Mke ajiua kwa sumu ya Wadudu baada ya kupekua na kusoma SMS kwenye simu ya mumewe

View attachment 2809543
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma (ACP) Marco G. Chilya akielezea kuhusu tukio hilo

Mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Marietha Bosco Sagana (32) Mkazi wa Kitongoji cha Matarawe, Kijiji cha Marungu Kata ya Tingi Tarafa ya Mpepo, Wilaya ya Nyasa amefariki Dunia wakati anapatiwa matibabu baada ya kwa kunywa sumu ya kuulia Wadudu chanzo kikiwa ni wivu wa Mapenzi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Marco G. Chilya amesema tukio hilo limetokea Novemba 8, 2023 Saa mbili usiku, ambapo mume wa marehemu alikuwa ameenda Shamba lakini alisahau simu yake nyumbani ndipo Marietha (marehemu) alivyoiona simu hiyo akaanza kuipekuwa.
View attachment 2809557
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma (ACP) Marco G. Chilya
Marietha alisoma meseji zote ikiwemo za WhatsApp na akafanikiwa kukuta jumbe za mume wake akiwasiliana na mwanamke Mwingine ndipo Marehemu alishindwa kuvumilia, hivyo akachukua Dawa ya Kuulia Wadudu ya Mahindi (ACTERIC) ambayo iliandaliwa kwa matumizi ya Shamba na kuinywa.

Baada ya kutenda tukio hilo majirani wanaoishi nae waligundua kitendo alichokifanya marehemu baada ya kuwaambia kuwa amekunywa dawa ya wadudu ambapo wakachukua uamuzi wa kumkimbiza Hospitali ya Mission Maguu ndipo akafariki Dunia wakati akipatiwa matibabu.
Kwa kilichomkuta hatarudia kamwe!!
 
View attachment 2809543
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma (ACP) Marco G. Chilya akielezea kuhusu tukio hilo

Mwanamke mmoja aliyefahamika kwa jina la Marietha Bosco Sagana (32) Mkazi wa Kitongoji cha Matarawe, Kijiji cha Marungu Kata ya Tingi Tarafa ya Mpepo, Wilaya ya Nyasa amefariki Dunia wakati anapatiwa matibabu baada ya kwa kunywa sumu ya kuulia Wadudu chanzo kikiwa ni wivu wa Mapenzi.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Marco G. Chilya amesema tukio hilo limetokea Novemba 8, 2023 Saa mbili usiku, ambapo mume wa marehemu alikuwa ameenda Shamba lakini alisahau simu yake nyumbani ndipo Marietha (marehemu) alivyoiona simu hiyo akaanza kuipekuwa.
View attachment 2809557
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ruvuma (ACP) Marco G. Chilya
Marietha alisoma meseji zote ikiwemo za WhatsApp na akafanikiwa kukuta jumbe za mume wake akiwasiliana na mwanamke Mwingine ndipo Marehemu alishindwa kuvumilia, hivyo akachukua Dawa ya Kuulia Wadudu ya Mahindi (ACTERIC) ambayo iliandaliwa kwa matumizi ya Shamba na kuinywa.

Baada ya kutenda tukio hilo majirani wanaoishi nae waligundua kitendo alichokifanya marehemu baada ya kuwaambia kuwa amekunywa dawa ya wadudu ambapo wakachukua uamuzi wa kumkimbiza Hospitali ya Mission Maguu ndipo akafariki Dunia wakati akipatiwa matibabu.
Na wengine wakome 😂😂😂

Huyo alikuwa anawaambia wenzie kwamba yeye ni.pisi Kali 🤣🤣
 
Mtumishi Mwamposa alifundisha kuwa wanawake acheni kusoma sms za wanaume zenu, hata mpambe akikwambia twende ukamfumanie mumeo Loji ya pale kataa usiende, sababu mwanamke eventually ndiye atakuwa victim.

Mwanaume mwingine ukienda kumfumania anakuacha atakwambia umemdhalilisha.
 
Jamani wanaume mtatumaliza! Hadi wa vijijini?
Sijui huyo dada alikutana na nini huko masikini?
Halafu alisoma meseji zote hadi za WhatsApp!

Apumzike kwa amani!
Japo mimi sitojiua, siwezi kumwachia mchepuko mume.
Mambo mengine yanasikitisha sana. Nimekumbuka visa viwili vilivyotokea mkoani Kilimanjaro miaka ya nyuma. Enzi hizo ulizuka mtindo wa watu kujiua kwa kunywa dawa ya kunyunyizia kahawa ikiitwa DDT. Kisa cha kwanza kilikuwa hiví: Dada mmoja aliudhiwa na mama yake jambo dogo kabisa akajiua kwa kunywa hiyo dawa. Siku ya mazishi mmoja ya vijana waliokuwa wanachimba kaburi alikuwa amelewa huku anakandia na kumtukana sana yule marehemu, akisema inakuwaje mtu na akili zake ajiue kwa sumu. Kupita miezi miwili tukasikia naye amejiua kwa hiyo hiyo sumu. Tulipigwa mshangao. Kisa cha pili: Mama mmoja alikuwa anadai anateswa na mama mkwe wake hivyo siku moja akaibugia hiyo sumu. Watu waliwahi kumpeleka hospital na akapona lakini mara alipofikishwa hospital aliharisha wale wadudu wanaoitwa tegu fundo kubwa kweli, akatoa na yale ma-vichwa yake yote.

1699640932975.jpeg
 
Mtumishi Mwamposa alifundisha kuwa wanawake acheni kusoma sms za wanaume zenu, hata mpambe akikwambia twende ukamfumanie mumeo Loji ya pale kataa usiende, sababu mwanamke eventually ndiye atakuwa victim.

Mwanaume mwingine ukienda kumfumania anakuacha atakwambia umemdhalilisha.
Sio swala la wanawake tuu ni swala la wote
 
Sio swala la wanawake tuu ni swala la wote



Lakini Victims wengi huwa ni wanawake.

Wanaoenda Nyumba za ibada kuomba kurudiana na watalaka wao ni wanawake kwa zaidi ya asilimia 90 na sio wanaume.

Sasa anamwambia wajifunze kuzuia matengano badala ya kutumia ujinga Halafu baada ya muda anataka kurudiana na mumewe wakati Kama alianzisha mahusiano mengine unakuta yameweka mizizi.

Na Ukitaka kurudiana manake ukubali kuwa hautamfuatilia Tena na Kama Kuna mtoto kazaliwa umuelewe.
 
Lakini Victims wengi huwa ni wanawake.

Wanaoenda Nyumba za ibada kuomba kurudiana na watalaka wao ni wanawake kwa zaidi ya asilimia 90 na sio wanaume.

Sasa anamwambia wajifunze kuzuia matengano badala ya kutumia ujinga Halafu baada ya muda anataka kurudiana na mumewe wakati Kama alianzisha mahusiano mengine unakuta yameweka mizizi.

Na Ukitaka kurudiana manake ukubali kuwa hautamfuatilia Tena na Kama Kuna mtoto kazaliwa umuelewe.
Wanaume ndio Wanaongoza kujiua, wanawake Huwa ni nadra sana
 
Mwanamke kuolewa sio kwamba ndio umefungiwa kila kitu kwa huyo Mwanaume.

Wewe kama binadamu umebeba kusudi la maisha yako binafsi na you are 100% responsible for your life no one to help you.

Mwanamke anatakiwa kuwajibika, kuzalisha mali, kuwa na maisha na sio kuwaza mume na kumtafuta makosa na sababu.

Avoid idle mind.
 
Back
Top Bottom