Mizengo Pinda for Pres 2015?

Status
Not open for further replies.
Kabla hajaondoka arudishe hela zetu kuanzia na zile 280000/-jambo hil lifanyike mapapema hata kesho..ili asiondoke na deni letu
 
Jamani kwanini tunarudia habari hizi? alisema mwenyewe hatagombea tena Ubunge huu ni wa Mwisho kwake...

Alitangaza alipokuwa anachukua form ndio maana hakuwa na Mpinzani...

SIO CHA AJABU JAMANI - LETENI HABARI MPYA... CCM INATUNYIMA HABARI MPYA INAONEKANA...
 
Hapa ni sebuleni kwangu, si mtandaoni.

Naongelea mtandaoni kwenye source iliyotolewa hapa, Deutsche Welle.

Najua Pinda ni tutusa, ila haya mambo kama kasema kweli atajipatia taji la ututusa zaidi. Wananchi wakikupa dhamana ya uongozi, ama unawatumikia mpaka mwisho, ama unasema kazi imenishinda unaachia wengine.

Kusema "kazi imenishinda lakini nitakuwepo kuwepo tu mpaka 2015" ni ujuha uso kifani.

Ndiyo maana napata tabu kuamini kwamba huyu Mizengo Pinda ni juha kiasi hicho kweli. Na kila nikiitafuta habari siioni ingawa imethibitishwa na "watu" wawili hapa.Mmoja akisema kwamba imetoka "Deutsche Welle".

Direct quote ni muhimu ili tupate maneno yake mwenyewe alivyoyapanga bila mtu kututafsiria, maana tafsiri inaweza kuongeza au kupunguza maana.

Nimekupata mkuu. Mimi pia nimesikia sauti ya ujerumani.
Nukuu ya karibu kabisa ya alichosema ni " kazi hii ni ngumu sana, hata usingizi unashindwa kupata usiku, ni bora sasa niwapishe wengine".
Nina uhakika ukiingia mtandao wa Deutsche Welle Kiswahili na kusikiliza taarifa ya habari ya leo jioni utaipata, kwa sababu alinukuliwa moja kwa moja na kiswanglish chake anachokipenda sana.
 
Ameshajenga kiwanja cha ndege kwa ajili ya wale wawekezaji wake wakubwa toka Marekani (Agraisal) kwa hiyo 2015 hatotaka kufanya siasa uchwara. Atakuwa mkulima mkubwa!
 
Why 2015 and not now? Kwa nini mzee avumilie hadi 2015 wakati hata usingizi unakua haupatikani jamani? Namhurumia mzee wa watu kwa kweli. Mimi sijui kuvumilia. Ningekuwa nishajitoa. Mwee!

kwa hiyo ungependa aondoke sasa ili tuzidishe msururu wa mawaziri wakuu tunaopaswa kuwahudumia sio?....
 
Jamani kwanini tunarudia habari hizi? alisema mwenyewe hatagombea tena Ubunge huu ni wa Mwisho kwake...

Alitangaza alipokuwa anachukua form ndio maana hakuwa na Mpinzani...

SIO CHA AJABU JAMANI - LETENI HABARI MPYA... CCM INATUNYIMA HABARI MPYA INAONEKANA...

Hii habari ni zaidi ya kutogombea ubunge, amesema kazi ngumu sana, kimsingi imemshinda.

Sasa kama kazi ngumu anasubiri nini mpaka 2015? Kwa nini asijiuzulu leo?
 
Kwani nani anamtaka tena, watu tuliweka matumaini makubwa kwake. Cha ajabu mtu tuliyemtegemea ndo huyo analialia bila ufumbuzi. "Mtoto wa mkulima" umekula vya kutosha nenda katumie sasa.
 
Angepata heshima kubwa angeyasema haya ya kungatuka mwk 2015 na si sasa ni uchuro!!
 
mtu mzima kama kinyonga, hana lolote zaidi ya kuwa kigeugeu. Angechukua nafasi ya Regia mbona ingekuwa freshi.
 
Huyu pinda nae mpaka 2015! Aaa hata angesema kesho kafanya nn zaidi ya kulia bungeni! (waziri mkuu wa kwanza kulia live
bungeni!) ndo ntakachomkumbukia!!!.
 
Si ni huyu nasikia leo katanganza kuhalalisha posho za wabunge ziwe 200,000??????
Anawaza kukimbia kesi baada ya kuwa ameliibia taifa?? anajidanganya
 
Kuna viongozi ambao kauli zao hazina uhalisia na huyu jamaa ni mmoja wao,yuko kinafikinafki zaidi,nwy kama ni hivyo basi ni bora lakini atuambie mpaka 2015 mbona ni parefu?...huyu jamaa simwamini hata kidogo let wait n see
 
Ana makosa mengi!!!

1. Kauza ardhi yote kwao kwa wamarekani akishirikiana na Masha. Wkajengewa uwanja wa ndege, na Masha akajengewa shule hata hivyo haikumsaidia kwani ubunge alikosa.
2. Hakumshauri vizuri JK kuhusu wakimbizi wa Burundi; akataka kuwasambaza nchi nzima akagomewa na wakuu wa mikoa sasa anaona aibu.

Pia aliopanga wamsaidie JK kawaondoa. wa kwanza Mkuchika akiwa naibu katibu mkuu na mkuu wa watumishi wote wa CCM Tanzania. Alitegemea angempangia atakaowatumia. Fagio la awali CCM likamng'oa. Pia alitaraji kuwa Yambesi angepata nafasi ya Ukatibu mkuu kiongozi ili ampangie watumishi wa kumsaidia, JK kafanya suprise si kwa Pinda pekee bali kwa wengi.

Vilevile msisahau kuwa anaendelea kumhujumu JK kwa kila hali. Anaendeleza kwao hata kwa kuuza rasilimali ya watu wa Rukwa. Hawaelewani na Arfi kwa hili.

Msisahau pia kuwa ni mgonjwa anaona hali inaendelea kuwa si nszuri!! Tumuombee!!
 
Amini usiamini habari za kiintelijensia zimetonya kuwa tayari Mheshimiwa Mizengo Pinda ndie Raisi mtarajiwa baada ya Mheshimiwa Kikwete kumaliza nngwe yake.
Habari za ndani ya kasha zimesema kuwa Mheshimiwa Pinda ameshapewa baraka zote za wakuu na kinachoendelea sasa ni mikakati ya kumpa kipau mbele katika harakati nyingi zinazohusisha jamii.
Kwa ufupi hana mpinzani wa kweli zaidi ya vivuli ambavyo vitajiengua katika hatua za mwisho.
 
Mkuu naona umechoka na pilika pilika za leo pale jangwani! Lala salama maana umeanza kuota hata kabla hujalaa. Usiku mwema.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom