Mke wangu anakuja ofisini -kuleta tifu

Benno

JF-Expert Member
Nov 21, 2009
332
51
:angry: "Kijana amekumbwa na Mkasa, Mke wake alianza na Kumtuma Baba mkwe aje kwa mume wake waongee matatizo ya Ugomvi wao, bila hata taarifa. Unafungua ofisi unaenda kwa bossi unarudi unakuta baba mkwe amekaa mezani kwako toka Mkoani na begi. Baada ya hapo Mke nae amegeuza ofisi ndio sehemu ya kusuluhisha matatizo ya Nyumbani.






"Dunia ina Mengi"
 
Kabla ya kufunga ndoa ni vyema ujue uwezo wa mwenzio wa kuvumilia mambo magumu, ufahamu wa jumla, kuchanganua mambo na uwezo wake wa kufanya maamuzi.
baba na mwanawe wote ni mapoyoyo wa kutupwa
 
Wazazi wa zamani kwa namna moja ama nyengine walikuwa sahihi sana kutafutia watoto wao wake/waume wa kuoa maana waliangalia mengi,,familia atokayo kijana,magonjwa ya kurithi etc,sasa hawa watu wa kukutana nao tu nyiani then mnacopy na kupaste ndo matatizo yenyewe hayo sasa!duh hatariiiiiiiiiiiiiii
 
pole
waambie kwa utaarabu twenden nyumbani tukayasuluhuishe ..au jamaa hata home akanyagi?
 
Hapo kuna kazi!Ila labda nyumbani mume anakua mkorofi na kiburi sana so inabidi aweke mambo live..ili angalau huyo mwanaume aone aibu kidogo!Upande wa pili wa habari unahusu sana hapa...kama huko nyumbani hasikilizi mama wa watu afanyeje?
 
Inawezekana jamaa kahama nyumbani; kwa hiyo ilikuwa hakuna jinsi zaidi ya kumfuata nyumbani. Kwanini ifikie hatua hiyo, mwanamume nae ajihoji. Sioni wa kumlau!
 
Ugomvi baina ya wanadoa ni kitu cha kawaida....
Mwisho wa yote watakuja kupatana warudie mapenzi yao matamu kama zamani wawaache watu wakijuliza " imekuwa vipi?"
Ndoa zote hupitia magumu lakini kuna siku shetani au kidudu mtu atashindwa kwa jina la yule aliye juu ya yote na wote.
Mke anayemfuata mume hadi ofisini huyo amekosa maarifa na subira tu.Aelekezwe kuvumilia kuna siku uvumilivu utalipa.Watu huvumilia hata miaka 20 ndivyo ndoa zilivyo, na katika kipindi hicho kuna mapito mengi ikiwemo vishawishi vya kila aina.Wengine hutafuta talaka kwa hali zote, wengine hupata wapenzi wapya, wengine kufanya fujo na kuonekana kituko mbele za jamii....YOTE YANA MWISHO MRADI UVUMILIVU.
 
[QUOTE=WomanOfSubstance;1419065]Ugomvi baina ya wanadoa ni kitu cha kawaida....
Mwisho wa yote watakuja kupatana warudie mapenzi yao matamu kama zamani wawaache watu wakijuliza " imekuwa vipi?"
Ndoa zote hupitia magumu lakini kuna siku shetani au kidudu mtu atashindwa kwa jina la yule aliye juu ya yote na wote.
Mke anayemfuata mume hadi ofisini huyo amekosa maarifa na subira tu.Aelekezwe kuvumilia kuna siku uvumilivu utalipa.Watu huvumilia hata miaka 20 ndivyo ndoa zilivyo, na katika kipindi hicho kuna mapito mengi ikiwemo vishawishi vya kila aina.Wengine hutafuta talaka kwa hali zote, wengine hupata wapenzi wapya, wengine kufanya fujo na kuonekana kituko mbele za jamii....YOTE YANA MWISHO MRADI UVUMILIVU.[/QUOTE]




nimeipenda hii

 
Wazazi wa zamani kwa namna moja ama nyengine walikuwa sahihi sana kutafutia watoto wao wake/waume wa kuoa maana waliangalia mengi,,familia atokayo kijana,magonjwa ya kurithi etc,sasa hawa watu wa kukutana nao tu nyiani then mnacopy na kupaste ndo matatizo yenyewe hayo sasa!duh hatariiiiiiiiiiiiiii

"Nadhani uko sahihi lakini pia si unajua mkiwa huku barabarani ndio mnaonana na wazazi unawapa taarifa?, Na Ningumu kidogo kutabiri
 
Hapo kuna kazi!Ila labda nyumbani mume anakua mkorofi na kiburi sana so inabidi aweke mambo live..ili angalau huyo mwanaume aone aibu kidogo!Upande wa pili wa habari unahusu sana hapa...kama huko nyumbani hasikilizi mama wa watu afanyeje?

Kwa hiyo ukimdhalilisha ofisini ndio unafaidika nini?
 
:angry: "Kijana amekumbwa na Mkasa, Mke wake alianza na Kumtuma Baba mkwe aje kwa mume wake waongee matatizo ya Ugomvi wao, bila hata taarifa. Unafungua ofisi unaenda kwa bossi unarudi unakuta baba mkwe amekaa mezani kwako toka Mkoani na begi. Baada ya hapo Mke nae amegeuza ofisi ndio sehemu ya kusuluhisha matatizo ya Nyumbani.






"Dunia ina Mengi"

Hahaaaa jamani nacheka kama mazuri, hilo linaitwa sokomoko na tedi. Hee au timbwili la asha ngedere, mh baba mkwe na begi ofisini? Makubwa ndo tabu yakuoa familia zisizo na maadili. Sasa kama mzazi hatna hekima then wewe utaenda kushtaki wapi, mh hakuna ndoa hapo. Ni uswahili fuulu.
 
Dawa ya huyo dada anyimwe mashine na mumewe miezi mitatu, anageuziwa mgongo na mzee kila siku, ndo atanyooka afu amwambie babake sasa, mh lakina anaweza kwenda ofisini kushtaki kwa boss mh nawasiwasi.
 
Hahaaaa jamani nacheka kama mazuri, hilo linaitwa sokomoko na tedi. Hee au timbwili la asha ngedere, mh baba mkwe na begi ofisini? Makubwa ndo tabu yakuoa familia zisizo na maadili. Sasa kama mzazi hatna hekima then wewe utaenda kushtaki wapi, mh hakuna ndoa hapo. Ni uswahili fuulu.

sasa kama mume amekata miezi 6 haonekani nyumbani mkewe afanyaje?
 
kabla ya kufunga ndoa ni vyema ujue uwezo wa mwenzio wa kuvumilia mambo magumu, ufahamu wa jumla, kuchanganua mambo na uwezo wake wa kufanya maamuzi.
Baba na mwanawe wote ni mapoyoyo wa kutupwa
good one sis' tatizo hizi ndoa za mjini huwa tunaokotana tu
 
@bENNO;

Kwanza kabisa mpe pole jamaa kwani inaonekana kabisa kwamba either ameoa mke ambaye si mfanyakazi, au mke asiyeheshimu kazi, kuna usemi nadhani uko kwenye signature ya mtu mpenda hapa JF na inatumika ana inasema "usichezee kazi, chezea mshahara"

Kwangu naona matatizo yafuatayo

  1. Kuna poor communication nyumbani, ugomvi wa nyumbani lazima uishie nyumbani na kwa hili ndhani baada ya huyo kijana kutatua hili anatakiwa weke msimamo wake wazi kabisa kuhusu hilo... kwani anaweza kuishia kupoteza vyote, kazi na mke
  2. pili, dogo lazima ampe mkewe na baba mkwe somo kama mwanaume nini maana ya nyumbani na tofauti na workplace
  3. pia lazima tujiulize maswali magumu... hivi kweli wewe baba mkwe unaweza kweli ukaongoza hadi ofisini kwa mkweo kisa kuna tafrani? ni heshima kweli? huyo baba kwangu mimi hastahili heshima ya baba mkwe hadi apewe ukweli
  4. forum za usuluhishi siku zote lazima ziwe na watu wa pande zote
  5. Na hapo kazini kuna haja ya kijana kuweka mambo wazi na colleagues n walinzi kwani ni muhimu mtu aanayekuja kwako uwe na taarifa au muafikiane kwanza maana wa shari anaonekana tu

Nawaombea mema ila hapo dogo ana kazi ya ziada kwani yaelekea misingi ya msingi kabias ya ndoa na mahusiano yanayowazunguka vinaonekana havijakaa sawa
 
Matatizo ya ndoa ambazo mwanzo wake ulikuwa bar, mziki, au tatizo la kuchukua vyasaka.
 
Ugomvi baina ya wanadoa ni kitu cha kawaida....
Mwisho wa yote watakuja kupatana warudie mapenzi yao matamu kama zamani wawaache watu wakijuliza " imekuwa vipi?"
Ndoa zote hupitia magumu lakini kuna siku shetani au kidudu mtu atashindwa kwa jina la yule aliye juu ya yote na wote.
Mke anayemfuata mume hadi ofisini huyo amekosa maarifa na subira tu.Aelekezwe kuvumilia kuna siku uvumilivu utalipa.Watu huvumilia hata miaka 20 ndivyo ndoa zilivyo, na katika kipindi hicho kuna mapito mengi ikiwemo vishawishi vya kila aina.Wengine hutafuta talaka kwa hali zote, wengine hupata wapenzi wapya, wengine kufanya fujo na kuonekana kituko mbele za jamii....YOTE YANA MWISHO MRADI UVUMILIVU.

wengine talaka hupata kabisa lakini wanakuja kurudiana na maisha kuendelea kama kawaida. ila kufia ofisini sio vizuri kwani hiyo kazi ikiharibika familia nzima tateseka, nakubaliana nawe kuwa hao wanaleta mambo ya nyumbani ofisini ni wa kuelimishwa tu
 
Wazazi wa zamani kwa namna moja ama nyengine walikuwa sahihi sana kutafutia watoto wao wake/waume wa kuoa maana waliangalia mengi,,familia atokayo kijana,magonjwa ya kurithi etc,sasa hawa watu wa kukutana nao tu nyiani then mnacopy na kupaste ndo matatizo yenyewe hayo sasa!duh hatariiiiiiiiiiiiiii

Yaani nikutane na mtoto mzuri kama wewe niogope kumwaga sera eti nasubiri mzazi anitongozee anaemjua yeye! No binti haiwezekani.
 
sio mapopoyoyo, jaribu kwanza kujua tatizo ni nini? kuna uwezekano mwanamme hakutaka kusuluhishwa na mgogoro unaweza ukawa na mda mrefu, sasa mwanamke afanye je? akimwambia anakaataa
Kabla ya kufunga ndoa ni vyema ujue uwezo wa mwenzio wa kuvumilia mambo magumu, ufahamu wa jumla, kuchanganua mambo na uwezo wake wa kufanya maamuzi.
baba na mwanawe wote ni mapoyoyo wa kutupwa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom