mtafuta-maisha
JF-Expert Member
- Nov 5, 2016
- 1,982
- 2,915
Littleton, Colorado
Ilikuwa tarehe 30, mwezi wa 12 mwaka 1978, ambapo kama kawaida uwa ni msimu wa saruji katika maeneo mengi nchini Marekani ambapo saruji inakua ikianguka, ikiwa ni siku ya kawaida kama zilivyo siku nyingine kwa wakazi wa mji mdogo wa Littleton ulioko katika jimbo la Colorado waliamka na kuendelea na ratiba zao kama kawaida.
Wakati huu huu mji mdogo wa Littleton ulikuwa una wakazi wanaokadiriwa kufikia kiasi cha 40,000. Ulikuwa na mji mdogo kwa kipindi hiki ukiwa umepangiliwa vizuri na wenye utulivu wa hali ya juu ambapo ulifaa zaidi kwa watu wenye familia na watoto kwa ajili ya kuishi kwa kuwa mji huu kipindi hicho ulikuwa kati ya miji yenye matukio machache sana ya uhalifu. Kwa mwaka huo wa 1978, Littleton ilikuwa imekubwa na mauaji ya watu wawili na matukio ya uvamiji na uporaji matatu tu, hivyo utaona kiasi gani mji huu ulikuwa ni mji ambao ulikuwa na matukio machache sana ya uhalifu kwa wakati huo.
Katika familia zilizokuwa zikiishi katika mji huo kulikuwa na familia ya watu wanne ambao ni Robert Splingler akiwa na mkewe aliyejulikana kama Nancy na watoto wao wawili ambaye wakiume alijulikana kama David akiwa na umri miaka 17 huku wa kike akijulikana kama Suzan alikuwa na umri wa miaka 15. Robert akiwa ameajiliwa katika mamlaka ya usambazaji maji, Nancy yeye alikuwa mama wa nyumbani akiwa na jukumu la kulea familia na kuhakikisha majukumu yote ya nyumbani kama usafi, kupika, kufua n.k yanafanyika kila siku.
David yeye alikuwa anapendelea sana mziki huku akiwa anapenda san kupiga gitaa, wakati Nancy yeye alikuwa katika kipindi cha balehe hivyo muda mwingi alikuwa akiutumia kuwa na mpenzi wake ukizingatia muda huo ulikuwa kipindi cha likizo ambapo shule zilikuwa zimefungwa. Kwa mtazamo wa watu wengi hii ilionekana ni familia yenye furaha na ilikuwa ni familia iliyokamilika.
Hiyo tarehe 30, mwezi wa 12 ikiwa ni asubuhi, majirani wa familia ya Splingler wakiwa wameondoka kwa ajili ya likizo ya kuadhimisha sikukuu ya mwaka mpya, mpenzi wa Suzan ajulikanaye Tim aliyekuwa na umri wa miaka 16, aliamua kuja nyumbani kwao Suzan kumtembelea kama alivyozoea kufanya kila siku. Kawaida yao ilikuwa akifika nyumbani kwa akina Suzan alikuwa akichukua saruji na kurusha dirishani kwa Suzan mara tatu na Suzan alikuwa akisikia anakuja kumpokea nje ambapo anamuingiza chumbani kwake.
Siku hiyo baada ya kufika alifanya hivyo hivyo, lakini Suzan hakutokea, hivyo aliamua kuingia ndani kabisa na alishangaa kukuta nyumba ikiwa kimya kama vile hakuna mtu , alihisi uenda watakuwa bado wamelala kwakuwa wazo la kuwa wanaweza kuwa wamesafiri hakuwa nalo kwakuwa jana yake alikuwa na Suzan hakumwambia kama watasafiri na pia walipanga kuonana siku hiyo, na pia kama wangesafiri basi mlango ungekuwa umefungwa kwa funguo.
Tim aliamua kupanda ghorofani moja kwa moja kwenye chumba cha Suzan, na alipoingia chumbani alimuona Suzan akiwa amelala kitandani. Alianza kumuita akiwa kasimama mlangoni lakini Suzan hakuitika jambo lililomfanya Tim avue gloves alizokuwa kava na kumrushia lakini bado Suzan hakuitika wla kujitikisa. Tim aliamua kusogea karibu na kitanda na kwa mshangao ndipo alipogundua kuwa mwili wa Suzan ulikuwa kwenye dimbwi la damu huku akiwa na tundu la risasi kifuani. Tim alitoka chumbani kwa Suzan mbio na kukimbilia kwenye chumba cha David ili kumtaarifu alichokiona kwenye chumba cha mdogo wake, lakini alipofika alimkuta David naye akiwa kitandani kwake kalala kwenye dimbwi la damu pia, huku uso ukiwa umefunikwa na mto na kifuani kukiwa na tundu la risasi.
Kuona hivyo Tim alitoka ndani mbio na kwenda kupiga namba ya dharura 911, kuwataarifu polisi ambao walifika mara moja kwenye eneo la tukio. Askari polisi kutoka katika kituo cha polisi cha Arapahoe wanafika eneo la tukio na kukutana na hali ya tukio la kutisha. Kwa mazingira ya awali ya uchunguzi wa polisi ilionekana Suzan alikuwa kapigwa risasi ya kifuani kutoka kwenye bunduki iliyokuwa mbali kidogo kwa inches kadhaa toka alipokuwa amelala nah ii ilimfanya akate roho kwa haraka sana. David pia naye alikuwa kapigwa risasi moja tu kifuani kwake, ambayo iliondoa uhai wake.
Katika kuzidi kupekuwa nyumba, polisi walielekea upande wa chumba cha chini cha nyumba hiyo ambapo walikuta mwili wa Nancy ukiwa umekaa kwenye kiti kilichokuwa nyuma ya meza yenye type writer, huku kichwani kukiwa na tundu la risasi. Pembeni kidogo ya mwili wake, sakafuni kulikuwa na bunduki ndogo, na kwenye mashine ya type writer kulikuwa na karatasi, ambapo walipoichomoa waligundua ilikuwa ni barua iliyoonekana kuandikwa na Nancy akikiri juu ya kutenda mauaji hayo pamoja na sababu zilizomfanya kutekereza mauaji hayo kasha kujiua, na mwisho mwa hiyo barua ilikuwa imesainiwa kwa peni kwa kuewekewa herufi“n” ambapo polisi walihisi imetokana na herufi ya kwanza ya jina la Nancy.
