Mkapa above the law?: Allegations

Mkapa above the law?: Allegations

Bubu,

Aliyofanya Mkapa (1995-2005)

A: Positives
1. Kukusanya kodi
2. Daraja la Mkapa
3. Kufufua EA Community
4. Ujenzi na ukarabati wa barabara (various-Dar, Moro,Bkb-Mtkul)
5. Elimu-MES & MEMKWA
6. Afya- Health Sector Reforms (Basket fund n.k)
7. Kufutwa kwa madeni ya nje HIPC
8. Kuongezeka Foreign Direct Investment- Gold Minig etc
9. Ubinafshaji loss making Parastatals
10. Muafaka wa CUF na CCM

Ukiangalia huyu bwana pia kuna aliyofanya mwema kama wajibu- pia ana mapungufu! Je historia itasema BWM ni raisi aliyeshindwa au aliyefanikiwa? Hata Brair, Bush, Kibaki, Howard..kuna waliyojitahidi na pia wana mapungufu!
To be fair- shilingi ina pande mbili- hii ndiyo hoja yangu.

1. Ukusanyaji kodi. Ndio kweli katika awamu yake makusanyo ya kodi yaliongezeka. Je Watanzania walinufaika vipi? Bado wanafunzi walikuwa wanakalia matofali, mahospitali yetu yalikuwa hayana vifaa muhimu na madawa pia yalikuwa hakuna. Asilimia kubwa ya makusanyo hayo ilitumika kulipa madeni ya nje. Kwa kifupi Watanzania hawakunufaika na ongezeko hilo. Ni kama Baba anayetamba mtaani kwamba yeye ana mshahara mkubwa kuliko baba yeyote pale mtaani lakini watoto wake wanadhoofika maana mshahara wote unaishia nyumba ndogo na kwenye mabar.

2. Daraja la Mkapa hili ni fedha za mkopo na misaada ambapo yeyote yule angeweza kusimamia ujenzi huo.

3. Kama ulivyoona kwa kishindo kikubwa Watanzania hawalitaki shirikisho la EA, labda baadaye. Kwa sasa asilimia 76 wamesema NO na muungwana kasema atakeshimu matakwa yao.

4. Mabarabara ni machache mno yaliyotengenezwa. Asilimia kubwa ya barabara zetu bado hazipitiki na ni zile za mwaka 47. Angalia foleni ya Dar leo hii. Safari ya 15 to 20 minutes inaweza kukuchukua hata masaa mawili hata zaidi. Ikinyesha mvua kubwa kwa saa moja tu basi barabara nyingi hazipitiki. Hili pia kwa mtazamo wangu na Watanzania walio wengi sioni mafanikio yoyote!

.Elimu hili sioni mafanikio yako wapi kwani ukianzia shule za msingi mpaka vyuo vikuu kuna matatizo chungu nzima na yamesemwa na hata na haki elimu ambayo Mkapa aliipiga vita na hata kuifungia na sasa pia wanawekewa mikwara chungu nzima. Asilimia kubwa ya Watanzania sidhani kama waliona mafanikio yoyote katika elimu enzi za Mkapa.

6. Sera za afya katika awamu ya tatu zilikuwa ni mbovu sana na hadi hii leo bado zinasikitisha sana. Mifano ni mama wajawazito kati ya watano kushare kitanda kimoja!!!! na wengine kulala chini!! vitendea kazi hakuna kabisa na matokeo yake wanasiasa wote hutibiwa SA, Kenya, UK na hata USA. Sijui unazungumzia mafanikio yapi!!! 😕

7. Madeni hayakufutwa kwa sera za Mkapa. Pamoja na hayo Watanzania hawakuona wala hawajaona mafanikio ya kufutwa kwa mikopo hiyo. Maisha ya dhiki kwa Watanzania wengi hayajabadilika hata chembe!!!

8. FDI imeongezeka ndiyo lakini madini yetu yanachukuliwa bila Watanzania kufaidika na chochote. Nadhani umeshasikia kelele chungu nzima kuhusiana na mikataba ya madini iliyo siri hadi leo hii. Sijui hili ongezeko la FDI limewasaidia vipi Watanzania.

9. Breweries na Sigara hawa walikuwa wanapata faida kubwa tu lakini nao wakabinafsishwa sijui Mtanzania alifaidika nini. Mashirika mengi yaliyouzwa yaliuzwa kwa bei karibu na bure na Watanzania hawakufaidika chochote na mengi ya mashirika yaliyouzwa sasa hivi hayafanyi biashara au uzalishaji wowote.

10. Mmmmhhh! Muafaka wa CUF na CCM ambao mpaka leo hii hatujaona lolote la maana katika muafaka huo. Juzi juzi tu kulikuwa na habari kwamba CUF wanataka kujitoa katika mazungumzo hayo!!! Au kuna muafaka mwingine ambao labda hatuujui!!!! 😕

Sioni mafanikio yoyote ya Mkapa zaidi ya kujitajirisha yeye na familia yake na kuacha kashfa chungu nzima ambazo inaelekea anaogopa kuzijibu maana kila kukicha linaibuka bomu jingine la awamu ya tatu!!!
 
Bubu,
1. Development is not a one time event it is a process! Investment, education, health, infrastructure etc trickle effect could not necessary be seen during BWM era. BWM instituted a good discipline of tax collection we don't have problems of paying salaries as during Mwalimu or Mwinyi era!
2. BWM internationally was liked by West (for a poor country you need them) hence more loans and DFI and debt cancellation- why did West not found of Moi? Why BWM? He was even invented to G8. I hate foreign AID but if you are poor- we can not do without AID currently! Hence Mkapa bridge- why not during Mwinyi or Nyerere?
3. Viongozi kutibiwa nje- poor health services did not start during BWM era- started long time- and this is not particular in Tanzania. Unajua wananchi wengi vijijini sasa hukimbulia hospitali za serikali kwa kuwa siku hizi kuna dawa? Tafiti ninyi zimeonyesha- baadhi ya hospitali binafsi vijijini hawapati watu. Huduma bado sii nzuri 100% ila there is some improvement! IMR declined pia this time! Ila MMR has not changed!
4. Ubinafsishaji- serikali haikuuza Breweries, NMB, bali waliingia ubia- wanapata gawio na kodi!
5. Kuna mapungufu kweli- ila pia kuna mafanikio -sii vema kufumba macho na kuangalia mapungufu tu- tufanye mizania. Mimi simtetei BWM ila saa zote tumejikita kuangalia mapungufu yake tu kama vile basi ni malaika- yeye ni binadamu kama wewe na mimi!
 
Jamani nimeona hapa wanamtaja Peter kama mtoto wa Mkapa, mwingine kasema mtoto wa mama (yaani mama Mkapa) hivi ni huyu Peter Maro wa Simu 2000? je, n mtoto wa Anna Mkapa na nani?

Kuhusu daraja la "MKAPA" kuna jamaa mmoja wa Zanziba alisema, "halikua daraja lake kwani Mzee Mwinyi ndiye aliyestahili kupewa jina la hilo daraja kwani ndiye aliyoomba na kukamilisha makubaliano ya mkopo huo sawa na lami ya Zanzibar ambayo Dr Salmin aliomba Libya, na Karume akaja kujidai nayo"

Kuhusu barabara, kuna taarifa kwamba barabara zote alizojenga mkapa kuna faida kubwa imeingia kwa watu binafsi, kuanzia "upembuzi yakinifu" na baadaye katika mikataba na makandarasi... Kuna mtu mmoja aliwahi kusema, "PCB walikuwa wakichunguza hizo barabara wakakuta kwamba bei ya kila kilometa moja imeongezwaa mara mbili na hiyo tofauti inarudi kwa bwana mkubwa na hupelekwa Rome na baadaye Offshore banks.. PCB kuona hivyo wakati huo bado bosi yuko madarakani, wakafunga upelelezi",, sasa basi bado hata hayo mafanikio tunaweza kuanza kuyashuku, je, fedha zote za kodi zilikwenda na kutumika ipasavyo au ndio hizo za BoT? Misahama je, ilirudi kwa walengwa? ama ndio hayo mabilini ya fedha za madeni? BAdo kuna mengi ya kutafakari ili tuweze kujenga tabia ya kutokubali kushangilia kila kitu bila kuhoji undani wake
 
Kwa kifupi ni kwamba BWM aliongeza jitihada ya kukusanya kodi na kurudisha confidence ya wafadhili kwamba Tanzania inakopesheka kwa kuanza kulipa madeni. Hela alizokusanya kwenye kodi nyingi ziliishia kwenye kulipa madeni na nyingine zilizobaki ziliishia kwenye mifuko ya wajanja wachache.

Kulikuwa na faida gani kuwaita Net Group Solution waje ku-run TANESCO kwa gharama kubwa na bado hawakuongeza ufanisi wowote ndani ya shirika. Hela zilizokusanywa kwenye kodi zimeenda kulipa gharama za Net Group. Sasa tumeingizwa kwenye IPTL nyingine (Kiwira) ambako hela zitaendelea kuvuja. Yaani hapo ni sawa na kukinga maji kwenye ndoo iliyo na matobo kibao. Matokeo yake ndoo haiwezi kujaa hata ukeshe unajaza maji, hayo ndiyo yaliyotokea zama za BWM. Kwa hiyo sioni sababu ya kumpa CREDIT kwa kuongeza makusanyo ya kodi, maana alikamua wananchi na hakurudisha huduma kwa jamii. Watu wakaishia kulipa kodi tu kwa ajili ya kuwatajirisha wachache.

Msamaha wa madeni ulikuwa na lengo la kuboresha miundo mbinu na huduma za jamii (afya na elimu). Maajabu ni kwamba tumeendelea kupewa data za madarasa yaliyojengwa huku yakiwa hayana walimu sasa sijui elimu ni madarasa na wanafunzi bila walimu? Matokeo yake kuna wanafunzi wanamaliza darasa la 7 wakiwa hawajui kusoma na kuandika, lakini wanaitwa walisoma kwa kuwa walienda kupoteza muda shuleni kwa kushinda wanacheza au kufanyishwa kazi na mwalimu wao mmoja aliyepo. Bado hapo haiingii akilini kwamba hiyo misamaha ya madeni ilisaidia kuboresha elimu.

