Mizengo Pinda: Mnaitaka Tanganyika ipi?.

Mizengo Pinda: Mnaitaka Tanganyika ipi?.

Pinda acha kupotosha umma wa Watanzania na kauli zenu za kisiasa kwenye jambo la kisheria...

Wananchi wanaotaka serikali tatu na kutaja kuwa wanahitaji Tanganyika huru maana yao ni kwamba wanahitaji mamlaka huru ya Tanganyika na kwa mantiki hiyo mamlaka huru ya watu wa Zanzibar.

Wasiwasi wa CCM katika jambo hili ni moja tu, uwepo wa serikali tatu utapunguza kwa kiasi kikubwa usultani wa chama chao ndio maana hoja yao haina mashiko ya kisheria bali inatetewa kisiasa zaidi.

Mwalimu Nyerere sio Mungu kiasi cha kuamua hatma ya Taifa letu, alichofanya kutuunganisha kinastahili pongezi.
Kwa sababu hiyo basi kwa nini CCM kupitia maono ya Nyerere wasipiganie serikali moja? Hii si ndio itamaanisha umoja zaidi?
 
Huenda pinda alikuwa anaongea na watoto wadogo wa wajumbe wa jumuiya ya wazazi ya CCM, huwezi kumwaga pumba hizi mbele ya watu wazima.
 
Tunataka Tanganyika yetu tu! hizo anazoleta huyo mzigo ni mbembwe tu za kimagamba!
 
ccm mziki mtauona tu wala c muda mrefu. Historia ndio inayotufundisha. Nchi na watawala wote waliojaribu kutawala kimabavu waliingiza nchi zao ktk machafuko na huko ndiko mnakoelekea. Acheni watz waamue wenyewe wewe ni kiongozi wa serikali, kiherehere cha kuropokaropoka kinatoka wapi wakati mlishachagua watu kuijadili katiba, kwa nini mnawafundisha mambo ya kuamua? Futeni basi bunge la katiba mkaandike mawazo yenu mtuletee katiba mnayoitaka. Umburula mtupu
 
Kwa kauli hii ya Pinda wengi tuliozaliwa na kukuta Babu zetu waliishafariki tutawakana hadharani. Huu ulaghai wa CCM kukataa hata historia ya nchi yao unatia shaka sana. Huyu tapeli Pinda heri angekaa kimya kuliko kumwaga kinyesi kama hicho. Mdomo msafi hauwezi kutoa kauli kama hiyo.
 
Wataalamu wa sheria na mambo ya katiba serikalini walipotoa Hadidu za Rejea na kuikabidhi Tume ya Jaji Warioba kwa kupitia mkono wa Rais Kikwete, kuna wengine walidhani safari ya kisiasa kupata Katiba Bora waliyokuwa wanasafiri bila kufahamu walipo na wanakoenda, basi watakuwa wamefika.

Mwingereza anayejulikana kwa jina la kalamu kama Lewis Carroll alishawahi kusema, If you don’t know where you’re going, any road will get you there.

Well, kuna wanasiasa hawakufahamu kwa nini Hadidu za Rejea zilikuja na misingi kumi ambayo iliambatana na sheria ya mabadiliko ya Katiba 2013 iliyoacha milango ya kisheria wazi ambayo kwa sasa inatafsiliwa kwa namna yoyote bila hata kuvunja sheria. Wengine wanasema kazi ya Bunge la Katiba ni koboresha, huku wengine wakisema, kazi yake haina mipaka kisheria.

Majibu yake kwa sasa ndiyo haya yameanza kujitokeza kutoka kwa viongozi wakuu wandamizi wa serikali. Kama kuna viongozi wa siasa au vyama hawakufahamu kusuka au kunyoa lakini kwa sasa wako kwenye Bunge la Katiba, basi acha wanyolewe au wasukwe na serikali ya CCM ili wajitambue katika nafasi zao za kisiasa.