Katika maelezo yaliyokuwa kwenye hiyo barua Nancy alidai ya kwamba alipata hiyo bunduki ya mumewe kwa bahati mbaya na alipoipata aliamua kutenda jambo hilo kwakuwa walikuwa wanataka kutengana na walikuwa wakibishana ni nani hasa atakayebaki na watoto na Nancy anadai hakuwa tayari kuishi bila watoto wake hivyo aliamua bora awaue nay eye ajiue.
Barua yote ilikuwa imechpwa kwa mashine isipokuwa saini ya herufi “n”, na kwa kuitazama haraka haraka ile ule ujumbe ulikuwa unatosha kutumika kama ushahidi kuwa Nancy ndiye alitekereza mauaji hayo ni kasha kujiua mwenyewe kwa sababu alizozitoa kwenye hiyo barua. Lakini polisi hawakutaka kufikia tamati haraka kwa kuchukulia huo ushahidi kama ndicho kigezo tosha cha kukubari kuwa Nancy ndiye katekereza mauaji.
Jack Swanburg, aliyekuwa mkuu wa kituo cha polisi cha Arapohoe, anadai kwamba kosa kubwa ambalo polisi wengi hufanya ni kufikia hitimisho kwa kufanya maamuzi yao binafsi pasipo kuwa na ushahidi wa kutosha au kutazama ushahidi wote uliopo. Anazidi kusema kwamba ukifanya upelelezi huku kichwani ukiwa tayari na hitimisho binafsi basi huo upelelezi lazima ukupe matokeo yasiyo sahihi.
Kutokana na polisi kutotaka kufikia hitimisho kwa kutumia tu ile barua waliyokuta kwenye type writer, waliendelea kukusanya ushahid wote ulionekana kuwa unaweza kusaidia katika kutatua kesi hiyo ambayo ilikuwa mbele yao. Mpiga picha wa polisi alianza zoezi la kupiga picha eneo lote la tukio na kama kawaida utaratibu wa upigaji picha uanza kwa kupiga picha eneo lote, kasha uendelea kwa kupunguza ukubwa wa eneo mpaka kufikia kupiga picha kitu kimoja kimoja mfano tundu la risasi peke yake, bunduki peke yake n.k.
Aina ya silaha iliyokutwa sakafuni pembeni ya Nancy ilikuwa bunduki ndogo ijulikanayo kama 38 caliber Smith Mansen, ambapo nayo ilipigwa picha na mpiga picha wa polisi. Bunduki ilikuwa kama foot sita kutoka mwili wa Nancy ulipokuwa umekaa pale nyuyma ya meza kwenye kiti. Hii ilikuwa siyo jambo la kawaida kwamba mtu ajipige risasi ya kichwa kasha bunduki idondoke umbali huo kutoka alipo.
Wakati wa mchana mara Robert ambaye hakuwa nyumbani anawasili na kukuta nyumba yake ikiwa imezungushiwa utepe wa njano kuashiria kwamba ni eneo ambalo limefungwa na polisi kwa ajili ya kuchukua ushahidi na kufanya upelelezi baada ya tukio la kiharifu kufanyika pale. Polisi wanamtaarifu juu ya mauaji yaliyotokea nyumbani kwake na anaonekana kusikitika sana huku akijawa na majonzi.
Pia anapoonyeshwa bunduki iliyotumika katika kutekereza mauaji hayo, anakubari kuwa ni bundukui yake na anadai kwamba hakuwa nyumbani wakati tukio hilo linatokea. Katika kuzidi kumhoji polisi wanapata picha tofauti juu ya familia ya Bwana Robert tofauti na ambavyo watu wanje hasa majirani walivyokuwa wakiiona. Majirani na watu waliokuwa wakimfahamu walikuwa wakidai kwamba Robert alikuwa mtu mzuri, mwenye roho nzuri, mpenda watu, mchangamfu, jirani mwema na baba mpenda familia. Lakini kiuhalisia polisi wanagundua hii ilikuwa tofauti na hali halisi katika familia hiyo baina ya Nancy na Robert. Hata wazazi wa nancy hawakuwa wakimkubari Robert walikuwa wanamuona kama siyo mtu sahihi kwa mtoto wao, pia ndani ya familia kulikuwa na ugomvi wa mara kwa mara baina ya wazazi hawa.
Katika mahojiano kati ya polisi na Robert, Robert anakiri kuwa walikuwa wana ugomvi wa kindoa kwa muda mrefu kiasi kwamba walikuwa wametengana kwa muda na kurudiana hivi karibuni. Anaendelea kudai kwamba chanzo cha huo ugomvi ilikuwa kwasababu Robert alikuwa na mahusiano na mwanamke mwingine ambaye alikuwa ni mfanyakazi mwenzake kule ofisini alipokuwa akifanya kazi. Anazidi kudai kwamba japo Nancy alikuwa hapendi uhusiano huo, ila hakutegemea kama anaweza kuchukua maamuzi hayo hata yeye amestaajabu na kuogopa kwa tukioo hilo. Robert anaonekana kutoa ushirikiano wa kutosha kwa polisi na anaweza kueleza kila kitu alichofanya na wapi alipokuwa siku nzima.
Anadai kwamba yeye na Nancy waliingia kwenye ugomvi wa mabishano siku hiyo asubuhi, hivyo aliamua kuondoka nyumbani na kwenda kuzurura kwa kuendesha gari mitaa mbalimbali ili kupunguza msongo wa mawazo na anadai alitumia kama saa moja au moja na nusu akiendesha gari, baada ya hapo aliamua kwenda sinema kutazama filamu. Kuthibitisha kuwa maelezo yake ni sahihi Robert anakubari kufanyiwa kipimo cha kupima uongo na ukweli. Majibu yanapotoka mtaalamu wa kusoma matokeo ya kipimo hicho anadai kuwa hayawezi kuwasaidia polisi maana hayaeleweki kabisa hivyo hawezi kusema kama alikuwa anongea ukweli au hapana.
Polisi wanaamua kumkagua Robert ili kuona kama wanaweza pata ushahidi wowote unaoweza kumfunga kwenye tukio hilo la mauaji, na kitu walichokuwa wanajaribu kujua ni kuchukua kipimo cha kuonyesha kama mwili wa Robert ulikuwa na mabaki ya mlipuka wa risasi (Gun Powder residue) nah ii ingedhirisha kuwa ni yeye aliyefyatua risasi, au alikuwa karibu wakati risasi inafyatuliwa au uenda aliishika ile bunduki baada tu ya kufyatua risasi.
Kwa kipindi hicho matokeo ya kipimo hicho yalikuwa yanachukua muda kupataikana, ambapo ilikuwa inachukua zaidi ya wiki moja mpaka matokeo kutolewa. Kutokana na kutokuwa na ushahidi na sababu yoyote ya kumshikiria, polisi walimuachia Robert huru, huku wakingojea matokeo ya kipimo cha mabaki ya vumbi la mlipuko wa risasi kutoka katika maabara kinayomilikiwa na kitengo makosa ya jinai cha Colorado
Lakini nyumba ya Robert ilikuwa bado imefungwa polisi wakiendeleakuichunguza kwa ajili ya ushahidi zaidi hivyo hakuruhusiwa kukaa pale, na kutokana na sababu hiyo mkuu wa kituo cha polisi Bwana Jack Swanburg alijitolea kumpa hifadhi Robert ya muda pale nyumbani kwake,na anadai alistaajabu kumuona Robert akiwa ni mtu mwenye utulivu wa hali ya juu kama vile hakuwa kapatwa na tukio la kuogofya la kufiwa na mkewe pamoja na watoto wake wawili tena katika mauaji ya kutisha.
Tarehe 3 mwezi wa 1 mwaka 1979, polisi wanahitimisha kuwa lile tukio lilitekelezwa na Nancy, lakini baada ya siku kadhaa maotkeo ya kipimo cha mabaki ya mripuko wa risasi kutoka yanadhihirisha kwamba Robert anajua zaidi kuliko ambavyo amewambia polisi. Kipimo kinaonyesha kwamba Robert alikuwa na mabaki ya vumbi la mripuko wa risasi wakati Nancy binafsi hakuwa na vumbi hilo mkononi jambo ambalo linaashiria kuwa huenda Robert ndiye aliyefyatua risasi hiyo au alikuwa karibu wakati inafyatuliwa au aliishika bunduki pale baada ya risasi kufyatuliwa.
Polisi wanamwita Robert tena kwa ajili ya mahojiano na mara hii anabadirisha hadithi na maelezo yake ya awali. Anadai kwamba alirudi nyumbani na kukuta tayari mauaji yamekwishatokea, na alipoelekea chumba cha chini alimkuta nancy akiwa amekwishajiua huku bunduki ikiwa karibu na mwili wake. Anadai aliikota akarudi nyumba na kusema Mungu wangu kasha aliidondosha na kutoka ndani amekimbia akaingia kwenye gari lake na kuondoka.
Siku ya tukio wakati polsii wakiendelea na uchunguzi, waligundua uwepo wa alama za matairi ya gari eneo la nyumba ya Robert ambazo zilionekana kuwa zilikuwa zimeachwa na gari ambalo lilikuwa limetoka pale muda siyo mrefu sana kutokana na ukweli kwamba kwakuwa saruji ilikuwa inadondoka kama zilikuwa namuda mrefu zingekuwa zimefunikwa na saruji tayari. Alama hizo zilikuwa zinaonyesha kuwa gari lilikuja na kasha likaondoka hivyo kulikuwa na set mbili za alama ya matairi kwenye saruji, na alama hizo walikuja kugundua kuwa ni alama za matairi ya gari la Robert. Kutokana na maelezo yake mapya na uwepo wa hizo alama, zilithibitisha kuwa Robert alikuwa akisema ukweli kuhusu kuja nyumbani kwake na kuondoka.
Polisi walimuondoa Robert kama mshukiwa wa mauaji hayo na kuhitimisha kabisa kuwa mtendaji alikuwa Nancy, ila familia ya Nancy haikukubari kabisa hili jambo wao waliamimini kwamba Robert anajua ukweli kuliko kile anachowambia polisi. Na mbaya zaidi wakati wazishi Robert alikuja na mwanamke wake kwenye mazishi ambapo miili ya marehemu ilichomwa moto. Watu waliokuwepo walishangaa kwakuwa hakuonyesha dalili zozote za majonzi kama mtu ambaye kapoteza familia yake katika mauaji akiwemo mke na watoto wake wawili.
Pia kabla ya kifo cha Nancy alikuwa amemwandikia binamu yake barua akimwambia kuwa kwasasa yeye na Robert wanaelewana na wako vizuri akiwa anamwambia mipango yake ya baadae na maisha ya mbeleni, jambo ambalo familia ya Nancy inadai kwamba linaonyesha kuwa Nancy hakuwa na mpango wa kujiua ama kuua watoto ndiyo maana alikuwa akizungumzia mipango ya baadaye kweye barua ile.
Hivyo maneno ya chini chini yaliendelea kuzungumzwa na watu mbalimbali katika mji wa Littleton juu ye uhusika wa Robert katika mauaji hayo, lakini japo kuna watu walikuwa na mashaka akiwemo baadhi ya maafisa polisi juu ya Robert kuhsuika katika mauaji hayo, polisi waliamua kufunga kesi hiyo kwa kuhitimisha kwamba Nancy ndiye alitenda mauaji hayo. Bunduki na kila kitu kasoro ile barua ya Nancy vilirudishwa kwa Robert.
Robert hakuchukua muda mrefu alirudi na kuanza kuishi kwenye nyumba yake ambayo mauaji yale yalitekelezwa, jambo ambalo majirani waliona kama ni la ajabu kwakuwa siyo rahisi kwa mtu wa kawaida kuishi kwa amani bila wasiwasi kwenye nyumba ambayo familia yake nzima iliteketezwa. Na kwa mshangao zaidi Robert tarehe 14, mwezi wa 7 mwaka 1979 Robert anaoana na huyo mwanamke aliyekuwa mfanyakazi mwenzake ajulikanaye kama Sheron Cooper na wote wanaishi pamoja kwenye nyumba ya Robert. Robert anawambia polisi kuwa yeye siyo mtu wa kuishi kwenye mambo yaliyopita kwakuwa ni lazima maisha yaendelee hivyo ameamua kusahau mabaya yaliyopita.