Ninasikitika data za Mzalendohalisi kwamba zahanati za vijijini zina dawa wakati kila siku bungeni tunaambiwa zahanati hazina hata wahudumu. Unadhani ni kwanini serikali imeongeza jitihada za kuwa wa wakunga wa jadi? Hiyo ni ushahidi tosha kwamba huduma za afya vijijini zina walakini. Unatoa data za vijijini kwa kuwa hatuwezi kwenda kujionea, mbona huongelei huduma za Hospitali za Rufaa kama Muhimbili ambako watu tunapita kila siku na kujionea hali halisi. Kama Muhimbili ambayo iko Dar ina hali mbaya, unategemea zahanati za vijijini zitakuwa kwenye hali gani?

Swala la ubinafshaji hapo naona Mzalendohalisi umetumia mfano mbaya maana sioni hata kitu kimoja ambacho kilifanyika sawa. TBL na Sigara walibinafsishwa enzi ya Mwinyi, so BWM hahusiki. Angalia ubinafsishaji wa NBC jinsi ulivyokuwa umezungukwa na mizengwe. Kwa kifupi ni kwamba mashirika mengi yaliyobinafsishwa zama za BWM yamezungukwa na harufu ya RUSHWA. Mifano iko mingi ambayo ni pamoja na hiyo NBC, TTCL, urekebishaji wa TANESCO na sasa NIC. Kwa kifupi ubinafsishaji wa mashirika zama za BWM ni balaa tu na watu wake wa PSRC ndiyo waliokuwa wanasaidia kuhujumu hilo zoezi. Angalia jinsi PSRC wanavyoumbuka sasa hivi kwenye kubinafsisha NIC, ni aibu tupu valuation ya PSRC inapokuwa ni ndogo na wakipewa kampuni nyingine ya valuation wanakuja na figure ambayo ina tofauti ya mamilioni ya fedha. Hiyo ni ushahidi tosha kwamba kuna mashirika mengi yaliuzwa kwa bei ya kutupwa na watu wamekula commission yao kwa kuwa madalali wazuri.

Umaarufu wa BWM kwa nchi za Magharibi haumaanishi kwamba alikuwa ni mzuri katika utendaji wake. Kilichompandisha chati ni kitendo cha kuvutia wawekezaji na hasa katika sekta ya madini ambako kila siku hapa JF tumekuwa tukilalamika kwamba mikataba ya huko ni uozo mtupu na kuna dalili za ulaji. Kuna kipindi team ya watafiti kutoka UDSM ilienda bungeni Dodoma kuongea na wabunge ili kuwajulisha jinsi nchi inavyoliwa katika sekta ya madini. BWM alikuja juu kwa kuwatukana akidai kwamba hao ni wasomi uchwara wanatumia UD kama kichaka! Siku zote ukitaka kuona ukali wa BWM gusa kwenye anga zake za ulaji, alikuwa ni mkali hasa. Wote tuliona jinsi alivyotetea deals za rada, ndege ya rais, Net Group na kasheshe ya madini. Yet tunasimama mbele za watu na kuanza kutafuta mazuri aliyoyafanya ambayo mimi kwa macho yangu na mawazo yangu sijaona hata moja zaidi ya wajanja wachache kujitajirisha.

Nchi za Magharibi zilimpenda kwa sababu alikuwa anatoa fursa kwa wawekezaji wa kutoka Magharibi ambayo inatoa ajira kwa watu wao na pia wanaongeza mapato kwa kuwa mitaji ya watu wao inawekezwa nje kwa kupata faida kubwa kuliko wakiwekeza kwenye nchi zao. Ndiyo maana alikuja kuonekana kwamba anafaa kwenye kampeni za UTANDAWAZI na ndiyo kisa cha kuingizwa kwenye Tume ya Blair, na hilo sioni kama ni credit kwa kuwa halikusaidia chochote kwenye uchumi wa Tanzania. Uzuri wa globalization ni pale unapoweza kuuza na kununua, lakini siyo utumike kama soko wakati wewe huna kitu cha kuuza kwa wenzako. Tanzania pamoja na kusifiwa BWM kwamba ameiingiza TZ kwenye utandawazi, bado tunaendelea kutumika kama soko la wenzetu wakati sisi hatuwezi kuuza kitu chochote nje. Matokeo yake exchange rate imeendelea ku-depreciate kila mwaka tena kwa kiasi kikubwa na soon tutawafikia Uganda!
 
