Kapeace
JF-Expert Member
- May 26, 2017
- 25,624
- 69,367
Maisha ni safariSikia dada yangu,huyo ni mmeo wala usihofie ule uongo. Kuna wakati wanaume huwa tunalazimika kudanganya baada ya kujua huyo mtu uliyenaye anataka kusikia nn! Yaani km mwanamke nampenda,na nnajua kuna vitu hapendi nitasema uongo kwenye hiyo category. Nikuhakikishie huyo mtu wala usihangaike na talaka,talaka ni makaratasi tu,mtakuwa mnachelewa tu kuanza kutengeneza familia. Kumbuka ndoa ya kanisani haina talaka. Mimi nilioa mwaka 1997,lkn kufikia mwaka 2005 ndoa yangu ilikuwa jehanam. Lkn nilivumilia kulinda heshima ya watoto wangu. Mwaka 2008,nilipata mtu na nikaanza naye urafiki nikiwa ndani ya ndoa. Sikuwa nimemuacha mke wangu,na muda mwingi niliutumia sana kwa mke wangu ingawa ukweli ndoa haikuwepo. Mwaka 2010 nikabahatika kupata mtoto na huyo rafiki yangu,huyu wa ndoa hata kujamiiana tulikuwa tumeacha. Tulibaki hivyo,na hakujua km nimezaa nje na nilikuwa kila ijumaa jioni naenda kwa mpenzi wangu narudi jpili. Mwaka 2013 niliumwa jicho na kufanyiwa upasuaji,nilikuwa nahitaji mtu mwenye upendo nami kunihudumia. Hapo ndo ulikuwa mtihani. Nilichagua kwenda kwa mke wangu wa ndoa baada ya kutoka hospital. Lkn kilichonipata Mungu anajua,siku 3 baadae nikaita taxi nikatimkia Kwa mpenzi wangu. Na siku iliyofuata nikampigia simu mke wangu nikaweka wazi uhusiano wangu na kwamba tayari tulikuwa na mtoto wa miaka 3. Hakuweza kustahimili zile taarifa,kesho yake akapeleka canter akabeba kila kitu cha ndani na watoto wangu akawaacha hapo. Sikumfanya chochote,kesho yake nikaenda keko nikanunua fenicha zote mpya. Na maisha yanaendelea na yule aliyekuwa mpenzi wangu,ndo mke wangu hadi leo. Na huwezi amini yaani hapa naona km nimekutana naye jana tu. tunapendana ile mbaya na tayari tuna mtoto mwingine now ana miaka 4. Baada ya maelezo haya marefu,leo ukienda usirudi tena kule kwako..
Ndoa hizi ni kama kubet usiombe mkeka uchanike