Mke wangu ameanza dharau baada ya kumfungulia duka

Mke wangu ameanza dharau baada ya kumfungulia duka

Muhimu ni kumnyoosha kwa kutompa pesa kuzidi kuendeleza duka hilo, acha life ajitambue.

Pia kuwa na duka lazima anakutana na wateja na wanaume wanampa bichwa la maneno anayoambiwa.

Pole kama hana kazi ya kuajiliwa muache akae akipata shida then akae nyumbani, fungua biashara ingine wewe.
Hana kazi ya kuajiriwa ni mama wa nyumbani. Nikaona asikae bure. Lakini ndo imekuwa changamoto. Leo karudi alianika nguo. Mi nilivyorudi nikaziweka ndani. Karudi ananiambia kwanini hujakunja nguo. Nikamwambia kama umenioa ntazikunja ila kama nimekuoa siwezi. Anajifanya ana amri mpaka sometime ananidhalilisha mbele za watu. Ila sasa nimeamua kumkazia.
 
Anauza na kujiuza huko dukani,.. Na kama kampata wa kusimamia kucha, biashara haina mda itakufa tu, ndio maana hawezi kukupa mahesabu.... Kalakabaho
 
Jaribu kutafuta njia itakayoweza kurudisha heshima na upendo kama hapo awali hata kwa kufunga hilo duka ilimradi unusuru papuchi yako
 
Hana kazi ya kuajiriwa ni mama wa nyumbani. Nikaona asikae bure. Lakini ndo imekuwa changamoto. Leo karudi alianika nguo. Mi nilivyorudi nikaziweka ndani. Karudi ananiambia kwanini hujakunja nguo. Nikamwambia kama umenioa ntazikunja ila kama nimekuoa siwezi. Anajifanya ana amri mpaka sometime ananidhalilisha mbele za watu. Ila sasa nimeamua kumkazia.

Sasa kama umeanua si ukunje? Nani alikutuma ukaanue!!
 
kiukweli hakuna wanandoa wanaoishi kama malaika bila ya mikwaruzano
lakini sasa haya mengine yanauma sana.
Moja kwa moja najiona ninamapungufu makubwa kwasababu vitu kama hivi ziwezi kuvivumilia hata kidogo.
Kwakweli tutaendelea kuvuta muda wa kuoa.
yaani kukujali kote bado tu unifanyie hivo!!??. hapana kwakweli sitaweza.
 
Habari wanajamvi,

Nimeoa miaka 2 iliyopita. Changamoto kubwa niliyonayo ni huyu mwanamke nimemfungulia kaduka. Basi dharau zimezidi hatari, ananijibu anachotaka.

Nikimuuliza mahesabu kuhusu duka hataki kunipa, unyumba mpaka nimbembeleze. Inaweza kupita wiki 2 anatoa visingizio kibao.

Naombeni ushauri wenu.
Mulika mwizi
 
Jaribu kutafuta njia itakayoweza kurudisha heshima na upendo kama hapo awali hata kwa kufunga hilo duka ilimradi unusuru papuchi yako
hata kama akifunga hilo duka hawezi kubadili chochote mke kesha onja vya nje tayari hawezi kubadilika tena.
Na siku ya kufunga hiyo biashara nakuhakikishia ndoa itavunjika siku hiyo hiyo.
 
Tunatofautiana tunavyoyachukulia mambo.....na tofauti ya mitazamo hiyo ndio inayoleta mikingamo ndani ya nyumba.........inawezekana malalamiko ya mkeo yakawa sahihi lakini akili yako ikagoma kuukubali ukweli kutokana na hitaji la haja yako kwa wakati huo......

Jitahidi sana kuyasoma mazingira kabla ya kuulizia jambo fulani kwenye nyumba....hata kama ni la kawaida kwani hujui kuwa mwenzako wakati huo yupo kwenye hali kiakili na kimtazamo juu ya jambo hilo unaloliulizia.....

Kwanza nikupongeze kwa kufanya jambo la maana kwenye ustawi wa familia yako.....kasoro yako ni kuwa umeanzisha jambo ambalo wewe umeshindwa kulisimamia..........wakati unapanga jambo hilo ulitakiwa pia upange na mbinu za kulisimamia mapema mno.......

Kwa jinsi hali ilivyo ni kuwa kuna viashiria vya mabadiliko ya mkeo ambayo wewe ulishindwa kuyasimamia mapema........na kwa kuwa umeliacha muda mrefu na mkeo ameshalifanya kama sehemu ya maisha yenu mapya.......

Kwa hapo ilipofikia mabavu na maguvu hayawezi kutatua tatizo hilo hekima busara.......

Kutokana na mfumo mpya wa maisha ya familia yako ni wazi kuwa mkeo atakuwa anachoka sana kutokana pirika pirika za dukani......uchovu huo unamfanya awe mtu wa kisirani hata katika mambo ya kawaida....ambayo mwanzo alikuwa akiyafanya kwa hiyari yake.......

Tafuta siku moja ambayo hatakuwa na shughuli nyingi za dukani au hata kama ikiwezekana afunge kaisa duka.....kitendo cha yeye kukaa na wewe siku nzima.....kutamfanya akumbuke majukumu yake mengi aliyokuwa akikufanyia....ikifika usiku muda wa kupumzika....mueleze kwa mahaba ni jinsi mabadiliko hayo yanavyokufanya uwe mnyonge.......

Hadi kufikia hapo ndio muda muafaka wa wewe kusimamia kile ambacho ulikianzisha.......ikiwamo na suala la kumtafutia kijana wa kazi ili awe anamsaidia shughuli za dukani......hiyo itapelekea yye kupunguza uchovu na kurejea kwenye hali yake ya kawaida......,,

NB; unatakiwa uwe mvumilivu kwenye kipindi hiki kigumu...,,,
 
Back
Top Bottom