( Makala hii imechapwa na RAI juma hili)
Ben Mkapa Na Awamu Yake (1)
Na maggid mjengwa
ZAIDI ya mwaka mmoja umepita tangu Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu, Mh. Benjamin William Mkapa aondoke madarakani. Kuna mengi yanasemwa juu yake. Hii ichukuliwe kama tathmini ya utendaji wake alipokuwa madarakani.
Bado nina kiu ya kuona mijadala ya kina yenye kutathmini utendaji wa Serikali ya Awamu ya Tatu. Bahati mbaya, baadhi yetu wameishia kwenye kujadili mkopo aliokopa Rais Mstaafu na kufungua kampuni yake. Binafsi ningependa kuona tunainua kiwango cha mijadala, tuzame zaidi ya hapo, kwani, fedha anazodaiwa Mkapa kukopa amezikopa, hakwenda kuiba benki.
Tuna mfano wa Rais Mobutu wa Zaire ya zamani aliyekuwa akmwita gavana wake wa Benki Kuu na kumwamuru aende kuchota fedha benki. Hoja ya msingi hapa ingekuwa ni kwanini tunawaandalia marais wetu mazingira yenye kuwafanya walazimike kukopa na kufanya shughuli binafsi wakiwa madarakani. Kama tunaona mapungufu ya kimaadili kwa Rais aliye madarakani kukopa na kufanya biashara, basi, jambo hili lisiishie kwenye kudhani, kuwa kila rahisi atazingatia maadili ya uongozi hata yale yasiyoandikwa popote. Tukikubaliana kuwa ni mapungufu, basi, hayo na mengineyo yawekwe wazi katika Katiba yetu.
Lakini, katika maisha, binadamu tunapenda sana tuache kumbukumbu nyuma yetu ( Legacy). Kwamba hata siku tukiondoka hapa duniani, tuwe na mambo ambayo jamii inayotuzunguka tungependa wayakumbuke na kutuhusianisha nayo. Na hapa ndipo ilipolala hoja yangu ya msingi. Kwamba ni kwa yepi tunataka tuukumbuke utawala wa Awamu ya Tatu wa Rais Mkapa? Na, je Mkapa mwenyewe alipenda akumbukwe vipi?.
Naam! Historia n mwalimu mzuri, na ili tuyaelewe yanayotokea sasa na kesho hatuna budi kuitazama historia. Itakumbukwa, kuwa safari ya Mkapa kwenda Ikulu ilianzia Mei 8, 1995, mara ile alipotangaza rasmi azma yake ya kuwania kuteuliwa kugombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi.
Mkapa aliyekuwa Waziri wa Sayansi na Elimu ya Juu hakufahamika vema kwa Watanzania wengi. Hakupewa nafasi kubwa hata na vyombo vya habari; ” Mkapa naye achukua fomu,” ilikuwa ni moja ya vichwa vya habari katika moja ya magazeti yetu. Neno ”naye” limetumika kuonyesha mtu huyo Mkapa hakuwemo katika waliofikiriwa kuchukua fomu.
Miaka kumi na moja iliyopita, umaarufu wa mwanasiasa Ben Mkapa ambao haukuzidi ule wa mwanasoka Kenny Mkapa wa Yanga, ukaja kuvuka mipaka ya Tanzania na bara hili la Afrika. Kutoka Afrika Kusini hadi Asia na Marekani ya Kusini. Kama ni darasani, Mkapa aliwakuta wenzake akina Museveni, Kagame, Thabo Mbeki , Obasanjo na wengine wakiwa wanashika nafasi za mbele. Katika ukanda wa Maziwa Makuu, Museveni ndiye aliyekuwa ”Kiranja Mkuu”. Haikuchua muda kabla ya Mkapa kuonyesha kuwa alikuwa ” Hodari Darasani”. Kimsingi, Mkapa akaja kuchukua nafasi ya Ukiranja kutoka kwa Museveni.
Mkapa yule Benjamin akaonekana kwenye majukwaa mengi ya kimataifa, aliitangaza Tanzania na aliifanyika kazi Afrika. Pamoja na mapungufu yake ya kibinadamu, katika kipindi chake cha miaka kumi ya utumishi wa umma, Mkapa ametoa mchango mkubwa kwa watu wa nchi hii, bara hili na dunia kwa ujumla.
Maishani, binadamu hutenda mazuri na mabaya, lakini lengo hasa ni kutenda yaliyo mema na ya kimaadili. Mara nyingi anayemaliza kwa mazuri hufuta mabaya yake mengi aliyoyafanya nyuma. Na swali Je, Mkapa angependa akumbukwe kwa lipi alipata kuulizwa Mkapa mwenyewe na mwandishi David Martin miaka kumi na mbili iliyopita. Ilikuwa ni muda mfupi kabla ya kuingia madarakani. Mwandishi alimwuliza; ”Mwisho, ukiangalia mbele miaka mitano au labda kumi, ungependa historia ikukumbuke kwa namna gani?”
Mkapa anajibu; ”Ningependa nikumbukwe kama mtu niliyeongoza Utawala ambao kwa vitendo umepiga vita rushwa na umeimarisha aina ya uongozi, utumishi wa umma, thamani na wajibu uliokuza utawala bora. Kwamba katika utawala wangu nimeongoza juhudi za kuimarisha nidhamu katika mchakato wa utawala, nidhamu kwa maana ya sheria, kanuni na taratibu, lakini ndani yake zikiwa na misingi ya uhuru. Hivyo basi, kukuza misingi ya huru na maendeleo ya haraka, lakini katika mtazamo wa sheria na taratibu, hivyo basi nidhamu.
Kwamba nimehamasisha ajenda ya vyama vyingi, mfumo wa vyama vingi, bila kuharibu. Lakini zaidi kwa dhamira ya wazi ya kujenga utaifa katika Jamhuri hii ya Muungano wa Tanzania. Nitatumaini kuwa itasemwa kuwa, nimejaribu kwa bidii zangu zote kufikia matoeo hayo bila kujidai ambako mara nyingi kiujumla uhusishwa na ofisi kuu ya nchi, lakini zaidi, kinyume chake, kuyafanya hayo kwa heshima na unyenyekevu mkubwa.”
Hapa ni kwa Mkapa mwenyewe na jamii kwa jumla kufanya tathimini ya kile alichokieleza na alichokitenda. Kabla ya kumhukumu kwa matendo yake, kumtendea haki Mkapa ni kujaribu kumwelewa alichokisema na alichokitenda na katika mazingira aliyoyakuta na kuanza kuyafanyia kazi aliyosema. Na wenye kupitisha hukumu tusome hukumu zao kwa kuyaangalia mazingira ambayo chama cha mapinduzi kiko nayo sasa.