Waziri Mkuu ni mjumbe tu kwenye Bunge la Katiba pamoja na kwamba ni Mwenyekiti wa wabunge wa CCM lakini huwezi kuondoa msingi wa athari za matamko yake katika jamii. Kwa sasa yuko pale kutetea hoja na sera ya chama chake ambacho kina wanachama 'milioni tano'.

Hii ndiyo habari ya Mjini. Mnaotaka Serikali ya Tanganyika, mnakusudia Tanganyika ipi?. Tanganyika ya mkoloni au ya baada ya uhuru ya miaka mitatu!,

Mimi ninachotaka ni kuvunja Muungano au kama haiwezekani, basi serikali moja itanitosha kwa miaka 50 ijayo. Siitaki Tanganyika kwa sababu zijawahi kuiona. Sihitaji serikali mbili kwa sababu hazijajenga mazingira halisi ya serikali mbili. Serikali tatu ni kupoteza muda tu kwa sababu haziwezi kudumu. Serikali nne ni kuongeza gharama wakati shule hazina hata ubao wa kufundishia achilia mbali chaki na madawati.

Unapoona wingu linatanda, huna budi kutarajia mvua kunyesha lakini vile vile disappointment is all part and parcel of Homo sapiens.
mkuu yaani nimependenzw sana tu na ulivyomalizia katika "paragraph" mbili za mwisho. Serikali iwe moja tu kama kweli tunamapenzi ya kweli na dhati na TANZANIA. si hawataki tuitambue Tanganyika, yanini leo ndio wadamke na kuona Zanzibar ilikua imemezwa.????
 
Nyerere aliasisi Muungano akitarajia Kuwa Muungano huu Analojia utakuwa ukijiboresha kulingana na wakati yaani Muungano Digtal
Ninakubaliana na msingi wa hoja yako lakini ninatofautiana na wewe kidogo kwenye neno "Kujiboresha". Muungano hauwezi kujiboresha bali lazima uboreshwe na walioungana kwa pamoja kulingana na mazingira yaliyopo au yanayokuja.
Sidhani Kama Nyerere alitaka Muungano ubaki Kama ulivyo pasipo Kuwa Muungano tulivu Kama muungano wa kule U.S.A au kule UK kwa Malikia
Ni kweli dhana nzima ya kuungana ni kutengeneza mazingira ya utulivu na amani katika mataifa yaliyoungana.

Sikubaliani na wewe unaposema Muungano wa nchi zinazotengeneza UK ni tulivu. Muungano wa UK una matatizo sana pamoja na kwamba hayaonekani kwenye Television.

Siwezi nikagusia kuhusu U. S.A. kwa sababu sifahamu sana siasa zao.
Tiba Pekee na nzuri ni Kuwa na Serikari Moja tu Yaana ZNZ atawale Gavana kisha Bara atawale Gavana na Rais awe Mmoja tu na makamu wake wahamie Dodoma hakika huu Mvutano Kati ya Visiwa vyenye watu 1.5 million tu na Nchi kubwa ya watu million 43 utakwisha na Nchi kubwa itaepuka kupelekeshwa na watu wachache wajanja kuliko wengi wapole.
Yes, njia pekee ni kuwa na serikali moja na taifa moja. Haya mengine ya serikali mbili, tatu, nne ni "madudu" ambayo athari zake ni kubwa sana Kisiasa, Kiuchumi na Kijamii.
 
Ningemsifu ka ma angeuliza swali hilohilo kwa Zanzibar. Unafiki ni mbaya sana. Anawaogopa?
Swali lake ameuliza kwa wananchi wote na kulitolea majibu!. Inawezekana wewe ndiyo hujamuelewa!.
 
There is no logic kwenye maneno ya Mizengo Pinda, yeye kama mwanaCCM alikuwa wapi kuzungumza na Wazanzibar ili kutatua hizo shida? hadi leo anakuja kubwabwaja hapa maneno kama hayo? Hata sisi amabao hatukuishi miaka yake hiyo anayosema hatuutaki huo muungano wa serikali mbili kwa sababu kipindi hizo nchi zinaungana hatukuwepo.

Lakini wanaCCM bwana wanafikiri wao tu ndiyo wana hatimiliki ya kufikiri na sio wenzao!!!!!!!!!!!!!!!!!!!
 
Ninakubaliana na msingi wa hoja yako lakini ninatofautiana na wewe kidogo kwenye neno "Kujiboresha". Muungano hauwezi kujiboresha bali lazima uboreshwe na walioungana kwa pamoja kulingana na mazingira yaliyopo au yanayokuja.

Ni kweli dhana nzima ya kuungana ni kutengeneza mazingira ya utulivu na amani katika mataifa yaliyoungana.

Sikubaliani na wewe unaposema Muungano wa nchi zinazotengeneza UK ni tulivu. Muungano wa UK una matatizo sana pamoja na kwamba hayaonekani kwenye Television.

Siwezi nikagusia kuhusu U. S.A. kwa sababu sifahamu sana siasa zao.

Yes, njia pekee ni kuwa na serikali moja na taifa moja. Haya mengine ya serikali mbili, tatu, nne ni "madudu" ambayo athari zake ni kubwa sana Kisiasa, Kiuchumi na Kijamii.
Wanaotaka serikali Tatu ,Nne ,Tano ,Shirikisho n.k wanalao jambo yawezekana ni wahaini hawa
 
Sisi tuliozaliwa wakati Karume aliishakufa msituambie kitu kuhusu huyu muasisi maana CCM haitambui historia. Pia wale mliozaliwa baada ya Nyerere kufa achaneni na hao wazee ni misukule tu hakuna kitu kinaitwa historia. Hao wazee waliishajifia kama ilivyokufa Tanganyika...

Hii ndio tafsiri ya alichokiongea Pinda kwa mapana kwamba forget about the past, jali ya sasa. Jali Tanzania bara, Tanganyika ni msukule kama walivyo Nyerere na Karume kwa kuwa hawapo.
 
Jamani Tanganyika yetu mkoloni kaikuta mmetusomesha wenyewe tumeelewa tulipotoka na tunapoenda. Sasa napatata picha behind the scene ya katiba mpya
Kwani nani aliileta Tanganyika?.
 
Wataalamu wa sheria na mambo ya katiba serikalini walipotoa Hadidu za Rejea na kuikabidhi Tume ya Jaji Warioba kwa kupitia mkono wa Rais Kikwete, kuna wengine walidhani safari ya kisiasa kupata Katiba Bora waliyokuwa wanasafiri bila kufahamu walipo na wanakoenda, basi watakuwa wamefika.

Mwingereza anayejulikana kwa jina la kalamu kama Lewis Carroll alishawahi kusema, If you don’t know where you’re going, any road will get you there.

Well, kuna wanasiasa hawakufahamu kwa nini Hadidu za Rejea zilikuja na misingi kumi ambayo iliambatana na sheria ya mabadiliko ya Katiba 2013 iliyoacha milango ya kisheria wazi ambayo kwa sasa inatafsiliwa kwa namna yoyote bila hata kuvunja sheria. Wengine wanasema kazi ya Bunge la Katiba ni koboresha, huku wengine wakisema, kazi yake haina mipaka kisheria.

Majibu yake kwa sasa ndiyo haya yameanza kujitokeza kutoka kwa viongozi wakuu wandamizi wa serikali. Kama kuna viongozi wa siasa au vyama hawakufahamu kusuka au kunyoa lakini kwa sasa wako kwenye Bunge la Katiba, basi acha wanyolewe au wasukwe na serikali ya CCM ili wajitambue katika nafasi zao za kisiasa.

Waziri Mkuu ni mjumbe tu kwenye Bunge la Katiba pamoja na kwamba ni Mwenyekiti wa wabunge wa CCM lakini huwezi kuondoa msingi wa athari za matamko yake katika jamii. Kwa sasa yuko pale kutetea hoja na sera ya chama chake ambacho kina wanachama 'milioni tano'.

