Mke wangu hana nidhamu?

Mke wangu hana nidhamu?

Tatizo wanaume wengi mnapendwa kubembelezwa hata ambako hakuna maana. Maji kakuwekea bafuni. Mpaka akuambie karibu?


Binafsi naona kama jambo dogo sana kwa mtu mwenye mapenzi ya kweli kwa mkewe au mmewe. Labda kama anatumia lugha mbaya. Je akikwambia maji tayari utaridhika au mpaka uambiwe karibu maji ya kuoga? Mambo madogo madogo husiyatilie maanani yatakuvunjia ndoa na kuleta dosari ambazo hazina maana.
 
Hehehehee umaskin unazua matatizo mengi sana, ndomana nimesema sitakaa niingie kwenye ndoa hasa na mtz, wanaume wa kitz wamelelewa kuwa mke ni chombo cha ngono, hausigel, punda etc usitegemee watabadilika thats how they are

Mwenzio alisema mchumba yuko Finland kachezea kapa, usitukane mto kabla ya kuvuka mamba tehe tehe teheeeeeeeeeeeeeeee
 
nimeoa mtu wa manyara....mbulu, mbona dada zake wanaonekana wana heshima? hata kama hayupo wao wakinitengea maji bafuni utasikia wanasema..''shem kaibu maji bafuni'' lakini yeye mwenye mali utasikia anafyatuka ''nyanyuka ukaoge wengine wanataka kuoga utawachelewesha'' basi mi namwangalia simumalizi!
INAWEZEKA HUYU MWANAMKE NI MATAWI ya JUU KUKUZIDI. TAFUTA SAIZI YAKO
 
ambebe mdada wa watu atoke chembe ya moyo????
eti kabisaaaa analalamika mke wangu hanibembelezi akiniwekea maji kuoga
ebooo yaani mkeo atakuwa ana shida sana inaonekana wewe si muelewa

Ndo hawa wanaodangawa na nyimbo za Mzee Yusuph za 'Nalishwa huku nikipepewa'
 
Mimi nina mke na tuna mtoto mmoja. Lakini tangu nimemuoa huyu mwanamke maka mitatu iliyopita hajawahi hata siku moja kunikaribisha kwenda kuoga maji bafuni kwa adabu ambazo mimi nimekuwa nikiziona katika maeneo mengine. Kwa mfano anaweza kuandaa maji bafuni na kuniambia...nyanyuka ukaoge maji yako bafuni...hivi ina maana anshindwa kusema maneno kama karibu mme wangu ukaoge maji yako tayari bafuni? Hata kwa chakua hali ni hiyohiyo.
Kutokana na hili pamoja na mengine nimekuwa nikimchukulia kuwa hana adabu kwa mme wake au nakosea wadau?
Naombeni msaad wenu nifanye ninikumfanya anitendee ninavyopenda kutendewa maana nikimwambia kuwa sifurahii jinsi anavyonifanyia anaonekana kunishangaa tu na kuishia kunilaumu eti labda nina visa vingine tofauti na hilo!
ifanye nini ndugu zangu? naomba mnishauri tafadhali!
Kwanza usiseme hana nidham, ila nakuomba angalia back ground yake, alikozaliwa, na je mama yeka alikuwa anayafanya hayo? je amelelewa katika mazingira gani. ukishajua unaweza ukamrekebisha, kwa sababu inawezekana yeye akawa anaona hiyo ni lugha ya kawaida kukueleza hivyo, lakini kumbe anakosea.
So pls mchunguze halafu chukua hatua ya kumrekebisha, sisi wanawake kubadilika ni rahisi. pale anapokwambia kwa ukali wewe mwambie kwa upole kuwa hupendezwi na kauli yake, atajisikia vibaya na kuona aibu so anaweza akarekebika.
usikasirike, wala kumchukia ila mpende na mrekebishe taratibu atarekebika.
 
Namshangaa mwanaume unawezaji kuja kulalamika kwenye JMF kuhusu kupelekewa maji ya kuoga?


Kuna mwanume mmoja ambaye hawajibiki kwa lolote katika familia, akikaa na wanaume wenzie ana mlalamikia mkewe mara hafui, hapeleki maji bafuni? wakati yeye kutwa anaangalia video na siku hizi ving'muzi vimeleta mambo. Mkewe anashinda kazini, kurudi saa 12 jioni, kuwa mke ni kosa la jinai ndugu zangu?

Punguzeni kulalamika ishini kwa akili katika familia zenu. Kama mtu anakuvumilia kwa makubwa wewe madogo unayashikiaje bango?

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Kama anataka kubebwa mpaka bafuni akaoe Mgada. Maana yeye kubembeleza ni jadi hata kama anakung'ong'a. Maana wanaume wetu wa kiswahili wanapenda maigizo katika mapenzi kuliko kitu chochote.
 
ma wife is ma gift from almight GOD.nikiwa busy na lap top naombwa nikaogeshwe kama mtoto na miaka 8 ya ndoa.ngoja niendelee kupenda na kumjari huyo mwanamke anaye pendwa na ndugu zangu kuliko hata wanavyo nipenda
 