Ni vema pia tukafikiri kwa bidii. Tucambue kwa kina na kujiuliza. Mkapa alisema alikuwa na nia ya kuimarisha ajenda ya vyama vingi vya kisiasa. Je, ni nani wa kumlaumu leo kama ajenda hiyo inaelekea kukosa mwelekeo na pengine kuwa kinyume chake? Na, je, shutuma anazobebeshwa Mkapa sasa zinalenga kwenye kulinda maslahi ya nchi au ya kikundi cha wachache?
Muhimu katika jamii yeyote ile ni kwa wanajamii kuaminiana. Kuwepo kwa moyo wa utaifa na uzalendo miongoni mwa wanajamii. Si jambo jema kuanza kuingiwa na hofu juu ya dhamira halisi za baadhi yetu. Ni muhimu kwa waongozwa kuwaamini viongozi wao, na viongozi kuwaamini wanaowaongoza. Imani huchangia katika kujenga misingi ya amani na utulivu katika jamii. Kwani, msingi mkuu wa amani ni imani.
Unayemwamini utakuwa na amani naye. Kutoaminiana kidhamira, kutiliana mashaka ni chachu za kukosekana kwa amani katika jamii yeyote. Hata katika siasa za upinzani watu huaminiana. Ndivyo wanavyofanya wenzetu walioendelea katika demokrasia. Kutofautiana kifikra, kiitikadi, kimitazamo hakuna maana ya uadui. Kwenye kulinda maslahi ya taifa kuna ”wenzetu katika chama” na wenzetu katika upinzani. Katika siasa hata upinzani una umuhimu mkubwa katika kujenga taifa. Hakuna ”Hawa wenzetu” na ”Wale si wenzetu”. Hilo la mwisho linatoa tafsiri ya ubaguzi. Itaendelea juma lijalo. Kwa makala zaidi, maoni na picha, tembelea; http://mjengwa.blogspot.com
 
Babu Ataka kusema,

Ongezeko la ukusanyaji wa kodi wakati wa serikali ya BWM lilisaidia kwenda kulipia madeni yetu ya nje ndiyo sababu tukapata msamaha wa kufutiwa madeni. Madeni yamefutwa wakati BWM anaondoka. Hivyo ni vizuri mumuulize JK amefanyia nini pesa za msamaha. BWM aliikuta nchi ina matatizo mengi hivyo ilikuwa vigumu kushulikia yote, nafikiri aliamua kuweka periority kwenye kuinua uwezo wa ukusanyaji kodi kwanza na kuservice madeni yetu ya nje na kuinua uwezo wa serikali ambayo hata kulipa mishahara watumishi wake ilikuwa tabu. Ukilinganisha na sasa (toka JK aingie) uwezo wa nchi umeanza kwenda chini kwa kasi kubwa ndiyo maana percentage ya budget tegemezi imeongezeka kwa asilimia 3 ingawa tumefutiwa madeni.

Kipindi cha BWM ujenzi wa barabara nyingi ambazo zilianza kipindi chake either zilimalizika kwa wakati au zilikuwa na maendeleo mazuri mpaka JK alipoingia. Nakumbuka siku alipotembelea ughabuni huku niliko aliahidi barabara ya Mwanza-Dodoma ingeisha last December. Lakini source zangu zinaniambia hata wakandarasi kwa sasa wnalipwa kimachalechale. Mfano mwingine Ni uwanja wa mpira ambao ulikuwa unakaribia kuisha mpaka JK akawa anawaalika Real Madrid kuja kufungua leo hii bado ni kitatawiri kw sababu ya usimamizi mbovu.

Of course TZ inategemea misaada ili iweze kujenga mabarabara, lakini bila usimamizi mzuri bado itakuwa ni ndoto kwetu. Lakini BWM kwa mara ya kwanza aliweza kuanza kujenga barabara kwa kutegemea pesa za serikali. Lakini toka JK aingie madarakani uwezo wa serikali umepungua ndiyo sababu unasikia Makandarasi wa Kichia wamesimama kwa vile hawajalipwa.

Makampuni ya TBL na Sigara yalibinafsishwa tangu enzi za AHM. TBL ilikuwa mahututi inangojea kufa. Biashara ya bia za Kenya ndipo iliposhamiri na Kenya Breweries wakaanza kupenetrate TZ. Mashirika ambayo hayakupaswa kuuzwa kwa maooni yangu ni kama NBC, TTCL, NIC lakini siyo sigara na TBL. Makampuni kama at least sasa ndiyo yanaweza kulipa kodi vizuri na kulipa divident kwa serikali.

Upande ambao BWM ametuangusha ni upande wa rushwa na kuuzwa kwa madini yatu bure! Damage aliyoifanya ni kubwa may be kuliko alivyo achieve. Kibaya zaidi serikali ya JK inayaendeleza mabaya yote ya BWM kwa kasi kubwa ndiyo sababu hali ya nchi inakuwa mbaya siku hadi siku!!!
 
