KakaJambazi
JF-Expert Member
- Jun 5, 2009
- 18,830
- 12,291
Mpelekee ww siku moja, mkaribishe kuoga kwa kupiga magoti, ndo atajua anapaswa kufanya ivo.
dah! ngoja tu nitumie sehem ndogo ya hekima yangu manake ningegeuza side B pasingetosha.
jibu jepesi ni kwamba mkeo hajazoea hayo unayoyataka kufanyiwa, hivyo kumlazimisha inakuwa kero kwake. nakushauri kama unapenda hayo uliyoyasema basi mwonyeshe mfano siku moja chukua maji tia wenye ndoo mwambie mke wangu mpenzi karibu tukaoge, najua atakwenda kuoga lazima mkisha maliza una mwambia basi mwenzio ukinifanyia hivi nitafurahije?? napenda kubembelezwa mm na kutamkiwa maneno ya ukarimu namna hii. siku hiyo hiyo ataanza kukuambia.
alternatively weka maji ya shower bafuni kwako, hutohitaj kuwekewa maji ni kiasi cha wewe kuingia na kufungua bomba tu.
Uwe unaoga mtoni
Kama ishu ni maji ya kuoga tu, si uweke mabomba bafuni?
Na akikucheat si utamla alive?
Culture, culture, culture!
Usilaumu culture ilhali huyo mkewe naye ni wa culture hii hii...angekuwa mzungu u'd have a point.!!!
Kumbe mimi nina bahati sana, nakaribishwa mpaka raha.
So unadhani mhaya na msukuma wanafanana kiutamaduni? Ukizingati wanashare ziwa victoria?
kaka, kwanza nakupa pole kwa ndoa uliyo nayo. asikudanganye mtu, wanaume wooooooooooooooooooooooote wa Afrika, wanapenda kubembelezwa! sO UNAKOSA kitu muhimu sana. Ila jifunze tu kujua kuwa kwenye mahusiano ya ndoa, huwezi kupata kila kitu, kuna mwenzio anabembelezwa but mke wake anacheat. so mshukuru Mungu, kwa ajili ya huyo mke uliye naye, na kubali kuwa wewe kubembelezwa umushakukosa!polepole, you will learn to accept. bora hata anakuwekea na kukuita japo impolitely!
mimi nipo kwenye ndoa kwa zaidi ya miaka 10 na mpaka leo nikiweka chakula namkaribisha mume wangu "karibu mpenzi chakula" bafuni kwangu kuna maji siku zote tunaoga pamoja na several times ninamuogesha, namsugua miguu, namkata kucha, namchana nywele, nampasia nguo zake,,hata perfume ni mimi nampulizia...sio mara moja nampelekea chakula ofisini"lunch box" kwa surprise....naingia jikoni several times namuandalia vitu spesho hasa week ends ninapokuwa siendi ofisini... lkn bado alinicheat ...nyie wanaume bana hata mbebwe mgongoni na mbeleko hamriziki......
toa mfano dhahiriMkuu umeoa kabila gani? kuna baadhi ya makabila wanawake wao hawana hali ya unyenyekevu kabisa.
nimeoa mtu wa manyara....mbulu, mbona dada zake wanaonekana wana heshima? hata kama hayupo wao wakinitengea maji bafuni utasikia wanasema..''shem kaibu maji bafuni'' lakini yeye mwenye mali utasikia anafyatuka ''nyanyuka ukaoge wengine wanataka kuoga utawachelewesha'' basi mi namwangalia simumalizi!
asante kwa ushauri tatizo nikimwambia ivo anasema labda nimemchoka ili hali hata zamani hajawahi kunikaribisha...Mbona sisi tumeoa huko kaskazini na tunafanyiwa ya mahaba bwana? Ni huyo mwanamke tu. Kaa naye,mpe elimu kidogo. Mwambie,mke wangu nakupenda sana lakini katabia ka kutonyenyekea kanani hasira sana. Jirekebishe,nami nitakupenda zaidi halafu mwangalie anafanyaje?
Hulka haina dawa. Chunguza ukoo wao ukoje ili uweze kujua kama amerithi toka kwa wazazi wake.
Pili jaribu kumfanya awe mcha Mungu.
Tatu wewe jipime mwenyewe pengine haridhiki na wewe au ana bwana mwingine ambaye mapenzi yake yako kule,
Bora Kamusi umetoa ushuhuda. Mwenye macho haambiwi soma.
Ushauri wangu ni mwanamke kuwa jinsi ulivyo; anayetaka kupigiwa magoti ajue wewe si type yake.
Haya mambo si heshima wala nini ni mazoea. Kama mimi sijawahi ona baba yangu akipigiwa magoti na mama don't expect it from me....na nikikupigia magoti basi jua na pretend na nitaaacha soon.
Ndoa hailindwi na magoti ni compatibility.
Mtakuwa watumwa kwa ku pretend badala ya ku enjoy life. Maisha yenyewe mafupi....nani wa ku pretend au kutumikishwa.
Na tunadunda na hamna dalili ya kuachwa wala kuachika.