Mkataba wa TFF kuipa TBC haki miliki ya kutangaza live mechi zote za NBC premier league ni wa kishenzi

Izia maji

JF-Expert Member
Dec 1, 2021
2,155
3,797
Kwanza mkataba huu ni wa kifisadi na unazinyima haki ya kibiashara radio za jamii. TBC ni redio ya umma na ina vyanzo vingi vya mapato ikiwa na pamoja na kodi zetu hivyo kuipa hati miliki hiyo siyo haki kabisa kwa radio binafsi ambazo pia zingependa kuwapa uzoefu watangazaji wake na kuongeza mapato.

Pili katika maeneo mengi ya mikoani usikivu wake siyo mzuri na mengine haisikiki kabisa hivyo wananchi hutegemea redio za jamii.

Tatu inapotokea shughuli za kitaifa kuwa muda mmoja na mechi TBC hutoa umuhimu katika shughuli na kuhamishia matangazo ya mpira TBC FM ambayo ni hafifu sana katika kuisikiliza.

Nne mkataba huu unawanyima haki wafanyabiashara wa mikoani kutangaza biashara zao na hasa katika mechi za mikoani ambako ingekuwa rahisi kwao kutangaza kupitia redio za jamii ambazo zinasikika vizuri.

Kwa hoja hizi chache na nyingine nyingi ambazo zijazitaja nashauri TFF kupitia upya mkataba huu ili ikiwezekana kila mechi ipate mkataba wake wa kuitangaza na hasa mechi za mikoani.
 
mkuu si iltangazwa tenda. tbc wanaweka hela au ulikuwa bado uko kwenu Tandahimba huko? tbc wanafanya biashara pia.
Usikurupuke na kujifanya punguani kwani hufahamu TBC inatumia kodi zetu? Redio za jamii zina ubavu wa kushindana na chombo kinachotumia fedha za umma? Hufahamu kuwa TBC haisikiki nchi nzima?

Kwa nini kwa mechi za mikoani zisingeshindanishwa redio za jamii zilizopo huko?
 
Usikurupuke na kujifanya punguani kwani hufahamu TBC inatumia kodi zetu? Redio za jamii zina ubavu wa kushindana na chombo kinachotumia fedha za umma? Hufahamu kuwa TBC haisikiki nchi nzima?

Kwa nini kwa mechi za mikoani zisingeshindanishwa redio za jamii zilizopo huko?
Amenunua haki ya matangazo ya mpira, ambayo faida yake inapatikana kwa wadhamini wanaotangaza bidhaa zao.So kwa kifupi hiyo hela haijapotea kwani inatengeneza faida.

Halafi hii biashara hamna redio iliyonyimwa haki ya kutangaza hizi mechi, kama kuna redio inataka waongee na TBC na wawalipe wapewe haki ya kutangaza. Mfano UFM imenunua haki matangazo ya kutangaza hizo mechi kupitia redio kutoka TBC.

So hii ni biashara wakiweka mzigo wanapewa haki ya kutangaza mpira.
 
Kulalamika imekuwa tabia sugu kwa watanzania
Yani Wewe mkurupushe muambie kuna ufisadi mkubwa kwenye oxygen, ataanza kulalamika kwa namna ya ajabu
Kwa hiyo watu waache kulalamikia mikataba mibovu kwa kuwa malalamiko yamekuwa mengi!

Ebo!
 
Amenunua haki ya matangazo ya mpira, ambayo faida yake inapatikana kwa wadhamini wanaotangaza bidhaa zao.So kwa kifupi hiyo hela haijapotea kwani inatengeneza faida.

Halafi hii biashara hamna redio iliyonyimwa haki ya kutangaza hizi mechi, kama kuna redio inataka waongee na TBC na wawalipe wapewe haki ya kutangaza. Mfano UFM imenunua haki matangazo ya kutangaza hizo mechi kupitia redio kutoka TBC.

So hii ni biashara wakiweka mzigo wanapewa haki ya kutangaza mpira.
Kwa nini mikataba isiwe na TFF? Huoni huo ni ufisadi?
 
Kwa nini mikataba isiwe na TFF? Huoni huo ni ufisadi?
Hamna ufisadi huo ndio utaratibu na zipo wazi kama hujui hata Azam alicompete na Star times mwaka jana ila Azam dau lake likawa zuri na hata hao TBC kabla ya kupewa alicompete akashinda so yy ndiye mwenye haki ukitaka mfuate yy au subiri mkataba wake ukiisha then mkacompete tena TFF akiwaita.
 
Usikurupuke na kujifanya punguani kwani hufahamu TBC inatumia kodi zetu? Redio za jamii zina ubavu wa kushindana na chombo kinachotumia fedha za umma? Hufahamu kuwa TBC haisikiki nchi nzima?

Kwa nini kwa mechi za mikoani zisingeshindanishwa redio za jamii zilizopo huko?
Mjomba kama una redio yako fuata utaratibu Utangaze mpira.
TBC wanafanya biashara....
Wameshinda tenda ....
Wamelipa pesa, tatizo liko wapi?
 
Mjomba kama una redio yako fuata utaratibu Utangaze mpira.
TBC wanafanya biashara....
Wameshinda tenda ....
Wamelipa pesa, tatizo liko wapi?
Tatizo liko kwenye muda miaka 10 ni mingi mno! Pili usikivu wa TBC siyo mzuri na haijaenea nchi nzima!
 
Hamna ufisadi huo ndio utaratibu na zipo wazi kama hujui hata Azam alicompete na Star times mwaka jana ila Azam dau lake likawa zuri na hata hao TBC kabla ya kupewa alicompete akashinda so yy ndiye mwenye haki ukitaka mfuate yy au subiri mkataba wake ukiisha then mkacompete tena TFF akiwaita.
Utaratibu ndiyo tunaoupigia kelele unapaswa kuboreshwa ili washiriki wawe wengi zaidi na kuwezesha hata timu za mpira kunufaika zaidi kwa mapato!
 
Utaratibu ndiyo tunaoupigia kelele unapaswa kuboreshwa ili washiriki wawe wengi zaidi na kuwezesha hata timu za mpira kunufaika zaidi kwa mapato!
TFF waliwashirikisha wengi kwani tenda ilitangazwa hadharani TBC ndiye aliyeshinda mbona hamna ubaya.
 
Back
Top Bottom