Siongei kishabiki, ila kasi ya ukuaji wa miji ambayo ipo kandokando ya ziwa Victoria na karibu na miji mikubwa huwa kubwa sana. Kilichokuwa kinaleta shida ni mpangilio mbovu wa Miji.
Nani atakaa Chato? Kwanza wapo waliopo lakini pia itategemea kasi ya ukuaji wa kiuchumi. Ki-nchi tunaweza kusema eneo hilo si landlocked kwa sababu linapakana na ziwa Victoria (kuna bandari kongwe ambayo iliwekwa na Wakoloni, na nafikiri unajua sehemu mkoloni alipoweka miundombinu kama hiyo alikuwa anafikiria mbali kiasi gani), Mji wa Geita, Mkoa wa Kagera na urahisi wa kufika Nchi za Rwanda na Uganda.
Kwani kipi cha kushangaza kuanzishwa Chato? Barabara? Majengo ya huduma za kijamii? Uwanja wa ndege.
Kwa hili la Uwanja wa ndege ni vyema kujikumbusha ilipoanzishwa Kia eneo ulipo Uwanja halafu rudi miaka zaidi ya 30 nyuma, Mtu angejiuliza 'unajenga vipi Kiwanja cha Kimataifa porini!' Kumbuka wakati huo zao linaloingiza fedha nyingi za kigeni ni Pamba, Katani na Korosho.
Hapa ndipo inakuja hoja hii aspect ya 'Kaskazini' ndo wenye maono kama Mtanzania mzalendo siwezi kuiunga mkono, ni kuchochea chuki.
Na ushauri wangu, Chama chochote cha siasa kisije kujinasibisha na hili