Keil,
Kula tano. Kwa usemi mwingine huyu alijigeuza kuwa kuwadi wa utandawazi. In the process akauza nchi na kutanua mifuko yake.
 
Bubu,
1. Development is not a one time event it is a process! Investment, education, health, infrastructure etc trickle effect could not necessary be seen during BWM era. BWM instituted a good discipline of tax collection we don’t have problems of paying salaries as during Mwalimu or Mwinyi era!
2. BWM internationally was liked by West (for a poor country you need them) hence more loans and DFI and debt cancellation- why did West not found of Moi? Why BWM? He was even invented to G8. I hate foreign AID but if you are poor- we can not do without AID currently! Hence Mkapa bridge- why not during Mwinyi or Nyerere?
3. Viongozi kutibiwa nje- poor health services did not start during BWM era- started long time- and this is not particular in Tanzania. Unajua wananchi wengi vijijini sasa hukimbulia hospitali za serikali kwa kuwa siku hizi kuna dawa? Tafiti ninyi zimeonyesha- baadhi ya hospitali binafsi vijijini hawapati watu. Huduma bado sii nzuri 100% ila there is some improvement! IMR declined pia this time! Ila MMR has not changed!
4. Ubinafsishaji- serikali haikuuza Breweries, NMB, bali waliingia ubia- wanapata gawio na kodi!
5. Kuna mapungufu kweli- ila pia kuna mafanikio -sii vema kufumba macho na kuangalia mapungufu tu- tufanye mizania. Mimi simtetei BWM ila saa zote tumejikita kuangalia mapungufu yake tu kama vile basi ni malaika- yeye ni binadamu kama wewe na mimi!

We have to measure his success and failure during his era in office in my opinion and opinion of most of Tanzanians as well his success are very minimal as compared to his failure, therefore the conclusion he was not a good president at all, only few Tanzanians and most of them from well to do families were able to benefit during his era.
 
Kwa assessment yangu ya mazuri na mabaya ya Mkapa , i can say he is currently the most failed President in Tanzania History, hata hivyo vitu vilivyo pewa majina yake Havifai kuitwa Benjamin William Nkapa, inasikitisha lakini ndio ukweli wenyewe.
Alikuwa na nafasi tosha ya Kufanya Vizuri on this earth lakini sijui akili yake ilikuwa Nzito au Ulafi.
Infact kutokana na History yake Mbaya hilo Daraja la Rufiji afadhali liitwe Ali Hassan Mwinyi.
Na ile Shule Ilala Pale tutafute Jina Jingine
 
MIMI kwa mtizamo wango TZ hakuna rais ambaye alifanikiwa. Ukianzia na JKN alitaifisha mguzo kuu za uchumi akaziweka mikononi mwa serikali, akatumia akiba ya serikali kuanzisha vijiji (Villagerisation) akaleta vita na Uganda matokeo yake uchumi ukaporomoka. Akamleta AHM.

AHM yeye hamna hata haja ya kumraumu. Simply the guy did not know what to do. Akatoa rukhsa kila mahali. Bahati nzuri hakutufikisha Zimbabwe!!!

BWM kagawa natural resources zetu na kutuingiza kwenye mikatba ambayo itatucost miaka nenda miaka rudi, akaimarisha grand corruption na kutuletea JK.

JK baada ya mwaka na nusu hata mwelekeo hajui. Anaendeleza mabaya ya waliomtangulia na kuporomosha uchumi kwa kasi mpya. Sasa huyu bwana ambaye baada tu ya muda mfupi kasha onekana weakness zake sasa tutafika kweli???
 
MIMI kwa mtizamo wango TZ hakuna rais ambaye alifanikiwa. Ukianzia na JKN alitaifisha mguzo kuu za uchumi akaziweka mikononi mwa serikali, akatumia akiba ya serikali kuanzisha vijiji (Villagerisation) akaleta vita na Uganda matokeo yake uchumi ukaporomoka. Akamleta AHM.

AHM yeye hamna hata haja ya kumraumu. Simply the guy did not know what to do. Akatoa rukhsa kila mahali. Bahati nzuri hakutufikisha Zimbabwe!!!

BWM kagawa natural resources zetu na kutuingiza kwenye mikatba ambayo itatucost miaka nenda miaka rudi, akaimarisha grand corruption na kutuletea JK.

JK baada ya mwaka na nusu hata mwelekeo hajui. Anaendeleza mabaya ya waliomtangulia na kuporomosha uchumi kwa kasi mpya. Sasa huyu bwana ambaye baada tu ya muda mfupi kasha onekana weakness zake sasa tutafika kweli???

Nyerere kwa kiasi fulani alifanikiwa na ukilinganisha na marais wa nchi nyingine za Kiafrika alifanikiwa sana.

Sera za Mwalimu ziliwalenga Watanzania na baadhi ya matunda yake mpaka leo tunayaona. Wasomi wa Kitanzania waliotapakaa katika sehemu mbali mbali duniani ni matunda ya Mwalimu.

