Muuza Kangala
JF-Expert Member
- Jul 21, 2021
- 1,126
- 4,169
MKAZI wa Kijiji cha Gininga wilayani Busega mkoani Simiyu, Luli Shibone (29) amefariki dunia baada ya kunywa sumu ya kuulia wadudu waharibifu wa mazao iitwayo Celphos, baada ya mume wake kupekua simu wakati akiwa amelala usiku na kubaini mawasiliano kati yake na mwanaume mwingine.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu, Edith Swebe amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, na amesema Jeshi hilo linaendelea kufanya uchunguzi wa kifo cha Luli Shibone ambaye amejiua kwa kunywa sumu ya kuulia wadudu waharibifu.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Simiyu, Edith Swebe amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, na amesema Jeshi hilo linaendelea kufanya uchunguzi wa kifo cha Luli Shibone ambaye amejiua kwa kunywa sumu ya kuulia wadudu waharibifu.