Mke hataki ndugu zako, utafanyaje?

Mke hataki ndugu zako, utafanyaje?

Kwenu wakuu,
Kwa muda mchache nimepata ushauri wa kutosha kazi iliyobaki ni kufikisha ujumbe.

Kuna majibu ya aina tatu hapa:
1. Kuna ambao wanakubaliana na maamuzi ya mwanamke, mtoto aondoke
2. Kuna ambao wanapinga tabia ya mwanamke, bora mwanamke aondoke.
3. Kundi la mwisho wanachukizwa na tabia ya mwanamke lakini wanashauri mtoto aondoke kuepusha ugomvi.

Binafsi naungana na kundi la pili, mwanamke asepe. Kuna sababu ya msingi kwa mfano aliotoa scolastika

Ukichunguza kwa umakini hapa mwanamke ana roho mbaya tu Hana sababu yoyote ya msingi. Kama alivyosema scolastika leo kafanyiwa mtoto kesho akimfanyia mzazi wako?!

Naenda kufunguka kwa jamaa akiona ushauri unamfaa auchukue akiona haufai auwache

Jamaa anaitwa Memtata?
 
Mpr pole Sana jamaa!

Wanawake wengi wapo hivyo cha msingi atumie ubabe tu!

Kama hataki kuishi na Mtoto au ndugu upande wake waachane akaolewe na MWANAMME ambae yupo tayari kuburuzwa!!!!

SHERIA ZA NDOA NI KITU KIBAYA SANA UMASKINI KWA MWANAMME NI NJE NJE!
 
Leo naomba mumsaidie rafiki yangu kumshauri, mimi ni nimeshashauri kwa upande wangu lakini nataka kuona fikra za watu zaidi.

Jamaa ana mke na watoto, hivi karibuni kaka yake alipoteza kazi ndugu wakamuomba asaidie kulea mtoto mmoja ambaye alikuwa kidato cha pili. Jamaa alimshirikisha mke wake kuhusu mgeni huyo mke akakubali lakini inaonekana alikubali kwa shingo upande.

Kwa sasa sio siri tena mwanamke kasema wazi kabisa hataki kuishi na huyo mtoto tena akaenda mbali zaidi kampigia simu mama wa mtoto kumueleza yeye hawezi kuishi na mtoto wake. Habari zikamfikia jamaa akashangaa sana aliporudi kumlaumu mwanamke kwanini amefanya hivyo mwanamke kaja juu na kusema hata yeye ana maamuzi kwenye familia na msimamo wake ndio huo, hataki kuishi na huyo mtoto.

Jamaa kabembeleza sana mke akawa kama kaelewa kumbe bado. Hivi juzi kalianzisha tena na sasa amefika mbali kamwambia mume wake achague moja aidha kuishi na yeye(mke) ama mtoto wa ndugu yake........

Mzozo uko hapo, mimi nilimshauri kama hana uwezo wa kumlea huyo mtoto amrudishe kwao lakini si kwasababu ya kukataliwa na mke wake maana hata yeye hajui kesho yake. Jamaa alinijibu uwezo anao maana mtoto anasoma shule za serikali halipi ada hata mia zaidi ya uniform na vifaa vya shule.

Kama nimekosea naombeni sababu, bado tuna nafasi ya kumsaidia jamaa. Kwa ndugu upande wa mume na narafiki zake wanashangaa sana maamuzi ya mwanamke lakini kwa ndugu wa mke anasema zaidi ya 80% wanamsapoti mwanamke
Wanawake asilimia80 awapendi ndugu wa mume hata wa kwangu naona Yuko Ivo lakn mdogo wake anakaa Kwa Amani hapa home lakn ujichanganye ulete ndugu zako
 
Wengi mnafurahisha sana! Hii kitu ni ngumu sana. Sijaona familia iliyosaidia ndugu akaondoka (baada ya mission completed) kwa kuishukuru. Mwisho wa yote huwa ni lawama tu.

Mtoto umejizalia mwenyewe akikua anakuita mchawi. Anakuua refer case za rombo, moshi mjini na hii ya kwimba ya juzi juzi.

