Mke anaweza kukuharibia mafanikio maishani

Mke anaweza kukuharibia mafanikio maishani

Brother mnyakyusa wako anakupa stress sana....mbombongafu.
 
Mmeulizwa mke akidai haki sawa utamnyima kama hautaki kuhudumia kila kitu? Hili swali hamjaliona au?
 
Naona huu mtazamo ni wa zamani sana, maisha yamebadilika sana, binafsi mzee alifariki nikiwa na 13 yrs japo nna wadogo 2, na dada aliyenizidi 1.5 yr, home Hanna kilichobadilika, tuliendelea kusoma na maisha kwa ujumla yaliendelea vzuri, kama mama angekuwa na huu mtazamo wa kutunzwa na mumewe, tusingetoboa, kutunzwa kupo, bytheway hapo zamani kutunzwa kulimaanisha chakula (basic), mavazi (basic), na makazi (basic), nadhani hata leo mkioana mime aweze kutoa hayo ya msingi kinachoongezeka hapo liwe jukumu la pamoja, sio mwanamke mshahara wote uishie saluni na duka la nguo, mke ajue anawajibika kwa familia beyond kutoa uroda na kupika, by the way nowadays mpishi ni house girl kwenye nyumba nyinhi
Kwahiyo unamaanisha kwenye ndoa mwanamke ndiyo ana majukumu mengi kuliko mwanaume? Au mimi ndiyo sijaelewa?
 
Kwahiyo unamaanisha kwenye ndoa mwanamke ndiyo ana majukumu mengi kuliko mwanaume? Au mimi ndiyo sijaelewa?
Hapana, ni jukumu la msingi la mwanaume kuhudumia familia, ila mwanamke awe msaidizi yani ashiriki moja kwa moja kuhudumia familia, kama anaingiza kipato, kipato chake kihusike moja kwa moja kuhudumia familia, kama haingizi kipato achangamke kuingiza kipato, yani majukumu ya familia yabebwe na wrote, japo mmoja atakuwa kuongozi
 
Yamenikuta jamani mke wangu hataki kujishughulisha kabisa kisa ni mrembo sana nadhani nikiwa kazini wananichapia. Maendeleo yamekwama kabisa
Pole,Mwanamke Tabia.
 
Mmeulizwa mke akidai haki sawa utamnyima kama hautaki kuhudumia kila kitu? Hili swali hamjaliona au?
Kwanini unahusisha kumpa haki sawa na kumhudumia, haki apewe, na majukumu atimize, ni sawa na uhusiano wa baba na watoto wake, mtoto akikosea haumuadhibu kwa kutompa chakula,
 
Ulikuwa unamfahamu hivyo kabla ya kumuoa?
Yamenikuta jamani mke wangu hataki kujishughulisha kabisa kisa ni mrembo sana nadhani nikiwa kazini wananichapia. Maendeleo yamekwama kabisa
 
Hapana, ni jukumu la msingi la mwanaume kuhudumia familia, ila mwanamke awe msaidizi yani ashiriki moja kwa moja kuhudumia familia, kama anaingiza kipato, kipato chake kihusike moja kwa moja kuhudumia familia, kama haingizi kipato achangamke kuingiza kipato, yani majukumu ya familia yabebwe na wrote, japo mmoja atakuwa kuongozi
Kwahiyo wewe mume uhudumie familia tu ila mke ahudumie familia na bado afanye na kazi za ndani ??
 
Kwanini unahusisha kumpa haki sawa na kumhudumia, haki apewe, na majukumu atimize, ni sawa na uhusiano wa baba na watoto wake, mtoto akikosea haumuadhibu kwa kutompa chakula,
Mkuu hebu tusizunguke sana sote tunafahamu kuwa kwa tamaduni za kiafrika ilikuwa mwanaume ndiye anayetafuta pesa na kuhudumia familia wakati mwanamke ndiye anayefanya kazi za ndani na kulea familia

Sawa mnasema siku hizi dunia imebadilika sasa hiyo dunia mbona mnaibadilisha kwa upande wa mwanamke tu ila kwa upande wa mwanaume hamuibadilishi maana mnataka wanawake wawasaidie majukumu yenu ya kutafuta pesa ila ninyi hamtaki kuwasaidia majukumu yao ya kufanya kazi za ndani
 
Kwahiyo wewe mume uhudumie familia tu ila mke ahudumie familia na bado afanye na kazi za ndani ??
Inategemea na mazingira specific ya hapo kwako, familia nyingi nnazoziona sikuhizi mjini zina msaidizi wa ndani na mama anafanya shughuli ya kumuingizia hela, hyo hela anayoingiza itumike kwenye familia, hata hzo kazi za ndani kwani zinafanyika Siku nzima, huo muda wa ziada alio nao utumike kwa maufaa ya familia, maisha yamebadilika, enzi hizo wanawake wanakaa tu home akisubiri kuhudumiwa mahitaji yalikuwa machache sana, hakukuwa na shule, ukiumwa huendi hospitality, hamna bili za maji na umeme, chakula kinalimwa tul shamba, sikuhizi kila kitu kinanunuliwa, maisha yamebadilika hivyo jamii ibadilike pia,
 
Mkuu hebu tusizunguke sana sote tunafahamu kuwa kwa tamaduni za kiafrika ilikuwa mwanaume ndiye anayetafuta pesa na kuhudumia familia wakati mwanamke ndiye anayefanya kazi za ndani na kulea familia

Sawa mnasema siku hizi dunia imebadilika sasa hiyo dunia mbona mnaibadilisha kwa upande wa mwanamke tu ila kwa upande wa mwanaume hamuibadilishi maana mnataka wanawake wawasaidie majukumu yenu ya kutafuta pesa ila ninyi hamtaki kuwasaidia majukumu yao ya kufanya kazi za ndani
Sijui kwako, ila naona wengi sikuhizi tunaajiri wasaidizi wa ndani, sikuhizi MTU akipata mtoto tu analeta house girl kumsaidia mama kulea, zamani hiyo haikuwepo, mama analea watoto kibao na shamba anaenda
 
Inategemea na mazingira specific ya hapo kwako, familia nyingi nnazoziona sikuhizi mjini zina msaidizi wa ndani na mama anafanya shughuli ya kumuingizia hela, hyo hela anayoingiza itumike kwenye familia, hata hzo kazi za ndani kwani zinafanyika Siku nzima, huo muda wa ziada alio nao utumike kwa maufaa ya familia, maisha yamebadilika, enzi hizo wanawake wanakaa tu home akisubiri kuhudumiwa mahitaji yalikuwa machache sana, hakukuwa na shule, ukiumwa huendi hospitality, hamna bili za maji na umeme, chakula kinalimwa tul shamba, sikuhizi kila kitu kinanunuliwa, maisha yamebadilika hivyo jamii ibadilike pia,
Sijui kwako, ila naona wengi sikuhizi tunaajiri wasaidizi wa ndani, sikuhizi MTU akipata mtoto tu analeta house girl kumsaidia mama kulea, zamani hiyo haikuwepo, mama analea watoto kibao na shamba anaenda
Sasa mbona hata akiwepo housegirl bado mnalalamika kuwa mke anamuachia kazi zote housegirl?? Na mnaenda mbali zaidi na kutembea na hao mahousegirl kwa kisingizio cha kuwa wanafanya majukumu yote anayotakiwa afanye mke??

Sasa hebu nikuulize wewe unaona ni sawa mume na mke wote wanatoka asubuhi lakini mke ndiyo afanye usafi na aandae chai halafu wote mnarudi usiku ila mke ndiyo aingie jikoni kupika na kuosha vyombo wakati huo wewe umekaa tu?? Halafu bills zikija mnalipa pasu kwa pasu na ada za watoto mnalipa pasu kwa pasu hiyo kwako unaona ni sawa??
 
Sasa mbona hata akiwepo housegirl bado mnalalamika kuwa mke anamuachia kazi zote housegirl?? Na mnaenda mbali zaidi na kutembea na hao mahousegirl kwa kisingizio cha kuwa wanafanya majukumu yote anayotakiwa afanye mke??

Sasa hebu nikuulize wewe unaona ni sawa mume na mke wote wanatoka asubuhi lakini mke ndiyo afanye usafi na aandae chai halafu wote mnarudi usiku ila mke ndiyo aingie jikoni kupika na kuosha vyombo?? Halafu bill zikija mnalipa pasu kwa pasu na ada za watoto mnalipa pasu kwa pasu hiyo kwako unaona ni sawa??
Huyo anaelalamika anakosea, inategemea na kazi, kama house girl anafua boxer zangu hapo tatizo, ila chakula apike tu, wote kutoka asubui ni poa tu, ndo maisha ya sasa, ilimradi nishaajiri mtu nyumbani , tatizo halipo
 
Huyo anaelalamika anakosea, inategemea na kazi, kama house girl anafua boxer zangu hapo tatizo, ila chakula apike tu, wote kutoka asubui ni poa tu, ndo maisha ya sasa, ilimradi nishaajiri mtu nyumbani , tatizo halipo
Haya unaona sasa ndiyo yale yale ninayoyasemea!! Yaani mke anakusaidia kutafuta hela na kuhudumia familia ila unataka akufulie na boxer kwani wewe unashindwa??

Na je kama unashindwa ni kipi hasa kinachokufanya ushindwe hadi utake mke akufulie?? Maana kumbuka kama ni kazi wote mnafanya mnatoka muda mmoja na mnarudi muda mmoja na pesa za matumizi wote mnachangia nusu kwa nusu!!
 
Hapana, ni jukumu la msingi la mwanaume kuhudumia familia, ila mwanamke awe msaidizi yani ashiriki moja kwa moja kuhudumia familia, kama anaingiza kipato, kipato chake kihusike moja kwa moja kuhudumia familia, kama haingizi kipato achangamke kuingiza kipato, yani majukumu ya familia yabebwe na wrote, japo mmoja atakuwa kuongozi
Ili mume apate salio la kuhonga? Hiyo hela bora nikajengee kodi ale mamaangu.
 
Back
Top Bottom