Kama siyo sera za mwalimu sidhani kama Mkapa na Kikwete na watoto wa walala hoi wengi wa Tanzania wangeenda shule. Shule ingekuwa ni kwa wale walio na uwezo tu wahindi na wabongo wachache wenye kutoka katika familia zenye uwezo wa kifedha. Wasomi wengi wa Tanzania waliosoma enzi za Nyerere ukiwauliza kuhusu elimu yao mpaka kesho bado wanampa credit kubwa mwalimu, kama siyo sera zake wengi wasingefanikiwa kukanyaga shule.

Sera za vijiji vya ujamaa pia zilikuwa nzuri ili kuharakisha upayikanaji wa huduma bora kama maji, zahanati, elimu n.k. lakini utekelezaji wake ulikuwa hafifu.

Sera za kupinga devaluation ya shilingi, hili pia Mwalimu aliangalia Watanzania watanufaika vipi kwa kushusha thamani ya shilingi yetu. Alichoona ni kwamba trekta lile lile tulilokuwa tunanunua na magunia 10 ya kahawa, baada ya kushusha thamani tungehitaji magunia 15 au zaidi ya kahawa ili kununua trekta lile. Alikuwa sahihi kabisa na mpaka hii leo hao walioshusha thamani ya shilimgi yetu hawawezi kukwambia chochote kuhusiana na manufaa ya sera hiyo kwa Watanzania. Watakwambia FDI iliongezeka, wachukuaji nyinyi mnawaita "wawekezaji" walikuja kwa wingi pia tulifutiwa baadhi ya madeni yetu ya nje. Ukiwauliza je haya yaliwasaidiaje Watanzania katika kupunguza ukali wa maisha, kuongeza ubora wa elimu, upatikanaji wa maji, upatikanaji wa matibabu siku zote hawatakupa jibi linaloweka na kuna ushahi wa kutosha kwamba pamoja na kuongezeka FDI, kuja wachukuaji na kufutiwa madeni Watanzania walio wengi hawakuona mafanikio yoyote.

Mwinyi aliwahi kusema yeye ni kichuguu ukimlinganisha na Mwalimu ambaye ni mlima. Mwalimu hakuwa perfect lakini mafanikio yake ni mengi uklinganisha na failures zake, ndio maana hadi hii leo bado ni kipenzi miongoni mwa Watanzania wengi na Waafrika waliopata bahati ya kumfahamu wakati wa uhai wake.
 
Babu,

Mafanikio ya Nyerere yapo both domestic and international. Lakini domestic hakufanikiwa sana zaidi ya kuondoa ukabila na kuunganisha watanzania. Kama elimu ni kweli ilikuwa bure lakini bado waliofaidika ni wachache tu although from all groups. Elimu ya Tanzania zaidi ya kujua kusoma na kuandika walioendelea mbele walikuwa wachache sana. Mfano mzuri, mimi nilipomaliza primary school miaka katikati ya themanini wanafunzi wasiozidi 10,000 ndiyo waliofaulu kuendelea secondary school. Kumbuka wakati ule private school zilikuwa za kuhesabu. Then O level kwenda A level 2500. Chuo about 1400. Sasa unaweza kuona kuwa elimu yetu imekuwa nyuma siku zote. Pia usisahau mambo ya UPE ndiyo yalianza wakati uleule wa JKN.
 
Babu,

Mafanikio ya Nyerere yapo both domestic and international. Lakini domestic hakufanikiwa sana zaidi ya kuondoa ukabila na kuunganisha watanzania. Kama elimu ni kweli ilikuwa bure lakini bado waliofaidika ni wachache tu although from all groups. Elimu ya Tanzania zaidi ya kujua kusoma na kuandika walioendelea mbele walikuwa wachache sana. Mfano mzuri, mimi nilipomaliza primary school miaka katikati ya themanini wanafunzi wasiozidi 10,000 ndiyo waliofaulu kuendelea secondary school. Kumbuka wakati ule private school zilikuwa za kuhesabu. Then O level kwenda A level 2500. Chuo about 1400. Sasa unaweza kuona kuwa elimu yetu imekuwa nyuma siku zote. Pia usisahau mambo ya UPE ndiyo yalianza wakati uleule wa JKN.

Hilo la kuondoa ukabila na na kuwaunganisha Watanzania ni kubwa sana na ndiyo maana limeasaidia sana kuifanya nchi yetu ikawa ina amani kwa kiasi fulani ukilinganisha na nchi nyingi za Kiafrika. Angalia Burundi na Rwanda, nchi hizi zin makabila mawili tu Wahutu na Watutsi lakini wanachinjana kwa idadi kubwa kabisa kila kukicha. Kama utakumbuka mwaka 94 watu milioni walipoteza maisha huko Rwanda kwa mfarakani wa makabila mawili tu, je hali ingekuwaje Tanzania ambako tuna makabila zaidi ya 120 kama sio juhudi za Mwalimu kutufanya tujione ni Watanzania kwanza kabla ya ktu kingine chochote. Kwa mtazamo wangu hayo ni mafanikio makubwa sana na yasingewezekana katika awamu ya tatu au hii ya sasa kwa upendeleo ulio wazi kabisa kwa familia za viongozi na marafiki wao walio karibu. Tungechinjana kila kukicha!!! Si umesikia mtandao ndani ya CCM!!! na huu hauishii CCM tu umejitandaza mpaka kwenye sirikali.

Ukilinganisha na wakati wa mkoloni idadi ya Watanzania walionufaika kielimu ni wengi sana, na ndio maana nafasi karibu zote za juu katika mashirika yetu zilishikwa na Watanzania kitu ambacho hakikuwezekana wakati wa mkoloni na 100% ya uchumi wetu ilikuwa mikononi mwa Watanzania, siyo kama leo hii uchumi umeshikwa na wageni ambao wanamiminika Tanzania kila kukicha ili waje wachukue zaidi.

Mwalimu alitamka hatuwezi kuwa huru kama nchi jirani bado zimetawaliwa na wakoloni. Tanzania ilitumia pesa nyingi katika kuzikomboa nchi za majirani zetu na kuwatunza wakimbizi toka nchi hizo. Hili kuna wanaoliunga mkono na kuna wengine wanasema tulitumia pesa nyingi kuliko uwezo wa nchi yetu na kusahau maendeleo ya nchi yetu.

Kama nilivyosema Nyerere hakuwa perfect pia alikuwa na mapungufu yake, lakini sera zake ziliwalenga Watanzania kwa ujumla na wako wengi waliofanikiwa kielimu na leo wanapeta nchi mbali mbali ulimwenguni bado wanamkubuka sana Mwalimu. Kwa kifupi aliyoyafanya mazuri ni mengi mno ukilinganisha na mabaya. Pia ukumbuke crisis ya mafuta duniani mwaka 73/74 ambayo ilisababisha bei ya mafuta kupanda iliiumiza sana nchi changa ya Tanzania wakati huo tukiwa na miaka 12 tu tangu tujitawale. Pia vita vya kumng'oa nduli tulitumia pesa za kigeni nyingi ili kununua silaha za kupambana na nduli na njaa kali ilitokea katika mwaka 74 na 75 ambayo ilisababisha kampeni ya kilimo cha kufa na kupona nayo iliathiri sana uwezo wa serikali ya Nyerere.
 
Sehemu kubwa ya majadiliano ya ujenzi wa Daraja la Mkapa ulifanywa wakati wa mzee Ruksa.
 
Mkapa anajibu; "Ningependa nikumbukwe kama mtu niliyeongoza Utawala ambao kwa vitendo umepiga vita rushwa na umeimarisha aina ya uongozi, utumishi wa umma, thamani na wajibu uliokuza utawala bora. Kwamba katika utawala wangu nimeongoza juhudi za kuimarisha nidhamu katika mchakato wa utawala, nidhamu kwa maana ya sheria, kanuni na taratibu, lakini ndani yake zikiwa na misingi ya uhuru."

Mhhhh! Nidhamu halafu unafanya biashara ndani ya Ikulu!!!! ulipiga vita rushwa!!! I reserve my comments.
 
LOL! Mwewe unazengea vifaranga vya kuku au Bata! Majina ya humu mengine yanavunja mbavu. Ahsante kwa mchango wako.
 
Babu
Nashukuru kwa somo zuri ulilotoa, na kwa kuongezea challenge za Nyerere zingine ziliongezewa na Vita Baridi kati ya Nchi zenye mlengo wa kulia na zenye kufauta mlengo wa kushoto.
Nchi za magaribi zilikuwa zikitu black mail na kutu-zoofisha nchi zenye kufuata siasa za kijamaa kama wanavyo ifanyia CUBA mpaka sasa.
Pia kusaidia liberation struggle kulisababisha nchi za magharibi kutuhujumu kiuchumi ili tushindwe kusaidia hivyo vita
Sasa huyu ndugu yetu Ben Nkapa njia ilikuwa nyeupe lakini alishindwa kuiona, sasa sijui kwa maksudi au lense ya miwani yake ilikuwa zimekwisha nguvu
 
Bubu,

Aliyofanya Mkapa (1995-2005)

A: Positives


7. Kufutwa kwa madeni ya nje HIPC
8. Kuongezeka Foreign Direct Investment- Gold Minig etc
10. Muafaka wa CUF na CCM


Kufutwa madeni sijanona faida yake zaidi ya kuwasaidia Watawala wetu waeendelee kukopa na kutumia vibaya mikopo kwa kuingia mikata hewa na kuifukarisha nchi yetu zaidi na zaidi pia kutuongezea madeni tu.

Kuongezeka kwa FDI labda lakini kwenye Madini hata Muungwana anajua tumeliwa, ingawa alikuwepo na ndo maana anawapigia magoti wawekezaji wafikiri kukubali turekebishe mikataba hiyo.

Sula la Mwafaka yalikuwa ni Mazingaombwe na Maigizo ambayo CCM wanaelekea kuyarudia tena, wanavuta-vuta hadi 2010. Fukurto linazidi kuwa kali. Si wasikia kauli za Makmba na Kingunge? BWM hakufanya kitu na Muungwana ameamua kuanzisha Mwafaka mpya ingawa kina Kingunge na Makamba wanafanya usanii.
 
Babu,
Kilichomponza Mkapa ni tamaa. Ukisoma makala alizoandika Philip Ochieng, ambaye alifanya naye kazi inakuwa wazi kuwa tamaa ilimzidi alipoingia Ikulu. Nasikia yeye mwenyewe alikuwa akichukua 30% ya kila deal na alisikika akiwaambia marafiki zake kule NY baada ya kustaafu kuwa he is well taken care of financially.
 
Back
Top Bottom