Ndoa mpya baina ya Robert na Sheron
Kama ilivyo kawaida ya ndoa inapokuwa mpya, inakuwa imejaa bashasha ya mapenzi motomoto, Robert na Sheron walikuwa na kitu kimoja ambacho walipenda sana kufanya, wote walikuwa wpenzi wa kutembelea na kupanda miamba na milima ijulikanayo kama Grand Canyon (hiking) iliyopo katika jimbo la Colorado. Sheron alikuwa mwandishi wa kitabu maarufu sana kinachojulikana ka ON FOOT of the GRAND CANYON kinachohusiana na muongozo wa kutembelea na kupanda milima na mabonde ya Grand Canyon, hivyo alikuwa ni mtu maarufu katika jimbo la Colorado kutokana na ukweli kwamba watalii na watu wengi walikuwa wamesoma na kutumia mwongozo wa kitabu chake. Hiki kitabu uwapa muongozo wapandaji na watembeleaji wa milima hiyo juu ya hatari inayoweza kuwapata, sehemu za kujiepusha kupita, sehemu zenye miinuko na hatari zaidi pia uwaongoza kwa kuwaelekez sehemu salama za kupita ili kuepuka hatari ya kuanguka na kudondoka.
Robert akiwa na familia yake mpya ambapo alikuwa akiishi yeye mke wake mpya pamoja na mbwa wake wawili, alionekana kuwa ni mtu mwenye furaha kabisa na kuwa alikuwa kasahau yaliyopita na kuanza maisha mapya. Watu wengi wanadai kwamba Robert alikuwa akiwambia kuwa Sheron ndiye mwanamke wa maisha yake, na kuwambia kuwa wanaendana na wana tabia na haiba zinazofanana kwa kupenda vitu na mambo yanayofanana. Sheron alikuwa ni mwanamke anayependelea kwenda kwenye mitoko, mchangamfu na mzungumzaji tofauti kabisa na Nancy, nah ii ilikuwa ni haiba sawa sawa na aliyokuwa nayo Robert hivyo ni kweli walionekana kuendana kabisa.
Lakini baada ya miaka kadhaa ya kuishi Robert na Sheron, mambo yanaanza kwenda kombo na matatizo yanaanza kujitokeza katika ndoa yao. Baada ya baba mzazi wa Robert kufariki, Robert alibadirika kitabia sana kiasi ambacho Sheron alianza kuhisi Robert hakuwa mtu sahihi kwake kama ambavyo alikuwa amefikiria awali, jambo hili lilimfanya Sheron kuwa mtu wa mawazo na kufanya kuwe na kutoelewana katika ndoa yao ambapo mara kwa mara walijikuta wakigombana na kujibizana sana. Inaelekea Bwana Robert hakuwa na bahati na wanawake au huenda wanawake ndiyo hawakuwa na bahati na Bwana Robert.
Mwezi wa 12 mwaka 1986, polisi wanapokea simu kutoka kwa Sheron ambaye anadai kwamba mumewe anamtafuta anataka kumdhuru, hivyo polisi waliwahi na kwenda nyumbani kwa Robert ambapo walimkuta Sheron akiwa kajifungia kwenye kabati la nguo huku akiwa kapandwa presha hivyo ilibidi wamkimbize hospitali. Baada ya ya hili tukio ndoa yao inavunjika kwa kupeana taraka nah ii inakuwa ndoa ya pili ya Bwana Robert kuvunjika katika mazingira yasiyo ya kawaida. Sheron anaamua kuondoka kwenye nyumba ya Robert na kuhama mji wa Littleton.
Lakini taraka hii inamuumiza Robert kwakuwa inamlazimu kugharamia gharama za Sheron za kila mwezi kama mojawapo ya sharti la taraka, kutokana na hilo inambidi Robert arudi kufanya kazi maana kwa kipindi hicho alikuwa ameacha kazi. Kwa sasa Robert alikuwa na umri wa miaka 55, na alikuwa karudi kuwa mseja hivyo bila kupoteza muda anaanza kutafuta mke mpya kwa ajili ya ndoa.
Kutoka na haiba yake na muonekano wake mzuri, haikuwa shida sana kwake kupata mwanamke maana. Robert anaweka tangazo la kutafuta mpenzi kwenye gazeti na kati ya watu waliojibu tangazo lake alikuwa mwanamama Donna Sundlin, mkazi wa mji wa Eveline Colorado ambaye alikuwa kastaafu kazi ya maktaba. Donna na Robert baada ya kukutana wanaanzisha mahusiano moja kwa moja na wanaonekana kila mmoja kumkubari mwenzake.
Mwezi wa 8 mwaka 1990 wanafunga ndoa, na Robert anamshawishi Donna wahamie kwenye mji mdogo wa kitalii wa Durango. Durango ni mji mdogo uliozungukwa na milima na mabonde, watu wengi wanaoishi mji huo ni wapenzi wa kupanda milima na wanajishughulisha na shughuli za utalii. Pia ni mji ambao nao una kiwango kidogo cha uhalifu, umetulia una hali ya hewa nzuri japo umejitenga kwa kuzungukwan amilima lakini una madhari ya kuvutia.
Baada ya kuhamia mji mpya Robert akiwa amefunga ndoa kwa mara ya tatu, walijitahidi kwa kadri wawezavyo kukubarika kwenye jamii mpya, na haikuwa tatizo kutokana na haiba na ucheshi wa Robert aliweza kufahamika kwa kila mtu na alijihusisha kwenye masuala ya mpira wa miguu na kuwa refa katika mechi za kawaida za mji huo. Donna alifanikiwa kupata kazi katika klabu ya mpira ya Durango, wakati Robert naye alipata kazi kama mtangazaji na Dj wa kituo cha redio kidogo cha Durango ambapoa alikuwa akiendesha kipindi cha mziki wa Country, jambo ambalo lilimfanya awe maarufu katika mji wa Durango afahamike na kupendwa na watu wengi.
Lakini Robert mara zote alikuwa hapedi kuzungumzia maisha yake, na ilipomlazimu kujibu maswali juu ya familia yake ya awali, Robert alikuwa akitoa hadithi tofauti tofauti kuhusu ni nini kiliikuta familia yake. Kuna wakati aliwambia watu kuwa mwanaye wa kiume yani David, alikuwa natumia dawa za kulevya na zilimfanya amuue mama yake na dada yake kasha kujipiga risasi mwenyewe, na kuna wakati aliwambia watu kuwa familia yake ilipata ajali ya gari huku yeye ndiye aliyekuwa akiendesha gari hilo na kwamba familia yake yote ilikufa kwenye hiyo ajali isipokuwa yeye tu japo naye aliumia na pia aliwahi wambia baadhi ya watu kuwa mkewe ndiye aliwaua watoto nay eye kasha kujiua.
Inaendelea kwenye comment number 6.
