lee Vladimir cleef
JF-Expert Member
- Feb 5, 2013
- 9,154
- 33,366
Haya ni mawazo yangu.
Mume na mke sio ndugu kabisa, ni Aina ya uhusiano wa kipekee kabisa,uhusiano wa Hawa watu wawili ni uhusiano wenye nguvu na mkubwa Sana kushinda uhusiano wa ndugu wa kuzaliwa tumbo moja.kushinda uhusiano wa baba na mtoto,au marafiki wawili. Lakini pamoja na uzito wa uhusiano huu bado unaweza kuvunjika.
Hali hii ya kuvunjika inaweza kutokea kwa uhusiano mwingine wowote. Mfano Kaka na mdogo wake,baba na mtoto,mama na mtoto,Kaka na dada ama ndugu wengine ama marafiki, wanaweza kufarakana na wasiongee Wala kuwasiliana milele. Uhusiano wa mke na mume unaweza kufuatiwa na uhusiano wa mtoto na mzazi. Uhusiano wa mume na mke unapata nguvu kwa sababu zifuatazo.
Mke na mume katika mahusiano yao wanafanya Mambo mazito kuliko Mambo ambayo yanfanywa na uhusiano wa watu wengine. Mfano kulala uchi pamoja, Kufanya tendo la ndoa,kitendo Cha kufanya mapenzi ni Jambo kubwa Sana na la ajabu Sana.
Unaweza ukamuona mtu unaemheshimu Sana akiwa njiani ama kazini,mfano mwalimu wako ,waziri Fulani,mkuu wako,ama kiongozi wako wa dini akiwa katika hali yake ya kawaida,anaonekana mtulivu ama mkorofi,lakini lakini muonekano huo ni tofauti kabisa na akiwa anafanya mapenzi.
Anayejua hali anayikua nayo mmoja wa wawili Hawa ni mwenza wake ,yaani mume wake ama mke wake.Baba,mama,ndugu na wengine hawajui hali anayikua nayo akiwa katika dimbwi la mapenzi.
Hali hi ndio inafanya uhusiano wa wawili Hawa kuwa wa kipekee kabisa. Kuuguzana wakati wa magonjwa makubwa na madogo, Kuvumilia shida katika maisha yao. Kuna hali anakua nayo mmoja wa watu Hawa akiwa katika changamoto ama shida ama magonjwa,hakuna mtu mwingine awezae kujua hali hiyo zaidi ya mke ama mme. Kuuguzana.wazazi,Ndugu jamaa na marafiki wanaweza kusaidia tu,lakini mateso yote ya kuuguzana wanayapata wenyewe.
Kufurahia raha katika maisha yao, Hakuna awezae kujua kiwango Cha raha Kati ya wawili Hawa.
Furaha ya kupata watoto,
Kupeana raha nyingine,
Kutiana moyo wakati wa shida,
Kugombana na kupatana,
Kujuana mapungufu katika maisha, Mfano wakati wakiwa wamelala,baadhi ya watu huonesha tabia za ajabuajabu Sana,lakini mke na mme huhifadhiana. Uhusiano mwingine unaofuata uhusiano huu ni wa:_
Mzazi na mtoto,
Ndugu kwa ndugu,
Marafiki na
Jamaa.
Natanguliza shukurani.
Mume na mke sio ndugu kabisa, ni Aina ya uhusiano wa kipekee kabisa,uhusiano wa Hawa watu wawili ni uhusiano wenye nguvu na mkubwa Sana kushinda uhusiano wa ndugu wa kuzaliwa tumbo moja.kushinda uhusiano wa baba na mtoto,au marafiki wawili. Lakini pamoja na uzito wa uhusiano huu bado unaweza kuvunjika.
Hali hii ya kuvunjika inaweza kutokea kwa uhusiano mwingine wowote. Mfano Kaka na mdogo wake,baba na mtoto,mama na mtoto,Kaka na dada ama ndugu wengine ama marafiki, wanaweza kufarakana na wasiongee Wala kuwasiliana milele. Uhusiano wa mke na mume unaweza kufuatiwa na uhusiano wa mtoto na mzazi. Uhusiano wa mume na mke unapata nguvu kwa sababu zifuatazo.
Mke na mume katika mahusiano yao wanafanya Mambo mazito kuliko Mambo ambayo yanfanywa na uhusiano wa watu wengine. Mfano kulala uchi pamoja, Kufanya tendo la ndoa,kitendo Cha kufanya mapenzi ni Jambo kubwa Sana na la ajabu Sana.
Unaweza ukamuona mtu unaemheshimu Sana akiwa njiani ama kazini,mfano mwalimu wako ,waziri Fulani,mkuu wako,ama kiongozi wako wa dini akiwa katika hali yake ya kawaida,anaonekana mtulivu ama mkorofi,lakini lakini muonekano huo ni tofauti kabisa na akiwa anafanya mapenzi.
Anayejua hali anayikua nayo mmoja wa wawili Hawa ni mwenza wake ,yaani mume wake ama mke wake.Baba,mama,ndugu na wengine hawajui hali anayikua nayo akiwa katika dimbwi la mapenzi.
Hali hi ndio inafanya uhusiano wa wawili Hawa kuwa wa kipekee kabisa. Kuuguzana wakati wa magonjwa makubwa na madogo, Kuvumilia shida katika maisha yao. Kuna hali anakua nayo mmoja wa watu Hawa akiwa katika changamoto ama shida ama magonjwa,hakuna mtu mwingine awezae kujua hali hiyo zaidi ya mke ama mme. Kuuguzana.wazazi,Ndugu jamaa na marafiki wanaweza kusaidia tu,lakini mateso yote ya kuuguzana wanayapata wenyewe.
Kufurahia raha katika maisha yao, Hakuna awezae kujua kiwango Cha raha Kati ya wawili Hawa.
Furaha ya kupata watoto,
Kupeana raha nyingine,
Kutiana moyo wakati wa shida,
Kugombana na kupatana,
Kujuana mapungufu katika maisha, Mfano wakati wakiwa wamelala,baadhi ya watu huonesha tabia za ajabuajabu Sana,lakini mke na mme huhifadhiana. Uhusiano mwingine unaofuata uhusiano huu ni wa:_
Mzazi na mtoto,
Ndugu kwa ndugu,
Marafiki na
Jamaa.
Natanguliza shukurani.