenda Nachingwea kwa bodaboda.
Tanroad ya Mtwara inajitahidi sana maana barabara ya Nachingwea - Masasi ipo chini ya Tanroad za mikoa.Tanroad ya kila mkoa ingeweza kujenga km 1 kila mwaka kwa kila mkoa kwahyo barabara ya Nach-Masasi ingesaidia kwa hii njia.
 
Wakazi wa mtwara wanawasifia sana mabinti wa Lindi kwa maadili hasa ukitaka kuwaweka ndani kama mke tofauti na mabinti wa mtwara ambao wanaanza kusahau sana maadili kutokana na utandawazi unaotokana na maendeleo ya kasi ya mtwara.

Je! Unalisemeaje hili mkuu? Na utaratibu wa kuchukua jiko kwa ujumla kutoka Lindi nini hasa cha muhimu zaidi hasa kwa,wale shombeshombe wa kiarabu?
 
Mi nimeanzisha kampeni, mwaka jana mwezi wa saba nilihamasisha ukoo wetu tukachanga tukakodi coaster ikatupeleka kijijini kwetu.

Tulipofika tukagawana maeneo na tunashindana kujenga sasa!! Lengo ni kuhakikisha tunajenga kwetu Mtwara, naona wamenogewa sasa hivi tupo kwenye maandalizi ya kukodi coaster tena ili twende kama mwaka jana. Nimefurahi kwa kweli

Wazo zuri sana na mabadiliko huanza kwa kila mtu then familia ukoo ujumuiya mpaka taifa.. kuliko kusubiri muujiza au serikali hata kwa mambo binafsi
 
Back
Top Bottom