Bams
JF-Expert Member
- Oct 19, 2010
- 16,555
- 41,066
Mkataba ule wa bandari, nasema ni wa kishenzi kwa sababu unapima uwezo wa Watanzania katika Kufikiri. Kila mwenye akili anajua kuwa mtu yeyote ambaye yupo kwenye utimamu wa akili hawezi kuukubali mkataba kama ule.
Nani atakubali kitu chake ambacho amewekeza trilioni kadhaa ampe mtu anayekodi halafu yeye awe na umiliki 0%?
Nani mwenye akili timamu atakubali etu abadilishe sheria za nchi kwa sababu ya mwekezaji mmoja?
Nani mwenye akili timamu atakubali, umpe mpangaji umiliki wa 100% ili achukue faida yote yeye pekee yake, halafu tena na kodi alipe pungufu ya wengine, wakati wenzake wote kwenye mali za asili wanatoa umiliki wa bure kwa Serikali wa 16%, wanalipa kodi 30%, wanalipa mrabaha, n.k. Yeye anapewa mradi ambao tayari kuna uwekezaji mkubwa, anakupa umiliki 0%, hataki kulipa kodi ya 30% (anataka alipe pungufu) ambayo wengine wanalipa, halipi mrabaha, apewe ardhi yoyote anayoitaka na fidia tulipe sisi (wakati wawekezaji wengine wote gharama ya fidia ya ardhi huwa wanalipa wenyewe), ana nini cha pekee mpaka apewe hayo yote?
Eti anawekeza dola 500m. Barrick kule Buly kwenye mgodi mmoja waliwekeza zaidi ya dola 600m. Dangote uwekezaji wa awali likuwa zaidi ya dola 700m. Bomba la gas zaidi ya dola 1billion. Wachina kule Liganga na Mchuchuma walisema watawekeza dola bilioni 7 (japo hawa nao ni wahuni wengine, mpaka leo hawajawekeza hata dola 1m). Tulimkataa mwekezaji wa uhakika Rio Tinto aliyetaka kuwekeza dola bilioni 3 kwa kudanganywa na Wachina kuwa watawekeza dola bilioni 7, kumbe ni ya maneno, nalo hilo ni uzembe wa Serikali.
Nayanukuu maneno ya Baba wa Taifa, Mwakimu Nyerere:
"Mtu akikuambia jambo la kijinga, na wewe ukakubali, anakudharau"
"Ukiwa mjinga, unaweza kuwa na almasi yako, halafu anakuja mtu na kipande cha chupa, anakuambia chukua hiki wewe, hicho ulichoshika ni chupa, chukua hii almasi, kwa kuwa wewe ni mjinga, unampa almasi yako, unachukua kipande cha chupa halafu unaenda unachekelea kama zuzu"
Waarabu wa DP wametufanya waafrika wa Tanzania ni mazuzu. Wanaona ule ubinadamu wetu wa kale uliofishwa, na kisha kufanywa bidhaa kama zilivyo nyanya au vitunguu, haujatutoka mpaka leo. Ndio maana kuna hizo tetesi za wabunge wale batili kununuliwa. Utu wao na utashi wao umefutwa na kugeuzwa kuwa ni bidhaa.
Kama DP watakuwa wamejirudi na kuwaona Watanzania ni binadamu kama walivyo wao, yaani wana akili na utashi, ule mkataba wa kishenzi utupwe. Majadiliano yaanze upya yakiwahusisha watu wenye weledi, maadili na wanaojitambua. Mbarawa na kundi lake, na wale wabunge bidhaa wasihusike kwa chochote.
Wakikishindwa hilo, waende zao. Japo bandari ni kichaka cha rushwa, na kama taasisi nyingine za umma zilivyo, ni mahali pasipo na ufanisi kutokana na ulegevu wa Serikali, kuna siku nchi itapata serikali imara iliyo thabiti, na viongozi thabiti, bandari na mashirika mengine ya umma, vitasimama na kufanya kazi stahili kwa namna istahiliyo.