Pia unaweza kusoma makala nyingine kwa kubonyeza link hii Earn money on short links. Make short links and earn the biggest money - shorte.st kisha subiri kwa sekunde 5 halafu utaona neno next upande wa juu kulia bonyeza hapo ili kusoma
Ilikuwa tarehe 30, mwezi wa 12 mwaka 1978, ambapo kama kawaida uwa ni msimu wa saruji katika maeneo mengi nchini Marekani ambapo saruji inakua ikianguka, ikiwa ni siku ya kawaida kama zilivyo siku nyingine kwa wakazi wa mji mdogo wa Littleton ulioko katika jimbo la Colorado waliamka na kuendelea na ratiba zao kama kawaida.
Wakati huu huu mji mdogo wa Littleton ulikuwa una wakazi wanaokadiriwa kufikia kiasi cha 40,000. Ulikuwa na mji mdogo kwa kipindi hiki ukiwa umepangiliwa vizuri na wenye utulivu wa hali ya juu ambapo ulifaa zaidi kwa watu wenye familia na watoto kwa ajili ya kuishi kwa kuwa mji huu kipindi hicho ulikuwa kati ya miji yenye matukio machache sana ya uhalifu. Kwa mwaka huo wa 1978, Littleton ilikuwa imekubwa na mauaji ya watu wawili na matukio ya uvamiji na uporaji matatu tu, hivyo utaona kiasi gani mji huu ulikuwa ni mji ambao ulikuwa na matukio machache sana ya uhalifu kwa wakati huo.
Katika familia zilizokuwa zikiishi katika mji huo kulikuwa na familia ya watu wanne ambao ni Robert Splingler akiwa na mkewe aliyejulikana kama Nancy na watoto wao wawili ambaye wakiume alijulikana kama David akiwa na umri miaka 17 huku wa kike akijulikana kama Suzan alikuwa na umri wa miaka 15. Robert akiwa ameajiliwa katika mamlaka ya usambazaji maji, Nancy yeye alikuwa mama wa nyumbani akiwa na jukumu la kulea familia na kuhakikisha majukumu yote ya nyumbani kama usafi, kupika, kufua n.k yanafanyika kila siku.
David yeye alikuwa anapendelea sana mziki huku akiwa anapenda san kupiga gitaa, wakati Nancy yeye alikuwa katika kipindi cha balehe hivyo muda mwingi alikuwa akiutumia kuwa na mpenzi wake ukizingatia muda huo ulikuwa kipindi cha likizo ambapo shule zilikuwa zimefungwa. Kwa mtazamo wa watu wengi hii ilionekana ni familia yenye furaha na ilikuwa ni familia iliyokamilika.
Hiyo tarehe 30, mwezi wa 12 ikiwa ni asubuhi, majirani wa familia ya Splingler wakiwa wameondoka kwa ajili ya likizo ya kuadhimisha sikukuu ya mwaka mpya, mpenzi wa Suzan ajulikanaye Tim aliyekuwa na umri wa miaka 16, aliamua kuja nyumbani kwao Suzan kumtembelea kama alivyozoea kufanya kila siku. Kawaida yao ilikuwa akifika nyumbani kwa akina Suzan alikuwa akichukua saruji na kurusha dirishani kwa Suzan mara tatu na Suzan alikuwa akisikia anakuja kumpokea nje ambapo anamuingiza chumbani kwake.
Siku hiyo baada ya kufika alifanya hivyo hivyo, lakini Suzan hakutokea, hivyo aliamua kuingia ndani kabisa na alishangaa kukuta nyumba ikiwa kimya kama vile hakuna mtu , alihisi uenda watakuwa bado wamelala kwakuwa wazo la kuwa wanaweza kuwa wamesafiri hakuwa nalo kwakuwa jana yake alikuwa na Suzan hakumwambia kama watasafiri na pia walipanga kuonana siku hiyo, na pia kama wangesafiri basi mlango ungekuwa umefungwa kwa funguo.
Tim aliamua kupanda ghorofani moja kwa moja kwenye chumba cha Suzan, na alipoingia chumbani alimuona Suzan akiwa amelala kitandani. Alianza kumuita akiwa kasimama mlangoni lakini Suzan hakuitika jambo lililomfanya Tim avue gloves alizokuwa kava na kumrushia lakini bado Suzan hakuitika wla kujitikisa. Tim aliamua kusogea karibu na kitanda na kwa mshangao ndipo alipogundua kuwa mwili wa Suzan ulikuwa kwenye dimbwi la damu huku akiwa na tundu la risasi kifuani. Tim alitoka chumbani kwa Suzan mbio na kukimbilia kwenye chumba cha David ili kumtaarifu alichokiona kwenye chumba cha mdogo wake, lakini alipofika alimkuta David naye akiwa kitandani kwake kalala kwenye dimbwi la damu pia, huku uso ukiwa umefunikwa na mto na kifuani kukiwa na tundu la risasi.
Kuona hivyo Tim alitoka ndani mbio na kwenda kupiga namba ya dharura 911, kuwataarifu polisi ambao walifika mara moja kwenye eneo la tukio. Askari polisi kutoka katika kituo cha polisi cha Arapahoe wanafika eneo la tukio na kukutana na hali ya tukio la kutisha. Kwa mazingira ya awali ya uchunguzi wa polisi ilionekana Suzan alikuwa kapigwa risasi ya kifuani kutoka kwenye bunduki iliyokuwa mbali kidogo kwa inches kadhaa toka alipokuwa amelala nah ii ilimfanya akate roho kwa haraka sana. David pia naye alikuwa kapigwa risasi moja tu kifuani kwake, ambayo iliondoa uhai wake.
Katika kuzidi kupekuwa nyumba, polisi walielekea upande wa chumba cha chini cha nyumba hiyo ambapo walikuta mwili wa Nancy ukiwa umekaa kwenye kiti kilichokuwa nyuma ya meza yenye type writer, huku kichwani kukiwa na tundu la risasi. Pembeni kidogo ya mwili wake, sakafuni kulikuwa na bunduki ndogo, na kwenye mashine ya type writer kulikuwa na karatasi, ambapo walipoichomoa waligundua ilikuwa ni barua iliyoonekana kuandikwa na Nancy akikiri juu ya kutenda mauaji hayo pamoja na sababu zilizomfanya kutekereza mauaji hayo kasha kujiua, na mwisho mwa hiyo barua ilikuwa imesainiwa kwa peni kwa kuewekewa herufi“n” ambapo polisi walihisi imetokana na herufi ya kwanza ya jina la Nancy.