Ndugu yangu, tupo katika safina moja ila tofauti ni watu tu kwani yanayokusibu ni kama umekopi kwangu. Tatizo ukimwambia ukweli khs hilo wala hashtuki mi binafsi nimekuwa na mawazo mengi sn nahisi ni ujivuni wa wanawake wa kaskazini kwani nami wangu atoka huko kazi kujisifia tu nimefanyiwa vichenipati v3 so what....!? Mbaya zaidi ni kutokubali ukweli na hali halisi mi nimetumia njia ya udikteta kdg kabadilika jaribu mwambie... Ndoa ni katiba mbili zinavunjwa kutengeneza iwe moja, ni lazima mmoja awe chini na awe tayari kupokea amri na maagizo toka kwa mwenzie ndo tutaenda tofauti na hapo hakuna katiba 1 wala ndoa hakuna. Mkumbushe kuwa waafrika mwanaume huwa anaoa na wala hatuoani! inawezekana timiza wajibu wako!
 
duh, nilidhani yananikuta mimi tu kumbe na wenzangu yanawakuta! ushauri wako ni mzuri na nitauzingatia. unajua wanawake wa kibongo wanataka kutuletea mambo ya kiulaya..eti tumeoana..inawezekanaje?
Ndugu yangu, tupo katika safina moja ila tofauti ni watu tu kwani yanayokusibu ni kama umekopi kwangu. Tatizo ukimwambia ukweli khs hilo wala hashtuki mi binafsi nimekuwa na mawazo mengi sn nahisi ni ujivuni wa wanawake wa kaskazini kwani nami wangu atoka huko kazi kujisifia tu nimefanyiwa vichenipati v3 so what....!? Mbaya zaidi ni kutokubali ukweli na hali halisi mi nimetumia njia ya udikteta kdg kabadilika jaribu mwambie... Ndoa ni katiba mbili zinavunjwa kutengeneza iwe moja, ni lazima mmoja awe chini na awe tayari kupokea amri na maagizo toka kwa mwenzie ndo tutaenda tofauti na hapo hakuna katiba 1 wala ndoa hakuna. Mkumbushe kuwa waafrika mwanaume huwa anaoa na wala hatuoani! inawezekana timiza wajibu wako!
 
INAWEZEKA HUYU MWANAMKE NI MATAWI ya JUU KUKUZIDI. TAFUTA SAIZI YAKO
hana matawi yoyote..yaani kama ni kuwa juu mi ndo niko juu kwa kila kitu sema tu ni mambo ya kuoana ambayo huwezi kumwambia mwenzako ulikomtoa maana atajihisi kuwa unamnyanyasa ukimkumbusha ya nyuma!
 
Kama ishu ni maji ya kuoga tu, si uweke mabomba bafuni?

Na akikucheat si utamla alive?

Culture, culture, culture!

Kwa kauli kama hizi ndio maana the other day nilimuita yule jamaa yenu mwingine mpuuzi aliposema 'WANAWAKE NI WENGI KULIKO WANAUME'.

Upuuzi ni kwamba, kuna tofauti kubwa kati ya wanawake na viruka njia. Mtu anapolalamika kuwa wanawake wengi hawataolewa kwa kuwa wanaume ni wachache huwa namshangaa. Si wanawake wote wanafaa kuwa wake. Kuna some kind of viruka njia fit for Hit & Run.

Mwanamke anayelala fofofo hata asijue mumewe aliondoka saa ngapi kwenda kazini HAKUSTAHILI KUOLEWA. Na hii si sehemu ya ukorofi wangu, ni NATURE. Kuna ng'ombe wa maziwa na wengine wanafaa tu kwa kulimia.
 
duh, nilidhani yananikuta mimi tu kumbe na wenzangu yanawakuta! ushauri wako ni mzuri na nitauzingatia. unajua wanawake wa kibongo wanataka kutuletea mambo ya kiulaya..eti tumeoana..inawezekanaje?

Mkuu, mtafute Bi. Chau, yule mama anakuwaga kwenye kipindi cha Yaliyomo Yamo cha Radio One umkabidhi hiyo kesi. Nahisi Kitchen Party inapaswa kurudiwa. Au kama wewe ni wale wenye ruksa ya kuoa wake wengi, tafuta mwingine wa maana halafu huyu kumshikisha adabu, uwe unampa mimba kila baada ya mwaka kwa maana hana maana yeyote hapa duniani zaidi ya kizazi
 
Kama umeoa uchagani/mkurya/upareni ni kawaida yao kuwa wababe
 
Mawasiliano madogomadogo ndani ya nyumba yanaweza kuvunja ndoa au yasivunje,kukawepo na usaliti au usiwepo.Mfano unaomba chakula, unanyooshewa mguu "kile pale"halafu upate nyumba ndogo anaejua majukumu,atasoma namba na kubaki kulaumu.

sawa kabisa ila kosa lake kwa nini asimwambie kuhusu tabia yake na je naye akiwa na kasoro kidogo mke naye atafute wa kando? mawasiliano ni muhumu sana katika ndoa
 
Kama ishu ni maji ya kuoga tu, si uweke mabomba bafuni?

Na akikucheat si utamla alive?

Culture, culture, culture!

Mweeeeeeeee! Hata mie nimechoka kabisa kuhusu kumkaribisha mtu maji ya kuoga! Labda hilo la chakula naweza kuelewa lakini kuoga? Yaani maji yanatoka bafuni nikukaribishe kuoga? Ha ha haaaaaa! Mila nazo sometimes zinatuponza!
 
wanaume bwana mnaboajeeee <br />
utajijuuuu and u wil keri uaself we huwezi kuweka??kama ameshindwa kukwambia jiambie mwenyewe kimoyomoyo

Dalili za ugume gume
 
wanaume bwana mnaboajeeee <br />
utajijuuuu and u wil keri uaself we huwezi kuweka??kama ameshindwa kukwambia jiambie mwenyewe kimoyomoyo

Dali za ugume gume...... Kazi ipo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom