Ukisikia janga la taifa ndio hili, Tunajua Tanganyika wamesha uza, maneno tuliyokuwa nchi imeuzwa ooo imeuzwa kumbe ni Tanganyika? Nashukuru sana Pinda kwa kufafanua, Tumesoma vitabu mzee tunaambiwa muungano ni watanganyika na Zanzibar na ninakumbuka zamani tulikuwa tunasherehekea uhuru wa Tanganyika mwaka 1961 sio Tanzania Bara, Kweli leo nimeamini Tanzania hakuna wasomi maana tunadanywa hata kwenye Elimu,
nikijiuliza Zanzibar ni muunga vilevile, Unguja na Pemba, Mbona unguja ipo na Pemba Ipo kwanini Tanganyi ife? Zanzibar iwepo? Na kama Pinda anasema Tanganyi ipi tunataka? Yeye alizaliwa kwenye nchi inayotwa Tanganyika? Au Tanzania Bara? Maana kazaliwa kabla ya uhuru wa Tanganyika,
Jamani naomba niishie hapo maana nisije kutukana maana naona hapa hawa viongozi bado wanatuona ni wale wale wa kuambiwa ukichagua upinzania wataleta vita, yaaani bado wanatuona hatuna akili wametubebea, Wanachi wanataka Serikali tatu, ni maoni yao na wenyine muungano wa mkataba ni maoni yao, Sasa inakuwaje maoni ya CCM yawe mjadara? Na kwanini wajione hii nchi yao? Kuna maoni ya makanisa vyama vya Siasa vyote vilitoa maoni, jumuiya ya Waislamu, Sekta binafsi na makundi mbali mbali, wametoa kwa maandishi, je wote wasimamie kwenye maoni yao? Wasiifate tume ambayo ilikaa na kuyachambua maoni na kuona ni yapi yanafaa kuwepo? Kama wanataka basi tume ya katiba ilicho kifanya kiondolewe na waweke wanachotaka wao maana inaonekana tume walitutengenezea kwa danganya toto,
tusubiri tuone tutpata nini pale lakini sifikirii kupata kitu cha maana katika Bunge hili maana ccm kama watoto, oooo mara posho ndogo nina uhakika wanataka kuvuruga mchakato soi bure
aksante