Katika maelezo yaliyokuwa kwenye hiyo barua Nancy alidai ya kwamba alipata hiyo bunduki ya mumewe kwa bahati mbaya na alipoipata aliamua kutenda jambo hilo kwakuwa walikuwa wanataka kutengana na walikuwa wakibishana ni nani hasa atakayebaki na watoto na Nancy anadai hakuwa tayari kuishi bila watoto wake hivyo aliamua bora awaue nay eye ajiue.
Barua yote ilikuwa imechpwa kwa mashine isipokuwa saini ya herufi “n”, na kwa kuitazama haraka haraka ile ule ujumbe ulikuwa unatosha kutumika kama ushahidi kuwa Nancy ndiye alitekereza mauaji hayo ni kasha kujiua mwenyewe kwa sababu alizozitoa kwenye hiyo barua. Lakini polisi hawakutaka kufikia tamati haraka kwa kuchukulia huo ushahidi kama ndicho kigezo tosha cha kukubari kuwa Nancy ndiye katekereza mauaji.
Jack Swanburg, aliyekuwa mkuu wa kituo cha polisi cha Arapohoe, anadai kwamba kosa kubwa ambalo polisi wengi hufanya ni kufikia hitimisho kwa kufanya maamuzi yao binafsi pasipo kuwa na ushahidi wa kutosha au kutazama ushahidi wote uliopo. Anazidi kusema kwamba ukifanya upelelezi huku kichwani ukiwa tayari na hitimisho binafsi basi huo upelelezi lazima ukupe matokeo yasiyo sahihi.
Kutokana na polisi kutotaka kufikia hitimisho kwa kutumia tu ile barua waliyokuta kwenye type writer, waliendelea kukusanya ushahid wote ulionekana kuwa unaweza kusaidia katika kutatua kesi hiyo ambayo ilikuwa mbele yao. Mpiga picha wa polisi alianza zoezi la kupiga picha eneo lote la tukio na kama kawaida utaratibu wa upigaji picha uanza kwa kupiga picha eneo lote, kasha uendelea kwa kupunguza ukubwa wa eneo mpaka kufikia kupiga picha kitu kimoja kimoja mfano tundu la risasi peke yake, bunduki peke yake n.k.
Aina ya silaha iliyokutwa sakafuni pembeni ya Nancy ilikuwa bunduki ndogo ijulikanayo kama 38 caliber Smith Mansen, ambapo nayo ilipigwa picha na mpiga picha wa polisi. Bunduki ilikuwa kama foot sita kutoka mwili wa Nancy ulipokuwa umekaa pale nyuyma ya meza kwenye kiti. Hii ilikuwa siyo jambo la kawaida kwamba mtu ajipige risasi ya kichwa kasha bunduki idondoke umbali huo kutoka alipo.
Wakati wa mchana mara Robert ambaye hakuwa nyumbani anawasili na kukuta nyumba yake ikiwa imezungushiwa utepe wa njano kuashiria kwamba ni eneo ambalo limefungwa na polisi kwa ajili ya kuchukua ushahidi na kufanya upelelezi baada ya tukio la kiharifu kufanyika pale. Polisi wanamtaarifu juu ya mauaji yaliyotokea nyumbani kwake na anaonekana kusikitika sana huku akijawa na majonzi.
Pia anapoonyeshwa bunduki iliyotumika katika kutekereza mauaji hayo, anakubari kuwa ni bundukui yake na anadai kwamba hakuwa nyumbani wakati tukio hilo linatokea. Katika kuzidi kumhoji polisi wanapata picha tofauti juu ya familia ya Bwana Robert tofauti na ambavyo watu wanje hasa majirani walivyokuwa wakiiona. Majirani na watu waliokuwa wakimfahamu walikuwa wakidai kwamba Robert alikuwa mtu mzuri, mwenye roho nzuri, mpenda watu, mchangamfu, jirani mwema na baba mpenda familia. Lakini kiuhalisia polisi wanagundua hii ilikuwa tofauti na hali halisi katika familia hiyo baina ya Nancy na Robert. Hata wazazi wa nancy hawakuwa wakimkubari Robert walikuwa wanamuona kama siyo mtu sahihi kwa mtoto wao, pia ndani ya familia kulikuwa na ugomvi wa mara kwa mara baina ya wazazi hawa.
Katika mahojiano kati ya polisi na Robert, Robert anakiri kuwa walikuwa wana ugomvi wa kindoa kwa muda mrefu kiasi kwamba walikuwa wametengana kwa muda na kurudiana hivi karibuni. Anaendelea kudai kwamba chanzo cha huo ugomvi ilikuwa kwasababu Robert alikuwa na mahusiano na mwanamke mwingine ambaye alikuwa ni mfanyakazi mwenzake kule ofisini alipokuwa akifanya kazi. Anazidi kudai kwamba japo Nancy alikuwa hapendi uhusiano huo, ila hakutegemea kama anaweza kuchukua maamuzi hayo hata yeye amestaajabu na kuogopa kwa tukioo hilo. Robert anaonekana kutoa ushirikiano wa kutosha kwa polisi na anaweza kueleza kila kitu alichofanya na wapi alipokuwa siku nzima.
Anadai kwamba yeye na Nancy waliingia kwenye ugomvi wa mabishano siku hiyo asubuhi, hivyo aliamua kuondoka nyumbani na kwenda kuzurura kwa kuendesha gari mitaa mbalimbali ili kupunguza msongo wa mawazo na anadai alitumia kama saa moja au moja na nusu akiendesha gari, baada ya hapo aliamua kwenda sinema kutazama filamu. Kuthibitisha kuwa maelezo yake ni sahihi Robert anakubari kufanyiwa kipimo cha kupima uongo na ukweli. Majibu yanapotoka mtaalamu wa kusoma matokeo ya kipimo hicho anadai kuwa hayawezi kuwasaidia polisi maana hayaeleweki kabisa hivyo hawezi kusema kama alikuwa anongea ukweli au hapana.
Polisi wanaamua kumkagua Robert ili kuona kama wanaweza pata ushahidi wowote unaoweza kumfunga kwenye tukio hilo la mauaji, na kitu walichokuwa wanajaribu kujua ni kuchukua kipimo cha kuonyesha kama mwili wa Robert ulikuwa na mabaki ya mlipuka wa risasi (Gun Powder residue) nah ii ingedhirisha kuwa ni yeye aliyefyatua risasi, au alikuwa karibu wakati risasi inafyatuliwa au uenda aliishika ile bunduki baada tu ya kufyatua risasi.
