Mizengo Pinda: Mnaitaka Tanganyika ipi?.

Mizengo Pinda: Mnaitaka Tanganyika ipi?.

Pinda acha kupotosha umma wa Watanzania na kauli zenu za kisiasa kwenye jambo la kisheria...

Wananchi wanaotaka serikali tatu na kutaja kuwa wanahitaji Tanganyika huru maana yao ni kwamba wanahitaji mamlaka huru ya Tanganyika na kwa mantiki hiyo mamlaka huru ya watu wa Zanzibar.

Wasiwasi wa CCM katika jambo hili ni moja tu, uwepo wa serikali tatu utapunguza kwa kiasi kikubwa usultani wa chama chao ndio maana hoja yao haina mashiko ya kisheria bali inatetewa kisiasa zaidi.

Mwalimu Nyerere sio Mungu kiasi cha kuamua hatma ya Taifa letu, alichofanya kutuunganisha kinastahili pongezi.
Kwa sababu hiyo basi kwa nini CCM kupitia maono ya Nyerere wasipiganie serikali moja? Hii si ndio itamaanisha umoja zaidi?

Mkuu, huyu pinda anatumia wadhifa wake vibaya kwa kutetea hoya ya chama chake ya usultan. Nothing important!
 
Pinda Pinda Pinda!!! tunalitaka hilo Pinda liombe radhi kwa Wazanzibar kwa kuukashfu UHURU wetu adhimu iliyoitambulisha Zanzibar Kimataifa pale tupipoipandisha bendera yetu ktkt jiii la Washington Umoja wa Mataifa!!

Matunda na neema za Uhuru wa Zanzibar 1963 wanajua Wazanzibar wenyewe sio mtu wa Nyika kama wewe!!
lakin sisi kama Wazanzibar Pinda tunakuelewa kwa ilee kauli uliyodhihirisha chiki yako juu ya nchi yetu adhimu ya Zanzibar na Wazanzibar kwa ujumla, ulisema kwamb Zanzibar sio nchi, lakin Dk Karume akakujibu kwa marekebisho ya katiba ya Zanzibar ya 2010, sasa Zanzibar ni nchi na mipaka yetu inatambuliwa!!

Ama kuhusu ujio wa Tanganyika ipi, ilo Wazanzibar halituhussu, sisi jukumu letu ni kuirejesha Jamhuri ya Watu wa Zanzibar aliyotuachia Mzee karume, baada ya maponduzi yetu yalopoteza damu za watu na kwa hilo kattu halizuiliki, Zanzibar itarudi tu hata hata kwa mtutu!!

Pinda hupiganii serikali 2 bali leo CCM wabadili waseme tunataka serikali 1 basi utafurahi kwa MAKALIO yako kwa jinsi chuki yako ilivyozidi kwa Wazanzibar, lakin tunawwambia Zanzibar kumezwa na Tanganyika sawa na Ngamia kupenya kweny tundu ya sindano, kattu haiwezekanii?
 
teh....teh...teh....teh......serikali moja inatosha au tuvunje muungano au kipengele hicho kiondolewe kwenye mjadala wa bunge la katiba unaoendelea bungeni sasa na badala yake turudishiwe wananchi tukipigie kura ya maoni na kuamua kati ya serikali moja, mbili, tatu au kuuvunjilia mbali muungano. baada ya kura ya maoni ndiyo kipengele hicho kiingizwe kwenye katiba na kuwekewa utaratibu. maana yake ni kwamba kazi ya bunge la katiba itakuwa ni kuweka utaratibu tu lakini maamuzi tutakuwa tumefanya sisi wananchi.
Hapoo kwenye kura una uhakika Kama kura hazitachakachuliwa ? Unaweza piga kura ya maoni na motokeo yakawa kinyume
 
Nadhani pinda anakosa hekima na busara ndio maana kazungumza hivyo. Jamani kazi tunayo na huyo ndio waziri mkuu!
 
Kwa maoni yako, hutaki Tanganyika kwa sababu hujawi kuiona, lakini wakati huo huo unapendekeza kuvunja muungano kitendo ambacho kitarejesha Serikali ya Tanganyika moja kwa moja ambayo huitaki! Je si vyema ukawa na Serikali hiyo ndani ya muungano?
Mkuu napenda uelewe mantiki nzima ya Tanganyika ndiyo maana unawaona hawa makada wa CCM kwa sasa wanaanza kuja na maswali ya Tanganyika ipi?. Hili neno Tanganyika ipi lina maana kubwa sana kimantiki.

Tukivunja muungano hatuwezi kuwa tena na Tanganyika bali tukakuwa na nchi nyingine kabisa ambayo ni tofauti na Tanganyika ya 1960's.