Hivi humu ndani mnajua maana ya ndoa nyie? Unadhani ndoa ni mbususu? Ndoa unatafuta Rafiki wa ukweli, msaidizi wakati wa shida; mtu wa kukufichia madhaifu yako, mtu wa kukufariji etc,

Ndo maana Mie namchumbia To yeye ili Watoto awapeleke kwa Depal ili gharama ziwe kwa Demi na Antonnia awe Mchepuko
"Ndoa unatafuta Rafiki wa ukweli, msaidizi wakati wa shida; mtu wa kukufichia madhaifu yako, mtu wa kukufariji etc,"

Kati ya Siku zako zote jf leo ndio umeongea point ✌️✌️

Kumbe ukitulia unakuaga na akili sana!!
 
Kama mtoto anasoma shule za serikali na umesema ada bure,
Nafikiri msaada alioutafuta ni wa chakula tu au sio?
Asaidiwe akiwa huko huko kwao unarundika ndugu wanini
 
Fanya hivi. Waite wazazi au ndugu wa mke mkae kikao pamoja na mkeo. Waonyeshe msimamo wako kuwa unampenda mkeo na pia unapenda umsaidie mtoto wa ndugu yako.
Toa condition hii.
"Kwa kuwa mke wangu amekataa kukaa na mtoto bila sababu za msingi na mimi sitaki ndugu yeyote wa mke wangu hata ninyi wazazi mje kukaa kwangu zaidi ya wiki 1. Kama kusalimia njooni lkn isizidi week 1" Then funga kikao kisha wape week 1 wakajisort then wakupatie maamuzi yao.
Kama wataendelea na msimamo wao tafuta namna ya kumsaidia mtoto, option zipo nyingi tu za kumsaidia pasipo kuishi nae. Lkn pia simamia maamuzi yako kama ndugu wa mke akija kwako fanya kama mlivokubaliana.
 
Kama mtoto anasoma shule za serikali na umesema ada bure,
Nafikiri msaada alioutafuta ni wa chakula tu au sio?
Asaidiwe akiwa huko huko kwao unarundika ndugu wanini



Sometimes sio rahisi kiivyo kusema asaidiwe akiwa mbali.
Hiyo bajeti ya kugawa nyumba 2 utaipataje kirahisi?

Halafu shule hazipatikani mahala pote na convenient ya kwenda na kutoka Shule hutofautiana.

Sehemu nyingine kwenda na kutoka Shule ni mbali sana na gharama.

Mtu hawezi Soma Shule yoyote.
 
Halafu hata akigairi kuondoka na huyo mtoto akaendelea kuwepo hapo basi inabidi kumfuatilia Kwa umakini na ukaribu asije akamdhuru mtoto wa watu hiyo mtesi mkubwa!
 
"Ndoa unatafuta Rafiki wa ukweli, msaidizi wakati wa shida; mtu wa kukufichia madhaifu yako, mtu wa kukufariji etc,"

Kati ya Siku zako zote jf leo ndio umeongea point ✌️✌️

Kumbe ukitulia unakuaga na akili sana!!
Nitatulia nitakapo kumiliki jumla
 
Mkalishe mtoto chini mpe sheria zako anazopaswa kufuata hapo nyumbani kisha mpe uhuru mke wa kuamua kukaa nae ama kuondoka.
Muda utasema kama tatizo ni mke ama mtoto.
 
Wanawake asilimia80 awapendi ndugu wa mume hata wa kwangu naona Yuko Ivo lakn mdogo wake anakaa Kwa Amani hapa home lakn ujichanganye ulete ndugu zako
We walete tu ndugu zako waje waishi tu, mke akilalamika mwambie wazazi wa hao ndugu yako walikusaidi tokea upo mchanga
 
Ni vizuri ulipoamua kuoa siulimuoa yeye Sasa ndugu wakazi gani??
Huo ni usumbufu hata wazungu baada ya ndoa wanaishi na ndugu zao Tena .??
Hapana Kwa sababu ulishakubali kuanza familia na umpendaye .
Sasa hivi ni utandawazi waende bhana kwani wamemuoa nani?