Tatizo letu kubwa siyo bandari, siyo ATCL, siyo TANESCO, BALI NI UBOVU NA ULEGEVU WA SERIKALI, AMBAYE NDIYE MSIMAMIZI MKUU. Na ubovu huu wa Serikali haujaanza wakati wa Rais Samia, umekuwepo wakati wote, na unaendelezwa mpaka sasa.
Nani atakubali kitu chake ambacho amewekeza trilioni kadhaa ampe mtu anayekodi halafu yeye awe na umiliki 0%?
Nani mwenye akili timamu atakubali etu abadilishe sheria za nchi kwa sababu ya mwekezaji mmoja?
Nani mwenye akili timamu atakubali, umpe mpangaji umiliki wa 100% ili achukue faida yote yeye pekee yake, halafu tena na kodi alipe pungufu ya wengine, wakati wenzake wote kwenye mali za asili wanatoa umiliki wa bure kwa Serikali wa 16%, wanalipa kodi 30%, wanalipa mrabaha, n.k. Yeye anapewa mradi ambao tayari kuna uwekezaji mkubwa, anakupa umiliki 0%, hataki kulipa kodi ya 30% (anataka alipe pungufu) ambayo wengine wanalipa, halipi mrabaha, apewe ardhi yoyote anayoitaka na fidia tulipe sisi (wakati wawekezaji wengine wote gharama ya fidia ya ardhi huwa wanalipa wenyewe), ana nini cha pekee mpaka apewe hayo yote?
Eti anawekeza dola 500m. Barrick kule Buly kwenye mgodi mmoja waliwekeza zaidi ya dola 600m. Dangote uwekezaji wa awali likuwa zaidi ya dola 700m. Bomba la gas zaidi ya dola 1billion. Wachina kule Liganga na Mchuchuma walisema watawekeza dola bilioni 7 (japo hawa nao ni wahuni wengine, mpaka leo hawajawekeza hata dola 1m). Tulimkataa mwekezaji wa uhakika Rio Tinto aliyetaka kuwekeza dola bilioni 3 kwa kudanganywa na Wachina kuwa watawekeza dola bilioni 7, kumbe ni ya maneno, nalo hilo ni uzembe wa Serikali.
Nayanukuu maneno ya Baba wa Taifa, Mwakimu Nyerere:
"Mtu akikuambia jambo la kijinga, na wewe ukakubali, anakudharau"
"Ukiwa mjinga, unaweza kuwa na almasi yako, halafu anakuja mtu na kipande cha chupa, anakuambia chukua hiki wewe, hicho ulichoshika ni chupa, chukua hii almasi, kwa kuwa wewe ni mjinga, unampa almasi yako, unachukua kipande cha chupa halafu unaenda unachekelea kama zuzu"
Waarabu wa DP wametufanya waafrika wa Tanzania ni mazuzu. Wanaona ule ubinadamu wetu wa kale uliofishwa, na kisha kufanywa bidhaa kama zilivyo nyanya au vitunguu, haujatutoka mpaka leo. Ndio maana kuna hizo tetesi za wabunge wale batili kununuliwa. Utu wao na utashi wao umefutwa na kugeuzwa kuwa ni bidhaa.
Kama DP watakuwa wamejirudi na kuwaona Watanzania ni binadamu kama walivyo wao, yaani wana akili na utashi, ule mkataba wa kishenzi utupwe. Majadiliano yaanze upya yakiwahusisha watu wenye weledi, maadili na wanaojitambua. Mbarawa na kundi lake, na wale wabunge bidhaa wasihusike kwa chochote.
Wakikishindwa hilo, waende zao. Japo bandari ni kichaka cha rushwa, na kama taasisi nyingine za umma zilivyo, ni mahali pasipo na ufanisi kutokana na ulegevu wa Serikali, kuna siku nchi itapata serikali imara iliyo thabiti, na viongozi thabiti, bandari na mashirika mengine ya umma, vitasimama na kufanya kazi stahili kwa namna istahiliyo.
Tatizo letu kubwa siyo bandari, siyo ATCL, siyo TANESCO, BALI NI UBOVU NA ULEGEVU WA SERIKALI, AMBAYE NDIYE MSIMAMIZI MKUU. Na ubovu huu wa Serikali haujaanza wakati wa Rais Samia, umekuwepo wakati wote, na unaendelezwa mpaka sasa.