Kwa kipindi hicho matokeo ya kipimo hicho yalikuwa yanachukua muda kupataikana, ambapo ilikuwa inachukua zaidi ya wiki moja mpaka matokeo kutolewa. Kutokana na kutokuwa na ushahidi na sababu yoyote ya kumshikiria, polisi walimuachia Robert huru, huku wakingojea matokeo ya kipimo cha mabaki ya vumbi la mlipuko wa risasi kutoka katika maabara kinayomilikiwa na kitengo makosa ya jinai cha Colorado
Lakini nyumba ya Robert ilikuwa bado imefungwa polisi wakiendeleakuichunguza kwa ajili ya ushahidi zaidi hivyo hakuruhusiwa kukaa pale, na kutokana na sababu hiyo mkuu wa kituo cha polisi Bwana Jack Swanburg alijitolea kumpa hifadhi Robert ya muda pale nyumbani kwake,na anadai alistaajabu kumuona Robert akiwa ni mtu mwenye utulivu wa hali ya juu kama vile hakuwa kapatwa na tukio la kuogofya la kufiwa na mkewe pamoja na watoto wake wawili tena katika mauaji ya kutisha.
Tarehe 3 mwezi wa 1 mwaka 1979, polisi wanahitimisha kuwa lile tukio lilitekelezwa na Nancy, lakini baada ya siku kadhaa maotkeo ya kipimo cha mabaki ya mripuko wa risasi kutoka yanadhihirisha kwamba Robert anajua zaidi kuliko ambavyo amewambia polisi. Kipimo kinaonyesha kwamba Robert alikuwa na mabaki ya vumbi la mripuko wa risasi wakati Nancy binafsi hakuwa na vumbi hilo mkononi jambo ambalo linaashiria kuwa huenda Robert ndiye aliyefyatua risasi hiyo au alikuwa karibu wakati inafyatuliwa au aliishika bunduki pale baada ya risasi kufyatuliwa.
Polisi wanamwita Robert tena kwa ajili ya mahojiano na mara hii anabadirisha hadithi na maelezo yake ya awali. Anadai kwamba alirudi nyumbani na kukuta tayari mauaji yamekwishatokea, na alipoelekea chumba cha chini alimkuta nancy akiwa amekwishajiua huku bunduki ikiwa karibu na mwili wake. Anadai aliikota akarudi nyumba na kusema Mungu wangu kasha aliidondosha na kutoka ndani amekimbia akaingia kwenye gari lake na kuondoka.
Siku ya tukio wakati polsii wakiendelea na uchunguzi, waligundua uwepo wa alama za matairi ya gari eneo la nyumba ya Robert ambazo zilionekana kuwa zilikuwa zimeachwa na gari ambalo lilikuwa limetoka pale muda siyo mrefu sana kutokana na ukweli kwamba kwakuwa saruji ilikuwa inadondoka kama zilikuwa namuda mrefu zingekuwa zimefunikwa na saruji tayari. Alama hizo zilikuwa zinaonyesha kuwa gari lilikuja na kasha likaondoka hivyo kulikuwa na set mbili za alama ya matairi kwenye saruji, na alama hizo walikuja kugundua kuwa ni alama za matairi ya gari la Robert. Kutokana na maelezo yake mapya na uwepo wa hizo alama, zilithibitisha kuwa Robert alikuwa akisema ukweli kuhusu kuja nyumbani kwake na kuondoka.
Polisi walimuondoa Robert kama mshukiwa wa mauaji hayo na kuhitimisha kabisa kuwa mtendaji alikuwa Nancy, ila familia ya Nancy haikukubari kabisa hili jambo wao waliamimini kwamba Robert anajua ukweli kuliko kile anachowambia polisi. Na mbaya zaidi wakati wazishi Robert alikuja na mwanamke wake kwenye mazishi ambapo miili ya marehemu ilichomwa moto. Watu waliokuwepo walishangaa kwakuwa hakuonyesha dalili zozote za majonzi kama mtu ambaye kapoteza familia yake katika mauaji akiwemo mke na watoto wake wawili.
Pia kabla ya kifo cha Nancy alikuwa amemwandikia binamu yake barua akimwambia kuwa kwasasa yeye na Robert wanaelewana na wako vizuri akiwa anamwambia mipango yake ya baadae na maisha ya mbeleni, jambo ambalo familia ya Nancy inadai kwamba linaonyesha kuwa Nancy hakuwa na mpango wa kujiua ama kuua watoto ndiyo maana alikuwa akizungumzia mipango ya baadaye kweye barua ile.
Hivyo maneno ya chini chini yaliendelea kuzungumzwa na watu mbalimbali katika mji wa Littleton juu ye uhusika wa Robert katika mauaji hayo, lakini japo kuna watu walikuwa na mashaka akiwemo baadhi ya maafisa polisi juu ya Robert kuhsuika katika mauaji hayo, polisi waliamua kufunga kesi hiyo kwa kuhitimisha kwamba Nancy ndiye alitenda mauaji hayo. Bunduki na kila kitu kasoro ile barua ya Nancy vilirudishwa kwa Robert.
Robert hakuchukua muda mrefu alirudi na kuanza kuishi kwenye nyumba yake ambayo mauaji yale yalitekelezwa, jambo ambalo majirani waliona kama ni la ajabu kwakuwa siyo rahisi kwa mtu wa kawaida kuishi kwa amani bila wasiwasi kwenye nyumba ambayo familia yake nzima iliteketezwa. Na kwa mshangao zaidi Robert tarehe 14, mwezi wa 7 mwaka 1979 Robert anaoana na huyo mwanamke aliyekuwa mfanyakazi mwenzake ajulikanaye kama Sheron Cooper na wote wanaishi pamoja kwenye nyumba ya Robert. Robert anawambia polisi kuwa yeye siyo mtu wa kuishi kwenye mambo yaliyopita kwakuwa ni lazima maisha yaendelee hivyo ameamua kusahau mabaya yaliyopita.
