Huyu mtoto angepata div1 ya point saba nina uhakika kingeandaliwa kipindi maalumu kwa ajli yake ili awasihi wanafunzi wengine namna alivyokuwa anasoma ili na wao wafaulu.....lakini kwa kuwa amefeli na kupata four ya point 27 watu wakiuliza imekuwaje mtoto mwenye kila kitu nyumbani akapata daraja hilo wanaonekana ni wachochezi....tena ilifaa waandishi wamfate huyo mtoto na wamuulze imekuwaje akapata hivyo....nini kilipungua?
Lakini ukweli utabaki pale pale juu ya mwanaasha......huyu mtoto alikuwa mzito na wazazi wake hawakujua mapungufu yake toka alipotimuliwa kifungiro baada ya kushindwa kufikisha wastani na wakamuhamishia hapo Feza.... Wazazi walishindwa kujua kuwa binti ni mzito wa kuelewa na walikuwa hawafuatilii maendeleo yake ya shule...kama wote mjuavyo wazazi wa huyu binti wanashinda angani na kwenye bembea na wakirudi nyumbani badala ya kufatilia maendelea ya mtoto wao wao...wenyewe wazazi wanamchukua mtoto na kumpeleka kwenye shows kama inavyoonekana hapa chini...
Sasa hivi mama Salma na Kikwete waongeze nguvu na ufatiliaa kwa watoto wao wengine..kuna huyo mmoja anaitwa Ali nae ni mzito wa kuelewa tena sana.....kwa kuwa wako Botswana najua matokeo yao hayataonekana kama ya huyu Mwanaasha...ila ukweli utabaki kusemwa kuwa juu ya Mwanaasha, ni uzembe wake na uzembe wa wazazi wake...
Siku zote huwa nasema hivi:
Anayepata div one na anaepata div.iv wote msuli wao uko sawa ila in opposite direction.....wakati huyu anakomaa kupata div one huyu mwingine nae yuko bize na shows kama hizi :