Serikali moja haiwezi kuwa na Tanganyika tena au Zanzibar bali itakuwa ni taifa tofauti kabisa.
 
Watakaopinga serikali 2 wapigwe tu. Kwani wale waTanganyika waliokuwepo 1961-1964, 90% hawapo sasa nyie mnadai ipi wakati wenyewe hawapo? Zanzibar tutahakikisha inapata hadhi yake kwa kuwa wao wana uchungu na nchi yao kumezwa, na hawa waliopo ni kizazi cha wale waZanzibar hivyo wana haki kubaki waZanzibar
 
Ndiyo maana mimi niliamua kujiunga na CDM kwa kuwa hili li CCM nililikuta limeshazaliwa na walioanzisha ndio wana haki kulitetea. Sasa sie tutaka CCM ipi?
 
Tanganyika ya mkoloni?!!!
Hivi Pinda ana akili? Lini Tanganyika iliwahi kuwa ya mkoloni? Tanganyika imekuwa ya Watanganyika kabla, wakati na baada ya ukoloni. Muungano iliodhamiriwa na Nyerere na Karume umeshindwa kuwepo.
 
Kwa hiyo msimamo wa C.c.m unakinzana na matakwa ya wananchi wenye nchi yao?ni kwa maslahi ya nani?ya wana ccm wachache au ya Watanzania walio wengi?hawa tuliowapa dhamana ya kutuongoza naona wamejisahau sana,wanapotaka kutufikisha ni pabaya!
 
Kama swala ni kupunguza gharama na kuimarisha umoja wetu, kwa nini tusiwe na serikali moja? Mbona ccm hawaongelei kuhusu serikali moja?
 
Tanganyika ya mkoloni?!!!
Hivi Pinda ana akili? Lini Tanganyika iliwahi kuwa ya mkoloni? Tanganyika imekuwa ya Watanganyika kabla, wakati na baada ya ukoloni. Muungano iliodhamiriwa na Nyerere na Karume umeshindwa kuwepo.

pinda amepinda; amepinda akili, mawazo, maamuzi,uelewa, lakini pia kapinda sura
 
pinda amepinda; amepinda akili, mawazo, maamuzi,uelewa, lakini pia kapinda sura

Ukimwona muulize eti kama Zanzibar ni nchi yenye katiba na mipaka yake, je upande wa magharibi imepakana na nchi gani?
 
Kwa hiyo msimamo wa C.c.m unakinzana na matakwa ya wananchi wenye nchi yao?ni kwa maslahi ya nani?ya wana ccm wachache au ya Watanzania walio wengi?hawa tuliowapa dhamana ya kutuongoza naona wamejisahau sana,wanapotaka kutufikisha ni pabaya!

Sina Uhakika Kama Serikali Tatu Ni Hoja Ya Wananchi Au Wanasiasa......
 
Namuunga mkono moja kwa moja eti mtu ana miaka 25 eti kwa sababu kapata tiketi ya kuingia bungeni kama mjumbe unasikia anasema serikali Tatu wakati hata wakati Tanganyika inapata uhuru hakuwepo,Pinda nakupongeza kwa msimamo wako thabiti

Kwani angekuwepo wakati Tanganyika inapata uhuru angefanyaje? Unataka kusema suala la muungano lijadiliwe na watu waliokuwepo wakati Tanganyika inapata uhuru pekee? Sina shaka hii ni hoja dhaifu sana. Umeusoma waraka uliowekwa hapa jana na Al Sharpton? Wewe au Pinda aliyekuwepo miaka hiyo, ulishiriki kufanya maamuzi ya kuunganisha Tanganyika na Zanzibar?
 
Kuna maneno sio mazuri ila kuna kipindi inabidi tukumbushane!!!!!!
Wazee tunawaheshimu sana ila heshima ni pamoja na kuyapa uzito mawazo ya huyo unayemuona mdogo!!!!!

Maneno yenyewe ni haya; wazee wenu wamekufa mnafanya yenu sasa,na nyie mtakufa nasi tutafanya yetu kwa muda wetu!!!!!!

Much as sisi vijana tupo wengi na hatutaki muungano huu wa sasa basi ipo siku tutaupasua tu na kama kuna umuhimu wa kushirikiana tutafanya hivyo ila mtaondoka tu! !!!!!!!Sasa ni juu yenu kuondoka na heshima au muziache humo maofisini mkitoka mtoke watupu!!!!!!!!

Kuna mmoja wenu humo alikuwa na nguvu sana lakini sasa si anateuliwa tu kwa ridhaa na heshima huo ni mfano kuwa nguvu kitu cha kupita!!!!!!
 
Back
Top Bottom