Ndoa mpya baina ya Robert na Sheron
Kama ilivyo kawaida ya ndoa inapokuwa mpya, inakuwa imejaa bashasha ya mapenzi motomoto, Robert na Sheron walikuwa na kitu kimoja ambacho walipenda sana kufanya, wote walikuwa wpenzi wa kutembelea na kupanda miamba na milima ijulikanayo kama Grand Canyon (hiking) iliyopo katika jimbo la Colorado. Sheron alikuwa mwandishi wa kitabu maarufu sana kinachojulikana ka ON FOOT of the GRAND CANYON kinachohusiana na muongozo wa kutembelea na kupanda milima na mabonde ya Grand Canyon, hivyo alikuwa ni mtu maarufu katika jimbo la Colorado kutokana na ukweli kwamba watalii na watu wengi walikuwa wamesoma na kutumia mwongozo wa kitabu chake. Hiki kitabu uwapa muongozo wapandaji na watembeleaji wa milima hiyo juu ya hatari inayoweza kuwapata, sehemu za kujiepusha kupita, sehemu zenye miinuko na hatari zaidi pia uwaongoza kwa kuwaelekez sehemu salama za kupita ili kuepuka hatari ya kuanguka na kudondoka.
Robert akiwa na familia yake mpya ambapo alikuwa akiishi yeye mke wake mpya pamoja na mbwa wake wawili, alionekana kuwa ni mtu mwenye furaha kabisa na kuwa alikuwa kasahau yaliyopita na kuanza maisha mapya. Watu wengi wanadai kwamba Robert alikuwa akiwambia kuwa Sheron ndiye mwanamke wa maisha yake, na kuwambia kuwa wanaendana na wana tabia na haiba zinazofanana kwa kupenda vitu na mambo yanayofanana. Sheron alikuwa ni mwanamke anayependelea kwenda kwenye mitoko, mchangamfu na mzungumzaji tofauti kabisa na Nancy, nah ii ilikuwa ni haiba sawa sawa na aliyokuwa nayo Robert hivyo ni kweli walionekana kuendana kabisa.
Lakini baada ya miaka kadhaa ya kuishi Robert na Sheron, mambo yanaanza kwenda kombo na matatizo yanaanza kujitokeza katika ndoa yao. Baada ya baba mzazi wa Robert kufariki, Robert alibadirika kitabia sana kiasi ambacho Sheron alianza kuhisi Robert hakuwa mtu sahihi kwake kama ambavyo alikuwa amefikiria awali, jambo hili lilimfanya Sheron kuwa mtu wa mawazo na kufanya kuwe na kutoelewana katika ndoa yao ambapo mara kwa mara walijikuta wakigombana na kujibizana sana. Inaelekea Bwana Robert hakuwa na bahati na wanawake au huenda wanawake ndiyo hawakuwa na bahati na Bwana Robert.
Mwezi wa 12 mwaka 1986, polisi wanapokea simu kutoka kwa Sheron ambaye anadai kwamba mumewe anamtafuta anataka kumdhuru, hivyo polisi waliwahi na kwenda nyumbani kwa Robert ambapo walimkuta Sheron akiwa kajifungia kwenye kabati la nguo huku akiwa kapandwa presha hivyo ilibidi wamkimbize hospitali. Baada ya ya hili tukio ndoa yao inavunjika kwa kupeana taraka nah ii inakuwa ndoa ya pili ya Bwana Robert kuvunjika katika mazingira yasiyo ya kawaida. Sheron anaamua kuondoka kwenye nyumba ya Robert na kuhama mji wa Littleton.
Lakini taraka hii inamuumiza Robert kwakuwa inamlazimu kugharamia gharama za Sheron za kila mwezi kama mojawapo ya sharti la taraka, kutokana na hilo inambidi Robert arudi kufanya kazi maana kwa kipindi hicho alikuwa ameacha kazi. Kwa sasa Robert alikuwa na umri wa miaka 55, na alikuwa karudi kuwa mseja hivyo bila kupoteza muda anaanza kutafuta mke mpya kwa ajili ya ndoa.
Kutoka na haiba yake na muonekano wake mzuri, haikuwa shida sana kwake kupata mwanamke maana. Robert anaweka tangazo la kutafuta mpenzi kwenye gazeti na kati ya watu waliojibu tangazo lake alikuwa mwanamama Donna Sundlin, mkazi wa mji wa Eveline Colorado ambaye alikuwa kastaafu kazi ya maktaba. Donna na Robert baada ya kukutana wanaanzisha mahusiano moja kwa moja na wanaonekana kila mmoja kumkubari mwenzake.
Mwezi wa 8 mwaka 1990 wanafunga ndoa, na Robert anamshawishi Donna wahamie kwenye mji mdogo wa kitalii wa Durango. Durango ni mji mdogo uliozungukwa na milima na mabonde, watu wengi wanaoishi mji huo ni wapenzi wa kupanda milima na wanajishughulisha na shughuli za utalii. Pia ni mji ambao nao una kiwango kidogo cha uhalifu, umetulia una hali ya hewa nzuri japo umejitenga kwa kuzungukwan amilima lakini una madhari ya kuvutia.
Baada ya kuhamia mji mpya Robert akiwa amefunga ndoa kwa mara ya tatu, walijitahidi kwa kadri wawezavyo kukubarika kwenye jamii mpya, na haikuwa tatizo kutokana na haiba na ucheshi wa Robert aliweza kufahamika kwa kila mtu na alijihusisha kwenye masuala ya mpira wa miguu na kuwa refa katika mechi za kawaida za mji huo. Donna alifanikiwa kupata kazi katika klabu ya mpira ya Durango, wakati Robert naye alipata kazi kama mtangazaji na Dj wa kituo cha redio kidogo cha Durango ambapoa alikuwa akiendesha kipindi cha mziki wa Country, jambo ambalo lilimfanya awe maarufu katika mji wa Durango afahamike na kupendwa na watu wengi.
Lakini Robert mara zote alikuwa hapedi kuzungumzia maisha yake, na ilipomlazimu kujibu maswali juu ya familia yake ya awali, Robert alikuwa akitoa hadithi tofauti tofauti kuhusu ni nini kiliikuta familia yake. Kuna wakati aliwambia watu kuwa mwanaye wa kiume yani David, alikuwa natumia dawa za kulevya na zilimfanya amuue mama yake na dada yake kasha kujipiga risasi mwenyewe, na kuna wakati aliwambia watu kuwa familia yake ilipata ajali ya gari huku yeye ndiye aliyekuwa akiendesha gari hilo na kwamba familia yake yote ilikufa kwenye hiyo ajali isipokuwa yeye tu japo naye aliumia na pia aliwahi wambia baadhi ya watu kuwa mkewe ndiye aliwaua watoto nay eye kasha kujiua.
Inaendelea kwenye comment number 6.
Pia unaweza kusoma makala nyingine kwa kubonyeza link hii Earn money on short links. Make short links and earn the biggest money - shorte.st kisha subiri kwa sekunde 5 halafu utaona neno next upande wa juu kulia bonyeza hapo ili kusoma