Lycaon pictus
JF-Expert Member
- Jan 31, 2021
- 7,243
- 12,767
- Thread starter
- #21
Nashukuru sana mkuu.Ngoja nisaidie mtoa mada kufanya watu wamwelewe.
Yaani anamaanisha kuwa mti huinyonya dunia (ardhi) katika ukuaji wake kwenda juu. Kama mti utakuwa na uzito wa tani 8 hivyo utakuwa umechukua tani nane ya udogo toka uliposimamia. Nikama jengo la tani 8 ili lijengwe litasababisha shimo kwa ajiri ya udongo huo wa tani nane ulipotoka. Sasa swali lake ni kuwa. Mti umechukua tani nane duniani ukazipandisha juu kama wajenzi wa majengo wafanyavyo. Je yale mashimo ya hiyo sehemu inayonyonywa na miti mbona hatuyaoni. Je mti hupata malighafi kutoka mbali na eneo ulipo kama majengo ya mjini yananyosombewa mchanga na magari toka mtoni ili yasimame hapo nyerere road?