Hii ndiyo habari ya Mjini. Mnaotaka Serikali ya Tanganyika, mnakusudia Tanganyika ipi?. Tanganyika ya mkoloni au ya baada ya uhuru ya miaka mitatu!,

Mimi ninachotaka ni kuvunja Muungano au kama haiwezekani, basi serikali moja itanitosha kwa miaka 50 ijayo. Siitaki Tanganyika kwa sababu zijawahi kuiona. Sihitaji serikali mbili kwa sababu hazijajenga mazingira halisi ya serikali mbili. Serikali tatu ni kupoteza muda tu kwa sababu haziwezi kudumu. Serikali nne ni kuongeza gharama wakati shule hazina hata ubao wa kufundishia achilia mbali chaki na madawati.

Unapoona wingu linatanda, huna budi kutarajia mvua kunyesha lakini vile vile disappointment is all part and parcel of Homo sapiens.
Kwa maoni yako, hutaki Tanganyika kwa sababu hujawi kuiona, lakini wakati huo huo unapendekeza kuvunja muungano kitendo ambacho kitarejesha Serikali ya Tanganyika moja kwa moja ambayo huitaki! Je si vyema ukawa na Serikali hiyo ndani ya muungano?
 
Serikari Moja ni Bora zaidi kuliko chochote Nina imani Hata Nyerere alikuwa na Ndoto ya kuelekea huko siku moja Lakini endapo itashindikana Kuwa na serikari moja ni vyema tukaiga Mfumo wa Muungano wa UK yaani Zenji akae Waziri Mkuu kisha Bara napo akae Waziri Mkuu alafu Rais Mmoja tu akiishi Dodoma Nina imani hao watu 1.5 million wanaowapelekesha watu million 43 watatulia huko Visiwani wataacha Malalamiko yasiyokwisha hata wengine tutawakaribisha kwenye Visiwa vya Mafia Ukerewe ukara na vinginevyo vingi vilivyopo pande za Tanganyika waje wajifunze jinsi ya kuishi pasipo kulalamika lalamika wakati Unahudumiwa kwa Hali na Mali . Serikari mbili zitakuwa bora endapo tu Rais atakuwa Mmoja tu lakini kinyume na hapo Malalamiko ya wachache dhidi ya wengi yatazidi kuongezeka kwani ZNZ ni Visiwa Vidogo Lakini Majimbo ya Ubunge ni mengi kuna wabunge wengi Hakuna Mfano Nchi ndogo wabunge kibao Eneo la jimbo analowakilisha mbunge bara Zenji linakuwa na wabunge kibao huku Pesa ya kuwahudumia wote ikitoka hazina wao Dodoma bungeni wanapata posho wana bunge Lao lakini mbunge wa bara hapati posho huko wana katiba Yao wimbo wao wa Taifa yaani Wao chao ni chao Lakini cha Tz bara ni cha cha wote Mfano harisi ni Vigumu kwa mtu wa bara kumiliki Aridhi Zenji lakini wao ni rahisi kumiliki Ardhi Bara hivyo Wazenji ni Wajanja zaidi ya Watanganyika Chezea Wazenji wewe
 
Hawajui walikotoka watajuaje wanako kwenda ndio maana wataka serikali Tatu ,Nne nk .Pinda tuko nyuma yako tuna kuunga mkono
 
Namuunga mkono moja kwa moja eti mtu ana miaka 25 eti kwa sababu kapata tiketi ya kuingia bungeni kama mjumbe unasikia anasema serikali Tatu wakati hata wakati Tanganyika inapata uhuru hakuwepo,Pinda nakupongeza kwa msimamo wako thabiti
waliokuwepo wamefanya nini toka walipokabidhiwa nchi??? mpaka imefikia hatua ya kutaka katiba mpya, wakati miongoni mwenu kunaealioenda mbali mpaka walifikia hatua ya kupinga hata hoja ya kuwa na katiba mpya??? muombe Mungu akupe "macho" uone.
 
Back
Top Bottom