Mtu hata hupewi penzi Kwa Raha unaguna Guna kama mwizi kha nani kwako???

Halafu kazi kuja kuleta ushirikina , ulaghai, uchonganishi .

Ni Usumbufu
Duh!acha kuwa mtumwa wa fikra wewe..Eti "wazungu"kwa kila kinachofanywa na wazungu ndio sahihi????
 
Jamani jamani!.. mnaosema kuwa mimi ndio muhusika niwatoe hofu mi sinaga mambo ya kuzunguka ninapopatwa na tatizo, ukifatilia nyuzi zangu nyingi utaona kabisa kila tatizo nikitaka msaada huwa nafunguka hatakama kuna wakati nakutana na majibu ya dharau na kuonekana kuomba ushauri hata kwa mambo ya kijinga.

Update ya huyu jamaa ni kwamba kwa msimamo wake anasema hana wazo la kumuacha mke wake lakini pia anakomaa kumjenga aweze kuwapennda ndugu zake, msaada alioombwa ndio huo kuishi na mtoto kwahiyo ni malazi, chakula na afya.

Yeye binafsi anasema hawezi kukataa kumsaidia sababu kwao wameishi hivyo na sio yeye tu ambae anasaidia ndugu kwahiyo kama mwanamke hatomuelewa basi hatojali akiondoka maana anaona kabisa haendani na taratibu zake. Kwenye hili ndugu zake wote wako upande wake ila anasema kwa upande wa mke aliwahi kuongea na dada mtu inaonekana naye yuko upande wa mkewe.

Hapa tunachangia tu na kupeana uzoefu lakini kama nilivyosema awali maamuzi anayo muhusika, tusichukiane wala kukashifiana.
 
Leo naomba mumsaidie rafiki yangu kumshauri, mimi ni nimeshashauri kwa upande wangu lakini nataka kuona fikra za watu zaidi.

Jamaa ana mke na watoto, hivi karibuni kaka yake alipoteza kazi ndugu wakamuomba asaidie kulea mtoto mmoja ambaye alikuwa kidato cha pili. Jamaa alimshirikisha mke wake kuhusu mgeni huyo mke akakubali lakini inaonekana alikubali kwa shingo upande.

Kwa sasa sio siri tena mwanamke kasema wazi kabisa hataki kuishi na huyo mtoto tena akaenda mbali zaidi kampigia simu mama wa mtoto kumueleza yeye hawezi kuishi na mtoto wake. Habari zikamfikia jamaa akashangaa sana aliporudi kumlaumu mwanamke kwanini amefanya hivyo mwanamke kaja juu na kusema hata yeye ana maamuzi kwenye familia na msimamo wake ndio huo, hataki kuishi na huyo mtoto.

Jamaa kabembeleza sana mke akawa kama kaelewa kumbe bado. Hivi juzi kalianzisha tena na sasa amefika mbali kamwambia mume wake achague moja aidha kuishi na yeye(mke) ama mtoto wa ndugu yake........

Mzozo uko hapo, mimi nilimshauri kama hana uwezo wa kumlea huyo mtoto amrudishe kwao lakini si kwasababu ya kukataliwa na mke wake maana hata yeye hajui kesho yake. Jamaa alinijibu uwezo anao maana mtoto anasoma shule za serikali halipi ada hata mia zaidi ya uniform na vifaa vya shule.

Kama nimekosea naombeni sababu, bado tuna nafasi ya kumsaidia jamaa. Kwa ndugu upande wa mume na narafiki zake wanashangaa sana maamuzi ya mwanamke lakini kwa ndugu wa mke anasema zaidi ya 80% wanamsapoti mwanamke 🤔
Huyo siyo mwanamke ni jini mla watu,

Fukuza HARAKA hilo shetani.
 
Kama wazazi wapo hai wamsaidie akiwa kwao.

Kwanza inaepusha mengi sana.......

Pia mtoto anakuwa comfortable na famikia yake
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom